Sitta: Sikukejeli vielelezo vya Dk Slaa kuhusu BoT

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Sitta: Sikukejeli vielelezo vya Dk Slaa kuhusu BoT

*Asema hakuvionyesha vyote kwenye televisheni
*Ataka wabunge watoe hoja hata kama ushahidi wao si asilimia 100
*Slaa asema propaganda za Spika, Makada wa CCM zimewaumbua
*Serikali yajikanganya kuhusu kurejeshwa Daudi Ballali


Na Joyce Mmasi

SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta, ameibuka na kupinga madai yanayoelekezwa kwake kuwa alivikejeli vielelezo vya Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk Wilbrod Slaa kuhusu tuhuma za ufisadi katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Vielelezo hivyo viliwasilishwa na Dk Slaa bungeni alipowasilisha hoja binafsi ya kutaka iundwe kamati ya bunge kukagua mahesabu ya BoT na baadaye kuiondoa baada ya kuhisi kwamba hatatendewa haki. Akizungumza na gazeti hili jana, Sitta alikana akisema kuwa tatizo hapo ni waandishi wa habari wenye tabia ya kuchonganisha watu.

"Hapa tatizo lipo kwa waandishi wa habari, wanakuwa na kitu kama kuchonganisha, wanapenda kuandika kile wanachoamini, wanachosikia au kupenda wao," alisema Sitta. Alipotakiwa kufafanua msimamo wake wa wakati huo, hasa baada ya kubainika kuwa baadhi ya hoja za Dk Slaa zimebainika ni za kweli, Sitta alisema; Mimi sikuwa nazungumzia ukweli au uongo wa hoja ya Dk Slaa, nilizungumzia kuhusu utaratibu wa kuziwasilisha hoja bungeni," alisema na kuongeza; "Kwa mfano, Dk Slaa alipeleka vielelezo vyenye kurasa 1,000, barua na vielelezo vingi kutoka kwenye mitandao ya komputa.

Haikuwa rahisi kwangu kuweza kuvipitia kwa wakati huo, hivyo niliomba nipatiwe muda zaidi ili niweze kuviangalia na kujiridhisha na niweze kutenda haki. "Naomba ifahamike tu kuwa, si kazi ya mbunge kupeleka hoja yenye uhakika kwa asilimia 100, ni hoja yoyote yenye mashaka juu ya jambo fulani, lakini tunachozungumzia hapa ni muda wa kuifanyia kazi.

"Mfano, moja ya kielelezo kilimtaja waziri mmoja kwa jina kuwa alitaka kupewa mgawo wake na mambo mengine ambayo mimi niliona hayana haja kuwepo kwenye vielelezo vile, nikamwambia Dk Slaa si lazima vielelezo vyote viende, sasa kama barua moja ilitiliwa mashaka haimaanishi kuwa tulitilia mashaka vielelezo vyote," alisema Sitta.

Spika huyo aliongeza kuwa, kama Slaa angepeleka au kuacha hoja yake kwa ajili ya kikao kingine cha bunge, yeye angeifanyia kazi na si kuitupa kapuni. Lakini pia Sitta alieleza kushangazwa kwake kusikia hoja hiyo ikizungumziwa mahali pengine nje ya bunge. Sitta aliongeza kuwa baada ya kupokea vielelezo vya Dk Slaa alikuwa amejiandaa kuvipeleka kwa wataalam wa kuvichunguza, jambo ambalo hakulifanya baada ya hoja hiyo kuondolewa bungeni.

Dk Slaa aliamua kuichomoa hoja yake baada ya kupata taarifa kuwa kulikuwa na mpango wa kumdhibiti kama ilivyofanyika kwa Mbunge mwenzake wa Chadema, Zitto Kabwe, ambaye alisimamishwa kazi za bunge kwa kuwasilisha hoja binafsi dhidi ya Waziri Nazir Karamagi kuhusu utiaji saini mkataba wa Mgodi wa Buzwagi.

Baada ya Dk Slaa kuchomoa hoja hiyo, aliamua kuitangaza kwa umma kupitia mikutano ya hadhara, huku Spika Sitta akionekana hadharani kwenye moja ya vipindi vya Televisheni ya Taifa akionyesha baadhi ya vielelezo vya hoja hiyo na kuviponda kuwa ni vya kibabaishaji na kuahidi kuvipeleka polisi kuchunguzwa.

Akizungumzia suala hilo, Dk Slaa alisema hana mpango wowote wa kumchukulia hatua Spika Sitta na badala yake wananchi ndio watakaoamua baada ya kuona ukweli wa hoja yake dhidi ya kauli za propaganda zilizokuwa zikitolewa na Sitta na viongozi wengine wa Chama Cha Mapinduzi. "Nitamshitaki kwa wananchi, na si yeye tu hata Makamba (Katibu Mkuu wa CCM), Aggrey Mwanri na Seif Khatib.

Wote hawa walionekana kutetea ufisadi ule na kutangaza propaganda za chama chao, lakini sasa wanaona aibu kutokana na ukweli kuwekwa hadharani," alisema Dk Slaa. Mbunge huyo ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), aliongeza kuwa anachokiona sasa ni umuhimu wa kuitazama upya nafasi ya Spika kwa kuwa inahitaji kushikiliwa na mtu asiye na masilahi na chama chochote cha siasa.

"Spika wetu anafanya kazi kwa masilahi ya CCM kutokana na yeye kuwa kada wa chama hicho. Tunachotaka sasa ni kuwa mtu akichaguliwa kuwa Spika hata kama alitokana na chama fulani asiruhusiswe tena kufungamana na kazi za chama ili awe huru. Hii itasaidia kumpa nafasi ya kutokuwa na upande kama ilivyo sasa ambapo Spika anaonekana kuwa upande wa CCM na serikali yake hata kama inakosea."

Alisema, Spika amekuwa shabiki wa CCM na amekuwa akipeleka hoja zinazojadiliwa na wabunge kwenye vikao vya CCM na hali hiyo akaifananisha na kuwa mwamuzi anayependelea upande mmoja wa timu huku akitaka kuonyesha haki katika kuchezesha mchezo.

Wakati huo huo; hatima ya kurejeshwa nchini kwa Gavana wa Benki Kuu (BoT) aliyetimuliwa, Daud Ballali ambaye inasemekana yuko Marekani kwa matibabu bado ni kitendawili baada ya watendaji kutupiana mpira kuhusu nani anahusika kutoa amri hiyo.

Awali, ilielezwa kuwa, vyombo vya kiintelejentsia vilipewa agizo na Rais Jakaya Kikwete kumrejesha Ballali nchini kufuatia wananchi kutaka kumwona, lakini vyombo hivyo vikashindwa kutekeleza agizo hilo kwa kile kilichoelezwa kuwa amri hiyo haikufuata taratibu.

Vyombo hivyo vilielezwa kuwa mtoaji agizo angekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Philip Marmo na si Rais mwenyewe, lakini Marmo alipoulizwa kuhusu taarifa hizo akasisitiza kuwa hafahamu lolote na hana taarifa kuhusu alipo Ballali. "Mimi nasikia tu kama wewe, sijui yuko wapi na kwa kweli niko safarini, sasa na sina taarifa ya kwamba natakiwa kutoa agizo hilo," Marmo aliliambia gazeti hili jana.

Jitihada za gazeti hili kubaini kama kuna jitihada zozote zilizokuwa zikifanywa na serikali kuhusu kurejeshwa kwa Ballali nchini, zilionyesha kuwa, kuna kazi iliyokuwa imeanza, lakini ikakosa baraka kufuatia kuwepo vyombo vingi vinavyotakiwa kujumuishwa kabla ya kufikia uamuzi wa ama kumrejesha au kumuacha huko aliko.

"Unajua Ballali ana mambo mengi sana ambayo hata sisi tunamtaka atusaidie, hivyo basi akipatikana mambo mengi zaidi yatawekwa hadharani," chanzo chetu kimoja kilieleza na kuongeza kuwa; "Kutokuwepo kwake hapa nchini, inaonyesha kama anageuzwa jalala la kila uchafu. Kila aliyefanya uchafu katika masuala ya fedha katika Benki Kuu anaelekeza shutuma kwake."

Aidha, taarifa zinaeleza kuwa, ujio wa Ballali utasaidia kutoa taarifa za kweli kuhusu kilichobainishwa na ukaguzi wa Kampuni ya Ernest and Young iliyofanya uhakiki wa hesabu za BoT katika Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA) na kubaini upotevu wa Sh133 bilioni.

Taarifa hizo zinaongeza kuwa, mbali na kuwasaidia kupata taarifa zinazohitajika, Ballali anatakiwa kuwekwa katika ulinzi ili asije akadhuriwa na hao waliohusika katika upotevu huo wa Sh133 bilioni pamoja na zile ambazo hazijakaguliwa, ambao wamekuwa wakimtupia lawama au kuhofu kuwa anaweza kuwachifua. "Unajua 'brother' hawa jamaa wanaweza kumfanyia lolote Ballali kabla sisi hatujapata lolote katika mambo yetu, hivyo anahitaji kuwa katika mikono yetu salama," alisema.

Chanzo chetu kingine kilieleza kuwa, mmoja wa wahusika katika kundi linalotakiwa kutoa maamuzi ya ama Ballali arejeshwe au kuachwa ni Kamishna wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Robert Manumba. Kamishna huyo alipoulizwa kuhusu nafasi yake na maamuzi aliyokwisha kuyafikia alisema; "Muulize mwenyekiti ambaye ni Mwanasheria Mkuu, ndiye mwenyekiti wa Kamati, hebu muulize huyo ndiye msemaji."

Hata hivyo, Johnson Mwanyika ambaye ni Mwanasheria Mkuu hakuweza kupatikana jana kufuatia kuwepo taarifa kuwa yuko likizo na pia simu yake kubakia kuita bila kupokewa.. Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utoh, alipoulizwa kama mmoja wa wajumbe waliokabidhiwa jukumu la kuhakikisha wanawafuatilia waliohusika na ubadhirifu wa fedha za BoT, jukumu walilopewa na Rais Kikwete alisema; "Mimi si mjumbe wa kamati, kama suala ni kutazama kuhusu kamati inayohusika na jambo hili la BoT tafadhali jaribu kuwatafuta wajumbe wengine waliomo katika kamati hiyo."

Utoh alitangazwa kuwa mjumbe wa kamati hiyo na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo. Wajumbe wengine walitajwa ni; Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hosea, Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema na Johson Mwanyika. Kamati hii ilipewa miezi sita ya kukamilisha zoezi zima la kufuatilia waliohusika na utafunaji huo mkubwa wa fedha za umma.

Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa tata hasa kutoka kwa viongozi wa upinzani zikieleza kuwa, Ballali amehama kutoka Boston, Marekani kwenda katika visiwa vya Malta. Taarifa hiyo ilitolewa siku moja baada ya kuelezwa na Marekani kuwa imefuta viza ya Ballali huku msemaji wa masuala ya Habari wa Ubalozi wa Marekani nchini, Jaffery Salaiz, akieleza kuwa hana uhakika wa alipo Ballali.

Kwa mujibu wa taratibu za Marekani, Idara ya Mambo ya Nje ndiyo inayohusika na masuala ya viza na mtu anapoingia ndani ya nchi hiyo hubakia chini ya Wizara ya Ulinzi wa Ndani na anaweza kutolewa humo kama idara hizo mbili zimehusishwa kwa pamoja na sio moja peke yake
.
 
SPIKA FISADI SITTA: ""SIKUKEJELI VIELELEZO VYA DK SLAA KUHUSU BOT""

WANAFORUM HABARINI MKO MLIKO SALAMU ZAO KWA WALIO NJE YA TANZANIA,,,HUKU TUNASHUKURU MUNGU TUNAZIDI KUPATA VIOJA NA VIJIMAMBO VYA 2008:KWA WALE MSIONAMENO TUBAKI KU SMILE SOMENI VIOJA HIVI

GAZETI LA MWANANCHI:J2:TAR:20:01:2008
SPIKA WA BUNGE LA TANZANIA SAMUEL SITTA AMEIBUKA NA KUPINGA MADAI ALIVIKEJELI VIELELEZO VYA ...MH:DK:pADRE:MJASIRIAMALI HALISI:MSEMAKWELI:""WILLBROD SLAA".VIELELEZO HIVYO VILIWASILISHWA NA DK SLAA ALIPOWASILISHA HOJA BINAFSI KUTAKA IUNDWE KAMATAI KUCHUNGUZA BOT,
AKIZUNGUMZA SITTA ALISEMA TATIZO LIPO KWA WAANDISHI HABARI KUCHONGANISHA WATU;ALIPOHOJIWA BAADA YA KUGUNDULIKA HOJA ZA "SILAAA""NI ZA KWELI ALIDAI ATI MIMI SIKUWA NAZUNGUMZIA UKWELI AU UHONGO WA HOJA YA SLAA BALI UTARATIBU WA KUWASILISHA HOJA BUNGENI,

"""TEEHE TEEEH TTEEEH" SIKIA HIYO""MPFANO ALIPELEKA VIELELEZO VINGI TOKA KWENYE INTERNET BAUA ZA KURASA 1000TOKA KWENYE MITANDAO YA KOMPUTA..SIKUWA NA MUDA KUVIPITIA VYOTE NA KURIDHIA NI KWELI AMA UOWONGO NIWEZE KUTENDA HAKI.NAOMBA IFAHAMIKE TU KUWA ""SI KAZI YA MBUNGE KUPELEKA HOJA YENYE UHAKIKA ALIMIA 100""NI HOJA YOYOTE TUNACHOZUNGUMZIA HAPA NI MUDA WA KUIFANYIA KAZI,.MFANO KUNA KIELELZO KILIMTAJA WAZIRI MMOJA ALITAKA KUPATA MGAWO WAKE NA MENGINEYO MIMI NILIONA HAYANA HAJA KUWEPO KWENYE VIELELEZO,,SPIKA HUYO AMEDAI KAMA SLAA ANGEACHA HOJA YAKE KWA KIKAO KIJACHO ATI ASINGEIWEKA KAPUNI,,,SITA ALISHANGAA KUSIKIA HOJA HIYO IKIZUNGUMZIWA NJE YA BUNGE,,ALIDAI ALIPANGA KUVIPELEKA KWA WATAALAMU WA KUVICHUNGUZA ,,HAKUFANYA HIVYO BAADA YA HOJA KUTOLEWA BUNGENI;;DK SLAA ALIFANYA HIVYO BAADA YA KUSIKIA KUNA MPANGO WA KUMTENDA KAMA WALIVYOMTENDA PROF "ZITTO" BAADA YA DK SILAA KUCHOMOA HOJA BUNGENI ALIAMUA KUITANGAZA KWA UMMA KUPITIA MIKUTANO YA HADHARA,,HUKU SPIKA AKIONEKANA ADHARANI KWENYE TVT AKIONYESHA VIEELELEZO ALIVYOVIITA BATILI NA KUVIPONDA NI VYA UBABAISHAJI NA KUHAIDI KUVIPELEKA POLISI,,,
AKIZUNGUMZIA HILO DK SILAA YEYE AMESEMA YEYE HANA HAJA YA KUMHUKUMU SPIKA WANANCHI NDIO WATAKAOMWADHIBU BAADA YA KUONA UKWELI WA HOJA YAKE DHIDI YA PROPAGANDA ZILIZOKUWA ZIKITOLEWA NA SSITA SPIKA WA """BUNGE LA JAMHURIII YA MUUNGANO WA TANZANIAAAA"""AKINUKULIWA SILAA ALISEMA NITAMSHITAKI KWA WANANCHI NA SI YEYE TU HATA MAKAMBA WOTE HAWA WALIONEKANA KUTETEA UFISADI ULE NA KUTANGAZA PROPAGANDA ZA CHAMA CHA MAFISADI LAKINI SASA WANAONA AIBU SILAA AKINUKULIWA ANASEMA KUNA UMUHIMU SASA WA KUITAZAMA UPYA NAFASI YA USPIKA KWA KUWA INAHITAJI KUSHIKILIWA NA MTU ASIE NA MASILAHI NA CHAMA CHOCHOTE..HIIKI NI CHEO MUHIMU KWA WANANCHI HASA UKIANGALIA YALIOTOKEA JUU YA UFISADI WA BOT WATANZANIA MLIWASIKIA NA MATUSI HAYO NA WENGINE KUONEKANA KWENYE TVT LEOO HII WANAJIKANA NAFSI ZAO
 
Hah! hah! hah! Spika alikuwa wapi siku zote hizo kutoa ufafanuzi huu? Kaona mambo yamegeuka ndio anajidai hakumkejeli Mheshimiwa Slaa. NA bado, watasema yote
 
kazi si kidogo embu angalia huyu fisadi mwingine asivyo nahaya bado anajitetea wakati hadi watoto wameangalia kwenye tvt aliyokuwa akikanusha,,mi nashauri hawa watu wakae kimya kupunguza dhambi zao uko juu
 
Sitta hana maslahi kwa Watanzania hata kidogo . hebu tupitie kote aliko pita hadi kuja kwua speaker tuone kama kweli kalitendea taifa langu haki .
 
No! that cant be true..its serious. How can he dare say that!!!Hivi vyombo vyahabari viki_replay ikadhibitishwa kuwa anachosema sicho? Kuna hatua zozote ..!!

AND:

Administrator..or anybody: unganisha hizi threads. Re: Beaking news(about spika Sitta) na hii Sitta: Sikukejeli vielelezo vya Dk Slaa kuhusu BoT
 
No! that cant be true..its serious. How can he dare say that!!!Hivi vyombo vyahabari viki_replay ikadhibitishwa kuwa anachosema sicho? Kuna hatua zozote ..!!

AND:

Administrator..or anybody: unganisha hizi threads. Re: Beraking news(about spika Sitta) na hii Sitta: Sikukejeli vielelezo vya Dk Slaa kuhusu BoT
 
kuna vitu vitatu ambavyo vimeniacha hoi
1. Spika na kauli yake!!
hawezi kurecall alivyoonekana kwenye luninga wakati ule?
hawa jamaa naona kula walichokicheua hadharani kwa si jambo la ajabu, na kutaka kuwafanya wananchi waamini kuwa walipiga miayo1

2.
vyombo vya kiintelejentsia vilipewa agizo na Rais Jakaya Kikwete kumrejesha Ballali nchini kufuatia wananchi kutaka kumwona
Jamani! yaani sababu kubwa ili wananchi wamuone!
halafu ili iweje? au huu ni mtazamo wa mwandishi mwenyewe?

3.
Vyombo hivyo vilielezwa kuwa mtoaji agizo angekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Philip Marmo na si Rais mwenyewe,
...."Mimi nasikia tu kama wewe, sijui yuko wapi na kwa kweli niko safarini, sasa na sina taarifa ya kwamba natakiwa kutoa agizo hilo," Marmo aliliambia gazeti hili jana.
.....Muulize mwenyekiti ambaye ni Mwanasheria Mkuu, ndiye mwenyekiti wa Kamati, hebu muulize huyo ndiye msemaji."
....Mimi si mjumbe wa kamati, kama suala ni kutazama kuhusu kamati inayohusika na jambo hili la BoT tafadhali jaribu kuwatafuta wajumbe wengine waliomo katika kamati hiyo."
Nani anatakiwa kutoa hilo agizo?
Je watendaji wakuu 'hawajui job descriptions' zao?
 
Fala mwingine, afie mbali. Watu kama Sitta ndio wanafanya mtu uchukie mpaka utumie lugha mbaya.

Yaani pamoja na ukweli wote na vyombo vya habari kumwonyesha akisema wazi, leo hii anajifanya Watanzania tumesahau?

Itafika siku Tanzania tutachapana bakora shauri ya watu kama hawa. Hivi
Sitta ana credibility yoyote iliyobaki?

Ilitakiwa angalau awe mwanaume na aseme alikosea lakini sio kuanza ku SPIN.
 
dat real men today newspaper mwananchi shame upon him,,walijua watanznaia ni mambumbu wa kutupa
but mungu siwa azimo jipya wala la kale mungu ni wa wote

ushindi lazima
 
Mi na shangaa vyombo vya habari wanavo mlea lea Six, huyu kwanini wasimuwekee marudio ya kipindi chake wamuumbue live?? yaani huyu mzee ni kisiki kikubwa sana katika mpambano wa ufisadi TZ, hasa pale anapo tumika kuwabana watetezi wetu bungeni! ananikera sana!
 
Kwani aliyesema kuwa vielelezo vyake vingi vina mashaka na ataviwasilisha polisi kwa uchunguzi nani kama sio Sita? Nani aliyemlinda Mzindakaya dhidi ya hoja ya Slaa kuwa jamaa ana maslahi katika mikopo ya BOT? Nani aliyetakiwa kutoa ruhusa ya kuiwasilisha hoja ya Slaa bungeni kama sio Sita? nini lilikuwa jibu lake..."vielelezo vya Slaa havikumridhisha" si ndio? Sasa leo anajaribu kujikosha kwa lipi? naona maji mengi yalishapita chini ya daraja and Mr. Speaker is too late.
 
mimi ningeshauri wabunge waanzishe hoja binafsi ya pika kusema uongo na yeye aadhibiwe kama alivyopanga kumwadhibu silaa akamuwahi,,,bado najiuliza kule bungeni kazi yao nini jamani??????
again shame upon them
 
o...e it is.......
ni mshu=tuko mkumbo,,,kw atu mwenye heshima kaam yeye kujibu vioja kama hivyo....
 
Wana JF hapa kinachotakiwa ni real changes. lakini huyo Sita na wana-CCM wenzanke wote ni mafisadi na wanajitahidi kulindana kadri wanavyoweza kwa kutumia vyeo vyao. Yaani hiyo ni kuona kama Watanzania ni mbumbumbu hatujui kitu.
 
Kwa mwendo huu JK hatapata nafuu hata mara moja . Kama anadhani anajenga Nchi basi anajidanganya maana bora sisi tunao mwambia ukweli kila mara kuliko walio mzunguka . Kuna issues kibao Sitta kazi sababishia ubishi na ukweli unakuja.Akili ya Sitta na Meghji mimi sioni tofauti maana wote husema na wote hupinga kuto kusema .
 
kunapovuka moshi, kuna jambo. je sitta kaona nini? je wanasisiem kama muungwana wamemwaibisha? tutapata jibu hapa hapa.
 
Nina ngoja Slaa aje na hoja binafsi Bungeni na Zitto ili tuone nini kitatokea . By the way Mudhihiri yuko wapi ? Mzee wa Pekecha je naye kimya ?
 
Back
Top Bottom