Slaa anyaka skendo lingine

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Slaa anyaka skendo lingine

2008-01-24 17:22:18
Na Job Ndomba, Jijini

Yule mbunge maarufu wa kulipua maskendo, Dokta Wilbroad Slaa (CHADEMA-Karatu) amenyaka skendo jingine bab`kubwa linalohusisha ulaji wa mabilioni kibao ya pesa za walalahoi.

Akizungumza na Alasiri leo asubuhi, Dk.Slaa amesema pesa hizo zilizoliwa na vigogo ni kutoka katika mfuko wa Import Support uliokuwa ukifadhiliwa na Serikali ya Japan.

Amesema mfuko huo uliokuwa na mabilioni kibao ulilenga kuwasaidia wafanyabiashara wadogo, lakini mapesa hayo yakaliwa hivi hivi na vigogo baada ya kukopeshana na kushindwa kulipa.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, mfuko huo sasa umefutwa baada ya kugundulika umetumiwa vibaya na vigogo hao anaodai, wengi wao walifungua makampuni hewa kwa ajili ya kukamilisha ulaji wao.

``Vita dhidi ya ufisadi haijaisha, kwani baada ya hili la BoT najiandaa kulipua hili la upotevu wa mabilioni, kutoka katika mfuko wa Import Support,`` akasema Dk. Slaa.

Amesema nchi hii ina maskendo mengi sana yanayofanywa na vigogo na hivyo lazima wachache wajitolee kuwashitaki kwa wananchi kwa ajili kuokoa uchumi wa taifa.

``Unajua tunapowataja mafisadi hawa, wananchi wanatakiwa watuunge mkono kwa kuwa kuna mapesa kibao yameibwa na vigogo,`` akaongeza.

Amesema mfuko wa Import Support ulianzishwa kwa ajili ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, lakini wakapigwa changa la macho na mapesa hayo kuwafaidisha vigogo wachache.

Hata hivyo Dk. Slaa hakutaka kutaja ni lini atalipua bomu hilo, lakini amesisitiza kuwa yuko katika hatua za mwisho mwisho kukamilisha uchunguzi wake.

``Kwa sasa siwezi kukuambia ni lini nitalipua ila wakati ukifika, nitawasilisha madai yangu mahali husika kama ilivyokuwa kwa lile skendo ya BoT, licha ya kwamba baadhi ya watu walianza kunibeza,`` akasema.

Dk. Slaa ndiye aliyeibua skendo la BoT Julai mwaka jana, katika kikao cha Bunge wakati Waziri wa Fedha Bi.Zakhia Meghji akiwasilisha ripoti ya mapato na matumizi ya wizara hiyo.

Hata hivyo baada ya kuibua hilo, Dk. Slaa alitakiwa kutoa hoja binafsi ambapo pia aliamua kushitaki kwa wananchi kwenye mkutano wa hadhara pale Mwembeyanga, Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya matokeo ya skendo la Benki Kuu ni kubainika kwa ulaji wa zaidi ya shilingi bilioni 133 na kutimuliwa kazi kwa aliyekuwa gavana wa taasisi hiyo, Dk. Daud Balali.

SOURCE: Alasiri
 
Kikwete alishawahi kutuambia kwamba pesa zilizofisadiwa si za nchi wafadhili ni zetu Watanzania, sasa hili scandal lingine nalo sijui atafanya usanii upi!
 
Hii Import support wamekula wengi, kuna mawaziri (majina kapuni) ambao pia wako katika list na wengine hizo pesa ndio zilizowapa ubunge...
 
Unajua Sitaki kuamini kwamba hii nchi itakua na Nidhamu pale tutakapoamua kutumia Nguvu.

Hivi utawala wetu ukijiita wa kidemokrasia kwa hili itakua umetofautiana vipi na utawala wa kiimla?Kwa masuala ya ufisadi ina tofauti gani hasa na Serikali ya yule Dikteta aliyelaaniwa Nigeria Generali Sani Abacha?
 
Hii Import support wamekula wengi, kuna mawaziri (majina kapuni) ambao pia wako katika list na wengine hizo pesa ndio zilizowapa ubunge...

Huu mchezo wa kusema majina kapuni utaisha lini? Ebu soma motto ya JF... Where we Dare to Talk Openly
 
taja majina umsaidi Slaa maana hata ukisema Kapuni Slaa atasema tu .Labda Mwanahalisi waogope kucha kwa kuwa watakuwa wamelambishwa sasa.
 
Yes JK alisema pesa zilizoliwa hazikuwa za wafadhili. Binafsi pia sikumwelewa rais kabisa. Hv ana uhakika gani kwani mwaka uliochunguzwa ni 05/06 peke yake katika hiyo EPA pekee achilia mbali areas zingine ambaozo hazijachunguzwa. I thought yy kma presidaa alipaswa kuqualify statement zake. Aache kutoa statements zinazogonga ukuta na kumrudia.

In addition, hela yeyote inayoliwa na mafisadi inauma sana sana ila hii ya ndani ambayo Jk anaona its nothing mm inaniuma kupita maelezo kwani walipa kodi wa developed countries wanahali nzuri kuliko mwanakijiji wa kantalamba maskini ambaye amemebeshwa mzigo mkubwa wa kodi kupitia bidhaa mbalimbali anazonunua, mwisho wa siku jasho lake balaa na wenzanke wanagawana kama njugu.

Tajeni majina wakuu msiweke kapuni. Hv vita ni kali sana toeni data tupambane, inaweza kusaidia.
 
Ben,mambo ya majina kampuni maana yake nini? Tupe majina hayo,kama na wewe humo tuambie. Spendi kuamini mpaka raia wa nchi hii wageuke wakimbizi ndiyo ufisadi uuishe. Wasubiri machozi haya ya raia yatakapogeuka damu
 
Kikwete alishawahi kutuambia kwamba pesa zilizofisadiwa si za nchi wafadhili ni zetu Watanzania, sasa hili scandal lingine nalo sijui atafanya usanii upi!

Haijalishi kama pesa zilizoliwa ni za wafadhili au wafadhiliwaa tunachojua ni kuwa dhambi ya ufisadi inawaumiza watanzania,
 
Hivi Kikwete alivyosema hela za wafadhili hazijafujwa alikuwa hajui hili au alifikiri watu hawajui?

Usahihi wa Slaa hauwezi kutiliwa mashaka hasa baada ya kutuonyesha kwa ufasaha mkubwa mambo ya ufisadi uliofanyika BOT.

Kuna mawili, Kikwete hajui mambo mengi yanavyoenda kiasi cha kusikitisha ndiyo maana anatoa kauli zinazomrudia vibaya, au anajua lakini hajali na anafikiri kwamba watu hawatajua.

Yote mawili ni mabaya, kati ya rais zuzu asiyejua nini kinachoendelea chini ya pua yake na rais muongo asiyejali wananchi hakuna mwenye afadhali.

Kikwete must go.CCM must go.
 
Mimi sikumwelewa kabisa mhe.alivyosema zilizoliwa si za wafadhili yaani hii nchi yetu ina mambo ya kusikitisha kana kwamba hizi za kwetu ndio hazina tatizo zilkiliwa,kweli inauma sana.
 
Nchi hii kila unapogusa ni uchafu tuu ,ni kweli pesa zililiwa za Import support na miongoni mwa wala pesa hizi ni R.A na Manji .

Tutaweka majina hapa na nyaraka vuteni subira kidogo na mwingine alete majina ya mawaziri hapa ili tuangalie wanahusika je kwani wameanza kupoteza ushahidi sasa na pia waweza pitia nyaraka za bunge za miaka ya 90 liliibuliwa na kamati ya bunge na kufa...
 
Pundit you are very right this man must go for sure. Binafsi sielewi anatupeleka wapi hv alilazimishwa kugombea au? Maana at times nahisi kama vile hatuna rais kwani anapwaya kupita maelezo
 
Ben,mambo ya majina kampuni maana yake nini? Tupe majina hayo,kama na wewe humo tuambie. Spendi kuamini mpaka raia wa nchi hii wageuke wakimbizi ndiyo ufisadi uuishe. Wasubiri machozi haya ya raia yatakapogeuka damu


Heshima yako mkuu,

Umenikandamiza bure ndugu yangu.Sio mimi niliyesema "MAJINA KAPUNI" mkuu wangu.

Pia unanisingizia kitu ambacho Nakichukia kwa Moyo wangu wote.Aliyesema ni Insurgent na si mimi.
 
Binafsi sielewi anatupeleka wapi hv alilazimishwa kugombea au?

Mkuu Boby, hizo hisia zako zimenikuna sana na nimericall jibu nililopata juzi juzi tena kutoka kwa mdingi amabaye nilikuwa simtegemei. Well tulikuwa tunaongelea mambo ya ufisadi na mimi nikakomenti kwamba mafia ya kibongo bado changa hivyo kuitokomeza kama kuna nia ni kazi rahisi mno. Mzee aling'aka na kunijibu kijana try to be serious "mafia ya bongo imekomaa mpaka wametuchagulia rahisi". Nadhani hata swali lako inawezekana limejibiwa!!!
 
taja majina umsaidi Slaa maana hata ukisema Kapuni Slaa atasema tu .Labda Mwanahalisi waogope kucha kwa kuwa watakuwa wamelambishwa sasa.
Mkuu pengine hapa una point hapa, lakini sijakupata sawasawa.
 
Kinachonikasirisha zaidi ni pale JK anapoulizwa maswali yenye uzito katika maswala yanayogusa na kuumiza watanzania walio wengi anabaki kucheka na kusmile bila kuona hata haya.

We unakenua meno wakati watu wametilia sura ya kazi. Wanayouliza wengi wao ni mambo yanayohitaji kupewa kipaumbele kama hauwezi kujibu heri useme siwezi kuliko kubaki ukitucheka.

Hata kama mafia ndio wamekulazimisha your time is coming it might not be very soon but it is coming.
 
Hii mbona tulishaijadili sana huko nyuma.....na kinara wa hii skendo akiwa "Don" Manji!!.......unajua kuna vitu hapa JF vinajadiliwa na kufanyiwa kazi.......na haya ndio matokeo..........tusubiri bomu sasa!!

go Slaa go.....
 
Hii Import support wamekula wengi, kuna mawaziri (majina kapuni) ambao pia wako katika list na wengine hizo pesa ndio zilizowapa ubunge...

Hapa imebidi nicheke!

Yaani mtu achukue mkopo meant for import support alafu badala yake anaupeleka na kuinvest kwenye biashara ya ubunge.

Ama kweli hapo kuna kazi kweli kweli..
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom