Jibaba Bonge
JF-Expert Member
- May 6, 2008
- 1,246
- 401
Tamko lilitolewa na Shimbo la kututishia watanzania haliwezi kuachwa lipite hivihivi na waitakiao amani nchi yetu.
Sitaki kuamini kuwa Shimbo hana ufahamu wa kutosha kuelewa kuwa kuna watu wenye ufahamu mkubwa wa kuelewa mambo kwa kusoma hata katikati ya mistari!
Tofauti na wanavyotaka tuamini kuwa JW na polisi wanajali sana amani ya tanzania katika kipindi hiki cha uchaguzi; tamko lao linaonyesha, kwa uwazi mkubwa sana, lengo lililokusudiwa na wakubwa hawa. Hakuna jingine ni kutaka kuisadia chama wanachukitumikia, ingawa wanadai wao si wanachama wa chama chochote kwa mujibu wa kazi zao na bosi wao mkuu kuendelea kushika madaraka ya nchi kwa gharama yoyote ile!
Ni ukweli uliowazi kuwa katika chaguzi mbalimbali na hasa ambazo zina ushindani kama huu wa sasa kunaweza kutokea mambo yafuatayo; kwanza ni lazima mshindi apatikane, pili, kama ukuchaguzi ni huru na / au wa haki basi mshindi atapatikana kwa halali na tatu, kama uchaguzi si huru na si wa haki basi mshindi anweza kupatikana isivyo halali na hapa ndiyo tatizo litakapoanzia kwani umma utataka kudai haki yao.
Umma wa watanzania ni pamoja na wafanyakazi, wakulima, wasio na kazi, wanajeshi wa JW, polisi, magereza na wengine wote ili mradi ni raia halali wa tanzania wakubwa kwa wadogo, wazee kwa vijana, wanaume kwa wanawake.
Shimbo anaposema lazima matokeo yakubaliwe kuna walakini. Matokeo yanayokubalika ni yale to yakiyo halali. Nilitegemea Shimbo asema LAZIMA MATOKEO HALALI YAKUBALIWE NA KUHESHIMIWA. Haiwezekani umma wa watanzania wakubali matokeo yoyote yale hata kama yamechakachuliwa eti tu kwa sababu shimbo ametishia kwa tamko lake!
Hakika hatutaki kumwaga damu lakini kama haki yetu itapatikana kwa kumwaga damu basi hatuna budi kuimwaga.
kwa kutokujua ama kujisahau, pengine kwa sababu ya maisha bora aliyonayo yeye, hafikirii kuwa hata wanajeshi anaotutishia nao, wale askari wa kawaida kabisa, wavuja jasho, wachovu, wanaodai maisha bora na mishahara mizuri, wanaolala kwenye mahanga na mahema watakuwa pia wanadai haki yao, wanaweza wakawa ni sehemu ya umma utakaokuwa umeporwa haki yao (kama ikitokea haki imeporwa) na hivyo wakawa upande wa kudai haki yao ndiyo maana nasema nguvu ya umma ni kubwa kuliko tamko la Shimbo.
Ni jambo la ajabu sana kwamba chaguzi zinazohusisha vyama vingi zimefanyika mara tatu katika nchi yetu, hakukuwa na vitisho vya akina Shimbo, uchaguzi wa mwaka huu una nini cha ziada kilichomkurupusha Shimbo kutoa tamko ‘biased' kama alilolitoa? Kwa mtu makini anayechunguza mwenedo wa kampeni ataona kuwa ‘pepo ni za kusi na jahazi la anachokitumikia linaelekea kaskazi na bahari imechafuka ni ya mawimbi makubwa'.
NGUVU YA UMMA NI KUBWA KULIKO TAMKO LA SHIMBO.
Sitaki kuamini kuwa Shimbo hana ufahamu wa kutosha kuelewa kuwa kuna watu wenye ufahamu mkubwa wa kuelewa mambo kwa kusoma hata katikati ya mistari!
Tofauti na wanavyotaka tuamini kuwa JW na polisi wanajali sana amani ya tanzania katika kipindi hiki cha uchaguzi; tamko lao linaonyesha, kwa uwazi mkubwa sana, lengo lililokusudiwa na wakubwa hawa. Hakuna jingine ni kutaka kuisadia chama wanachukitumikia, ingawa wanadai wao si wanachama wa chama chochote kwa mujibu wa kazi zao na bosi wao mkuu kuendelea kushika madaraka ya nchi kwa gharama yoyote ile!
Ni ukweli uliowazi kuwa katika chaguzi mbalimbali na hasa ambazo zina ushindani kama huu wa sasa kunaweza kutokea mambo yafuatayo; kwanza ni lazima mshindi apatikane, pili, kama ukuchaguzi ni huru na / au wa haki basi mshindi atapatikana kwa halali na tatu, kama uchaguzi si huru na si wa haki basi mshindi anweza kupatikana isivyo halali na hapa ndiyo tatizo litakapoanzia kwani umma utataka kudai haki yao.
Umma wa watanzania ni pamoja na wafanyakazi, wakulima, wasio na kazi, wanajeshi wa JW, polisi, magereza na wengine wote ili mradi ni raia halali wa tanzania wakubwa kwa wadogo, wazee kwa vijana, wanaume kwa wanawake.
Shimbo anaposema lazima matokeo yakubaliwe kuna walakini. Matokeo yanayokubalika ni yale to yakiyo halali. Nilitegemea Shimbo asema LAZIMA MATOKEO HALALI YAKUBALIWE NA KUHESHIMIWA. Haiwezekani umma wa watanzania wakubali matokeo yoyote yale hata kama yamechakachuliwa eti tu kwa sababu shimbo ametishia kwa tamko lake!
Hakika hatutaki kumwaga damu lakini kama haki yetu itapatikana kwa kumwaga damu basi hatuna budi kuimwaga.
kwa kutokujua ama kujisahau, pengine kwa sababu ya maisha bora aliyonayo yeye, hafikirii kuwa hata wanajeshi anaotutishia nao, wale askari wa kawaida kabisa, wavuja jasho, wachovu, wanaodai maisha bora na mishahara mizuri, wanaolala kwenye mahanga na mahema watakuwa pia wanadai haki yao, wanaweza wakawa ni sehemu ya umma utakaokuwa umeporwa haki yao (kama ikitokea haki imeporwa) na hivyo wakawa upande wa kudai haki yao ndiyo maana nasema nguvu ya umma ni kubwa kuliko tamko la Shimbo.
Ni jambo la ajabu sana kwamba chaguzi zinazohusisha vyama vingi zimefanyika mara tatu katika nchi yetu, hakukuwa na vitisho vya akina Shimbo, uchaguzi wa mwaka huu una nini cha ziada kilichomkurupusha Shimbo kutoa tamko ‘biased' kama alilolitoa? Kwa mtu makini anayechunguza mwenedo wa kampeni ataona kuwa ‘pepo ni za kusi na jahazi la anachokitumikia linaelekea kaskazi na bahari imechafuka ni ya mawimbi makubwa'.
NGUVU YA UMMA NI KUBWA KULIKO TAMKO LA SHIMBO.