Kamarade wa kamarade
Member
- Dec 6, 2013
- 10
- 5
Slaa atolewa kafara na wenye chama!
Uamuzi wa kumtumia Dr Slaa kwenda kumwaga sumu dhidi ya Zitto katika maeneo ambayo wanaamini ana wafuasi wengi na kujikuta akihutubia mikutano ya watu wachache na upinzani mkali uliomlazimu kuomba msaada wa polisi ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kuhakikisha kuwa hana nafasi ya kugombea urais mwaka 2015 na nafasi hiyo kuchukuliwa na Freeman Mbowe. Hii inaendana na mkakati maalum wa mmoja wa wawania ugombea wa CCM kutaka kuhakikisha kuwa hapati ushindani wa Dr Slaa ambaye anaonekana kuweza kuleta athari zaidi ya Freeman mbowe ambaye anaonekana kuwa hana nafasi yoyote ya kuaminiwa na Watanzania. Katika mkakati huu pia yumo mwenza wake Mama Josephine ambaye amekuwa mstari wa mbele kumlazimisha Dr Slaa kukubaliana na jukumu la kwenda mikoani kumwaga sumu dhidi ya Zitto ambaye anaonekana kama tatizo lingine ndani ya mkakati huo wa mgombea wa CCM. Hatua ya nguvu za Mama josephine kutumika kumlazimisha Dr Slaa na hata kumlazimisha aendelee na ziara hiyo baada ya kutokea mambo ya kumuaibisha na kumshusha hadhi yake imeanza kuzua maneno kuwa yawezekana Josephine ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa mgombea huyo wa CCM ambaye alikuwa na mahusiano naye hapo kabla na hata sasa.
Uamuzi wa kumtumia Dr Slaa kwenda kumwaga sumu dhidi ya Zitto katika maeneo ambayo wanaamini ana wafuasi wengi na kujikuta akihutubia mikutano ya watu wachache na upinzani mkali uliomlazimu kuomba msaada wa polisi ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kuhakikisha kuwa hana nafasi ya kugombea urais mwaka 2015 na nafasi hiyo kuchukuliwa na Freeman Mbowe. Hii inaendana na mkakati maalum wa mmoja wa wawania ugombea wa CCM kutaka kuhakikisha kuwa hapati ushindani wa Dr Slaa ambaye anaonekana kuweza kuleta athari zaidi ya Freeman mbowe ambaye anaonekana kuwa hana nafasi yoyote ya kuaminiwa na Watanzania. Katika mkakati huu pia yumo mwenza wake Mama Josephine ambaye amekuwa mstari wa mbele kumlazimisha Dr Slaa kukubaliana na jukumu la kwenda mikoani kumwaga sumu dhidi ya Zitto ambaye anaonekana kama tatizo lingine ndani ya mkakati huo wa mgombea wa CCM. Hatua ya nguvu za Mama josephine kutumika kumlazimisha Dr Slaa na hata kumlazimisha aendelee na ziara hiyo baada ya kutokea mambo ya kumuaibisha na kumshusha hadhi yake imeanza kuzua maneno kuwa yawezekana Josephine ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa mgombea huyo wa CCM ambaye alikuwa na mahusiano naye hapo kabla na hata sasa.