WanaJF,
Akiwa anahutubia wananchi wa jimbo lake, mhe Sitta amesema waziwazi bila kuficha chochote uhusika wa Lowassa kwenye sakata la RICHMOND.
Sitta alieleza kuwa, ni aibu kwa mtu fisadi kama Lowassa kuthubutu kugombea Urais.
Katika kukazia maelezo yake hayo, Sitta aliueleza umma wa Watanzania kupitia mkutano wake huo kuwa, Lowassa alishirikiana na rafiki yake Rostam kuunda kampuni hewa ya Dowans ambayo inaendelea kututafuna Watanzania hadi hii leo. Sitta aliongeza kuwa, "pesa ya kuwalipa Dowans imeingizwa kwenye deni la Taifa, deni ambalo mimi na wewe tunalilipa"
Aidha, Sitta amesema ikiwa Serikali ingetumia pesa ya kuwalipa Dowans pekee katika kuleta maendeleo, basi pesa hizo zingetosha kabisa kumaliza changamoto zote katika sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na kuboresha maslahi ya walimu, kujenga maabara na vifaa vingine vya kufundishia na kuongeza shule kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sitta zaidi ya 300. Badala yake kwa uovu wa Lowassa Serikali inatumia mabilioni hayo ya fedha kuwalipa Dowans.
Katika kuhitimisha hotuba yake hiyo mujarabu, Sitta amesema ikiwa Lowassa atapinga chochote kati ya hayo aliyosema, basi anamtaka Lowassa kufanya mdahalo kupitia kituo chochote cha televisheni upande mmoja akiwa yeye (Sitta) na Mwakyembe huku upande mwingine akiwa Lowassa na mafisadi wenzake atakao wataka.
My take,
Taifa haliwezi kuongozwa na FISADI.
Akiwa anahutubia wananchi wa jimbo lake, mhe Sitta amesema waziwazi bila kuficha chochote uhusika wa Lowassa kwenye sakata la RICHMOND.
Sitta alieleza kuwa, ni aibu kwa mtu fisadi kama Lowassa kuthubutu kugombea Urais.
Katika kukazia maelezo yake hayo, Sitta aliueleza umma wa Watanzania kupitia mkutano wake huo kuwa, Lowassa alishirikiana na rafiki yake Rostam kuunda kampuni hewa ya Dowans ambayo inaendelea kututafuna Watanzania hadi hii leo. Sitta aliongeza kuwa, "pesa ya kuwalipa Dowans imeingizwa kwenye deni la Taifa, deni ambalo mimi na wewe tunalilipa"
Aidha, Sitta amesema ikiwa Serikali ingetumia pesa ya kuwalipa Dowans pekee katika kuleta maendeleo, basi pesa hizo zingetosha kabisa kumaliza changamoto zote katika sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na kuboresha maslahi ya walimu, kujenga maabara na vifaa vingine vya kufundishia na kuongeza shule kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sitta zaidi ya 300. Badala yake kwa uovu wa Lowassa Serikali inatumia mabilioni hayo ya fedha kuwalipa Dowans.
Katika kuhitimisha hotuba yake hiyo mujarabu, Sitta amesema ikiwa Lowassa atapinga chochote kati ya hayo aliyosema, basi anamtaka Lowassa kufanya mdahalo kupitia kituo chochote cha televisheni upande mmoja akiwa yeye (Sitta) na Mwakyembe huku upande mwingine akiwa Lowassa na mafisadi wenzake atakao wataka.
My take,
Taifa haliwezi kuongozwa na FISADI.