The Informer
Senior Member
- Jun 14, 2010
- 119
- 29
DAR ES SALAAM, Oktoba 26, 2010
Nimetoka kuhudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika Manzese Bakhresa mchana wa leo hii ambapo Dk. Willibrod Slaa alimnadi mgombea wa ubunge wa Ubungo, John Mnyika.
Mkutano ulifana sana, Mnyika anakubalika sana na wapiga kura. Ni dhahiri kuwa tashinda na hatimaye kuwa mbunge licha ya njama za CCM za kuiba kura. Mnyika kasema kuwa amejipanga kuweka mawakala zaidi ya 3,000 kwenye vitua zaidi ya 1,000 vya kupiga kura jimboni Ubungo ili kulinda kura za ubunge na urais za CHADEMA zisiibiwe.
Kasema mawakala hawa ambao wamechujwa na kuchaguliwa vizuri ni pamoja na wasomi wa vyuo vikuu, marafiki zake na vijana wengine waliojitolea. Kasema wameapishwa kulinda kura zisiibiwe come what may.
Kwa upande wake, Slaa alitoa hotuba kali iliyoshangiliwa sana na wananchi wa Manzese.
Slaa alisema kuwa gari linalotumiwa na Tume ya Uchaguzi aina ya Nissan Patrol, T895 APR, lilionekana kaskazini mwa Tanzania likipita Manyara na jimbo ya Karatu eti wakidai NEC imesahau kusambaza vifuniko vya masanduku ya kupiga kura. Eti wafanyakazi wa NEC wamesambaza masanduku ya kupiga kura kwenye baadhi ya vituo na kusahau vifuniko vyake! Slaa aliwataka wananchi kufanya "Citizens' arrest" kwa kuwakamata watu bila kuwapiga na kuwafikisha kituo cha polisi pale wanapoona kura zinaibiwa au kuna kitendo chochote cha kuvunja sheria.
"Jukumu la kulinda kura ni letu wote," alisema Slaa huku akishangiliwa na umati mkubwa wa wananchi wa Manzese, wengine wakiwa juu ya miti na wengine juu ya trailer la takataka ili mradi wamuone Rais mtarajiwa akiongea.
Mabango ya wananchi yalisema: "Slaa kiboko cha mafisadi" na "Ridhwani, hii si nchi ya kifalme."
Slaa alisisitiza kuwa akiwa Rais atatoa elimu bure na kushusha bei ya mabati na simenti mpaka kufikia shilingi elfu 5. Alisema kama serikali inaweza kuweka ruzuku kwenye mbolea, haoni sababu ya kushindwa kuweka ruzuku kwenye vifaa vya ujenzi.
"Nikiwa Rais nitaondoa anasa Ikulu. Mbunge analipwa posho kwa siku ya shilingi 160,000 bila kodi na mshahara wa shilingi milioni 7 kwa mwezi wakati mwalimu analipwa mshahara huohuo wa shilingi 160,000 kwa mwezi na bado ukatwe kodi," alisema Slaa.
"Mwaka 2005, kilo ya sukari ilikuwa shilingi 400, sasa ni sh 1,800 na watu wameacha kunywa chai. Kilo ya nyama ilikuwa shilingi 800 sasa inafika mpaka sh 3,500," alisema.
Alisema kuwa kamwe bunduki haiwezi kupambana na nguvu ya umma -- people's power.
"Kikwete akubali kiume kuwa sasa muda wa kustaafu kiheshima umefika," alisema huku akishangiliwa sana.
"Serikali ya Kikwete ni serikali ya anasa. Inatenga sh bilioni 30 kwa chai na vitafunio kwenye ofisi za vigogo wakati Watanzania hawana chakula." Alisema serikali ya CCM inaweza kusambaza mabango ya Kikwete nchi nzima bure kwa kutumia kodi ya wananchi, halafu ina jeuri ya kusema kuwa elimu bure haiwezekani.
"Nimetoka nyumbani kwa Kikwete Bagamoyo, mashimo manne ya vyoo kwenye shule yamejengwa kwa shilingi milioni 700," alisema na kumshutumu Kikwete kwa kukosa dhamira ya kuleta maendeleo kwani anapotoka yeye Bagamoyo bado kuna nyumba za mbavu ya mbwa.
Slaa alimshangaa Kikwete kwa kuwashika mikono kina Edward Lowassa, Basil Mramba na Rostam Aziz kuwa ni wachapa kazi wakati wana tuhuma nzito za ufisadi.
Alienda kusisitiza kuwa vurugu au umwagaji damu utafanywa na serikali na CCM kupitia vijana wa green guard ambao wananuliwa pepper spray na pingu pamoja na kupewa mafunzo ya kijeshi.
"CCM kimekuwa sasa chama cha kigaidi!" Alisema na kuwataka wananchi kutojibu matusi au vurugu za vijana wa CCM na badala yake wapige kura kwa amani.
(Picha hizo zinaonesha Slaa akiwa Manzese leo)
Naomba kuwasilisha....
Nimetoka kuhudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika Manzese Bakhresa mchana wa leo hii ambapo Dk. Willibrod Slaa alimnadi mgombea wa ubunge wa Ubungo, John Mnyika.
Mkutano ulifana sana, Mnyika anakubalika sana na wapiga kura. Ni dhahiri kuwa tashinda na hatimaye kuwa mbunge licha ya njama za CCM za kuiba kura. Mnyika kasema kuwa amejipanga kuweka mawakala zaidi ya 3,000 kwenye vitua zaidi ya 1,000 vya kupiga kura jimboni Ubungo ili kulinda kura za ubunge na urais za CHADEMA zisiibiwe.
Kasema mawakala hawa ambao wamechujwa na kuchaguliwa vizuri ni pamoja na wasomi wa vyuo vikuu, marafiki zake na vijana wengine waliojitolea. Kasema wameapishwa kulinda kura zisiibiwe come what may.
Kwa upande wake, Slaa alitoa hotuba kali iliyoshangiliwa sana na wananchi wa Manzese.
Slaa alisema kuwa gari linalotumiwa na Tume ya Uchaguzi aina ya Nissan Patrol, T895 APR, lilionekana kaskazini mwa Tanzania likipita Manyara na jimbo ya Karatu eti wakidai NEC imesahau kusambaza vifuniko vya masanduku ya kupiga kura. Eti wafanyakazi wa NEC wamesambaza masanduku ya kupiga kura kwenye baadhi ya vituo na kusahau vifuniko vyake! Slaa aliwataka wananchi kufanya "Citizens' arrest" kwa kuwakamata watu bila kuwapiga na kuwafikisha kituo cha polisi pale wanapoona kura zinaibiwa au kuna kitendo chochote cha kuvunja sheria.
"Jukumu la kulinda kura ni letu wote," alisema Slaa huku akishangiliwa na umati mkubwa wa wananchi wa Manzese, wengine wakiwa juu ya miti na wengine juu ya trailer la takataka ili mradi wamuone Rais mtarajiwa akiongea.
Mabango ya wananchi yalisema: "Slaa kiboko cha mafisadi" na "Ridhwani, hii si nchi ya kifalme."
Slaa alisisitiza kuwa akiwa Rais atatoa elimu bure na kushusha bei ya mabati na simenti mpaka kufikia shilingi elfu 5. Alisema kama serikali inaweza kuweka ruzuku kwenye mbolea, haoni sababu ya kushindwa kuweka ruzuku kwenye vifaa vya ujenzi.
"Nikiwa Rais nitaondoa anasa Ikulu. Mbunge analipwa posho kwa siku ya shilingi 160,000 bila kodi na mshahara wa shilingi milioni 7 kwa mwezi wakati mwalimu analipwa mshahara huohuo wa shilingi 160,000 kwa mwezi na bado ukatwe kodi," alisema Slaa.
"Mwaka 2005, kilo ya sukari ilikuwa shilingi 400, sasa ni sh 1,800 na watu wameacha kunywa chai. Kilo ya nyama ilikuwa shilingi 800 sasa inafika mpaka sh 3,500," alisema.
Alisema kuwa kamwe bunduki haiwezi kupambana na nguvu ya umma -- people's power.
"Kikwete akubali kiume kuwa sasa muda wa kustaafu kiheshima umefika," alisema huku akishangiliwa sana.
"Serikali ya Kikwete ni serikali ya anasa. Inatenga sh bilioni 30 kwa chai na vitafunio kwenye ofisi za vigogo wakati Watanzania hawana chakula." Alisema serikali ya CCM inaweza kusambaza mabango ya Kikwete nchi nzima bure kwa kutumia kodi ya wananchi, halafu ina jeuri ya kusema kuwa elimu bure haiwezekani.
"Nimetoka nyumbani kwa Kikwete Bagamoyo, mashimo manne ya vyoo kwenye shule yamejengwa kwa shilingi milioni 700," alisema na kumshutumu Kikwete kwa kukosa dhamira ya kuleta maendeleo kwani anapotoka yeye Bagamoyo bado kuna nyumba za mbavu ya mbwa.
Slaa alimshangaa Kikwete kwa kuwashika mikono kina Edward Lowassa, Basil Mramba na Rostam Aziz kuwa ni wachapa kazi wakati wana tuhuma nzito za ufisadi.
Alienda kusisitiza kuwa vurugu au umwagaji damu utafanywa na serikali na CCM kupitia vijana wa green guard ambao wananuliwa pepper spray na pingu pamoja na kupewa mafunzo ya kijeshi.
"CCM kimekuwa sasa chama cha kigaidi!" Alisema na kuwataka wananchi kutojibu matusi au vurugu za vijana wa CCM na badala yake wapige kura kwa amani.
(Picha hizo zinaonesha Slaa akiwa Manzese leo)
Naomba kuwasilisha....