Slaa ni muda wake wa kukubali matokeo,.

tycoon sley

New Member
Nov 1, 2010
4
0
Kipindi hiki cha uhesabuji wa kura karibu kimemalizika na kilichobaki ni kutangazwa kwa mshindi wa mgombea wa uraisi kwa tanzania bara, hivyo basi slaa inabidi akubaliane na matokeo na sio kuanza kugomea matokeo, hiyo ndio reality , kilichobaki tutazame mbele maendeleo ya nchi yetu na sio kuanza purukushani siziso na msingi, tanzania ni moja na maendeleo ya watanzania wote.

muda wake ukifika wa kuitawala tanzania atakuwa tuuu, hakuna kitu kisichowezekana mbele ya mungu,
god bless tanzania ,
 
Maoni yako ni mazuri ingawa umemaliza vibaya. Mungu habariki wahuni wezi matapeli na manyang'au wa madaraka kusema god bless Tanzania unajifurahisha tu, watu wa aina hii hupelekwa polini na Mungu na kula nyasi kama ng'ombe. Tanzania haina amani ya kweli na huenda kuan siku utaamini haya. There is no a true peace without a true justice! Tanzania watu ni waoga tu wa mabomu kama ulivyoonyesha hapo juu ila siku waoga wakichoka na maisha you will trust me that there is no true peace without justice
 
umeona matokeo ya jimbo la geita na nyang'wale?

NYANG'HWALE. 505 ...17,792.. 3,789 ..1,042 ........51 ........18 ...........49......... 791...... 24,037

GEITA................ 505 ...17,792.. 3,789 ..1,042 ........51 ........18 ...........49......... 791...... 24,037


Wewe kweli ni choko,tena narudia wewe ni choko akubali upuuzi huu!!!



 
Kipindi hiki cha uhesabuji wa kura karibu kimemalizika na kilichobaki ni kutangazwa kwa mshindi wa mgombea wa uraisi kwa tanzania bara, hivyo basi slaa inabidi akubaliane na matokeo na sio kuanza kugomea matokeo, hiyo ndio reality , kilichobaki tutazame mbele maendeleo ya nchi yetu na sio kuanza purukushani siziso na msingi, tanzania ni moja na maendeleo ya watanzania wote.

muda wake ukifika wa kuitawala tanzania atakuwa tuuu, hakuna kitu kisichowezekana mbele ya mungu,
god bless tanzania ,

Nafikiri ulimwelewa vyema Dr Slaa anachodai NEC. Yeye sio kichaa kutaka tu kuwa Rais wa nchi wakati wananchi hawakumchagua. Na kwa hakika hapa tatizo si kuwa Rais au la. Tatizo ni kuangalia je misingi ya haki imetendeka??? Kutangazwa kwa mshindi wa urais na NEC leo hii au kesho bado hakutatuzuia wapenda haki kujadiliana nini kimetokea na nani kahusika na vipi kahusika katika kupotosha matakwa ya watanzania. Nina amini kuwa kwa mcha mungu yeyote yule kamwe hawezi furahia kutangazwa kuwa Rais wakati zaidi ya asilimia 50 ya raia wako wana wasiwasi na ushindi wako.
 
Kipindi hiki cha uhesabuji wa kura karibu kimemalizika na kilichobaki ni kutangazwa kwa mshindi wa mgombea wa uraisi kwa tanzania bara, hivyo basi slaa inabidi akubaliane na matokeo na sio kuanza kugomea matokeo, hiyo ndio reality , kilichobaki tutazame mbele maendeleo ya nchi yetu na sio kuanza purukushani siziso na msingi, tanzania ni moja na maendeleo ya watanzania wote.

muda wake ukifika wa kuitawala tanzania atakuwa tuuu, hakuna kitu kisichowezekana mbele ya mungu,
god bless tanzania ,

No thanks, hakuna kukubali upuuzi, vinginevyo nawe utakuwa mpuuzi tu.
 
Narudia tena: AKUBALI ASIKUBALI.... NDO WAMESHACHUKUA WAMEWEKA WAAA! Hivi nyie mnawajua sisiemu au mnawasoma tu hapa MTANDAONI:A S angry: hamkumbuki kwamba kuna watu waliwahi KUKOLIMBWA kwa kusema ukweli??? kama mnampenda MTAMLINDA:tape:
 
Suala kubwa linalobakia na litakalojidhihirisha kutokana na wakati sio Dr. Slaa kukubali matokeo. Suala ni je, Watanzania wote watayakubali haya matokeo? Je Kikwete atakuwa na legitimacy ya kuongozwa na Kikwete? kusimama kwenye majukwaa na kuapishwa sio kuongoza. Ili uwe kiongozi bora kazima unaowaongoza wakubaliane nawe kwa kushirikiana nawe. Kama basi Kikwete hakuchaguliwa kweli kwa kura hizo zilizotangazwa na nec, uongozi wake utakuwa ni mgumu sana. Ama sivyo abadili namna ya uongozi na kuugeuza kuwa utawala. Kwa hilo sijui Watanzania watavumilia mpaka lini.
 
Sasa huyo Slaa si aende mahakamani kama mulivyokuwa munamwambia Sefu Sharifu alipokuwa analalamika kuhusu uchakachuaji wa matokeo?

Ya nini ghasia na fujo yakheeeeeeeee?
 
Nadhani ushauri kuwa Dr. Slaa kuwa akubali matokeo hauna msingi wowote. Sababu za kutoendelea kushauri hivyo ni kama ifuatavyo:
1. Kama Tume ilikuwa inatangaza matokeo kama wanavyoona wenyewe. Basi wamtangaze mshindi kadiri wanavyona. Kama kuna umuhimu wa Dr. Slaa kukubali matokeo basi naomba maswali haya yajibiwe: (a)Utaratibu unasema nini kuhusu mgombea kukubali au kukataa matokeo? Kukataa au kukubali matokeo kutamwathiri nini aliyetangazwa na Tume kuwa ameshinda?
2. Dr. Slaa anatoa malalamiko yake lakini Tume haijasikiliza. Sasa mnataka akubali kipi kile kile alichokuwa akikilalamikia? Hata kama atawapelekea uthibitisho wa malalmiko yake sidhani kama tume kama ina muda wa kuyapitia wala nia ya kuyapitia. Sasa mnataka akubali?

3. Hakuna hoja ya maana inayotolewa kwanini Dr. Slaa ayakubali matokeo. Amelalamika kuwa matokeo ya tume si sahihi. Kama matokeo ya kura siyo sahihi kwanini Watanzania tulipiga kura kama kura zetu sizo zinazotangazwa.

Naomba Watanzania tuache upuuzi kwasababu ubabe unaoonyeshwa na Tume hauwezi kuvumilika na wala hauwezi kuelezeka.
 
Swala la uwezekano wa uchakachuaji lililwekwa wazi na JK alipozungumza na waandishi wa habari. Udhaifu wa mawakala wa vyama vya upinzani. Endapo kuna ushahidi wa hakika upelekwe mahakamani japo hautasikilizwa kutokana na sheria inayopinga kupinga tangazo la tume ya uchaguzi la mshindi wa kura za uraisi. Lakini for documentation purposes lifanywe ili awe na muda mgumu wa kuuza serikali yake nje.
Kwa dhati napongeza vyama vya upinzani vilivyotoa ushindani mkali hasa CHADEMA, swala sasa ni kuongeza kasi ya kueneza sera zao isiwe kama NCCR walivyotuangusha kwa kuanza kugombana na hivyo kurudisha nyuma kasi ya mageuzi mpaka mwaka huu. Slaa anaweza kusaini matokeo with protest. The cookie crumbles in bits it is not yet time to give up or jubilate. A luta continua!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom