SMZ yazidi kuubomoa Muungano yataka bara walipe kodi ya ardhi

Tatizo dilo hilo. Kwa nini ardhi ya Sengerema iwe ruksa kwa mpemba lakini ya Dole iwe marufuku kwa msukuma? hata hicho kipengele cha kukaa mfululizo kina matatizo. Huyo Msukuma akiomba uzanzibari baada ya miaka mitano si atakumbushwa pale alivyoenda kuhani msiba Sengerema akakaa zaidi ya mwezi mmoja! Na kwa hiyo miaka mitano anapofukuzia huo uzanzibari awe analipa hizo dola 5000 kwa kila kihekta kimoja!

Kuujua huu mfumo wetu wa Muungano haumaanishi kuwa kila kitu kifanywacho chini yake ni cha haki.

Amandla......
Usione taabu kurudi katika mijadala ya nyuma. Ndio pale tulipokwambia kuwa Zanzibar ni Nchi, na Tanzania ni Nchi. Hivyo Jamhuri ya Muungano ina nchi mbili. Kuna Watanzania wanye haki ya kumiliki ardhi ya Tanzania (Wakiwemo Wazanzibari) na Wazanzibari wanye haki ya kumiliki ardhi ya Zanzibar (iliyomo ndani ya Tanzania). Utekelezaji wa mambo unaweza ukawa na vijikasoro vya kiutendaji (na ndiyo maana tuna kero za Muungano). Lakini sheria ya Mzanzibari imezingatia sana haja ya Muungano wetu na imetoa provision kuruhusu Mtanzania asiye Mzanzibari kujumuika na wenziwe wa Zanzibar na kuwa Mtanzania -Mzanzibar.Wapo wasukuma na Wanyamwezi kule Dole waliokaa zaidi ya miaka mitano ( na hivyo kuwa Wazanzibari) mbona wanamiliki mashamba ya migomba na matuta ya viazi bila bughudha.
 
Usione taabu kurudi katika mijadala ya nyuma. Ndio pale tulipokwambia kuwa Zanzibar ni Nchi, na Tanzania ni Nchi. Hivyo Jamhuri ya Muungano ina nchi mbili. Kuna Watanzania wanye haki ya kumiliki ardhi ya Tanzania (Wakiwemo Wazanzibari) na Wazanzibari wanye haki ya kumiliki ardhi ya Zanzibar (iliyomo ndani ya Tanzania). Utekelezaji wa mambo unaweza ukawa na vijikasoro vya kiutendaji (na ndiyo maana tuna kero za Muungano). Lakini sheria ya Mzanzibari imezingatia sana haja ya Muungano wetu na imetoa provision kuruhusu Mtanzania asiye Mzanzibari kujumuika na wenziwe wa Zanzibar na kuwa Mtanzania -Mzanzibar.Wapo wasukuma na Wanyamwezi kule Dole waliokaa zaidi ya miaka mitano ( na hivyo kuwa Wazanzibari) mbona wanamiliki mashamba ya migomba na matuta ya viazi bila bughudha.

Sioni taabu. Na hao wasukuma na wanyamwezi unaowazungumzia wangeweza kulipa dola 5000 kwa mwaka kwa miaka mitano? Hapa tunazungumzia hii kodi mliyoiingiza ili kufanya hata hiyo option ya kukaa miaka mitano kuwa ngumu mno! Kama huku ndiko kuzingatia haja ya Muungano wetu ( kwa kumfanya mtanzania bara kuwa sawa sawa na mfilipino) basi sijui hapo mtakapoamua kutozingatia itakuwaje!

Amandla....
 
Hili ndiyo tatizo ya serikali mbili. Zanzibar wana platform ya kutoa madai yao. Zenji wana ZRA iliyo baki ni TRA which is ya muungano. Sasa ukiwatoza wazenji wanaokaa bara utawa tozaje wakati TRA ni Tanzania siyo Tanganyika Revenue Authority. Kungekua na serikali tatu at least yote haya isinge kua shida. Tatizo ni kwamba Zanzibar imekua ya wazanzibar na Tanganyika imekua ya Tanzania. Simply put the situation now on the point of view of Zanzibaris ni changu ni changu na chako ni chetu. It's sad but its the truth. Wazanzibarr wana mamlaka zao inayo shugulikia mambo yao wenyewe lakini Tanzania bara hakuna, kila kitu ni muungano.

Suluhisho la kumaliza dhulma hii ni:

1. Kuanzisha Serikali ya Tanganyika. Tunaona hii ya muungano haina meno kabisa dhidi ya Sheria kandamizi dhidi ya Watanganyika.

2. Kuvunja Serikali ya Zanzibar na kubaki na Serikali moja. wazenji hasa viopngozi wataipinga kuogopa kupoteza ulaji.

3. Kuvunja huu Muungano kabisa, ili wazanzibari wanaoishi huku Tanganyika wajulikane kama foreigners ili waombe vibali vya kuishi nchi jirani ya Tanganyika, watakaokubaliwa wavilipie, watakashindwa warudi kwao Zanzibar. Pia washindwe kumiliki ardhi etc. HII NDIYO BEST OPTION, kwanini tunawabembeleza hawa?

Kufuatia udhaifu wa kiuongozi na kimaamuzi wa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM kwenye kikao cha NEC Butiama, ilishaonekana kuwa wazanzibari wanajua udhaifu wake. Na watamyumbisha sana tu.


Ole wenu mnaotawaliwa na kiongozi dhaifu!
 
Hakuna ardhi ya bara. Ardhi ya bara ni ya watanzania wote na ya Zanzibar ni ya wazenji peke yao!

Utatusaidia kama utatutolea mfano wa nchi nyingine ambapo uhuru wa kumiliki ardhi kwa baadhi ya raia unawekewa vizingiti wakati wengine hawana vizingiti!
Mw.nyerere ndie aliyekataa serikali 3 . lakini wa-zenj walitaka mapema serikali 3,ili kila upande ufanye mambe yake binafsi na baadhi ya mambo ndio ya muungano. ujanja wake ulikua ameona kama wa zenj ni kidogo kwahiyo hata wote wakihamia bara bado hawatabadilisha kitu. madhumuni yalikua ni kuifanya zanzibar uwe mkoa. kwahiyo walikubaliana kama smz iendelee na serikali yake. na bara watatumia serikali ya muungano. lakini huu ni ujanja tu walichotaka ni kiufanya znz kua mkoa. mimi naona ni sawa kwasababu watanganyika ndio wamelemaa .wa-zenj wakidai haki zao mnawaona wakorofi wanaleta kero, lakini wako right! kwasababu yote wanayo yadai yako katika sheria zao. ambapo muungano umeruhusu kuwepo kwa smz . ufumbuzi ni ku uweka mezani muungano ,uangaliwe upya na sio kulazimishana kwa maslahi ya wachache.
 
Suluhisho la kumaliza dhulma hii ni:

1. Kuanzisha Serikali ya Tanganyika. Tunaona hii ya muungano haina meno kabisa dhidi ya Sheria kandamizi dhidi ya Watanganyika.

2. Kuvunja Serikali ya Zanzibar na kubaki na Serikali moja. wazenji hasa viopngozi wataipinga kuogopa kupoteza ulaji.

3. Kuvunja huu Muungano kabisa, ili wazanzibari wanaoishi huku Tanganyika wajulikane kama foreigners ili waombe vibali vya kuishi nchi jirani ya Tanganyika, watakaokubaliwa wavilipie, watakashindwa warudi kwao Zanzibar. Pia washindwe kumiliki ardhi etc. HII NDIYO BEST OPTION, kwanini tunawabembeleza hawa?

Kufuatia udhaifu wa kiuongozi na kimaamuzi wa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM kwenye kikao cha NEC Butiama, ilishaonekana kuwa wazanzibari wanajua udhaifu wake. Na watamyumbisha sana tu.


Ole wenu mnaotawaliwa na kiongozi dhaifu!
sio wapemba tu watakao lazimika kuomba hati za ukaazi tangayika . wandenge -nyamwezi -sukuma -konde -ruguru- chusa -masai na wengine amboa wanaishi zenj pia.
 
Sioni taabu. Na hao wasukuma na wanyamwezi unaowazungumzia wangeweza kulipa dola 5000 kwa mwaka kwa miaka mitano? Hapa tunazungumzia hii kodi mliyoiingiza ili kufanya hata hiyo option ya kukaa miaka mitano kuwa ngumu mno! Kama huku ndiko kuzingatia haja ya Muungano wetu ( kwa kumfanya mtanzania bara kuwa sawa sawa na mfilipino) basi sijui hapo mtakapoamua kutozingatia itakuwaje!

Amandla....

Ndugu yangum aya mambo yanataka uyaangalie kwa busara na siyo kuelemewa na jazba. Mtanzania (kutoka Bara) kwa nini umfananishe na Mfilipino katika kadhia hiyo. Unahitaji kurudi nyuma (narudia tena)na kuungalia kujiri kwa Muungano wetu na busara ziizotumika katika kuanzisha mfumo wa Serikali mbili. Watanzania wote ni Watanzania. Lakini imetumika busara kuulinda U-zanzibari. Na yule aliye bara hakuwekewa kizingiti kuwa Mzanzibari bali kuna prcess tu ya kumfanya awe Mzanzibzri. Hebu nenda kule Zanzibar kaangalie Watanzania kama hao wenye asili ya Bara wanagapi leo wanajinasibun kuwa Wa-Zanzibari na wana hakimsawa na Wazanzibari asilia (washirazi wa pale) wakiwa na haki sawa ya kuchagua viongozi na kuchaguliwa kuwa viongozi. Hilo la kulipa ardhi haliwatengi Watanzania kutoka Bara na kamwe halikusudii kuwanyima haki ya ya kumiliki ardhi iliyoko Zanzibar. Bila ya shaka watamiliki lakini kufuata utaratibu wetu wa MUJNGANO. Kinhume cha hivyo ni kuukana Muungano wenyewe.
 
Ndugu yangum aya mambo yanataka uyaangalie kwa busara na siyo kuelemewa na jazba. Mtanzania (kutoka Bara) kwa nini umfananishe na Mfilipino katika kadhia hiyo. Unahitaji kurudi nyuma (narudia tena)na kuungalia kujiri kwa Muungano wetu na busara ziizotumika katika kuanzisha mfumo wa Serikali mbili. Watanzania wote ni Watanzania. Lakini imetumika busara kuulinda U-zanzibari. Na yule aliye bara hakuwekewa kizingiti kuwa Mzanzibari bali kuna prcess tu ya kumfanya awe Mzanzibzri. Hebu nenda kule Zanzibar kaangalie Watanzania kama hao wenye asili ya Bara wanagapi leo wanajinasibun kuwa Wa-Zanzibari na wana hakimsawa na Wazanzibari asilia (washirazi wa pale) wakiwa na haki sawa ya kuchagua viongozi na kuchaguliwa kuwa viongozi. Hilo la kulipa ardhi haliwatengi Watanzania kutoka Bara na kamwe halikusudii kuwanyima haki ya ya kumiliki ardhi iliyoko Zanzibar. Bila ya shaka watamiliki lakini kufuata utaratibu wetu wa MUJNGANO. Kinhume cha hivyo ni kuukana Muungano wenyewe.

Hakuna cha jazba, ndugu yangu.

Hii sheria mpya tunayoijadili ( na si historia) haitofautishi kiwango anacholipa asie raia wa Tanzania ( Mfilipino na wengine) na mtanzania bara. Wote wanatakiwa kulipa dola 5000 kwa mwaka kwa hekta. Sasa utasemaje kuwa hauwatengi kama wewe mwenyewe umewaweka kundi moja na hao wageni? Talk is cheap. Hatuwezi kuuenzi Muungano kwa maneno tu wakati tunafanya vingine kwa matendo!

Tangu lini mshirazi amekuwa ana asili ya Zanzibar kuliko mtanzania bara? Kwani wakina Seyyid Said walipokuja hawakukuta watu? Na hao watu walitokea wapi? Na nauliza hivi, si kwa jazba, bali kutaka kuelewa. Maana naona inaelekea huo uzanzibari ni haki ya washirazi na wengine ( wenye asili ya bara, ungazija n.k.) wanafanyiwa feva tu!

Unasemaje watanzania bara watamiliki ardhi wakati unawawekea viwango ambavyo ni usury!
Au unataka wakae huko kitwana maana kazi zote za maana mmeishasema wapewe upendeleo wazanzibari. Na huko tena watanzania bara wamewekwa kundi moja na wasio watanzania.

Hapana, Mkuu. Ni vitendo vyenu vinavyotuambia kuwa huu Muungano ni gelesha tu. Unathaminiwa mnapofaidika lakini mnapoweza mnautumia kuwakomoa watanzania bara!

Amandla....
 
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imetangaza mkakati mpya wa kuwataka wawekezaji na watu wenye asili ya Tanzania Bara kusajiliwa na kuanza kulipa kodi ya ardhi ya dola za Marekani 5000 (Sh6.5 milioni), kila mwaka kwa kila hekta moja ya ardhi.

Palikuwa na taabu gani kuweka kiwango tofauti kwa watanzania watokao bara?
 
Hakuna cha jazba, ndugu yangu.

Hii sheria mpya tunayoijadili ( na si historia) haitofautishi kiwango anacholipa asie raia wa Tanzania ( Mfilipino na wengine) na mtanzania bara. Wote wanatakiwa kulipa dola 5000 kwa mwaka kwa hekta. Sasa utasemaje kuwa hauwatengi kama wewe mwenyewe umewaweka kundi moja na hao wageni? Talk is cheap. Hatuwezi kuuenzi Muungano kwa maneno tu wakati tunafanya vingine kwa matendo!

Tangu lini mshirazi amekuwa ana asili ya Zanzibar kuliko mtanzania bara? Kwani wakina Seyyid Said walipokuja hawakukuta watu? Na hao watu walitokea wapi? Na nauliza hivi, si kwa jazba, bali kutaka kuelewa. Maana naona inaelekea huo uzanzibari ni haki ya washirazi na wengine ( wenye asili ya bara, ungazija n.k.) wanafanyiwa feva tu!

Unasemaje watanzania bara watamiliki ardhi wakati unawawekea viwango ambavyo ni usury!
Au unataka wakae huko kitwana maana kazi zote za maana mmeishasema wapewe upendeleo wazanzibari. Na huko tena watanzania bara wamewekwa kundi moja na wasio watanzania.

Hapana, Mkuu. Ni vitendo vyenu vinavyotuambia kuwa huu Muungano ni gelesha tu. Unathaminiwa mnapofaidika lakini mnapoweza mnautumia kuwakomoa watanzania bara!
Amandla....
Na tubakie katika sheria mpya. Sheria mpya imekusudia zaidi wafanyabiashara ambao wanakuja Zanzibar kwa kufanya biashara kutoka nje yaTanzania na ndani ya Tanzania (upande wa bara). Hao ndio wanaotakiwa kulipa viwango hivyo kwa minajili ya biashara. Mtanzania kutoka Bara ukitaka kuweka makaazi Zanzibar hutakiwi kulipa ada hiyo unakaa katika ardhi bure na ukitimiza miaka mitano (wewe kisheria umeshajumuika na Watanzania wenzio wenyeji wa pale -ni Mzanzibari) ardhi unayoikalia unaweza kuiomba kuwa milki yako.
Seyyid Said si Mshirazi ni Mmanga wa Oman. Alipokuja Zanzibar aliwakuta Washirazi pale. Washirazi ni mchanganyiko wa wenyeji wa asili wa Zanzibar (ambao ni watu waliohamia mwanzo kabisa Zanzibar wakitokea sehemu za mwambao wa Mzizima "Dar es -salaam" waliingia visiwani kwa minajili ya uvuvi na wakajenga maskani) na wageni waliotoka Uajemi (eneo la pwani ya Shirazi)
Sithubuhtu kusema kuwa Muungano ni geresha. lakini mfumo wa Serikali mbili ndio msingi wake. Umewekwa mfumo huo ili kuihifadhi Zanzibar na kuinusuru kumezwa na Tanganyika. Sasa Wazanzibar wanaposimama imara kutaka tuufuate mfumo huo watu wengine mnaona kuwa wanataka kuvunja Muungano. Hivi wanataka kuvunja Muungano au wanauimarish Muungano kwa kuzingatia misingi yake mikuu- nayo ni Serikali mbili na kuihafadhi Zanzibar. Wanaotaka kuvunja Muungano ni wanaodai kuwepo kwa Tanganyika au kufutwa kwa SMZ na Zanzibar. Vitendo hivyo vikifanyika - hapo inakuwa ni kinyume na malengo na makusudio ya Muungano kama tunazungumzia ule tuliofikia Tarehe 26 April 1964.
 
Palikuwa na taabu gani kuweka kiwango tofauti kwa watanzania watokao bara?
Nafikiri ungekuwa unasoma vitu kwa jicho la uchambuzi . Hapo hiyo kodi anakusudiwa Mfanyabiashara mgeni (asiye Mzanzibari -na kwa maana hiyo asiye Mtanzania)). sasa Mfanyabiashara kutoka Bara siyo Mgeni yeye ni Mtanzania ambaye anafursa ya kuwa Mzanzibari baada ya kutimiza mambo fulani (ambayo tumeyakubali kwa mujibu wa Katiba na misingi ya Muungano wetu). sasa kwa nini anataka kujifanya kama mgeni (kwa kulipa kodi) baada ya kutimiza hayo mambo fulani akawa Mzanzibari na kufanya biashara zake kama Mzanzibari- Mtanzania (bila ya kodi ya ardhi?)
 
Asante kwa ufafanuzi wako.

Tatizo ni kumfafanua nani ni mfanya biashara na nani sie! Nikitaka kuweka makazi na kulima mboga mboga za kuuza markiti utaniita nani? Au kwenye hicho kibanda changu nikifungua kagenge ka uzia mbogamboga? Vyote hivi si vitanifanya kuwa mfanyabiashara. Mgeni mwekezaji!

Sheria hii itanihusu vipi mimi ambae nimeoa mzanzibari? Itawahusu vipi watoto wangu niliozaa na mzanzibari? Yaani na wao wakitaka kwenda kurithi shamba la mjomba wao wataambiwa kuwa wao ni wageni?

Kuna uwezekano mkubwa wa hii sheria kutumika kuwanyanyasa wenye asili ya bara! Na nilitegemea wenye uchungu na Muungano kama wewe, mngewaonya viongozi wenu! Katika mazingira kama haya ya leo, ilibidi waangalie itatafsiriwa vipi kabla ya kuileta. Kwa kufanya walivyofanya, wamewaongezea risasi wale wasioutaka Muungano ambao hata bara wako wengi tu.

Amandla........
 
Nafikiri ungekuwa unasoma vitu kwa jicho la uchambuzi . Hapo hiyo kodi anakusudiwa Mfanyabiashara mgeni (asiye Mzanzibari -na kwa maana hiyo asiye Mtanzania)). sasa Mfanyabiashara kutoka Bara siyo Mgeni yeye ni Mtanzania ambaye anafursa ya kuwa Mzanzibari baada ya kutimiza mambo fulani (ambayo tumeyakubali kwa mujibu wa Katiba na misingi ya Muungano wetu). sasa kwa nini anataka kujifanya kama mgeni (kwa kulipa kodi) baada ya kutimiza hayo mambo fulani akawa Mzanzibari na kufanya biashara zake kama Mzanzibari- Mtanzania (bila ya kodi ya ardhi?)

Hapa unazidi kunichanganya.

Huyo mtanzania bara atalipa kiasi gani wakati anangoja kuwa mzanzibari? Kitu ambacho kitamchukua si chini ya miaka mitano hapo hapo Zanzibar! Au una maana wakati akisubiri asifanye biashara? Afanye nini basi ili aweze kuishi? Maana hata katika ajira nae amewekewa vikwazo.

Mfanyabishara mgeni asie mzanzibari inamjumlisha na mtanzania bara!


Amandla...
 
Chadema wameishiwa . Sera ya Majimbo, anaitaka nani ulimwengu huu wa leo. Lets keep,our Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Lakini tuwe serious katika huili

Pakacha, majimbo sio kuvunja muungano!!!! Unajua NY, LA TX n.k ni majimbo ndani ya USA????
 
Hivi hawa Wazenj hawafahamu hicho kisiwa baada ya miaka 100 kitapotea chini ya bahari? Badala ya kutona sisi wa bara kuwa ni wa maana wao wanairingia kweli nchi yao. Siwezi kuwa mpuuzi nikanunue ardhi ambayo ninajua baada ya miaka 100 watukuu wangu hawataikuta. Naona watukuu wao ikifika huko watawalaani kuwa wazee wao walikuwa wapuuzi kama sisi tunavyowashangaa akina Lobengula na akina Kimweri kwa kuiuza nchi kwa wajerumani
 
Hivi hawa Wazenj hawafahamu hicho kisiwa baada ya miaka 100 kitapotea chini ya bahari? Badala ya kutona sisi wa bara kuwa ni wa maana wao wanairingia kweli nchi yao. Siwezi kuwa mpuuzi nikanunue ardhi ambayo ninajua baada ya miaka 100 watukuu wangu hawataikuta. Naona watukuu wao ikifika huko watawalaani kuwa wazee wao walikuwa wapuuzi kama sisi tunavyowashangaa akina Lobengula na akina Kimweri kwa kuiuza nchi kwa wajerumani

Maldives tayari watu wamehamishwa baada ya baadhi ya visiwa kupotea kutokana na Global Warming!

Zenji pia visiwa kuzama na maji inaweza kutokea: miaka ijayo!
 
Lipeni au muhame,yaani mmezoea kufanya ufisadi huko kwa style za Mengi ,mnawekeza kwa style ya Rostam ,mnafanya biashara kwa style ya Mkapa ,mnaongozana kwa style ya Kikwete , atakubali nani ?
Mhame tu msituambukize matatizo ambayo mmeshindwa kuyatibu na inaonyesha hayatibiki .
 
Maldives tayari watu wamehamishwa baada ya baadhi ya visiwa kupotea kutokana na Global Warming!

Zenji pia visiwa kuzama na maji inaweza kutokea: miaka ijayo!

Maji hayatushughulishi kuna watuwanaishi jangwani na maji kwao yamejaa tele.ukiritimba wa Serikali ya Muungano ndio unaotuchelewesha ,leo hii tungeliweza kabisa kuyaconvert maji ya bahari na kutumia tutakavyo na system za kuyageuza maji hayo siku hizi zimejaa lakini tukitaka kuanzisha wanazuka machogo na kututilia mguu eti tusubiri ushauri kutoka Serikali ya Muungano ,sijui mambo yanashugulikiwa ,Mwanakemia mkuu anafanya uchunguzi kama maji ya bahari yanaa kwa matumizi ya binadamu yaani ndio kujifanya ni wasomi kweli wakati waindi wachache tu wamewaibia na kuwatawala.
 
Maji hayatushughulishi kuna watuwanaishi jangwani na maji kwao yamejaa tele.ukiritimba wa Serikali ya Muungano ndio unaotuchelewesha ,leo hii tungeliweza kabisa kuyaconvert maji ya bahari na kutumia tutakavyo na system za kuyageuza maji hayo siku hizi zimejaa lakini tukitaka kuanzisha wanazuka machogo na kututilia mguu eti tusubiri ushauri kutoka Serikali ya Muungano ,sijui mambo yanashugulikiwa ,Mwanakemia mkuu anafanya uchunguzi kama maji ya bahari yanaa kwa matumizi ya binadamu yaani ndio kujifanya ni wasomi kweli wakati waindi wachache tu wamewaibia na kuwatawala.

Mwiba,

Je umeelewa?? unaongea mengine..wakati Science inaonyesha visiwa vinazama kutokana na maji kuongezeka as a result of global warming!!!

sasa wewe una story tofauti!! je unaelewa kinachoongelewa??
 
Asante kwa ufafanuzi wako.

Tatizo ni kumfafanua nani ni mfanya biashara na nani sie! Nikitaka kuweka makazi na kulima mboga mboga za kuuza markiti utaniita nani? Au kwenye hicho kibanda changu nikifungua kagenge ka uzia mbogamboga? Vyote hivi si vitanifanya kuwa mfanyabiashara. Mgeni mwekezaji!

Sheria hii itanihusu vipi mimi ambae nimeoa mzanzibari? Itawahusu vipi watoto wangu niliozaa na mzanzibari? Yaani na wao wakitaka kwenda kurithi shamba la mjomba wao wataambiwa kuwa wao ni wageni?

Kuna uwezekano mkubwa wa hii sheria kutumika kuwanyanyasa wenye asili ya bara! Na nilitegemea wenye uchungu na Muungano kama wewe, mngewaonya viongozi wenu! Katika mazingira kama haya ya leo, ilibidi waangalie itatafsiriwa vipi kabla ya kuileta. Kwa kufanya walivyofanya, wamewaongezea risasi wale wasioutaka Muungano ambao hata bara wako wengi tu.

Amandla........
Ndugu yangu tatizo lipo wapi hapo. Hivi Mfanyabiashara hajulikani kweli. Tena huyo tunaemzungumza kuwa anahitaji kulipa Dola 5000 kwa kuichukua ardhi ya hekta. Tatizo hili neno Mfanyabiahsra linazungumzwa sana pamoja na utani. Mathalani Ndugu zetu wa Kimachinga utasema wafanyabiashara?, swahibu zangu wa Kipemba wenye kijiduka cha kuchuuzia mabatata na vitunguuu hapo Kariakoo-utasema mfanyabiashara? Laa Mfanyabiashara kwa mfano wa Wa-Tanzania wanaoishi Bara ni kama kina Bw. Mengi, Bakhressa , Rostam, na wengineo-wenye viwanda na maduka makubwa na makampuni na majumba ya kukodisha na mashamba na mazizi ya ngombe.
Ukishaamua kuweka makaazi Zanzibar wewe Mtanzania kutoka Bara unajuilisha rasmi vyombo vinavyohusika. Unakaribishwa na wenyeji, unapewa sehemu kama una uwezo wa kujenga unajenga kibanda. Kuweka kijiduka cha kuchuuzia mboga kupata ugali wa watoto ni ruksa, lakini kupewa hekta kufungua kiwanda hiyo sheria ndiyo inasema hutoweza kupewa mpaka utakapokuwa Mzanzibari Mtanzania (baada ya kutimiza hayo matakwa ikiwa ni pamoja na kuishi hapo kwa muda wa miaka mitano na kuthibitisha kuwa kweli wewe umeamua kuwa mkaazi wa Zanzibar). Mbona ndugu zetu kutoka Bara walioingia kwa mtindo huo wapo wengi tu. Wengine (Wazanzibari- Watanzania) leo wana biashara kubwa kubwa pale za Guest House na Baa, wengine wana mashamba, na wasio wafanyabiashara ni mabosi wetu Maofisini mwa vyombo vya SMZ.
Tanzania ina uraia mmoja tu wa Mtanzania. Sote sisi ni raia wa Tanzania. Uzanzibari unahusiana sana na Ukaazi. Hivyo suala la ndoa halihusu hapo. Ukiwa umeoa au hujaoa kinachohitajika ni ukaazi wako(uwe ni wa kudumu nao huthibitishwa na kipimo cha angalau kukaa hapo kwa muda wa miaka mitano mfululizo). Watoto hawahusiki hapo. Watahusika watakapofikia umri wa maiaka kumi na nane (na hapo watakuwa wameshakuwa wakaazi wa kudumu).
Sheria haiwezi kutumika kiuwakandia Watanzania wenye asili ya Bara Na watakaoitumia kwa ajili hiyo ndio wale wachafuzi wetu tunaowatafuta. Ni wahaini hao- ha hukumu ya Wahai ni nafikiri unaifahamu. Viongozi wetu wako sahihi na makini na Tunawapongeza kwa hatua zao za busara za kuimarisha Muungano wetu na misingi yake mikuu(Mfumo wa Serikali Mbili na Kuepusha Zanzibar kumezwa na iliyokuwa Tanganyika katika mwamvuli wa Muungano wetu)
 
Maji hayatushughulishi kuna watuwanaishi jangwani na maji kwao yamejaa tele.ukiritimba wa Serikali ya Muungano ndio unaotuchelewesha ,leo hii tungeliweza kabisa kuyaconvert maji ya bahari na kutumia tutakavyo na system za kuyageuza maji hayo siku hizi zimejaa lakini tukitaka kuanzisha wanazuka machogo na kututilia mguu eti tusubiri ushauri kutoka Serikali ya Muungano ,sijui mambo yanashugulikiwa ,Mwanakemia mkuu anafanya uchunguzi kama maji ya bahari yanaa kwa matumizi ya binadamu yaani ndio kujifanya ni wasomi kweli wakati waindi wachache tu wamewaibia na kuwatawala.
Mwiba,
Mie na-support kabisa Zanzibar kujimegua na kufanya mambo yake. Kufuata Tanzania Bara ni kupoteza muda kwa sababu Tanzania bara kuna matatizo mengi na sugu ambayo hawana muda wowote wa kufikiria matatizo ya Zanzibar. Tanzania is too big for the Tanzania president; better leave Zanzibar total autonomy to the Zanzibar President. That will be the best for both Tanganyika and Zanzibar.
 
Back
Top Bottom