Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,702
Huyu jamaa anaishi na mwanamke wake kinyumba,ni kama mke na mume.
"
Wakati wanakutana,mwanamke alikua tayari ana watoto wawili aliozaa na wanaume wawili tofauti.
"
Tatizo ni kuwa mwanamke amekuwa analalamika kuwa jamaa huwa haachi matumizi.
Sasa leo ndo nimekutana na jamaa huyo na kumuuliza kulikoni?
Nae alijibu ifuatavyo;
"Sio kweli kuwa simpi hela ya matumizi ila ninaponunua mahindi debe moja likiisha nae anatakiwa anunue kwa kuwa anafanya kazi!
Tatizo la mke wangu huyu ananilazimisha nikisafiri anataka nimwachie hela,sasa nimwachie hela ya nini wakati mimi sipo na sina watoto pale"?
"
Sikujua hasa nimuulize nini,lakini jamaa aliposema kuwa hawezi kulisha watoto ambao sio wake na anapogharamia chakula wakati yupo ni kwa sababu na yeye anakula ndipo nilipomuelewa.
"
Lakini nilimuuliza kuhusu kumgharamia mkewe hata kwa kiasi kidogo kwakuwa yule ni mkewe,jamaa akasema angefanya hivyo kama mkewe angekua hana kazi!
"
Huyu jamaa haamini kama ni sahihi kumpa matumizi mwanamke mwenye ajira.
"
Lakini pia hataki kugharamia familia isiyo yake.
"
Je huyu yuko sahihi?
Kama yuko sahihi inawezekana hii ikawa sababu ya baadhi yetu kuwakimbia wanawake wenye watoto!!
"
Wakati wanakutana,mwanamke alikua tayari ana watoto wawili aliozaa na wanaume wawili tofauti.
"
Tatizo ni kuwa mwanamke amekuwa analalamika kuwa jamaa huwa haachi matumizi.
Sasa leo ndo nimekutana na jamaa huyo na kumuuliza kulikoni?
Nae alijibu ifuatavyo;
"Sio kweli kuwa simpi hela ya matumizi ila ninaponunua mahindi debe moja likiisha nae anatakiwa anunue kwa kuwa anafanya kazi!
Tatizo la mke wangu huyu ananilazimisha nikisafiri anataka nimwachie hela,sasa nimwachie hela ya nini wakati mimi sipo na sina watoto pale"?
"
Sikujua hasa nimuulize nini,lakini jamaa aliposema kuwa hawezi kulisha watoto ambao sio wake na anapogharamia chakula wakati yupo ni kwa sababu na yeye anakula ndipo nilipomuelewa.
"
Lakini nilimuuliza kuhusu kumgharamia mkewe hata kwa kiasi kidogo kwakuwa yule ni mkewe,jamaa akasema angefanya hivyo kama mkewe angekua hana kazi!
"
Huyu jamaa haamini kama ni sahihi kumpa matumizi mwanamke mwenye ajira.
"
Lakini pia hataki kugharamia familia isiyo yake.
"
Je huyu yuko sahihi?
Kama yuko sahihi inawezekana hii ikawa sababu ya baadhi yetu kuwakimbia wanawake wenye watoto!!