Serayamajimbo
Senior Member
- Apr 15, 2009
- 191
- 38
Tayari Kabuye ameshazikwa, Mungu amlaze mahali pema. Sasa nini kinasubiri kutangaza jimbo kuwa wazi? Leo ni tarehe 11 na Tume ya uchaguzi iliwahi kusema huko nyuma kuwa ikifika tarehe 15 Mei kama hakuna kiti kilichotangazwa kuwa wazi ndio hivyo tena hakuna uchaguzi mwingine wa marudio wa ubunge mpaka uchaguzi mkuu 2010. Je, CCM mnaogopa ya Tarime na Busanda ndio maana mmeamua kushirikiana na Sitta na Makame kuweka mpira kwapani?
Serayamajimbo
Serayamajimbo