Sitta: Marais watatu hapana, CCM iache kichwa ngumu iridhie serikali tatu

Huyu Sitta ni opportunist, tunakumbuka alikataa mwanzo Serikali tatu wananchi walioyeipendekeza katika maoni yao. Sasa ameona upepo haugeuzi uelekeo na yeye ameamua kuungana nasi kimwli lakini kiroho kuna kitu analenga. Huyu Mzee wa CCJ amechoka na anatakiwa apumzishwe maana majeraha ya kuukosa uspika au Uwaziri Mkuu bado yanamsumbua.

Tanganyika bila Zanzibar inawezekana!

tatizo si Samwel Sitta, tatizo ni kumbukumbu ndogo ya watu humu JF na kukurupuka bila kufanya research. Sitta tangu limeanza suala la katiba mpya yeye hoja yake ni kutotaka marais watatu.

Haya ni marudi tu ya kauli yake, na kwa sisi tunaokumbuka kauli yake ya kwanza ningeshangaa kama angesema tofauti na alivyosema.
 
Huyu Sitta ni opportunist, tunakumbuka alikataa mwanzo Serikali tatu wananchi walioyeipendekeza katika maoni yao. Sasa ameona upepo haugeuzi uelekeo na yeye ameamua kuungana nasi kimwli lakini kiroho kuna kitu analenga. Huyu Mzee wa CCJ amechoka na anatakiwa apumzishwe maana majeraha ya kuukosa uspika au Uwaziri Mkuu bado yanamsumbua.

Tanganyika bila Zanzibar inawezekana!

Jaribu kumsoma vizuri Sitta, pamoja kwamba awali alikataa, leo amekiri kwamba hoja nzito alizoziibua Warioba zimegeuza ukichwa ngumu na kukuali serikali tatu, ila tu lisilokaa vizuri nchi mmoja kuwa na marais watatu, hata mie limenishtua.
 
huyu MZEE NAMKUBALI SANA ILA ANA TATIZO LA KIGEUGEU MARA AISEME CCM VIBAYA KWA UBAYA KWELI MARA AISIFIYE KWA UNAFKI MARA AWAKUBALI UPINZANI.NAMTONYA SITA CCM SIO MAMA YAKE AJE CDM AWE HURU NA MAONI YAKE MAZURI
 
Warioba ni bonge la architect ambao wamepata kutokea nchi hii.
Maana ame design na kuichonga kwa umakini sana hii njia draft ya kuuvunjilia mbali huu muungano, akaweka hoja zisizoepukika hata kwa wenye akili za giza namna gani.
Menifurahisha tena hapa kwenye kubadili jina toka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hadi Shirikisho la nchi za Tanzania, hapa ni kuwa atakayeondoka hadi chake, and we all know nani atakuwa wa kwanza kuondoka.
 
Serikali tatu hazikwepeki. Kazi ya CCM sasa nikuangalia na kushauri majina na powers za hizi serikali. Naungana na 6 iwapo simwamini sana tuwe na Raisi Mmoja tu wengine wawe Waziri Mkuu au Makamu wa Raisi Tanganyika and Zanzibar
 
One new Country Tanganyika, Two head of states namely Tanganyika/Zanzibar Premieres and one President the President of URT. Ila kwa mamlaka watakayokuwa nayo hawa premiers sidhani kama President atakuwa na kibesi saana!

Kubadili jina la nchi ni pricey pointless. Ibakie hivi hivi tu, URT!
 
sisi kama watanzania hatuna shida na serikali tatu, tano au mia poa tu tunachotaka ni shule nzuri hospital nzuri mpaka vijijini hayo wanayogombania viongozi ni tamaa ya madaraka tu
 
Nakubaliana na Sitta kwenye hili la Marais watatu. Ilahili la yeye kusema amekuwa convinced na Warioba ........... yeye kama kiongoziwa serikali kwa miaka mingi tena akiwa na vyeo nyeti kama Uspika, Uwaziri wakatiba n.k. alitakiwa kuziona hizo kasoro siku nyingi.Anavyoibuka leo na kusema hivi inaonyesha ni jinsi gani propaganda za CCMzilivyoliharibu Taifa na ni aina gani ya viongozitulionao...................... they do not have independent mind rather theycannot speak their minds openly!!
mkuu msome sitta vizuri huyu ni miongoni mwa lile kundi la G55.
yaelekea kuna vitu vingi huvijui.
 
Zanzibar bila ya tanganyika inawezekana,msiwe waoga wa kuijadili tanganyika yenu anzeni sasa kujadili,zanzibar ipo na itaendelea kuwepo milele.
 
Hata Sita na lichwa ngumu. Ila nakubaliana na wewe juu ya seeikari tatu ongawa suluhisho la muumgano ni serikaei moja huko kwingine ni nyinyi ccm kutaka watu wawe na madaraka eti rais wa zanzibar na tanganyika. Wa nini one presida one government
 
SITTA ni mtu makini sana na ni mtu mwenye maono ya kisiasa,alilosma ni sawa kabisa na hapa anazingatia utaifa zaidi,nchi hizi ziwe za "SHIRIKISHO" na si za "MUUNGANO" ili nchi hizi ziwe huru na kujitgemea....iko wapi TANGANYIKA yetu hali wazanzibari wakiwa na ZANZIBAR yao...tunataka TANGANYIKA YETU enyi nnape na wenzio!
 
Mtazunguka sana lakini tatizo linafahamika na CCM hawataki kuli face, kwasababu wamewalea sana Wazanzibari.

Mworobani wa haya yote ILIKUWA SERIKALI MOJA, AMRI JESHI MMOJA.

Lakini kwakuwa Watanganyika tunawaogopa Wazanzibari mtapendekeza hata SERIKALI 20 lakini hamata waridhisha kamwe Wazanzibari, chokochoko zitaendelea na one day Muungano utavunjika tu.
Tuko kwenye dunia ambayo huwezi kusuppress fikra za wananchi kwa sasa. Watu wenye uwezo wa kufikiri na kuhoji kipi ni bora kwa jamii yao huwezi kutumia mabavu juu yao bali ni akili, hekima, busara na ujanja (hata kuwafool wakati mwingine). Huu mtazamo wako wa seriakli moja upo katika kundi la mabavu, ambao ni short term solution,hata ukifanikiwa leo ndani ya miaka michache ni crisis. Zanzibar kwa sasa wote viongozi kwa wananchi wanahitaji uhuru wa kuamua mambo yao wenyewe. Kuna idadi nzuri tu inayopenda muungano lakini pia freedom yao ya kujiamualia baadhi ya mambo ndo priority kwao.
 
sisi kama watanzania hatuna shida na serikali tatu, tano au mia poa tu tunachotaka ni shule nzuri hospital nzuri mpaka vijijini hayo wanayogombania viongozi ni tamaa ya madaraka tu

Hapo ndipo unapopotoka ndugu yangu, unamaanisha "we the people..." haina maana tena kwetu! Tusisingizie matatizo kama excuse ya kutokujadili katiba, inatuhuzu bana! Acheni kuwadanganya watu, tunahitaji katiba itakayo ainisha HAKi na WAJIBU wetu kama raia wa TZ. Katiba itakayo walazimisha wanasiasa kuheshimu haki zetu na si vinginevyo....

Haya mambo ya buku saba tuyaache ni upumbavu na tunawapa nafasi wanasisasa kututumia tu.

Happy new year...
 
Samweli Sitta ana mtazamo wa kitaifa zaidi katika kuangalia sura kamili ya rasimu ya katiba ilivyoandaliwa na Tume kuwa imekaa vema kwa misingi ya kuangalia kuondoa migongano iliyopo sasa na katiba ya Tanzania visiwani. Haoni shida kuwashushia shutuma wanachama wenzake wa CCM na msimamo wa chama kwa jumla kwa kuwaasa kuacha kichwa ngumu kwa kuwa ving'ang'anizi wa serikali mbili. Naona kati ya viongozi waandamizi ndani ya CCM na serikali Sitta kichwa chake kimetulia.


Kwani kuanza kumnadi mtu nako hakuondowi sifa ya kugombea huko CCM? Naona umelenga huko!
 
Mtazunguka sana lakini tatizo linafahamika na CCM hawataki kuli face, kwasababu wamewalea sana Wazanzibari.

Mworobani wa haya yote ILIKUWA SERIKALI MOJA, AMRI JESHI MMOJA.

Lakini kwakuwa Watanganyika tunawaogopa Wazanzibari mtapendekeza hata SERIKALI 20 lakini hamata waridhisha kamwe Wazanzibari, chokochoko zitaendelea na one day Muungano utavunjika tu.


Acha choyo na tamaa zako zikufanye ulaumu Wazanzibari. Mbona tulishasema kuwa hatutaki muungano nanyi mkangangania? Laumu jamaa zako na utuache Wazanzibari.
 
Back
Top Bottom