Sitta Azima Maswali BUNGENI: Richmond & BoT Zimsubiri Yeye Atoke Marekani!!

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Live toka hapa Dodoma . Sitta kwa mara nyingine amezima issue ya kutaka hoja iende Bungeni kwa kusema anashauriana na Serikali na anatatoa majibu baadaye . Hii ni baada ya wapinzani kuanza kuibana serikali na Zitto akiwa anakaribia kusimama kumwaga mambo basi Spika akasema basi inatosha atalisemea baadaye .So sasa ni matangazo maana kesha ua sooo. Hili ndilo Bunge letu la watukufu wetu wale .
 
Amesema wiki ijayo atakuwa safarini Marekani hivyo issues zote sensitive kama vile "richmonduli", EPA, etc. zisubiri hadi atakaporudi baada ya wiki moja.

Hii naona kama wana-personalise institutions, yaani mtu anasafiri na ofisi yake?
 
Amesema wiki ijayo atakuwa safarini Marekani hivyo issues zote sensitive kama vile "richmonduli", EPA, etc. zisubiri hadi atakaporudi baada ya wiki moja.

Hii naona kama wana-personalise institutions, yaani mtu anasafiri na ofisi yake?
Huu ni wizi mwingine, halafu kuhusu yeye kwenda Marekani akazima hoja kama hizo zisiendelee hadi arudi ina maana msaidizi wake hawezi kazi???? Thisi is Tanzania watu wapoooooleeeeeee!!!!!!
 
Kilichopo Tumchomee mali zake, tukifuatiwa na wakina Balali na akina njake
ndio wajue tunauchungu na nnji hii.
 
Huyu muheshimiwa six, alivyokuwa ustawishaji makao makuu, kweli alikuwa safi huyu? ninapata mashaka naye.
 
Hii haijatulia,iweje mtu akasafiri na ofisi? Kama daktari angesema anasafiri halafu hakutakuwa na huduma mpaka atakarudi,ingekuwaje? nini kazi ya makamu wa spika,Anna Makinda? Huyu spika anajua kinachofuata ndiyo maana anaanza kuleta mizengwe. Ushindi lazima
 
Live toka hapa Dodoma . Sitta kwa mara nyingine amezima issue ya kutaka hoja iende Bungeni kwa kusema anashauriana na Serikali na anatatoa majibu baadaye . Hii ni baada ya wapinzani kuanza kuibana serikali na Zitto akiwa anakaribia kusimama kumwaga mambo basi Spika akasema basi inatosha atalisemea baadaye .So sasa ni matangazo maana kesha ua sooo. Hili ndilo Bunge letu la watukufu wetu wale .

Lunyungu,

Hizi ni pesazipi tena? Kama unaweza fafanua kidogo, nimeshindwa kuelewa ni pesa za income support zipi?
 
Hizi pesa kwa mujibu wa Dr.Slaa zilitolewa na wafadhili mbalmbali wa nchi hii maskini hili kuwawezesha wajasiliamali wadogowadogo. Nchi mojawapo ni Japan,ilitoa mchango mkubwa sana. Sasa mafisadi wakagawana pesa yote na wakaufuta mfuko huo. Watu wanahitaji majibu ya kina kuhusu huo mfuko. Ngasongwa anaweza kutupa maelezo ya kina kupitia bunge
 
Ni pesa zilizokuwa zinatolewa na serikali ya Japani kusaidia wajasiriamali wadogo ama tuseme kujenga middle class economy ila wakina manji na Rostam Aziz walijichotea pesa zote, yupo pia mzindakaya alijichotea kiasi cahake na kulalua mbel na wengine wengi wapo hapa kwenye hili soo, huu ni mwaka wa kuwakomalia mafisadi mapka kieleweke.
 
This is ridiculuos ! What is wrong with Sitta, Does he think is the only smart guy in the room besides why he has to travel while the parliament is in session ?
 
Live toka hapa Dodoma . Sitta kwa mara nyingine amezima issue ya kutaka hoja iende Bungeni kwa kusema anashauriana na Serikali na anatatoa majibu baadaye . Hii ni baada ya wapinzani kuanza kuibana serikali na Zitto akiwa anakaribia kusimama kumwaga mambo basi Spika akasema basi inatosha atalisemea baadaye .So sasa ni matangazo maana kesha ua sooo. Hili ndilo Bunge letu la watukufu wetu wale .

Bunge linasimamiasha shughulu zake eti kwa kuwa spika anaenda US! Kwani hakuna naibu wa spika anayeweza kukaimu nafasi hiyo vizuri sana kuliko hata huyu msanii Sitta!? :confused:
 
This is ridiculuos ! What is wrong with Sitta, Does he think is the only smart guy in the room besides why he has to travel while the parliament is in session ?

Where is our priolity?
Ina maana hiyo safari yake ni muhimu kuliko hizo hoja anazopaswa kuzi table??, by the way, suppose amefariki dunia?? hoja zitamsubili hadi afufuke??

Huu ni ufisadi wa hali ya juu, bunge si mtu mmoja! Wabunge amkeni kataeni kuburuzwa!!.
 
Spikia kama hamwamini msaidizi wake hakuna haj ya kuuma maneno, nilimsikia wakati anaaga bunge alisema na namnukuu,naibu spika namwambia masuala nyeti asije akakurupuka nayo ---naamini ninaposema masuala nyeti naeleweka ni kama richmondnk hadi nitakaporudi wiki ijayo.

Naibu spika hiz ni dharau kwako kuwa kila wakati akikuachia vitu vya kufanya huwa uankurupuka sasa ni wewe uonyeshe uwezo wako wa kisheria ama mamlaka yako kama naibu spika la sivyo wabunge wekeni hoja ya kukosa imani nha naibu spika kwani hata spika wake hamwamini.
 
Bunge linasimamiasha shughulu zake eti kwa kuwa spika anaenda US! Kwani hakuna naibu wa spika anayeweza kukaimu nafasi hiyo vizuri sana kuliko hata huyu msanii Sitta!? :confused:
Huyo ndo spika wa Standard and Speed. Anazeeka vibaya mno kwani hata bunge anataka kulifanya kama lake. Asipokuwepo mambo hayaendi kama alivyoagizwa na Mafisadi. Ni kuzima moto na kupitisha muda ilimradi siku zinaenda. Kwa kweli kwa mtindo huu tunasafari ndefu. Mungu ibariki Tanzania.
 
This guy is a BULLY!!

http://www.jamboforums.com/showpost.php?p=132915&postcount=3

And I am sad since there seem to be no mechanism to oust him!

Few days ago, Rev. Kishoka brought foward a proposal: http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=9247
I think we ought look at this, focus on it and think harder. I know the intricacies of this are somewhat complex (at least to myself), but with hard work I believe there is possibility.

Lets all campaign for his removal, kwa kweli huyu mheshimiwa ana dololesha Bunge letu tukufu kwa kutumia ubabe na si kingine!

Napenda pia kuwaambia wote, heshima yangu kwake kama Mzee, Baba na Ndugu wa watu ni kubwa, lakini kama speaker wa Bunge imepungua mno kwa niliyoona mpaka hivi sasa, hivo basi ni muhimu wote tukitofautisha hili swala.

SteveD.
 
Heshima kwenu wakuu. Naamini kuwa masuala yote yanayopelekwa Bungeni kwa ajili ya kujadiliwa ni masuala ambayo ni muhimu na nyeti kwa mustakabali mzima wa Taifa letu. Naamini pia kwamba Naibu Spika anachaguliwa kwa misingi kwamba shughuli za Bunge zisikwame pale ambapo Spika anakuwa hayupo aidha kwa matatizo binafsi ama ya kiofisi kama ambavyo anasafiri kwenda US na kuwa Naibu Spika anachaguliwa kwa misingi kwamba upeo wake wa kuelewa kanuni za Bumge na tafsiri stahili ni sawa na ule wa Spika mwenyewe na akiwa kwenye kiti cha Spika anendesha Bunge kama inavyostahili. Pale inapotokea kuwa Mheshimiwa Sitta hamwamini Naibu wake na anatamka wazi kuwa asifanye maamuzi ya kukurupuka kwa mambo nyeti mpaka yeye awepo, basi wanannchi tunawaomba Wabunge wote wahoji kutoka kwa Spika ni mambo gani nyeti ambayo kujadiliwa kwake ni mpaka yeye awepo na yapi ambayo sio nyeti ambayo Naibu wake anaweza kuyajadili. Kama mambo yote yanayojadiliwa Bungeni ni nyeti basi nafasi ya Naibu Spika isiwepo la sivyo Spika awajibike ama amwombe radhi naibu wake kwa kutamka hadharani kuwa anafanya maamuzi ya KUKURUPUKA kwa mambo nyeti hapo Bungeni.
 
Spika has to apologize very immediately ama naibu wake ajiuzulu kama spika anamwona hana uwezo wa kuliendesha bunge kama hayupo.

This is a principal question kama ni kumnyanyas mwanamke basi hapa wanaharakati waje waseme , ila la kushangaza utaona media zetu zisivyo sensitive hawataona kuwa hili ni jambo kubwa na ambalo halipaswi kufumbiwa macho liendelee kuwepo.
 
Spika has to apologize very immediately ama naibu wake ajiuzulu kama spika anamwona hana uwezo wa kuliendesha bunge kama hayupo.

This is a principal question kama ni kumnyanyas mwanamke basi hapa wanaharakati waje waseme , ila la kushangaza utaona media zetu zisivyo sensitive hawataona kuwa hili ni jambo kubwa na ambalo halipaswi kufumbiwa macho liendelee kuwepo.

Huu ni mfano mojawapo ya bullying ambayo imemkaa kichwani na haoni haya kutamka!! Honestly, this Speaker should just go!


SteveD.
 
Hili jambo ni kubwa sana na nilikuwa naomba vyombo vya habari vitusaidie katika hili .Binafsi nimeshtushwa na ninashindwa kuelewa nini kinaendelea , inaonekana dhahiri ya kuwa spika amwamini naibu wake au anaamini ya kuwa yeye ndiye mtu pekee ambaye ni smart katika lile bunge.

Pia mimi sielewi umuhimu wa hiyo safari yake , kwa nini asafiri kipindi hiki ambacho bunge linaendelea . Neno kukurupuka alilolitumia Spika sio neno zuri, na wala sikutegemea mtu kama spika anaweza kulitumia ndani ya bunge kumdescribe naibu . Hon. Speaker you owe her an apology!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom