Beira Boy
JF-Expert Member
- Aug 7, 2016
- 17,895
- 25,944
Amani iwe nanyi wapendwa,
Inaniuma sana, nilikuwa na msichana mmoja mkali baraa yaani mzuri sana (kisu) hatari lakini kwa sasa siko naye tena.
Mimi naishi nyumbani lakini yule msichana nilimwambia kuwa hapa ninapoishi nimepanga na chumba nalipia laki moja kwa mwezi, shida ilikuwa inakuja pale alipokuwa ananiambia aje gheto apaone, hapo ndo shida ilipokuwa maana nilikuwa namkatalia. Nilikuwa namwambia mama mwenye nyumba hataki nipeleke msichana kwenye nyumba yake na ni mkali sana nikipeleka msichana anaweza vunja mkataba na mimi.
Hata siku nilipokuwa nataka kumpiga mikasa nilikuwa nampeleka gest maana kama unavyojua huwezi peleka msichana kwenye nyumba ya dada yako hata kidogo.
Sasa ile juzi sijui nani kamtonya kuwa mimi naishi kwa dada kafula ile mbaya kanipigia simu anaomba tuachane, ile kumuuliza sababu ndo akasema kuwa sababu ni kwa kuwa mimi ni muongo sana nilimuambiwa nimepanga kumbe naishi kwa dada.
HIVI HUYU MSICHANA ALIKUWA ANANIPENDA KWELI? MBONA KANITOSA KISA TU NAISHI NYUMBANI?
LONDON BOY
Inaniuma sana, nilikuwa na msichana mmoja mkali baraa yaani mzuri sana (kisu) hatari lakini kwa sasa siko naye tena.
Mimi naishi nyumbani lakini yule msichana nilimwambia kuwa hapa ninapoishi nimepanga na chumba nalipia laki moja kwa mwezi, shida ilikuwa inakuja pale alipokuwa ananiambia aje gheto apaone, hapo ndo shida ilipokuwa maana nilikuwa namkatalia. Nilikuwa namwambia mama mwenye nyumba hataki nipeleke msichana kwenye nyumba yake na ni mkali sana nikipeleka msichana anaweza vunja mkataba na mimi.
Hata siku nilipokuwa nataka kumpiga mikasa nilikuwa nampeleka gest maana kama unavyojua huwezi peleka msichana kwenye nyumba ya dada yako hata kidogo.
Sasa ile juzi sijui nani kamtonya kuwa mimi naishi kwa dada kafula ile mbaya kanipigia simu anaomba tuachane, ile kumuuliza sababu ndo akasema kuwa sababu ni kwa kuwa mimi ni muongo sana nilimuambiwa nimepanga kumbe naishi kwa dada.
HIVI HUYU MSICHANA ALIKUWA ANANIPENDA KWELI? MBONA KANITOSA KISA TU NAISHI NYUMBANI?
LONDON BOY