Siwaelewi Jaji Mkuu, Mwanasheria Mkuu, TLS, Tume ya Haki za Binadamu

StingRay

JF-Expert Member
Jun 28, 2014
503
628
NEC hii inawahusu sana.....!!!!!

Hivi kabisa kabisa kabisa watanzania pamoja na tunu zetu zooooote tunakubali hili kwa gharama sifuri?

Mgombea yupo kwenye kampeni za kiti cha uongozi wa juu kabisa katika nchi hii anaahidi wapiga kura watarajiwa na wananchi kwamba, "Mkichagua upinzani sitaleta maendeleo hapa" kweli? Kwani maendeleo hapa maanake nini? Ni kuboresha huduma za kijamii?? Au inamaana nyingine?

Kwamba mgombea anaahidi kuvunja katiba kwa kuwabagua wananchi katika maendeleao kwa minajili ya chama/vyama vya siasa??? Kweli kabisa??? Nec mpo kimya? Watanzania wote wapo kimya? Na wanashangilia na kupiga makofi?

Yaani kiongozi mkubwa kabisa wa nchi anayeaapa kuilinda katiba kabla ya kurudi ikulu anaapa kwabagua wananchi wake kwa minajili ya vyama vya siasa? Hivi huyu ni kiongozi au mtawala? Is he a leader or a ruler?

Hivi kodi hizo wanaolipa ni ccm pekee? Muda wote hii nchi inamatukio yatiayo kinyaa na kichefuchefu.

Ombi...Kanisa Katoliki Tanzania litoe tamko kali la hatuwatendei waumini wetu na watanzania wote yatupasayo mbele za Mungu..
 
Bahati mbaya kwake ni kuwa hatashinda na hawezi kuiba ushindi.

Wapambe mkumbusheni kuwa jaribio lolote la kuiba kura litaharibu maisha yake, ya mkewe, ya watoto wake, ndugu, jamaa na wapambe.

Katika hilo hatutamuonea huruma hata kidogo. Viongozi wa dini ndio wakati wenu wa kutahadharisha wale wote wanaopanga kupiga goli la mkono kuwa wasije kusema hawakuambiwa.

Hizi ni zama tofauti na zilizo pita hivyo wakae chonjo kabisa
 
Mkuu jpm nilikua na matumain naye Sana ila mpaka mda huu najiuliza Nini kimemkuta bahada ya kuingia ikulu, Sasa ole wako lissu uende ikulu alafu utuchezee akili watz
 
NEC, MWANASHERIA MKUU wa Serikali, JAJI MKUU, SPIKA wa Bunge wote ni VICHEKESHO vya uongozi katika nchi hii. Tumefika hapa kutokana na katiba ya hovyooo tuliokuwa nayo. Lazima Muswada wa Katiba ya Warioba ifanyiwe kazi haraka.
 
Back
Top Bottom