Sitta: Hakuna wa kunifunga mdomo

Mohammed Hamad

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
3,988
1,301
Wednesday, 19 January 2011 21:53 0diggsdigg

Ramadhan Semtawa
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amekoleza moto wa sakata la kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans, akisema kamwe hawezi kufungwa mdomo kupinga malipo ya Sh94 bilioni kwa kampuni hiyo.Kauli ya Sitta imekuwa wakati kukiwa na taarifa kwamba waziri huyo pamoja na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe wamebanwa na Ikulu wakitakiwa wasizungumzie tena suala hilo.

Hata hivyo, akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana Sitta alisema, "Naomba wananchi wafahamu, siwezi kufungwa mdomo kuhusu kupinga malipo kwa kampuni ya kitapeli ya Dowans."

Sitta ambaye msimamo wake umeibua mjadala mzito nchini na hata ndani ya baraza la mawaziri, alisema hajawahi kutishwa wala kufungwa mdomo kuhusu msimamo wake.

Kauli hiyo ya Sitta imekuja siku moja tangu gazeti moja la kila siku (siyo Mwananchi) kuripoti kwamba Rais Jakaya Kikwete amemfunga mdomo, uamuzi uliodaiwa kufikiwa juzi katika kikao cha Baraza la Mawaziri, kilichofanyika Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Habari hizo zilidai kuwa Sitta na Dk Mwakyembe walikuwa na wakati mgumu kutetea hoja ya kutaka Serikali isiilipe Dowans na kwamba hata Rais alisema hafurahishwi na hukumu ya malipo hayo, hivyo kikao hicho kuwaamuru mawaziri hao kutozungumzia tena suala hilo hadharani.

Lakini jana Sitta alisema: "Nitaendelea kupinga malipo ya Dowans. Sijawahi kuitwa popote wala na mtu yeyote na kuambiwa nisizungumze suala hilo, hivyo wananchi wasifikiri nimebadili msimamo".

Aliongeza: "Taarifa zinazosambaa ni za kupikwa tu, zisije zikawapotosha wananchi wakidhani nimewasaliti katika hili, narudia tena sijafungwa mdomo."

Mbunge huyo wa Urambo Mashariki ambaye aliliongoza Bunge la Tisa katika vita dhidi ya ufisadi, alifafanua kwamba si suala la Dowans tu bali ataendelea kupinga mambo yote machafu kuhusu nchi.

Aliweka bayana kwamba nchi inahitaji viongozi wenye uwezo wa kusimamia vema maslahi ya taifa bila hofu ili kulinda haki za wananchi na kuboresha maisha yao.

Sitta alinukuliwa akihoji kile kinachoitwa kukiuka dhana ya uwajibakaji wa pamoja na kuweka bayana, kama dhana hiyo ingekuwa inaheshimika basi uamuzi wa kuilipa au kutoilipa Dowans ungefanywa kwa pamoja.

Alisema haiwezekani dhana ya uwajibikaji wa pamoja ifanyike bila kushirikisha wengine halafu mwisho itolewe taarifa ya uwajibakaji wa pamoja.

"Halafu kuna watu wanazungumzia nimekiuka dhana ya uwajibikaji wa pamoja, uwajibikaji wa pamoja ni lazima uamuzi ushirikishe wengine si mmoja kuamua halafu ifahamike ni uwajibakaji wa pamoja," aliongeza.

Sitta pia amekuwa akihoji kasi ya malipo hayo kwa kampuni ya Dowans wakati nchi ina madeni mengine kama ya Benki ya Dunia na IMF, lakini bado hayajalipwa kwa kasi kama hiyo.

"Lakini, hii haraka ya kuilipa Dowans ni ya nini? Nchi hii ina madeni ya muda mrefu kama yale ya Benki ya Dunia na IMF, lakini hakuna uharaka wa kulipa kama huu sasa kasi hii inatoka wapi?" alihoji.

Alisema nchi ina matatizo mengi ikiwemo ya kiuchumi, hivyo haingii akilini kuona Watanzania wanalipa kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa kampuni ya kitapeli.

Tayari msimamo wa Sitta ulimfanya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe, kutoa vitisho kwa mawaziri wenzake akiwataka wakae kimya na kuacha kuzungumzia sakata hilo vinginevyo wajiondoe kwenye Serikali.

Hata hivyo, wakosoaji wamemwelezea Chikawe kama ambaye pia amekiuka taratibu kutokana na kuzungumza suala hilo kwenye vyombo vya habari, badala ya taratibu za kiserikali.

Tangu Mahakama ya Usuluhishi ya Biashara ya kimataifa (ICC Court) kutoa hukumu ya mwezi Novemba, ikitaka Tanesco ilipe Dowans, Sitta alikuwa waziri wa kwanza kupinga malipo hayo hadharani.

Hata hivyo, pamoja na Sitta kupinga, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema alikwisha kusema bayana kwamba Serikali haiwezi kukata rufani katika sakata hilo, lazima ilipe faini hiyo.
 
Good go ahead, wewe ni mpambanaji japo watu tunaweza kukutafsri tujuavyo. Lakini fanya sehemu yako na wakiendelea jiuzulu uwaachie serikali yao ya kisanii. Endelea tu kaka Samweli

Hawa jamaa wanacheza na maneno kukidhi haja zao, Kule Arusha walisema Intelijensia, sasa wanakuja na "Uwajibikaji wa pamoja" wakati ni uamuzi wa Jakaya, Fredrick na William pekee. Uwajibikaji wa pamoja unatoka wapi kwenye madudu kama haya ya Dowans. Hakika Samweli na Harison msikubali maana ninyi mnaijua vema Dowans kutoka A mpaka Z na ndio maana hata Edward aliamua kuachia ngazi na Jakaya akakubali kwa kuziba nafasi hiyo kwa uteuzi wa Mizengo
 
Good go ahead, wewe ni mpambanaji japo watu tunaweza kukutafsri tujuavyo. Lakini fanya sehemu yako na wakiendelea jiuzulu uwaachie serikali yao kisanii. Endelea tu kaka Samweli

Hawa jamaa wanacheza na maneno kukidhi haja zao, Kule Arusha walisema Intelijensia, sasa wanakuja na "Uwajibikaji wa pamoja" wakati ni uamuzi wa Jakaya, Fredrick na William pekee. Uwajibikaji wa pamoja unatoka wapi kwenye madudu kama haya ya Dowans. Hakika Samweli na Harison msikubali maana ninyi mnaijua Dowans kutoka A mpaka Z na ndio maana hata Edward aliamua kuachia ngazi na Jakaya akakubali kwa kuziba nafasi kwa uteuzi wa Mizengo

Napingana na hapo kwenye bold nyekundu mkuu, wanajf wengi wanaamini kuwa watu kama Samwel Sitta, Harrison Mwakyembe and company wapo in a wrong place "ccm" kwakuwa wapo against CCM mnapokuwa jumuia kubwa mfano wa chama sio wote watakao kuwa na muono mmoja kila mtu anamtazamo wake nadhani hata hapa JF tunashuhudia Zitto akisakamwa kwa kuwa na maono tofauti na kina Slaa na watu wanapendekeza ahame chama eti kwa kuwa mawazo yake ni tofauti na wengine ndani ya chama na kusahau dhana ya "demokrasia" Elimu ya urai bado sana miongoni mwa jamii ya kitanzania.
 
DSC01394.JPG
Ukweli mtupu!!!!!!!!!!!!
 
Ila nadhani mzee 6 kuna kitu anakitafuta kutoka kwa jk,kama si kufukuzwa uwaziri,basi kuna kitu kingine,maaana kakomaaa kweli kweli kuwa hato badili msimamo wake wa kupinga dowans,na gazeti la RA rai wameaanza kazi waliyo ambiwa na boss wao(RA)kuwa ripoti ya mwakyembe nanukuu"yadhibitika ripoti ya mwakyembe ilijaa maelezo mengi ya hadaa"mwisho wa kunukuu.kuan mchezo mchafu unafanywa sasa hivi ili kuweza kuwachafua 6 na mwakyembe.
 
Ila nadhani mzee 6 kuna kitu anakitafuta kutoka kwa jk,kama si kufukuzwa uwaziri,basi kuna kitu kingine,maaana kakomaaa kweli kweli kuwa hato badili msimamo wake wa kupinga dowans,na gazeti la RA rai wameaanza kazi waliyo ambiwa na boss wao(RA)kuwa ripoti ya mwakyembe nanukuu"yadhibitika ripoti ya mwakyembe ilijaa maelezo mengi ya hadaa"mwisho wa kunukuu.kuan mchezo mchafu unafanywa sasa hivi ili kuweza kuwachafua 6 na mwakyembe.

Wadau wa siasa wakubali wakatae hakuna wakati ambao kumekuwa na uhuru wa kutoa maoni kama wakati wa Jakaya,
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni
 
BULLDOZZER
user-online.png
Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
Join DateTue Jan 2011Posts10Thanks0Thanked 0 Times in 0 Posts Rep Power0
icon1.png
Uongo wa gazeti la Tanzania Daima


Jana kulikuwa na thread iliyokuwa na kichwa cha habari "Sitta na Mwakyembe wafungwa mdomo kuhusu Dowans" Source ya thread hiyo ilikuwa gazeti la "TZ Daima". Watu wengi tulipoteza MUDA mwingi kuchangia thread hiyo. Katika gazeti hilo kulinukuliwa habari zilizotoka katika kikao cha baraza la Mawaziri ambacho JK alikuwa ni mwenyekiti wake. Nukuu mbalimbali zilitolewa kama ushahidi wa kilichosemwa kikaoni.

Habari zilizothibitishwa na Sitta mwenyewe na Pia Katibu mkuu Ndg. Ph. Luhanjo zinasema HAPAKUWA NA KIKAO CHA MAWAZIRI WALA HAKUNA ALIYEWAZIBA MDOMO SITTA NA MWAKYEMBE. habari hizi zimeandikwa na magazeti yote ya leo kasoro TZ Daima.

Wadau: Katika tasnia ya habari, Je, hamuoni kama gazeti hili ni hatari kwa usalama wa nchi yetu?. Je, gazeti kama hili katika utawala unaojali sheria za vyombo vya habari halipaswi kufungiwa kwa muda? Je, si kweli kwamba waandishi wa gazeti hili ni MAKANJANJA?. naomba tuwe wazalendo katika kujadili hili. Tanzania ni yetu na ni sisi wenye damu mpya tunaoweza kuifikisha nchi tunapopataka kwa AMANI.​

Msisahau haya magazeti yapo kibiashara kwahiyo lazima wakati mwingine waandishi wawe innovative ili kuatract hadhira.
 
Msisahau haya magazeti yapo kibiashara kwahiyo lazima wakati mwingine waandishi wawe innovative ili kuatract hadhira.

Na ndio maana jana wamemchokoza leo kayatoa tuliyokua tunayataka. Lengo TZ daima jana lilikua kujua mzee 6 bado ana uleule msimamo au keshachakachuliwa. Thanx 6 kwa kuendelea kukomalia hii ishu
 
Mr. 6, tuko pamoja na usikubali kufungwa mdomo! Waambie pia wapambanaji wenzako-hakuna kufungwa mdomo mpaka tujue fedha za dowans analipwa nani na kwa nini???????hapo ndo tutakuwa na uwajibikaji wa sote (pamoja) yaani serikali na wananchi-siyo chikawe na mawaziri wake.
 
Mzee Six tuko pamoja nawe. Achana na hao wadhalimu, njoo kwetu sisi wana wa nchi tukupe kazi kubwa zaidi.
 
Back
Top Bottom