Siungi Mkono muundo wa bunge Maalumu la katiba unaojumuisha wabunge la jamhuri ya Muungano!

ungonella wa ukweli

JF-Expert Member
Mar 27, 2012
4,210
555
Ndugu wana jf, kama mjuavyo taifa letu liko katika mchakato mzima wa kujipatia katiba mpya! Ingawa kwa sasa kuna sintofahamu juu ya sheria ya mabadiliko ya katiba iliyopitishwa juzi bungeni kwa wabunge wa ccm na mzee mrema, kuna hili bunge maalumu kama inavyojulikana kuwa wajumbe wa bunge hilo wanatarajiwa kuwa ni wabunge wa bunge la muungano, wajumbe wa baraza la wawakilishi na wajumbe 166 watakaoteuliwa na rais kama muswada wa sasa unavyosema! Wasiwasi wangu zaidi upo kwa wabunge, kama watanzania wenzangu mjuavyo wabunge wetu wamekaa kimipasho zaidi, wengi masuala ya kitaifa huyachukulia kichama zaidi,tumeshuhudia wabunge wengi wakiuchapa usingizi mchana kweupe wakiwa bungeni badala ya kuwawakilisha wananchi waliowachagua, pia watanzania ni mashahidi wabunge wetu wengi ni wavivu wa kuchambua nyaraka za serikali bungeni, pia wabunge wetu ni mabingwa wa mipasho na lugha za matusi bungeni badala ya kujenga hoja kwa maslahi mapana kwa taifa letu, pia bunge letu la sasa limejaa ushabiki wa vyama badala ya utaifa zaidi, mbaya zaidi asilimia kubwa ya wabunge wetu ni watuhumiwa wa wauzaji wa madawa ya kulevya, pia wabunge wengi wameingia bungeni kwa rushwa za hapa na pale. Bunge lililopita tumeshuhudia ngumi za waziwazi bungeni. Je kwa mapungufu hayo hapo juu, je kweli watu hawa wanaweza kuwawakilisha watanzania kwenye bunge maalumu la katiba? Binafsi siwaamini watu hawa hata kidogo! Watanzania wenzangu kwa muundo huu wa bunge maalumu ni bure kabisa! Nawasilisha.
 
..."mbaya
zaidi asilimia kubwa ya
wabunge wetu ni watuhumiwa
wa wauzaji wa madawa ya
kulevya"...

...katiba itakayotokana na mawazo ya Lusinde,Nkamia,Selukamba,Komba,Mwingula,Wasira,Lukuvi!!!!???...itakuwa ni katiba ya kuliandalia taifa majanga zaidi...
 
nimejiuliza pia wabunge mia sita hadi kila mmoja aje aingee ni lini alafu hao wabunge
Komba
Lusinde
Nchemba.....
na hao pia watakuwemo?
 
Hukutoa mapendekezo yako!
Sasa mkuu hilo litakuwa ni bunge maalumu la katiba kweli?
watu kujibadilisha "chupa huku soda ni ile ile"?
Hatuwezi kupata katiba bora bali tutakayoipata itakuwa ni ya watawala badala ya wananchi.
Si tumeshaona vituko?
Napendekeza kila mkoa Tz atoke mbunge mmoja tu kwa wabuge na wawakilishi wa sasa kuchunjwe na wananchi wao wakipita sawa.

Idadi kubwa ya wajumbe wa bunge la katiba litoke kwenye makundi mengine kama taasisi za kidini,walemavu,taasisi za kisomi na kitaaluma,vyama vya wafanyakazi na wakulima,asasi za kiraia na wanaharakati,wawakilishi wa vyama vya siasa vilivyosajiliwa,jamiim ndogondogo zisizokuwa na wawakilishi kama wahadzabe n.k.na sio wabunge na wawakilishi wa sasa kuhodhi ujumbe bunge la katiba.
 
Na ndo hao tayari wanaharibu bunge la katiba sasa.kama wale wa kuteuliwa ndio hawafai kabisa kazi yao ni kuongeza idadi ili kukandamiza hoja za watu makini.
 
Back
Top Bottom