dosama
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 912
- 957
WAZIRI wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta, ametoboa siri nzito, akidai kuwa mmoja wa wabunge wa jumuia hiyo, kutoka hapa nchini alitia saini mkataba wa mazingira ambao ni hatari kwa taifa, kiasi cha kumlazimu yeye kukimbilia kwa Rais Jakaya Kikwete kumzuia asiukubali.
Bila kumtaja mbunge huyo, Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo, alidai kuwa mbunge huyo wa Afrika Mashariki alikubali kusaini muswada wa sheria ya mazingira (Transboundary Equal System), unaozitaka nchi wanachama kulifanya suala la mazingira lisimamiwe na jumuiya jambo ambalo ni hatari kwa taifa.
Sitta alitoboa jambo hilo jana jijini Dar es Salaam katika semina elekezi kwa wabunge hao, na kudai kuwa baadhi ya nchi wanachama wanacheza mchezo mchafu, ambao usipoangaliwa kwa makini unaweza kuleta matatizo hapa nchini.
Ukisema suala la mazingira lisimamiwe na jumuia ina maana suala la ardhi ni lazima liingizwe katika jumuia yetu jambo ambalo linaweza kusababisha athari katika nchi, alisema.
Waziri Sitta alisema kutokana na kutishwa kwa hatua ya mbunge huyo imemlazimu kuwasiliana na kumshauri Rais Kikwete ili asikubali kuupokea na kuusaini.
Aliwaonya wabunge wateule wa Bunge la Afrika Mashariki kuwa makini katika maamuzi mbalimbali yanayohusu taifa kutokana na baadhi ya nchi za jumuiya hiyo kutumia ujanja hasa katika suala la ardhi.
Aliitaja nchi moja (jina linahifadhiwa) kuwa inajaribu kwa kila njia kuhakikisha ardhi inaingizwa katika jumuia kutokana na Tanzania kuwa na ardhi kubwa kuliko nchi nyingine za jumuiya hiyo.
Hata hivyo Sitta aliwataka wabunge hao kuhakikisha wanaweka mbele vipaumbele vya taifa ikiwa ni pamoja na kilimo cha uzalishaji ili kuifanya Tanzania kuwa ghala la chakula na biashara kwa nchi za Afrika Mashariki.
Kuna mchezo unaoendelea ambapo wenzetu (anawataja) wananunua mahindi yetu na kuyasindika huku wakiyaweka katika mifuko ya sembe na kwenda kuyauza nchi ya Sudan Kusini.
Niwaombe wafanyabiashara wa hapa nchini wajaribu kuweka kinu cha kusindika mazao maana masoko yapo mengi ya uhakika, alisisitiza.
Naye, Spika wa Bunge la Tanzania, Anne Makinda, alisema kuwa kwa sasa watakuwa na kamati maalumu ya kushughulikia masuala ya Afrika Mashariki kutokana na kuweka ushirikiano baina ya ofisi yake na Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki baada ya kuunda kikosi kazi ili kuangalia namna ya kuimarisha uhusiano na wabunge wa EALA.
Ushirikiano huo utaondoa baadhi ya kasoro zilizojitokeza za kukosa taarifa za mwaka zinazofanywa katika Bunge hilo, kutokuwepo kwa nyaraka za majadiliano, alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa EALA, Adam Kimbisa, alisema kuwa watajitahidi kuangalia lipi halali na haramu huku wakitumia akili zao kuepuka kutumiwa na baadhi ya nchi katika Bunge hilo.
My concern;
Naona wanunge hawa wanafuata posho na kuuza sura kinachozungumzwa na kuchangiwa hawakijui mwisho wa siku wanaanguka sahihi
Bila kumtaja mbunge huyo, Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo, alidai kuwa mbunge huyo wa Afrika Mashariki alikubali kusaini muswada wa sheria ya mazingira (Transboundary Equal System), unaozitaka nchi wanachama kulifanya suala la mazingira lisimamiwe na jumuiya jambo ambalo ni hatari kwa taifa.
Sitta alitoboa jambo hilo jana jijini Dar es Salaam katika semina elekezi kwa wabunge hao, na kudai kuwa baadhi ya nchi wanachama wanacheza mchezo mchafu, ambao usipoangaliwa kwa makini unaweza kuleta matatizo hapa nchini.
Ukisema suala la mazingira lisimamiwe na jumuia ina maana suala la ardhi ni lazima liingizwe katika jumuia yetu jambo ambalo linaweza kusababisha athari katika nchi, alisema.
Waziri Sitta alisema kutokana na kutishwa kwa hatua ya mbunge huyo imemlazimu kuwasiliana na kumshauri Rais Kikwete ili asikubali kuupokea na kuusaini.
Aliwaonya wabunge wateule wa Bunge la Afrika Mashariki kuwa makini katika maamuzi mbalimbali yanayohusu taifa kutokana na baadhi ya nchi za jumuiya hiyo kutumia ujanja hasa katika suala la ardhi.
Aliitaja nchi moja (jina linahifadhiwa) kuwa inajaribu kwa kila njia kuhakikisha ardhi inaingizwa katika jumuia kutokana na Tanzania kuwa na ardhi kubwa kuliko nchi nyingine za jumuiya hiyo.
Hata hivyo Sitta aliwataka wabunge hao kuhakikisha wanaweka mbele vipaumbele vya taifa ikiwa ni pamoja na kilimo cha uzalishaji ili kuifanya Tanzania kuwa ghala la chakula na biashara kwa nchi za Afrika Mashariki.
Kuna mchezo unaoendelea ambapo wenzetu (anawataja) wananunua mahindi yetu na kuyasindika huku wakiyaweka katika mifuko ya sembe na kwenda kuyauza nchi ya Sudan Kusini.
Niwaombe wafanyabiashara wa hapa nchini wajaribu kuweka kinu cha kusindika mazao maana masoko yapo mengi ya uhakika, alisisitiza.
Naye, Spika wa Bunge la Tanzania, Anne Makinda, alisema kuwa kwa sasa watakuwa na kamati maalumu ya kushughulikia masuala ya Afrika Mashariki kutokana na kuweka ushirikiano baina ya ofisi yake na Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki baada ya kuunda kikosi kazi ili kuangalia namna ya kuimarisha uhusiano na wabunge wa EALA.
Ushirikiano huo utaondoa baadhi ya kasoro zilizojitokeza za kukosa taarifa za mwaka zinazofanywa katika Bunge hilo, kutokuwepo kwa nyaraka za majadiliano, alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa EALA, Adam Kimbisa, alisema kuwa watajitahidi kuangalia lipi halali na haramu huku wakitumia akili zao kuepuka kutumiwa na baadhi ya nchi katika Bunge hilo.
My concern;
Naona wanunge hawa wanafuata posho na kuuza sura kinachozungumzwa na kuchangiwa hawakijui mwisho wa siku wanaanguka sahihi