Siyo sahihi kumuweka mtu mahabusu kwa kisingizio cha usalama wake

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,121
7,877
Siyo sahihi kumuweka mtu mahabusu kwa kisingizio cha usalama wake

Nimeona hii trend mpya kwa mahakama kumrudisha mtu rumande kwa kisingizio cha usalama wake mwenyewe. Eti kwamba wakimuachia huru anaweza kudhuriwa na wabaya wake!

Hili sidhani kama ni sahihi kabisa kwa sababu serikali ina uwezo na inatakiwa kutoa ulinzi kwa mtu yoyote aliye victim, hasa kama mtu huyo ni muathirika kwa mambo muhimu ya kisheria na kikatiba kama 'uhuru wa kuongea' na haki nyingine za msingi za binadamu. Kama serikali na vyombo vya dola vinashindwa kulinda watu wa namna hiyo, ina maana kuwa umma kwa ujumla haupo salama na hakuna chombo cha dola kiko tayari kusimamia katiba ya nchi, kitu ambacho ni hatari sana.

Hivi serikali kweli haina uwezo huo au hii inatumika tu kama sababu ya kukomoa watu? Hivi serikali haina safe houses (nyumba za siri zilizo salama mfano kwa mashahidi muhimu)? Na wanapokuwa huko jela wanapodai ndiyo salama zaidi kwao, wanakuwa wametenganishwa na wafungwa wengine?

Tuliwezaje kuwaweka watu kama Aboud Jumbe katika ulinzi kwa miaka mingi tushindwe kumlinda mtu kama Joseph Mbilinyi 'Sugu', ambaye hana hata maadui, isipokuwa wale ambao wangeweza kumpata hata huko huko jela? Serikali inashindwaje kumlinda mtu kama Abdul Nondo huku akiwa anaendelea na masomo yake wakati kesi yake inaendelea kusikilizwa? Nakumbuka kuna mwanasiasa zamani enzi za Nyerere alirudishwa kijijini kwao na akazuiwa kabisa kutoka, huyo alilindwaje?

Hili jambo haliingii akilini na ningeomba kwa ujumla wetu tulikemee. Tukiliacha hili, watu watakuwa wanatupwa jela waozee huko huku kisingizio kikiwa 'upelelezi na kesi bado unaendelea na hatuwezi kumuachia kwa usalama wake mwenyewe'.
 
Mfumo wetu wa sheria, utoaji haki na kuadhibu wakosaji una mengi sana ya kurekebishwa.....kwenye kutoa haki ni rahisi sana mtu kuonewa kwa kutumia sheria hizohizo zinazokusudia kutoa haki
 
Hakuna sheria kama hiyo popote pale duniani ni hii Serikali dhalimu tu eti kawekwa mahabusu kwa usalama wake!!!!
 
Siyo sahihi kumuweka mtu mahabusu kwa kisingizio cha usalama wake

Nimeona hii trend mpya kwa mahakama kumrudisha mtu rumande kwa kisingizio cha usalama wake mwenyewe. Eti kwamba wakimuachia huru anaweza kudhuriwa na wabaya wake!

Hili sidhani kama ni sahihi kabisa kwa sababu serikali ina uwezo na inatakiwa kutoa ulinzi kwa mtu yoyote aliye victim, hasa kama mtu huyo ni muathirika kwa mambo muhimu ya kisheria na kikatiba kama 'uhuru wa kuongea' na haki nyingine za msingi za binadamu. Kama serikali na vyombo vya dola vinashindwa kulinda watu wa namna hiyo, ina maana kuwa umma kwa ujumla haupo salama na hakuna chombo cha dola kiko tayari kusimamia katiba ya nchi, kitu ambacho ni hatari sana.

Hivi serikali kweli haina uwezo huo au hii inatumika tu kama sababu ya kukomoa watu? Hivi serikali haina safe houses (nyumba za siri zilizo salama mfano kwa mashahidi muhimu)? Na wanapokuwa huko jela wanapodai ndiyo salama zaidi kwao, wanakuwa wametenganishwa na wafungwa wengine?

Tuliwezaje kuwaweka watu kama Aboud Jumbe katika ulinzi kwa miaka mingi tushindwe kumlinda mtu kama Joseph Mbilinyi 'Sugu', ambaye hana hata maadui, isipokuwa wale ambao wangeweza kumpata hata huko huko jela? Serikali inashindwaje kumlinda mtu kama Abdul Nondo huku akiwa anaendelea na masomo yake wakati kesi yake inaendelea kusikilizwa? Nakumbuka kuna mwanasiasa zamani enzi za Nyerere alirudishwa kijijini kwao na akazuiwa kabisa kutoka, huyo alilindwaje?

Hili jambo haliingii akilini na ningeomba kwa ujumla wetu tulikemee. Tukiliacha hili, watu watakuwa wanatupwa jela waozee huko huku kisingizio kikiwa 'upelelezi na kesi bado unaendelea na hatuwezi kumuachia kwa usalama wake mwenyewe'.

Hayo yanawezekana kwakuwa ni taifa la wajinga hamhoji na hamko tayari kuhoji

In short hamna tofauti na makondoo muda wote mnainamisha vichwa
 
Mahabusu ni sehemu ya usalama kwa mlalamikiwa au mshtakiwa, kama huamini we Fanya jaribio la kudhuru MTU afu baki mtaani utaona tu nini umuhimu wa mahabusu.
 
Mkuu umetoa hoja njema sana, lakini tukirudi kwenye misingi ya kisheria tunaona kuwa lengo hasa la sheria hii katika S. 148(5)(f) of Criminal Procedure Act inaeleza kwamba mtu anaweza kunyimwa dhamana iwapo mahakama itaona vyema kwa ajili ya usalama wake. Sasa basi hapa nadhani mahakama inakua imejiridhisha kwamba usalama wa mtuhumiwa unaweza kuwa hatarirni iwapo mtuhumiwa huyo atapatiwa dhamana. Hivyo basi, katika suala hili, sheria iliuachia uwanja huu kwa mwendesha mashtaka kuweza ku'rise hoja hii. Hivyo ili kuweza kupata hiyo haki ya dhamana baada ya hoja hii ya mwendesha mashtaka ni kufanya appeal kwa mamlaka za juu na kuonesha hoja zako ni kwanini usalama wako hauwezi kuwa hatarini iwapo utapewa dhamana rejea ile kesi ya Lema aliyokaa mahabusu kwa miezi minne.
Hivyo basi, kwa maoni yangu naona kifungu hiki ni sahihi kabisa kisheria kwani kama lengo hasa la kifungu hiki ni kutoa ulinzi kwa mtuhumiwa pale inapoonekana kuwa anaweza kuwa hatarini. Kama mtoa mada alivyosema katika aya yake ya pili kwamba '...serikali ina uwezo na inatakiwa kutoa ulinzi kwa mtu yoyote aliye victim..' basi hii njia ya kuweka mtuhumiwa mahabusu ni moja ya njia ya ulinzi kwa mtuhumiwa kwani tunaelewa ni kwa jinsi gani mahabusu ni mahali salama zaidi kuliko akiwepo mtaani kutokana na rasilimali watu ya walinzi wetu wa serikali nadhani pia hili linachangiwa na uelewa duni wa wananchi juu ya 'handling of accusations' kwamba tumekua na tabia ya kujichukulia sheria mkononi.
Hivyo nadhani badala ya kukiondoa kifungu hicho, ni vema mamlaka husika katika utekelezaji wa sheria hii zingeongozwa na busara na uhalisia zaidi katika kutekeleza sheria hii kwa watuhumiwa na kuacha kuitumia kama njia ya kumkomoa mtuhumiwa, lakini pia kwa mtuhumiwa ambaye atanyimwa dhamana kwa kifungu hiki, iwapo atajiridhisha pasipo shaka kuwa ameonewa, basi anaweza kukata rufaa juu ya maamuzi hayo ya kunyimwa rufaa. Rejea kesi ya Mh. Lema ile aliyowekwa mahabusu kwa miezi kadhaa. Asante
 
Back
Top Bottom