Sitta ahoji kuhusu Kagame kumuachia uenyekiti Kenyatta

bmalale

Senior Member
Mar 30, 2011
466
24
KIKAO CHA MAWAZIRI WA AFRIKA MASHARIKI: TANZANIA NA BURUNDI WAWASHA MOTO

Kulikuwa na kutokubaliana katika Baraza la Jumuiya ya Afrika Mashariki la Mawaziri Alhamisi juu ya jinsi Uganda, Kenya na Rwanda walikuwa kuharakisha mambo katika kuelekea shirikisho kisiasa, umoja fedha na miradi mingine, na kuacha nje wengine.

Mbali na mambo mengine Waziri Sita alihoji uhalali wa Rwanda kumuachia uenyekiti wa jumuia ya afrika mashariki Kenya

"The charter says the chair is on one year rotational basis. As far as we are concerned, Rwanda is the next chair. The rest of us don't know about this arrangement of Kenya taking over," he charged.

SOURCE: Tanzania, Burundi concerned with ‘isolation' in bloc

My take: Hivi kwanini TANZANIA TUNAKUWA KAMA WAPINZANI NDANI YA JUMUIA
 
Inawezekana hakusikia kauli ya Kenyatta jana kasema hataki na hapendi kuongelea haya mambo ya kipuuzi ya kuambiwa wanawatenga baadhi ya nchi wanachama wa eac. Niwazi kabisa wanaoongelea mambo haya kwa mtazamo wake anawaona ni wapuuzi tu.
 
KIKAO CHA MAWAZIRI WA AFRIKA MASHARIKI: TANZANIA NA BURUNDI WAWASHA MOTO

Kulikuwa na kutokubaliana katika Baraza la Jumuiya ya Afrika Mashariki la Mawaziri Alhamisi juu ya jinsi Uganda, Kenya na Rwanda walikuwa kuharakisha mambo katika kuelekea shirikisho kisiasa, umoja fedha na miradi mingine, na kuacha nje wengine.

Mbali na mambo mengine Waziri Sita alihoji uhalali wa Rwanda kumuachia uenyekiti wa jumuia ya afrika mashariki Kenya

"The charter says the chair is on one year rotational basis. As far as we are concerned, Rwanda is the next chair. The rest of us don't know about this arrangement of Kenya taking over," he charged.

SOURCE: Tanzania, Burundi concerned with ‘isolation' in bloc

My take: Hivi kwanini TANZANIA TUNAKUWA KAMA WAPINZANI NDANI YA JUMUIA

Tafadhali acha kurahisisha mambo namna hiyo! Anachohoji Waziri Sitta ni ukweli na Mtanzania wa kweli unatakiwa kuiona mantiki. Hatuwezi kuendesha mambo muhimu ya EAC kienyeji kienyeji tu namna hiyo!! Nina hakika ingelikuwa mpango huo wa kubadilishana ungeihusu Tanzania, haraka sana tungeambiwa sisi tunaleta "uswahili" katika serious issues!!! Kama Kagame hataki/amesusa uenyekiti, suala hilo linatakiwa lipelekwe katika vikao halali vya EAC ili lijadiliwe na uamuzi utolewe kwa consensus ya wanajumuiya wote sio wanajumuiya wawili au watatu wakae uchochoroni kisha waamue kwa niaba ya wote--hatukubali--na hakuna "upinzani" hapa, this is the reality of the matter!!!
 
Inawezekana hakusikia kauli ya Kenyatta jana kasema hataki na hapendi kuongelea haya mambo ya kipuuzi ya kuambiwa wanawatenga baadhi ya nchi wanachama wa eac. Niwazi kabisa wanaoongelea mambo haya kwa mtazamo wake anawaona ni wapuuzi tu.

Definitely hakuna mpuuzi katika suala hili na hatuwezi kukubali viongozi wetu waitwe wapuuzi. Na anayedhani viongozi wetu ni wapuuzi, kuna uwezekano mkubwa, ikawa yeye ndiye mpuuzi! Kiongozi wa ngazi ya juu kama ya Rais anatakiwa apime uzito wa kauli zake, na hasa kama zinawahusu viongozi wa nchi nyingine huru kama yake!! Mimi kama raia wa kawaida wa Tanzania, inaniuma sana kiongozi wangu mkuu akiitwa mpuuzi, tena na kiongozi wa nchi nyingine, regardless of my domestic political affiliation.
 
Inawezekana hakusikia kauli ya Kenyatta jana kasema hataki na hapendi kuongelea haya mambo ya kipuuzi ya kuambiwa wanawatenga baadhi ya nchi wanachama wa eac. Niwazi kabisa wanaoongelea mambo haya kwa mtazamo wake anawaona ni wapuuzi tu.

Hii EAC ni NGO au ni kitu gani jamani? mambo kwanini yasifanyike waziwazi kuna nini ndani ya usiri usiri hapa? maono yangu juu ya EAC ni haya - Nina wasiwasi majirani zetu walikuwa na ndoto za kuitawala tanzania kwa mtindo wa mikataba ya Carl Peters na Vasco dagama! na nina hofu walikuwa na hila ya kuiibia Tanzania utajiri wake wa asili kwa njia aliyotumia Muingereza baada ya vita kuu ya pili ya dunia kwa kusema uongo katika masuala yanayohusu utendaji na kimalengo, pia naona walidhani Tanzania ni easy go na matokeo yanapokuwa tofauti wanakasirika sana!
Cha kufanya hapa ni Tanzania kukomalia kutokutoka na kukomalia hakuna njia za mkato katika utendaji wa EAC na ikibidi Tanzania iendelee na mipango yake na SADEC kikamilifu.
 
mtu kama sitta kama wanguwa wanajitambua asingekuwa anaendelea kuaminisha watanzania ngonjera zake hizi angefikia hatua hata aweke rekodi yake ya kujiuzuru sio kulalamika kila kukicha waziri ana lalamika serikali kilio wabunge wa eac kilio wananchi wa kilio huu ni unafki
 
Definitely hakuna mpuuzi katika suala hili na hatuwezi kukubali viongozi wetu waitwe wapuuzi. Na anayedhani viongozi wetu ni wapuuzi, kuna uwezekano mkubwa, ikawa yeye ndiye mpuuzi! Kiongozi wa ngazi ya juu kama ya Rais anatakiwa apime uzito wa kauli zake, na hasa kama zinawahusu viongozi wa nchi nyingine huru kama yake!! Mimi kama raia wa kawaida wa Tanzania, inaniuma sana kiongozi wangu mkuu akiitwa mpuuzi, tena na kiongozi wa nchi nyingine, regardless of my domestic political affiliation.

Mimi naungana na wewe . Uhuru Kenyatta anajua kiswahili vizuri kabisa , anapotaja upuuzi anamaanisha na kukijua anachoongea. Hawa jamaa wanatudharau sana lakini na sisi tunakaribisha dharau hizo.
Hivi hatuna chochote cha kufanya (maamuzi ) kama NCHI?
 
Definitely hakuna mpuuzi katika suala hili na hatuwezi kukubali viongozi wetu waitwe wapuuzi. Na anayedhani viongozi wetu ni wapuuzi, kuna uwezekano mkubwa, ikawa yeye ndiye mpuuzi! Kiongozi wa ngazi ya juu kama ya Rais anatakiwa apime uzito wa kauli zake, na hasa kama zinawahusu viongozi wa nchi nyingine huru kama yake!! Mimi kama raia wa kawaida wa Tanzania, inaniuma sana kiongozi wangu mkuu akiitwa mpuuzi, tena na kiongozi wa nchi nyingine, regardless of my domestic political affiliation.

Ndio imeshatokea hivyo kinachotakiwa ni kuchukua hatua. Wanatohumiwa kututenga hawaoni kuwa wanakosea wanajiona wako sawa. Wanaohoji mienendo yao wanaambiwa wapuuzi. Ujue kuwa ndani ya nchi zao kuna wenzao nao wanawahoji mbona kama mnawatenga jirani zetu? wameambiwa wa achane na huo upuuzi.
 
Definitely hakuna mpuuzi katika suala hili na hatuwezi kukubali viongozi wetu waitwe wapuuzi. Na anayedhani viongozi wetu ni wapuuzi, kuna uwezekano mkubwa, ikawa yeye ndiye mpuuzi! Kiongozi wa ngazi ya juu kama ya Rais anatakiwa apime uzito wa kauli zake, na hasa kama zinawahusu viongozi wa nchi nyingine huru kama yake!! Mimi kama raia wa kawaida wa Tanzania, inaniuma sana kiongozi wangu mkuu akiitwa mpuuzi, tena na kiongozi wa nchi nyingine, regardless of my domestic political affiliation.

Nilisikiliza jana BBC , pamoja na Lugha za kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, kiukweli Rais Kenyata ameongea lugha tunayoita INAYOUDHI, haikuwa na staha, kwangu mimi nilikereka sana. Alipoozesha lugha yake pale alipohusisha miundo mbinu kutoka Kenya hadi kaskazini ya Tanzania kwa maana mikoa ya K'njaro n.k. Anachopaswa kujua ni kuwa yeye ni head of state kwao, hana mamlaka ya kuwa juu ya head of state wa Taifa lingine. Alinikera!
 
Till when !!!!!!!!!!! tutaendelea kuwa wapuuzi jamani,Kenyatta anaposema hivyo anaamanisha hayo,kwa kuwa anafahamu KISWAHILI kwa usahihi kabisa kuliko baba zake [Kenyatta Baba, Moi, na Kibaki] tufike sehemu nasi tujue matendo na maneno ya wenzetu ndio maana yaho hasa kwetu sisi.Na tunapochukua hatua nasi za ukweli tusiludi nyuma!!!

Hapa juzi tulipoongea kama Nchi kupitia Rais basi acha wakimbie kuja kwetu kujishaua nasi tunalidhika kuwa kweli awa ni wenza tunabweteka tena wanaludi,yani kwa watu wazima kanakuwa kama kamchezo ka Babu na mjukuuu wake.Yani wanatamka vitu vya kikweli babu akija juu mjukuu anawai kusema nilikuwa natania tu babu!!Ndio maana wengine tuliliona hili zamani tukasema USALAMA WA TAIFA hili kwenye EAST AFRICA uzingatiwe.

Huu mcheo mchezo ufike mwisho tujue kama TAIFA KWELI "THEIR EITHER WITH US OR NOT".Hii Diplomasia wakati wenzenu hawatumii hiyo diplomasia yao kwenye kauri na matendo yao!!!!!!Mwingine anasema I will hit you, mwingine ansema Upuuzi" sasa sie tumekali diplomasia till WHEN?
 
Sitta is a disrupter with a hidden agenda. Sitta should be thrown out akileta huo "upuz". Jubilee Kusema na Kutenda.
 
Till when !!!!!!!!!!! tutaendelea kuwa wapuuzi jamani,Kenyatta anaposema hivyo anaamanisha hayo,kwa kuwa anafahamu KISWAHILI kwa usahihi kabisa kuliko baba zake [Kenyatta Baba, Moi, na Kibaki] tufike sehemu nasi tujue matendo na maneno ya wenzetu ndio maana yaho hasa kwetu sisi.Na tunapochukua hatua nasi za ukweli tusiludi nyuma!!!

Hapa juzi tulipoongea kama Nchi kupitia Rais basi acha wakimbie kuja kwetu kujishaua nasi tunalidhika kuwa kweli awa ni wenza tunabweteka tena wanaludi,yani kwa watu wazima kanakuwa kama kamchezo ka Babu na mjukuuu wake.Yani wanatamka vitu vya kikweli babu akija juu mjukuu anawai kusema nilikuwa natania tu babu!!Ndio maana wengine tuliliona hili zamani tukasema USALAMA WA TAIFA hili kwenye EAST AFRICA uzingatiwe.

Huu mcheo mchezo ufike mwisho tujue kama TAIFA KWELI "THEIR EITHER WITH US OR NOT".Hii Diplomasia wakati wenzenu hawatumii hiyo diplomasia yao kwenye kauri na matendo yao!!!!!!Mwingine anasema I will hit you, mwingine ansema Upuuzi" sasa sie tumekali diplomasia till WHEN?

Ni kweli. Ni wakati wa kushika yetu na kushikiriana na majirani wa kweli na kuachana na wanafiki! Watz tunatakiwa sasa tuamue kuchapa kazi kwa kasi ya ajabu kujiletea maendeleo yetu na kutokudanganywa na hizi rhetoric za kutudhalilisha kila mara. Tufikie mahali tuchoshwe na madharau na tuamue kusimama na wajue tumeamua KUSIMAMA--a sleeping giant can't keep on sleeping forever!
 
Tafadhali acha kurahisisha mambo namna hiyo! Anachohoji Waziri Sitta ni ukweli na Mtanzania wa kweli unatakiwa kuiona mantiki. Hatuwezi kuendesha mambo muhimu ya EAC kienyeji kienyeji tu namna hiyo!! Nina hakika ingelikuwa mpango huo wa kubadilishana ungeihusu Tanzania, haraka sana tungeambiwa sisi tunaleta "uswahili" katika serious issues!!! Kama Kagame hataki/amesusa uenyekiti, suala hilo linatakiwa lipelekwe katika vikao halali vya EAC ili lijadiliwe na uamuzi utolewe kwa consensus ya wanajumuiya wote sio wanajumuiya wawili au watatu wakae uchochoroni kisha waamue kwa niaba ya wote--hatukubali--na hakuna "upinzani" hapa, this is the reality of the matter!!!

Ninavyofahamu katika hili kuna kanuni zinazofuatwa ikiwa mwanachama mmoja hayuko tayari kuchukua nafasi yake ya kuongoza wakati wake ukifika. Katika kanuni hizo hakuna inayoruhusu yeye kuchagua amtakaye achukuwe nafasi yake. Kumbukumbu zanamalama ni sahihi anatakiwa mwanachama anayefuatia katika mzunguko ndiye achukue. Tatizo nafikiri ni mshauri wa sheria wa Jumuiya (yaana CTC) Kama alikubaliana na mpango huu wa Kenya na Rwanda (pengine na Uganda wakiwemo) wa kutaka kurithishana uongozi wa Jumuiya.
 
Mm sielewi.kwani waliitaja Tz?nilizani labda wenyewe kwa wenyewe.Maana reli ile inatoka mombasa kwenda nairobi maana ilichakaa sana niliwahi kupata mwaka jana kutoka Nairobi kwensa Mombasa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom