Slaa anaamini katika nini? Kipenzi mbeba maono, msaliti wa umma au maslahi binafsi?

Je ni Nani huyu Slaa?

  • Mbeba Maono

    Votes: 6 11.1%
  • Msaliti wa Umma

    Votes: 9 16.7%
  • Opportunist/Maslahi Binafisi

    Votes: 39 72.2%

  • Total voters
    54
  • Poll closed .
Mimi niliacha kuwaamini siku nyingi tangu enzi zile Chadema wanamuita Lowasa fisadi halafu Lowasa akajiunga Chadema wakawa wanamuita rais wa mioyo yao.
Kama Lumumba walivyokuwa wanamuita fisadi leo wanamuweka high table, mafunzo ni kwa pande zote.
 
Kwamba, usimwamini mwanasiasa yeyote kwa 100%, nasema hivyo kwa sababu huyu ninayemuona leo siyo Slaa niliyekesha humu JF kumtetea huku nikiambulia matusi ya nguoni kutoka Lumumba, wanaomjua Quinine wataelewa namaanisha nini. Na kuanzia leo mtazamo wangu kuhusu siasa na wanasiasa utabadilika sana sitakuwa Quinine wa enzi za Slaa.

View attachment 1188090

Kufuatilia Siasa za Tanzania, Kuziamini na Kujikita nazo kunahitaji Akili za Kiuwendawazimu.
 
Wanasiasa waliowengi wa Afrika ni Wanafiki kuliko Yuda Escarioti..Usomi wao na Elimu yao vyote viko kwa ajili ya matumbo yao tu basi si kwa ajili ya Maslahi mapana ya taifa..Mwanasiasa mkweli na Uchungu na hii Nchi alikuwa Nyerere tu wengine wote wanajijua wenyewe..





















Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki Chakwale
Mungu Ibariki Morogoro
Mungu Ibariki Gairo
 
Huo msimamo ungeuonyesha wakati wa ujio wa Lowasa ungeonekana wa maana.

Lowasa alivyokuwa CCM tulimchafua na kumshushia tuhuma kibao kuwa ndio alama ya ufisadi ndani ya Tanzania... CHADEMA na Ccm kwa pamoja wakiungana

Alivyohamia Chadema, mkamsafisha, mkamtetea na kumkingia kifua tena na kumpa nafasi ya kugombea kuongoza nchi.

Leo amerudi ccm mnawalaumu tena ccm kuwa kwa nini mmempokea Lowasa wakati mlisema ni fisadi.

Kifupi CCM na Chadema hakuna tofauti
 
Kwamba, usimwamini mwanasiasa yeyote kwa 100%, nasema hivyo kwa sababu huyu ninayemuona leo siyo Slaa niliyekesha humu JF kumtetea huku nikiambulia matusi ya nguoni kutoka Lumumba, wanaomjua Quinine wataelewa namaanisha nini. Na kuanzia leo mtazamo wangu kuhusu siasa na wanasiasa utabadilika sana sitakuwa Quinine wa enzi za Slaa.

Kwenye tasinia ya siasa Slaa ametufundisha mengi ila amekatisha ndoto za vijana wengi.

View attachment 1188090
Uko sahihi! Jamaa katuonyesha vijana maisha yalivyo.
 
Kwamba, usimwamini mwanasiasa yeyote kwa 100%, nasema hivyo kwa sababu huyu ninayemuona leo siyo Slaa niliyekesha humu JF kumtetea huku nikiambulia matusi ya nguoni kutoka Lumumba, wanaomjua Quinine wataelewa namaanisha nini. Na kuanzia leo mtazamo wangu kuhusu siasa na wanasiasa utabadilika sana sitakuwa Quinine wa enzi za Slaa.

Kwenye tasinia ya siasa Slaa ametufundisha mengi ila amekatisha ndoto za vijana wengi.

View attachment 1188090
Kipi kinachokupelekea kusema maneno hayo kuhusu dr silaa. Kwa anayemjua dr huwezi kumuhofia. Kama hukushtuka mbowe alivyomleta lowasa chadema basi piga kimya tu. Huyu mzee hakutaka kuwa mnafiki.
 
Dr Slaa yuko mezani anakula tena amekuwa mkali kwa wanaoongelea chakula kilichopikwa. Anasema malalamiko yetu yaishie ndani yasifike nje kwa majirani zetu.
 
Watu wanabadilika, hata wewe jinsi unavyoiona Dunia leo hii, sivyo utakavyoiona miaka 5 ijayo, wote tunakuwa kadiri muda unavyokwenda tunajifunza mambo mapya na kuhoji yaliyopita, mfano mimi siwaoni Wazazi wangu jinsi nilivyokuwa nawaona zamani, nimekuwa, nimejifunza mengi na kuhoji mengi hivyo kubadili mtazamo wangu kimaisha.

Wote tuko hivyo, ndo maana kuna watu wanakutana wanapendana wanaamua kuona baada ya miaka kadhaa wanaiangalia Dunia kitofauti wanaamua kuachana, hivyo usihukumu mtu.

C’est la vie!
 
Tatizo kubwa la Watanzania hasa wale Wasomi na watumiaji wa Mitandao hii mbalimbali ya Kijamii tumekuwa wepesi katika Kulaumu, Kushambulia, Kudhihaki na hata Kutusi Watu ambao kwa wakati fulani walionyesha kuwa upande Wetu ila walipopata tu Uteuzi hasa kule ambako tunapachukia basi kwa haraka sana tunawaona hawafai na kuwabatiza kuwa ni Wasaliti na hawana maana tena.

Nimekuwa nikifuatilia sana Watu ( Wanasiasa ) fulani wanapokuwa wakiteuliwa na Mheshimiwa Rais JPM hasa wakiwa wanatokea Upinzani au kwa Makundi ya Wanaharakati ambako walikuwa wakiiponda mno Serikali wanaanza Kuambiwa ni Wasaliti huku ikionekana kama vile Thamani zao katika Jamii ndiyo zimekwisha wakati ukweli ni kwamba Kisaikolojia tu kwa Mwanadamu yoyote yule kubadilka Kwake ni jambo la dakika tu na hakuna la Kushangaza hapo.

Hebu tuacheni Unafiki Wetu na tuseme Ukweli wetu hapa kwa jinsi hivi sasa Maisha yalivyo ya Msoto ( Shida na Magumu ) ni nani kati yetu hasa kutoka huko Upinzani au kwa Wanaharakati akiteuliwa na Mheshimiwa Rais JPM katika nafasi yoyote ile ataikataa? Hivi nyi Njaa mnaijua au mnaisikia tu redioni au kwa jirani? Yaani upige Kelele Mitandaoni na Vijiweni Kutwa huku hata Kula yako tu ni ya Shida achilia mbali hata Nauli ya kwenda Mjini huna halafu eti uteuliwe na Bwana Mkubwa labda kuwa DED au DC au RC au Balozi au Mbunge au Mkurugenzi wa Shirika ukatae kwa ajili ya Wewe kuwa Mpinzani au Mwanaharakati?

Halafu hii Hoja kuwa huko nyuma sijui Dk. Slaa alikuwa akiiponda sana CCM na Serikali hadi mnaweka Ushahidi na kwamba mnamshangaa leo hii Yeye kuwa huko huko ni ya Kitoto sana kwani hakuna Dhambi yoyote ile kama Siku moja ukija Kuungana na wale ambao ulikuwa ukiwashutumu kwani inategemea labda wamebadilika vipi au unaoshirikiana nao sasa ni Watu makini vipi ukilinganisha na wale uliokuwa ukiwashutumu. Dk. Slaa alikuwa akiishutumu CCM ya JK na hii ya JPM ameona inafaa na ina Uthubutu pia ndiyo maana ameamua Kushirikiana nayo hivyo tuacheni Kumponda na Kumshangaa.

Kwa Tanzania hii ya sasa na hata Afrika ya sasa ambayo ina Wingu kubwa la Umasikini tena uliokithiri bado sijaona Mwafrika au Mwanasiasa ambaye hata akiwa ni Mkosoaji vipi kwa hizi Serikali siku akiteuliwa nayo atakataa Uteuzi na kubaki na Upinzani / Uanaharakati wake. Na msichokijua ni kwamba hata hao Wanasiasa wenu wengi barani Afrika mnaowasifu kuwa wanazinyoosha Serikali zao ukija nyuma ya Pazia utagundua kuwa wamewekwa tu hapo Kimkakati na wapo katika Payroll za Serikali ila wakija huku nje wanawahadaeni nanyi mnaona wapo pamoja nanyi kumbe wanawasanifu tu.

Na ndiyo maana Waungwana wanakumbia ukimnyooshea Mwenzako Kidole Kimoja angalia ni vingapi vimekugeukia Wewe ndipo utapata Majibu kuwa huenda Wewe unayemsema Dk. Slaa na wengineo wengi waliokuwa Upinzani au Wanaharakati na sasa wamehamia CCM ndiyo ukawa na Mapungufu zaidi kuliko hao unaowatuhumu kila Uchao. Mkitaka Watanzania wasiwe vigeugeu Kwanza tupambaneni Kuziimarisha Demokrasia zetu, Uchumi wetu na hata Katiba zetu ila kwa hali ilivyo sasa ya Njaa na Ugumu wa Maisha hakuna Mtanzania ( hasa mwana JamiiForums ) yoyote akiteuliwa na Rais JPM atakataa eti kwakuwa tu alikuwa anampinga au hampendi au hakipendi Chama cha CCM na kwamba Yeye ni Mpinzani na Mwanaharakati.

Najua mtanibishia kwa hili ila ninajua Mioyoni mwenu mtakubaliana nami tena kwa 100% kwani ndiyo Ukweli halisi na uliopo.
 
Tatizo kubwa la Watanzania hasa wale Wasomi na watumiaji wa Mitandao hii mbalimbali ya Kijamii tumekuwa wepesi katika Kulaumu, Kushambulia, Kudhihaki na hata Kutusi Watu ambao kwa wakati fulani walionyesha kuwa upande Wetu ila walipopata tu Uteuzi hasa kule ambako tunapachukia basi kwa haraka sana tunawaona hawafai na kuwabatiza kuwa ni Wasaliti na hawana maana tena.
Nimekuelewa..form Praise Team
 
Kwamba, usimwamini mwanasiasa yeyote kwa 100%, nasema hivyo kwa sababu huyu ninayemuona leo siyo Slaa niliyekesha humu JF kumtetea huku nikiambulia matusi ya nguoni kutoka Lumumba, wanaomjua Quinine wataelewa namaanisha nini. Na kuanzia leo mtazamo wangu kuhusu siasa na wanasiasa utabadilika sana sitakuwa Quinine wa enzi za Slaa.

Kwenye tasinia ya siasa Slaa ametufundisha mengi ila amekatisha ndoto za vijana wengi.

View attachment 1188090


Quinine ulipaswa uyajue hayo sio kupitia kwa Dr Slaa bali ni pindi pale nyinyi Chadema mkiongozwa na Mbowe mlipompokea Lowassa chamani na kumuidhinisha awe mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, ukizingatia nyinyi ndio mlituaminisha umma wa Tanzania kwa miaka nane mfululizo kwamba Lowassa ni gwiji la ufisadi nchini.

Msingekuwa wanafiki wakisiasa basi mngeendelea kuwa moja ya chama bora chenye itikadi nzuri za kisiasa, lakini hatujui mnachosimamia ni nini kwa sasa.

Once a NYUMBU always a NYUMBU...!!!
 
RAIS MAGUFULI ANATEKELEZA TULIYOKUWA TUNAYAPIGANIA, NAMPONGEZA - DKT. WILBROD SLAA

Balozi wa Tanzania nchini Sweden ambaye alikuwa Katibu mkuu wa zamani wa CHADEMA Dkt. Wilbrod Slaa, amesema yale yote waliyokuwa wanayasema ndio yanatekeleleza na Rais Magufuli.

"Yale yote tuliyokuwa tunayasimamia bila kubaki hata moja yanapiganiwa na kwa kuzidisha, Rais amevuka hata yale tuliyokuwa tunasema, hivyo natoa pongezi kwa Rais," amesema Dkt. Slaa. >>>
 
Kitu ambacho watu hawajamuelewa Slaa ni kuwa ndoa ndiyo imeyumbisha sana maisha yake (hadi dish kuyumba).
Slaa bado kiasili kabisa anapingana na utawala huu wa kukosa demokrasia na kuendekeza ufisadi, lakini upande wa pili kakamatika na Josephine ambaye kwake Slaa alimchukulia kama mtaji wa maisha bora na ya juu kabisa ikiwezekana Urais.
Zile habari za kufungiwa mlango na kulala kwenye gari pale mama anapochukia hazikuwa za kutunga Bali ukweli. Sasa hawezi tena kukubali aukose ubalozi tena atamweleza nini Josephine? Ukitaka kujua asemayo kwa sasa hayatoki moyoni mpe dakika 10 za kuzungumza mfululizo utagundua hilo.
Nawahakikishia kuwa mfano Jose atangulie kwenye haki (hatumuombei hivyo) Slaa hachukui miezi sita hajaitosa nafasi hiyo au kutoswa baada ya kuseme maneno yasiyo furahisha utawala wa CCM.
Matatizo na wanawake yatamtesa sana kwani alikiuka kiapo chake mwenyewe.
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom