Mwenda_Pole
JF-Expert Member
- Jul 5, 2008
- 281
- 66
Leo mida ya saa mbili usiku nilikuwa nasikiliza Radio Maria na walikuwa wanajadili hichi kisa ambacho kimenishangaza sana.
Kisa chenyewe ni hichi: Kuna jamaa alikuwa na mke wake wa ndoa na waliishi kwa kipindi cha takribani miaka 3 hivi lakini bahati mbaya hawakufanikiwa kupata mtoto muda wote huo. Sasa baada ya kuona miaka inakwenda lakini na mambo sio mazuri, familia za pande mbili walianza kulaumiana. Upande wa mume wanambwambia mtoto wao kuwa umeoa mke asiyezaa na upande wa mke nao wanamwambia mtoto wao umeolewa na mwanaume suruali. Baada ya presha hiyo kuzidi ili kujilindia heshima mwanaume akaibuka na wazo kwa mke wake kuwa amuombe rafiki yake (rafiki ya mwanamume) ashiriki na mke wake ili awasaidie kutafuta mtoto na wafanye siri yao. Baada ya kukubaliana na kweli haikuchukua muda jamaa akawa anakula na anapatiwa na support juu kimaisha kwani huyu mume (mwenye mke) alikuwa anajiweza na yule jamaa (Msaidizi) mambo yake yalikuwa sio mazuri kimaisha. Jamaa aliendelea kula kama kawaida na hatimaye wakafika watoto watatu. Kadri muda ulivyokuwa unaenda mke akawa hana heshima tena kwa yule mume wake na pia mambo ya yule jamaa (msaidizi) yakaanza kuwa mazuri na hatimaye anataka kuchukua watoto wake pamoja na mama yao (mke aliyezaa nae) ili aishi nao na kuwatunza mwenyewe. Jamaa ameshaamua kama noma na iwe noma lakini lazima achukue watoto wake, kutokana na hali hiyo jamaa sasavwameshakuwa maadui kabisa na yule.
Nimekuta kipindi kipo katikati lakini kifupi ni kuwa Msaidizi anamtolea vitisho vya hali ya juu huyu jamaa aachie watoto na mke nae heshima ndio imekwisha kabisa kwa mume wake na amekwishafika kwa yule jamaa (msaidizi).
Jamaa alikuwa anaomba wasikilizaji wamshauri afanye nini, anajilaumu sana kwani ameshagundua kuwa aliochukua haukuwa uamuzi mzuri wa kumuachia jamaa ajinafasi na wife wake na anajilaumu sana juu ya uamuzi huo.
My Take:
Hata kama sina uwezo wa kuzalisha lakini kumtafuta mume mwenzangu tena rafiki yangu na kumkabidhi mke hii ni zaidi ya kutokuwa na uwezo wa kuzalisha.
Wadau nyinyi mnasemaje kuhusu hii? manake sio siri mimi nilitamani kuibamiza chini na kuivunjilia mbali radio yangu.
Hivi mtu unapoomba jamaa akusaidie mke unakuwa anafikiria nini? Na mambo huwa yanakuwaje? Yaani jamaa anakuja nyumbani kwako unampisha chumbani na wewe kwenda kulala sebuleni ? au utajisikiaje mkeo anapokuaga asubuhi wakati akienda kazini kuwa leo ninajisikia nina hamu sana nikitoka kazini nitachelewa kurudi nitapitia kwa jamaa ama nitalala huko huko tutaonana kesho...damn...!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! yaani mpaka key kwenye keyboard hapa sizioni.
Unatarajia huyo mke ataendela kukuheshimu? Na hao watoto watakaozaliwa utawaitaje hata kama wao wanakuita baba?
Tusaidiane kwa mawazo kina dada pia mnalionaje suala hili.
NB : Hichi ni kisa cha ukweli na mtangazaji alikuwa pamoja na huyo jamaa yaliyomkuta.
Kisa chenyewe ni hichi: Kuna jamaa alikuwa na mke wake wa ndoa na waliishi kwa kipindi cha takribani miaka 3 hivi lakini bahati mbaya hawakufanikiwa kupata mtoto muda wote huo. Sasa baada ya kuona miaka inakwenda lakini na mambo sio mazuri, familia za pande mbili walianza kulaumiana. Upande wa mume wanambwambia mtoto wao kuwa umeoa mke asiyezaa na upande wa mke nao wanamwambia mtoto wao umeolewa na mwanaume suruali. Baada ya presha hiyo kuzidi ili kujilindia heshima mwanaume akaibuka na wazo kwa mke wake kuwa amuombe rafiki yake (rafiki ya mwanamume) ashiriki na mke wake ili awasaidie kutafuta mtoto na wafanye siri yao. Baada ya kukubaliana na kweli haikuchukua muda jamaa akawa anakula na anapatiwa na support juu kimaisha kwani huyu mume (mwenye mke) alikuwa anajiweza na yule jamaa (Msaidizi) mambo yake yalikuwa sio mazuri kimaisha. Jamaa aliendelea kula kama kawaida na hatimaye wakafika watoto watatu. Kadri muda ulivyokuwa unaenda mke akawa hana heshima tena kwa yule mume wake na pia mambo ya yule jamaa (msaidizi) yakaanza kuwa mazuri na hatimaye anataka kuchukua watoto wake pamoja na mama yao (mke aliyezaa nae) ili aishi nao na kuwatunza mwenyewe. Jamaa ameshaamua kama noma na iwe noma lakini lazima achukue watoto wake, kutokana na hali hiyo jamaa sasavwameshakuwa maadui kabisa na yule.
Nimekuta kipindi kipo katikati lakini kifupi ni kuwa Msaidizi anamtolea vitisho vya hali ya juu huyu jamaa aachie watoto na mke nae heshima ndio imekwisha kabisa kwa mume wake na amekwishafika kwa yule jamaa (msaidizi).
Jamaa alikuwa anaomba wasikilizaji wamshauri afanye nini, anajilaumu sana kwani ameshagundua kuwa aliochukua haukuwa uamuzi mzuri wa kumuachia jamaa ajinafasi na wife wake na anajilaumu sana juu ya uamuzi huo.
My Take:
Hata kama sina uwezo wa kuzalisha lakini kumtafuta mume mwenzangu tena rafiki yangu na kumkabidhi mke hii ni zaidi ya kutokuwa na uwezo wa kuzalisha.
Wadau nyinyi mnasemaje kuhusu hii? manake sio siri mimi nilitamani kuibamiza chini na kuivunjilia mbali radio yangu.
Hivi mtu unapoomba jamaa akusaidie mke unakuwa anafikiria nini? Na mambo huwa yanakuwaje? Yaani jamaa anakuja nyumbani kwako unampisha chumbani na wewe kwenda kulala sebuleni ? au utajisikiaje mkeo anapokuaga asubuhi wakati akienda kazini kuwa leo ninajisikia nina hamu sana nikitoka kazini nitachelewa kurudi nitapitia kwa jamaa ama nitalala huko huko tutaonana kesho...damn...!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! yaani mpaka key kwenye keyboard hapa sizioni.
Unatarajia huyo mke ataendela kukuheshimu? Na hao watoto watakaozaliwa utawaitaje hata kama wao wanakuita baba?
Tusaidiane kwa mawazo kina dada pia mnalionaje suala hili.
NB : Hichi ni kisa cha ukweli na mtangazaji alikuwa pamoja na huyo jamaa yaliyomkuta.