Rugemeleza
JF-Expert Member
- Oct 26, 2009
- 668
- 136
Hivi ndivyo mambo yanavyozidi kunoga. Angalizo ni katika kupiga na kulinda kura tu!
Slaa ampiku JK Kyela
Waahidi kumpa urais yeye, ubunge Mwakyembe
na Janet Josiah
KATIKA mazingira ya kisiasa ambayo hayajapata kutokea tangu kuanza kwa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, juzi jioni alilazimika kumnadi mgombea ubunge wa Kyela kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe. Hali hiyo ilitokea baada ya Dk. Slaa aliyekuwa katika jimbo hilo la uchaguzi kutaka kusikia maoni ya wananchi wa Kyela kuhusu namna watakavyopiga kura za kumchagua rais na mbunge.
Tukio hilo lilikuja baada ya Dk. Slaa kupanda jukwaani na kuwauliza wananchi waliokuwa wamefurika katika mkutano wake wa kampeni ni mgombea gani wa urais waliyekuwa wakimuunga mkono na kwa kauli moja wakamjibu wakisema ni wewe Dk. Slaa na ilipofika katika ubunge wakamjibu kwa sauti ya pamoja Mwakyembe.
Jibu hilo la wananchi lilisababisha Dk. Slaa akubaliane na masharti aliyopewa na wapiga kura hao wa Kyela na akawataka waende kwa Mwakyembe kumueleza kwamba atakuwa tayari kufanya naye kazi katika serikali yake ijayo atakayoiunda baada ya kutangazwa mshindi wa urais Novemba mwaka huu, iwapo tu (Mwakyembe) ataacha kumnadi mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Rais Jakaya Kikwete.
Kama mnamtaka Mwakyembe nitaweka masharti mwambieni lazima afuate masharti yangu. Kwamba afuate masharti ya rais tunayempenda lazima atetee maslahi ya wananchi kwanza kabla ya kutetea CCM...Nataka mbunge ambaye nitaweza kumtuma kazi. Mwambieni kuwa, Dk. Slaa anaenda kuchukua urais, kama huwezi kufanya naye kazi, katiza nimchukue Eddo (Makata), alisema Dk. Slaa.
Eddo Makata ndiye mgombea ubunge katika jimbo la Kyela kwa tiketi ya CHADEMA ambaye alipopewa nafasi ya kuhutubia alisema alikuwa tayari kusubiri miaka mitano iwapo tu Dk. Mwakyembe atakuwa tayari kumnadi Dk. Slaa katika kampeni zake.
Akizungumza kwa kujiamini huku akishangiliwa na wakazi wenzake wa Kyela, Makata alisema yeye si mwanasiasa mbinafsi na kwa hiyo anawapa uhuru wananchi wa Kyela kumchagua mbunge wanayemtaka japo kwa masharti waliyompa.
Kama Dk. Mwakyembe atamnadi Dk. Slaa na mimi nitasubiri hadi 2015. Nitayaheshimu maamuzi yenu, alisema.
Akimzungumzia Mwakyembe katika mkutano huo, Dk. Slaa alisema alikuwa tayari kufanya naye kazi kutokana na kutambua kwake kwamba amekuwa akinyanyaswa na kupigwa vita ndani ya CCM kutokana na msimamo wake wa kutetea wananchi.
Akionyesha kumuunga mkono mgombea wake wa ubunge, Dk. Slaa alisema, Mimi si mwamuzi, wananchi chagueni mbunge mnayemtaka na wewe Eddo, Kama Mwakyembe ataendelea kumnadi Kikwete, endelea na kampeni ukimnadi Slaa.
Dk. Mwakyembe ni mmoja wa wabunge wa CCM waliojipambanua kama wapambanaji wa ufisadi na ndiye aliyeongoza Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wenye utata wa kampuni ya kufua umeme ya Richmond, ambayo hatima yake ilimlazimisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujiuzulu wadhifa wake miaka mitatu iliyopita.
Wachambuzi wa kisiasa wanasema Dk. Mwakyembe anatambulika miongoni mwa wapiga kura wake kama shujaa wao, ambaye wiki iliyopita alifanya kazi ya ziada kuwaomba wana Kyela wawe watulivu wakati Rais Jakaya Kikwete alipokwenda kuomba kura.
Jana Dk, Slaa aliendelea na mikutano yake katika majimbo ya Mbeya Vijijini na Mbeya Mjini, akiwahutubia maelfu ya wananchi wa Mbalizi, aliwataka waichague CHADEMA ili iwapelekee dira ya maendeleo na siyo ahadi za bajaji 400 kwa kina mama wajawazito ambazo aliziahidi Kikwete akiwa katika kampeni zake.
Wananchi wa Mbalizi, mmeandika mabango kuwa Kikwete bye bye na bajaji zake na mimi nasema bye bye kwa kuwa wananchi wamechoshwa na sasa wanataka mabadiliko, si bajaji, alisema Dk. Slaa.
Alisisitiza kuwa iwapo ataingia Ikulu, serikali itaifanya elimu ya lazima kwa kila Mtanzania kuwa kidato cha sita, na italipiwa na serikali; na kwamba wananchi watatibiwa bure kwani ndizo huduma wanazostahili kwa kodi wanayolipa.
Chanzo: Tanzania Daima
Slaa ampiku JK Kyela
Waahidi kumpa urais yeye, ubunge Mwakyembe
na Janet Josiah
Tukio hilo lilikuja baada ya Dk. Slaa kupanda jukwaani na kuwauliza wananchi waliokuwa wamefurika katika mkutano wake wa kampeni ni mgombea gani wa urais waliyekuwa wakimuunga mkono na kwa kauli moja wakamjibu wakisema ni wewe Dk. Slaa na ilipofika katika ubunge wakamjibu kwa sauti ya pamoja Mwakyembe.
Jibu hilo la wananchi lilisababisha Dk. Slaa akubaliane na masharti aliyopewa na wapiga kura hao wa Kyela na akawataka waende kwa Mwakyembe kumueleza kwamba atakuwa tayari kufanya naye kazi katika serikali yake ijayo atakayoiunda baada ya kutangazwa mshindi wa urais Novemba mwaka huu, iwapo tu (Mwakyembe) ataacha kumnadi mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Rais Jakaya Kikwete.
Kama mnamtaka Mwakyembe nitaweka masharti mwambieni lazima afuate masharti yangu. Kwamba afuate masharti ya rais tunayempenda lazima atetee maslahi ya wananchi kwanza kabla ya kutetea CCM...Nataka mbunge ambaye nitaweza kumtuma kazi. Mwambieni kuwa, Dk. Slaa anaenda kuchukua urais, kama huwezi kufanya naye kazi, katiza nimchukue Eddo (Makata), alisema Dk. Slaa.
Eddo Makata ndiye mgombea ubunge katika jimbo la Kyela kwa tiketi ya CHADEMA ambaye alipopewa nafasi ya kuhutubia alisema alikuwa tayari kusubiri miaka mitano iwapo tu Dk. Mwakyembe atakuwa tayari kumnadi Dk. Slaa katika kampeni zake.
Akizungumza kwa kujiamini huku akishangiliwa na wakazi wenzake wa Kyela, Makata alisema yeye si mwanasiasa mbinafsi na kwa hiyo anawapa uhuru wananchi wa Kyela kumchagua mbunge wanayemtaka japo kwa masharti waliyompa.
Kama Dk. Mwakyembe atamnadi Dk. Slaa na mimi nitasubiri hadi 2015. Nitayaheshimu maamuzi yenu, alisema.
Akimzungumzia Mwakyembe katika mkutano huo, Dk. Slaa alisema alikuwa tayari kufanya naye kazi kutokana na kutambua kwake kwamba amekuwa akinyanyaswa na kupigwa vita ndani ya CCM kutokana na msimamo wake wa kutetea wananchi.
Akionyesha kumuunga mkono mgombea wake wa ubunge, Dk. Slaa alisema, Mimi si mwamuzi, wananchi chagueni mbunge mnayemtaka na wewe Eddo, Kama Mwakyembe ataendelea kumnadi Kikwete, endelea na kampeni ukimnadi Slaa.
Dk. Mwakyembe ni mmoja wa wabunge wa CCM waliojipambanua kama wapambanaji wa ufisadi na ndiye aliyeongoza Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wenye utata wa kampuni ya kufua umeme ya Richmond, ambayo hatima yake ilimlazimisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujiuzulu wadhifa wake miaka mitatu iliyopita.
Wachambuzi wa kisiasa wanasema Dk. Mwakyembe anatambulika miongoni mwa wapiga kura wake kama shujaa wao, ambaye wiki iliyopita alifanya kazi ya ziada kuwaomba wana Kyela wawe watulivu wakati Rais Jakaya Kikwete alipokwenda kuomba kura.
Jana Dk, Slaa aliendelea na mikutano yake katika majimbo ya Mbeya Vijijini na Mbeya Mjini, akiwahutubia maelfu ya wananchi wa Mbalizi, aliwataka waichague CHADEMA ili iwapelekee dira ya maendeleo na siyo ahadi za bajaji 400 kwa kina mama wajawazito ambazo aliziahidi Kikwete akiwa katika kampeni zake.
Wananchi wa Mbalizi, mmeandika mabango kuwa Kikwete bye bye na bajaji zake na mimi nasema bye bye kwa kuwa wananchi wamechoshwa na sasa wanataka mabadiliko, si bajaji, alisema Dk. Slaa.
Alisisitiza kuwa iwapo ataingia Ikulu, serikali itaifanya elimu ya lazima kwa kila Mtanzania kuwa kidato cha sita, na italipiwa na serikali; na kwamba wananchi watatibiwa bure kwani ndizo huduma wanazostahili kwa kodi wanayolipa.
Chanzo: Tanzania Daima