MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Urambo Mashariki, Tabora, kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samuel Sitta, ameelezea kushangazwa na kauli za baadhi ya wagombea wa vyama vya upinzani kwamba watafuta kodi na kufafanua kwamba hakuna serikali ya aina hiyo duniani.
Sitta ambaye Spika wa Bunge la Tanzania lililomalizika hivi karibuni pia aliwataka wananchi wasihadaiwe na wagombea wa vyama vya upinzani ambao wamekuwa wakitoa lawama badala ya kueleza wakipewa madaraka watafanya nini.
Akizindua kampeni za CCM katika jimbo hilo katika Kata ya Usoke, mbali na kuomba kura ili aendelee kuwa Mbunge, pia alimuombea kura mgombea wa urais wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete na wagombea wa udiwani wa chama ahicho.
Hotuba za wapinzani zimejaa lawama na kutumia lugha za matusi mambo yanayodhihirisha kuwa hawana sera walizoziandaa kama dira ya kuwatumikia wananchi endapo watachaguliwa katika uchaguzi mkuu ujao, alisema Sitta.
Mbali na kushangazwa na kauli hizo za kufuta kodi, Sitta ambaye alikuwa akishangiliwa na wananchi hao pia alielezea kushangazwa na ahadi za wapinzani za kutoa huduma ya elimu na afya bure.
Kutokana na hadaa hizo, Sitta aliwataka wananchi kuwapuuza wapinzani kwa kuwa wameonesha hawana ukomavu katika ulingo wa siasa na hawajui wananchi wa jimbo hilo wanahitaji mambo gani ya msingi katika kuwaboreshea maisha yao.
Mimi ni gia kubwa, msichague gia ndogo zitawachelewesha kupata maendeleo zaidi kutoka hapa tulipofikia katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Nimekuwa kiongozi wa Bunge na nimetambulika ndani na nje ya nchi na nimeliwezesha Bunge kujijengea heshima kubwa kitaifa na kimataifa, nimejenga uhusiano mzuri na viongozi wa kitaifa na nitatumia fursa hiyo kujenga hoja za kuharakisha maendeleo katika Jimbo la Urambo Mashariki, alisema Sitta alipokuwa akielezea rekodi yake.
Aliwasisitiza wananchi waliohudhuria uzinduzi huo kutofanya mzaha katika kupiga kura kwa kuwachagua viongozi goigoi wasio na uwezo wa kujenga hoja na kushindanisha sera na badala yake wajitokeze kwa wingi wawachague wagombea wa CCM.
Sitta alisema, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita akishirikiana na mkewe, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta wamekuwa wakiwasomesha watoto yatima 200 kwa kuwalipia ada na mahitaji mengine.
Aliahidi kuwa atawasomesha watoto yatima 40 wanaomaliza darasa la saba kila mwaka, ili wasikose elimu ambayo ni haki yao ya msingi kwa kisingizio cha kukosa fedha za kulipia ada pamoja na mahitaji mengine ya msingi.
Mbali na ahadi hizo, pia alielezea mafanikio ya uongozi wake katika miaka mitano iliyopita ukiwepo mradi wa matrekta madogo aina ya power tiller yaliyogawiwa katika kata zote za jimbo hilo ambao ulitokana na jitihada zake binafsi.
Soma maoni ya wasomaji kwenye link hii hapa, utafurahi mwenyewe lol
HabariLeo | Sitta: Wananchi msidanganyike
Sitta ambaye Spika wa Bunge la Tanzania lililomalizika hivi karibuni pia aliwataka wananchi wasihadaiwe na wagombea wa vyama vya upinzani ambao wamekuwa wakitoa lawama badala ya kueleza wakipewa madaraka watafanya nini.
Akizindua kampeni za CCM katika jimbo hilo katika Kata ya Usoke, mbali na kuomba kura ili aendelee kuwa Mbunge, pia alimuombea kura mgombea wa urais wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete na wagombea wa udiwani wa chama ahicho.
Hotuba za wapinzani zimejaa lawama na kutumia lugha za matusi mambo yanayodhihirisha kuwa hawana sera walizoziandaa kama dira ya kuwatumikia wananchi endapo watachaguliwa katika uchaguzi mkuu ujao, alisema Sitta.
Mbali na kushangazwa na kauli hizo za kufuta kodi, Sitta ambaye alikuwa akishangiliwa na wananchi hao pia alielezea kushangazwa na ahadi za wapinzani za kutoa huduma ya elimu na afya bure.
Kutokana na hadaa hizo, Sitta aliwataka wananchi kuwapuuza wapinzani kwa kuwa wameonesha hawana ukomavu katika ulingo wa siasa na hawajui wananchi wa jimbo hilo wanahitaji mambo gani ya msingi katika kuwaboreshea maisha yao.
Mimi ni gia kubwa, msichague gia ndogo zitawachelewesha kupata maendeleo zaidi kutoka hapa tulipofikia katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Nimekuwa kiongozi wa Bunge na nimetambulika ndani na nje ya nchi na nimeliwezesha Bunge kujijengea heshima kubwa kitaifa na kimataifa, nimejenga uhusiano mzuri na viongozi wa kitaifa na nitatumia fursa hiyo kujenga hoja za kuharakisha maendeleo katika Jimbo la Urambo Mashariki, alisema Sitta alipokuwa akielezea rekodi yake.
Aliwasisitiza wananchi waliohudhuria uzinduzi huo kutofanya mzaha katika kupiga kura kwa kuwachagua viongozi goigoi wasio na uwezo wa kujenga hoja na kushindanisha sera na badala yake wajitokeze kwa wingi wawachague wagombea wa CCM.
Sitta alisema, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita akishirikiana na mkewe, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta wamekuwa wakiwasomesha watoto yatima 200 kwa kuwalipia ada na mahitaji mengine.
Aliahidi kuwa atawasomesha watoto yatima 40 wanaomaliza darasa la saba kila mwaka, ili wasikose elimu ambayo ni haki yao ya msingi kwa kisingizio cha kukosa fedha za kulipia ada pamoja na mahitaji mengine ya msingi.
Mbali na ahadi hizo, pia alielezea mafanikio ya uongozi wake katika miaka mitano iliyopita ukiwepo mradi wa matrekta madogo aina ya power tiller yaliyogawiwa katika kata zote za jimbo hilo ambao ulitokana na jitihada zake binafsi.
Soma maoni ya wasomaji kwenye link hii hapa, utafurahi mwenyewe lol
HabariLeo | Sitta: Wananchi msidanganyike