Sms za matangazo ya michezo ya kamari ni kero TCRA tusaidieni.

Good Father

JF-Expert Member
Feb 28, 2014
10,275
18,352
Naandika hili moja kwa moja nikiwa ni muhanga wa jambo hili, naomba TCRA muingilie kati hizi meseji imekua kero sasa.

Kila dakika meseji ya kamari, uwe unacheza uwe hauchezi meseji utatumiwa tu.
Too much sasa mnaudhi aisee, mara Daka pesa, Instamoja, Weka bet n.k

Una block huyu anakuja mwingine kila dakika meseji.
Wenye mitandao acheni kutusumbua, watambuweni wanaocheza hiyo
Screenshot_20190221-200306_Messages.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naandika hili moja kwa moja nikiwa ni muhanga wa jambo hili, naomba TCRA muingilie kati hizi meseji imekua kero sasa.

Kila dakika meseji ya kamari, uwe unacheza uwe hauchezi meseji utatumiwa tu.
Too much sasa mnaudhi aisee, mara Daka pesa, Instamoja, Weka bet n.k

Una block huyu anakuja mwingine kila dakika meseji.
Wenye mitandao acheni kutusumbua, watambuweni wanaocheza hiyo
View attachment 1028409

Sent using Jamii Forums mobile app
hili ni tatizo kubwa mnoo simu zetu kugeuzwa mbao za matangazo
 
Kwa kweli wanakera sana tena sana!

Yaani SMS inaingia, unaacha kufanya shughuli zako uangalie inasemaje bahati mbaya kabisa unakutana na SMS zao hizi za ajabu ajabu.

Wanatupotezea mda sana na kutupunguzia concentration kwenye shughuli zetu yaani kwa kifupi wanaudhi sana ukiongezea na matangazo ya mitandao ndio inakuwa balaa kabisa.
 
Sikusoma hata hayo maelezo yote ila kichwa cha habari tu kimenitoshelza. Hawa jamaa sijui vipi yaani wanatupotezea muda sana kupokea na kusoma matangazo yao. Unakuta sometimes upo sehemu nyeti sana unasikia msg imeingia na huwezi kuangalia hspo inakubidi uinuke utoke eneo hilo kwenda kuangalia ujumbe unakutana na tangazo la hao jamaa...shit! Kwa kwel8 msaada zaidi unahitajika na TCRA fanyeni jambo hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tigo wamezidi, yaani unakuta ujumbe huo huo mmoja meseji zinajirudia Mara 10 kwa meseji kumi, ukiwapigia simu wanakwambia ni kwa kila mtu, mimi siku hizi kama sina mpango wa kupata simu ya maana nazima au ninapotaka kulala nazima kabisa line ya tigo naacha voda na Airtel
 
Tigo wamezidi, yaani unakuta ujumbe huo huo mmoja meseji zinajirudia Mara 10 kwa meseji kumi, ukiwapigia simu wanakwambia ni kwa kila mtu, mimi siku hizi kama sina mpango wa kupata simu ya maana nazima au ninapotaka kulala nazima kabisa line ya tigo naacha voda na Airtel
Tigo ni zaidi ya kero, mi mwenyewe nimehamua kuachana kbs ña laini yao sbb ya Kero, hii namba 15571 ,15570, kutwa wametuma msg hata mia ña zaidi, ña namba hii 15670, Yaani ni keroooooll
 
Back
Top Bottom