SMZ yataka marekebisho sera ya ushirikiano

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
kidogo kidogo tutafika, hatutochoka kudai haki yetu kwenye muungano hadi mambo yawe sawa.

hongereni wawakilishi na nnakuhusieni acheni siasa za kubaguana na kuweka uzanzibari kwanza kisha utanzania na uccm au ucuf

SMZ yataka marekebisho sera ya ushirikiano




na Mwandishi Wetu



SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar, imetaka kutazamwa upya kwa sera ya ushirikiano wa kimataifa ili kuepusha usumbufu kwa viongozi wa kitaifa.
Hayo yalisemwa jana na Naibu Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Tafana Kassim Mzee, wakati wa semina ya kujadili sera mpya ya Mambo ya Nje iliyoandiliwa kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.

Waziri huyo, alisema hatua za lazima zichukuliwe kutokana na tukio alilolishuhudia akiwa nchini Uingereza katika ziara ya Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Sheni.

ALieleza kushangazwa na kitendo cha kutaka kufanyiwa upekuzi, Dk. Shein wakati ni kiongozi wa kitaifa na kwamba jambo hilo halileti picha nzuri katika ushirikiano wa kimataifa.

Hata hivyo, waziri huyo alipongeza msimamo wa maofisa wa Makamu wa Rais kukataa kubaguliwa na kusema kuwa huo ni ujasiri katika masuala ya uhusiano wa kimataifa.

“Hivi jamani Waziri Mkuu wao wa Uingereza anaweza kufanyiwa kitu kama hicho (akimaanisha kupekuliwa akiwa uwanja wa ndege),” alisema Waziri Tafana.

Naibu waziri huyo, alitaka kujua faida za Zanzibar katika Jumuiya ya Madola kwa vile katika siku za nyuma ilinyimwa misaada na nchi wanachama wa jumuiya hiyo.Tafana, alisema ili kufanikisha sera hiyo ipo haja ya kutizama suala la watendaji na mabalozi likaangaliwa pia kutokana na ukweli kuwa watendaji wengi katika ofisi za ubalozi hivi sasa wanatoka upande wa Tanzania Bara.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, alisema Tanzania imepiga hatua katika kuzingatia itifaki kwa viongozi wanapokuwa ndani na nje ya nchi.

Hata hivyo alikiri kuwapo kwa matatizo yatokanayo na katiba, ingawa hakuwa wazi kubainisha vipengele vyenye utata.

http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/12/2/habari4.php
 
1. Kati ya balozi zaidi ya 30 tulizo nazo- Zanzibar wamepewa tu balozi 5- (17%) je hii ni sawia? Je kuna haja waongezewe idadi ya balozi kuongeza usawa?

2. Idadi ya watu Tanzania ni mil. 39 (38 Bara na 1 mil Zanzibar), ukifanya cross multiplication kwa kigezo cha idadi ya watu- Visiwani wana 2.5% ya watu- na kama ukiendelea na kigezo hicho2 basi ingebidi wapewe tu Idadi ya mabalozi 2 au max. 3 ili kuleta uwiano kwa kigezo cha Idadi ya watu!

3. Je kitumike kigezo gani kuleta uwiano ulio sawa kwa pande zote? Idadi ya watu? Vigezo vingine?
 
Hapa ni kwenda na idadi ya raia, na ikiwezekana na mchango wa kila upande kwenye serikali ya Muungano. Maana hapa inasound kama "changu changu chako changu"
 
Nafasi za Ubalozi ( Ukiondoa zile za "washkaji na maadui wa kisiasa wa Rais" ) hutolewa kwa kuzingatia MERITS.. Sifa na uwezo wa Kuchapa kazi.. mradi Mteule ni Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.. awe Mzanzibari, Mtanganyika au Mmafia.
Sometimes watu tunalalamika kiushabiki.. lakini on the grounds game linachezwa tofauti kabisa!
 
Nafasi za Ubalozi ( Ukiondoa zile za "washkaji na maadui wa kisiasa wa Rais" ) hutolewa kwa kuzingatia MERITS.. Sifa na uwezo wa Kuchapa kazi.. mradi Mteule ni Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.. awe Mzanzibari, Mtanganyika au Mmafia.
Sometimes watu tunalalamika kiushabiki.. lakini on the grounds game linachezwa tofauti kabisa!

Kwa hiyo miongoni mwa wazanzibari milioni moja ni watano tu ndio wenye sifa ya kuwa mabalozi? kuna ushabiki gani watu wakihoji mambo haya au kwa sababu ni wazanzibari?

hivi bado unamoderate wewe?
 
Si swala la Uzanzibari au Utanganyika.. swala ni Utanzania na uwezo wa kuchapa kazi!
Masalahi ya Taifa kwanza!
Yeah bado na-moderate... Vipi?
 
Rais wa Zanzibar anapokuwa katika ziara za kiserikali nje ya Nchi, hupeperusha Bendera ya Tz... Na ni mategemeo yangu kuwa hata kwa makamu wa rais ni hivyo hivyo. Tatizo la viwanja vya ndege vya huko Majuu, hasa UK na USA ni kuangalia majina ya wasafiri na eneo watokalo. Kimbembe alichopata Makamu wa Rais kimewahi pia kuwapata hata wabunge fulani miaka ya nyuma baada ya septemba 11
 
Si swla la Uzanzibari au Utanganyika.. swala ni Utanzania na uwezo wa kuchapa kazi!
Msalahi ya Taifa kwanza!
Yeah bado na-moderate... Vipi?

na katika huo uTanzania Uzanzibari upo! kwanini mnataka kuondoa identity ya kile kisiwa?

na swali ni kuwa kati ya mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania zaidi ya 30 kwanini kuna wazanzibari 5 tuu??

hebu lijibu hilo

U moderation upo kwa sababu majibu yako ya mwanzo yalionyesha bias
 
I can't wait to hear Alaskans and Hawaiians wakilalamika kwamba kati ya 100+ ya mabalozi.. Alaska na Hawaii wamepunjwa.!!
 
Brutus,
Si swla la Uzanzibari au Utanganyika.. swala ni Utanzania na uwezo wa kuchapa kazi!
Msalahi ya Taifa kwanza!

heshima mbeele mkuu...
Unajua Tanzania sio nchi pekee yenye Muungano lakini ajabu ni kwamba vigezo vinavyotakiwa kutumika Tanzania zisijawahi kusikia vikitumika ktk Muungano wa nchi yeyote duniani.
Kila swala siku hizi ni uuwiano nadhani itafikia wakati hata wanawake watataka kutawala ama kuwa na asilimia kubwa ya wabunge kutokana na idadi yao. Kisha yatafuata makabila na kadhalika...Yaani kila kitu kitafanyika kwa kufuata rangi zake.

Duh! ama kweli kazi ipo ndio maana Ubinafsi hauwezi kwisha Utengano ni moja ya asili yetu.
 
Kwa maneno mengine wewe Mkandara na Brutus hamuoni umuhimu wa WATU WENYE ASILI YA ZANZIBAR kupata nafasi za juu serikalini au vipi?

Ngoja nikupe mfano mogo tuuu.....

mtaji wa Zanzibar katika kuanzishwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilikuwa asilimia 11.4. Na kwamba ilikuwa wapate mgawo wa asilimia hiyo (11.4), lakini kwa miaka 20 hawakupewa hata senti moja, na walipoanza kupewa wanapewa asilimia 4.5.

hebu tetea hili nalo! sasa wazanzibari wakilalamika kuhusu hilo nalo nongwa?
 
Waziri huyo, alisema hatua za lazima zichukuliwe kutokana na tukio alilolishuhudia akiwa nchini Uingereza katika ziara ya Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Sheni.

ALieleza kushangazwa na kitendo cha kutaka kufanyiwa upekuzi, Dk. Shein wakati ni kiongozi wa kitaifa na kwamba jambo hilo halileti picha nzuri katika ushirikiano wa kimataifa.

Hata hivyo, waziri huyo alipongeza msimamo wa maofisa wa Makamu wa Rais kukataa kubaguliwa na kusema kuwa huo ni ujasiri katika masuala ya uhusiano wa kimataifa.

Tatizo hapa sio wapekuaji bali maafisa wa Ubalozi wa Tanzania UK. Kwanza lazima wao wanapita VIP na maafisa wa Ubalozi wa Tanzania walioko UK ndio wanakuwa wametoa taarifa kwamba wanamtegemea makamu wa rais n.k.

Vile vile nafikiri tukumbuke wakati balozi Diria (maybe somebody else lakini kutoka visiwani) kama sikosei alipopekuliwa kule Ujerumani (au kwenye ndege ya Luftansa) huenda jina ni lingine lakini alikutwa na madawa ya kulevya au kitu kingine ambacho hakikuwa appropriate kwa balozi. Sasa ni lazima tukubali kama viongozi wetu wanakuwa na ushirika na mipango ambayo siyo appropriate kwenye diplomatic bags etc. inaleta mashaka makubwa kwa nini wasipekuliwe tena kwa western system huwa hawajali kuwapekua kama wana information. Tukumbuke vile vile wakati Thatcher alipoamuru diplomatic bag ya Nigerian embassy ifunguliwe na alikuwamo mtu hai ambaye alikuwa anarudishwa Nigeria.

Kwa hiyo basi sio kutoa hukumu tu wakati hatufahamu mazingira yote ambayo yaliashiria hatua kama hizo kuchukuliwa, sisi wakati wote huwa hatuwapiganii walalahoi wetu wanapokutwa na matatizo nje ya Tanzania, lakini viongozi wanapokumbana nayo wanalia foul. Angalia UK walivyosimama kidete na mwalimu wao aliposhikwa kule Sudan na kuhukumiwa wiki mbili na bado hawaridhiki? Vile vile kumbukeni wakati mtanzania mwenzetu alivyofukuzwa Japan na kuacha mtoto wake kule na serikali ilivyoshindwa kufuatilia sakata lile.

HATUNA UZOEFU AU NI UVIVU WA DIPLOMATS WETU KUFANYA KAZI ZILE AMBAZO WANATAKIWA KUZIFANYA KWA RAIA WAO. NI WACHACHE SANA KWENYE BALOZI ZETU WANAFAHAMU WAJIBU WAO.
 
Dua,
Taabu yangu we treat them as Miungu wadogo hawa wazungu wakja kwetu!
Over madawa ya kulevya- kusema kweli Shein yeye anaonekana ni mtu mwadilifu- hana maskandali kama wengine, ni mpole na naamini sii type akina Diria over Madawa ya Kulevya!
 
GEME THEORY,

Umeniomba nitetee kuhusu mtaji wa Zanzibar ktk mchango wa kuanzishwa Bank kuu - sawa, nakuuliza kwanza ushahidi kamili wa habari zote hizi na ni kiasi gani hiyo benki kuu iikuwa ikipata kiasi kwamba wangepewa mgao unaotokana na asiimia waliyochangia.
Maanake tunavyofahamu wote ktk biashara zote mtaji sio fedha zinazogawanywa ila kile kinachopatikana ziada - Faida, pia yawezekana kilichopatikana kikaingizwa ktk kukuza mtaji zaidi ama kuwekeshwa ktk sehemu nyingine za uzalishaji ambazo sii lazima ziwe Zanzibar ama mgao utokee kwa uuwiano kwani inategemea na soko iiopo. Leo hii tukichanga mtaji mimi na wewe haina maana ni lazima kila uwekeshaji uwe na uuwiano wa asiimia ya mtaji wetu. Na yawezekana kabisa tukawa tunapata hasara hivyo mgao unaoutegemea hauwezi kuonekana. Biashara nzima itafikia mwisho mbaya ikiwa swala la location na Ubinafsi likianza kuleta utata.
Nchi zote duniani zenye muungano zimekuwa zikitazama nafasi ya wananchi wake ktk mchango wa kuijenga nchi.
Wazanzibar wengi wapo madarakani tena wana nafasi kubwa ktk Uongozi na na hata ku immigrate bara ambako wamejifunga kisawasawa. Sehemu kama Temeke ambayo ni kubwa kuliko kisiwa cha Pemba wamekamata Wapemba ktk biashara na uongozi hakuna mbara anayepiga kelele kwa sababu hizi ndizo faida za Muungano.
Mimi nachofikiria muhimu hapa ni nafasi ya Wazanzibar ktk Muungano huu ndio muhimu zaidi kuliko ugonvi wetu kuingia ktk mapato hali Zanzibar wana mipango yao. Pili hatuwezi kuwa na biashara mbili zenye thamani sawa hata kama tumekubaliana kila mmoja wetu kuongoza moja. Nikiwa mna maana kuwa kama wewe utaendesha Restaurant na mimi Bar na club basi mtaji utagawanywa kulingana na mahitaji ya biashara hizo na sio kugawa fedha sawa wakati kimoja wapo kinahitaji capital kubwa zaidi.
Muhimu kwetu sote ni kukubaliana wapi mtaji wetu uwekeshwe na tunaweza kupata good return badala ya kutazama mtaji umegawanywa vipi?
 
Dua,
Taabu yangu we treat them as Miungu wadogo hawa wazungu wakja kwetu!
Over madawa ya kulevya- kusema kweli Shein yeye anaonekana ni mtu mwadilifu- hana maskandali kama wengine, ni mpole na naamini sii type akina Diria over Madawa ya Kulevya!


Hilo ni tatizo la viongozi wetu unaweza kuliona vizuri zaidi katika mikataba, baada ya pipi chache hawawezi kuambilika.
 
Dua,Mkandara,Game-theory,
kuna uwezekano kuna mambo ambayo Wazanzibari wanayafanya mpaka kukaribisha vitendo vya kupekuliwa ktk viwanja vya ndege nje ya nchi. Ilianza na Ahmed Diria, sasa imemtokea Dr.Shein.

Game-theory,Mkandara,
Zanzibar inatuhumiwa kutokuchangia ktk masuala ya Muungano, na kutokuweka fedha zao ktk Hazina ya Taifa kwa muda mrefu tu.

Vilevile Zanzibar imekuwa ikipewa fedha nyingi toka Tanzania Bara bila mahesabu yake kuwekwa wazi. Hata Umeme na mishahara ya SMZ walikuwa wakipewa bure.

Hiyo asilimia 4.5% ya mapato ya Muungano haikuamuliwa na Idodomya. Kiwango hicho kiliamuliwa kwa kushirikisha wasuluhishi wa kimataifa wa masuala ya fedha na uchumi.
 
Shahid Malik, MP for Dewsbury and International Development Minister alikuwa detained pale Dulles Intl Aiport mwezi wa kumi na hii incident ilishamtokea mwaka 2006 pale JKF as well.
 
Icadon,
Unajua kuna maswala mengi yametokea kama coincidence lakini yamechukuliwa kama Conspiracy, hasa ktk maswala ya Airport.
Nitawaeleza kitu kimoja kuwa mtu yeyote yule mwenye majina matatu ya kiarabu yaani la kwanza, middle na surname akionyesha pasi yake tu huwekewa shaka la Ugaidi. Kwa bahati mbaya imetokea kuwa hawa watu wengi wao ni wananchi wazawa wa Zanzibar.
mchujo huu unatokea hata ukituma fedha nje ikiwa mpokeaji ana majina matatu ya kiarabu mjomba fedha inaweza kutofika ama kuchelewa sana hasa ukitumia Western Union, bank money transfer na kadhalika.
sasa hilo swala la makamu wa rais kuwa checked Airport nadhani hapo UK wamekiuka sheria na nashindwa kuelewa kiongozi wa ngazi ya juu kama yule kuingia pale bila kuwepo na taarifa kamili kwani haiwezekani kabisa wala hainingii akilini kuwa kasimamishwa kwa sababu ni Mzanzibar!..Kuamini huko ni sawa na kuamini kuwa hakuna Muungano na nadhani mawazo kama hayo ni utengano wa Wazanzibar ambao wanataka sisi tuamini kuwa hata UK wanafahamu tofauti hizi.
Hoja nzima ya mada hii ni kuonyesha tofauti zetu, na kila mara naposoma habari zinazohusu utengano hasa wakati mgumu kama huu ambao tunahitaji mshikamano wa pande zote mbili inanitisha sana...
 
1. Three of the nine Tanzanian legislators in EALA are from Zanzibar. Wakati population ratio ni 38 m kwa 1 million. A cross multiplication according to population criterion Visiwani ingibidi wapewe tu mbunge 1 ktk EALA.

2. Tungekuwa na serikali tatu- hali hii ingesaidia kuleta uwiano wa kweli wa 'fair representation'. Pia ingewafanya Zanzibar kuwajibika zaidi kuchangia garama za Muungano- kwa sasa inaonekana kama wanabebwa na bara kwa jina la Serikali ya Muungano.

3. Muungano ulivyo kwa sasa unaonekana kuinufaisha Zanzibar Kiuchumi na kiuwakilishi wakati Bara wananufaika Kisiasa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom