Siwaelewi CCM: Magufuli alipopiga marufuku mikutano ya kisiasa walipongeza, sasa hivi Samia kairuhusu wanapongeza pia!

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Kwa kweli sielewi kabisa misimamo ya wana-ccm, wakati ule mara tu alipoingia madarakani mwaka 2016, Rais wa wakati huo, Hayati Magufuli, alipopiga marufuku mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa, huku akijua wazi kuwa anaisigina Katiba ya nchi, walijitokeza wana-ccm kibao, waliopongeza hatua hiyo na kuiita ya kishujaa na kuvisihi vyama vya upinzani, vikachape kazi, Kwa kuwa muda wa kufanya siasa ulikuwa umekwisha!

Nimeshangazwa pia safari hii, wakati Rais wa awamu ya 6, Samia Suluhu Hassan, alipoiruhusu mikutano hiyo na akaeleza wazi kuwa ni ukiukwaji wa Katiba kuipiga marufuku mikutano hiyo, Kwa kuwa ni haki yao kikatiba, vyama hivyo kuifanya mikutano hiyo na wao kama Serikali, Kwa kutumia Jeshi lake la Polisi, wajibu wao mkubwa, ni kuilinda mikutano hiyo, Ili ifanyike Kwa njia ya amani na utulivu.

Nimeshangazwa pia kuwaona wana-ccm wale wale, wakitoa pongezi nyingi Kwa Rais Samia na kusema kuwa huyu mama ni mwana-demokrasia, Kwa hiyo anapaswa kupewa pongezi nyingi Sana!😎

Ndipo hapo ninapojiuliza hivi Hawa wana-ccm wanajielewwa kweli?

Ni kwanini wakati ule Mwenyekiti wao wa CCM, ambaye pia alikuwa ndiye Rais wa nchi, alipopiga marufuku mikutano hiyo, hawakuweza kumuhoji kuwa kitendo anachofanya, ni Cha kukiuka waziwazi Sheria za vyama vya kisiasa nchini, kama walivyofanya viongozi wa upinzani na kueleza wazi kuwa Mwenyekiti wa CCM, anatumia vibaya madaraka yake, Kwa kuvinyima haki yao ya kikatiba ya kufanya mikutano hiyo ya hadhara?

Tabia hii ya ukinyonga na unafiki inayofanywa na viongozi wa CCM, ambao wanashindwa kuwa na msimamo mmoja, ndiyo inayoweza kuliangamiza Taifa letu!

Mungu ibariki Tanzania
 
Tabia hii ya ukinyonga, inayofanywa na viongozi wa CCM, ambao wanashindwa kuwa na msimamo mmoja, ndiyo inayoliangamiza Taifa letu!

CCM chama dola ndiyo maana hakina misuguano ya idioloji wao wanafuata dola imesema nini hawana misimamo ya chama halisi cha kisiasa.

CCM ingekuwa chama halisi cha kisiasa kungetokea makundi ya mgawanyiko wale wahafidhina na wale maridhiano na chama kipya kingezaliwa kutokana na waliofukuzwa CCM au walioamua kujitoa kwa hiyari kwa kuwa wanaamini ktk mojawapo ya mirengo iwe uhafidhina au maridhiano.

Historia ya chama rafiki cha CCM kule China kilipasuka na kutokea vyama viwili kwa kuwa kilikuwa chama cha kweli cha kisiasa kabla ya mwaka 1927. Hii ililetwa na kuwepo mitazamo mizito kinzani baina ya makada chama kikagawanyika. CCM siyo chama cha kisiasa ni mkusanyiko wa watu wasio na agenda wala itikadi.

GlobalSecurity.org
https://www.globalsecurity.org › cc...
History of the Chinese Communist Party (CCP)

4 May 2022 — In early 1927 the Guomindang-CCP rivalry led to a split in the revolutionary ranks. A new policy was instituted calling on
 
Kwa kweli sielewi kabisa misimamo ya wana-ccm, wakati ule mara tu alipoingia madarakani mwaka 2016, Rais wa wakati huo, Hayati Magufuli...
Wewe ndio huwaelewi wana Siasa. Kwani Usiwaamini Wana Siasa ni waongo karibu wote Wana Siasa ni watu wanaosema maneno ya uongo.

Leo Rais Samia Suluhu ameruhusu wana Siasa waendeshe Siasa zao kesho au keshokutwa huyo huyo Rais Samia Atapiga marufuku mikutano ya wana Siasa ndio maana ikaitwa neno Siasa ni uongo mtupu usiwaamini wana siasa ni waongo .
 
Wewe ndio huwaelewi wana Siasa. Kwani Usiwaamini Wana Siasa ni waongo karibu wote Wana Siasa ni watu wanaosema maneno ya uongo. Leo Rais Samia Suluhu ameruhusu wana Siasa waendeshe Siasa zao kesho au keshokutwa huyo huyo Rais Samia Atapiga marufuku mikutano ya wana Siasa ndio maana ikaitwa neno Siasa ni uongo mtupu usiwaamini wana siasa ni waongo .
Hata hivyo huo uongo wa wana-ccm umepitiliza😀
 
Hata hivyo huo uongo wa wana-ccm umepitiliza😀
Uongo wa Wana Siasi wa CCM umepitiliza kiwango kutokana wanatawala nchi Wana Siasa wa CCM. Kesho au keshokutwa ikitokea chama cha Upinzani kinatawala nchi na wao pia watasema maneno ya uongo huo huo kifupi tu usiwaamini wana Siasa yoyote yule. Hata akiwa baba yako Mzazi ni mwana Siasa usimuamini kabisa atakuwa anakuongopea kisiasa
 
Si tawala wala upinzani bali wanasiasa ndivyo walivyo

Chadema enzi zile kiliutangazia umma kuwa Lowassa ni fisadi papa na mpaka kwenye website ya chama list ya mafisadi papa Lowassa alikuwemo, wanachama walishangalia na wakaunga mkono

2015 Lowassa ktk chaguzi za ndani akakatwa CCM na kuhamia Chadema, wanachama walewale wakamshangilia na kumpokea kisha wakampa tiketi ya kugombea urais

Lissu na Lema walikimbia nchi kwa kusema Jpm anawawinda, lakn leo ni mwaka wa pili JPM hatunae na vijamaa bado vimelowea ubeberuni

Hapo unaweza kuona kiwango cha uongo na unafiki huku upinzani
 
Kwa kweli sielewi kabisa misimamo ya wana-ccm, wakati ule mara tu alipoingia madarakani mwaka 2016, Rais wa wakati huo, Hayati Maguful...
Hawana tofauti na sigara kali
IMG-20230104-WA0110.jpg
 
Si tawala wala upinzani bali wanasiasa ndivyo walivyo

Chadema enzi zile kiliutangazia umma kuwa Lowassa ni fisadi papa na mpaka kwenye website ya chama list ya mafisadi papa Lowassa alikuwemo...
Huyo Lema na Lissu kuishi huko ubeberuni kunakupunguzia nini mbona kama unatumia sana?

Au ndio sababu ya gharama za maisha kua kubwa na umeme kua wa mgawo huku kukiwa na uhaba mkubwa wa maji
 
Kwa kweli sielewi kabisa misimamo ya wana-ccm, wakati ule mara tu alipoingia madarakani mwaka 2016, Rais wa wakati huo, Hayati Magufuli...
Tunaambiwa CCM unaweza kupewa nafasi kwani huku kichwani ubongo hawana!

Wengi ni zero brain hata ukimsikiza wasemayo hapo bungeni utajua tu! Na ndio maana wanaendelea kuwakumbatia COVID 19!


Sent from my T810S using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom