Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,425
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 34
ILIPOISHIA
Nikaenda nyuma ya gari na kulitoa lile shepe.
“Njoo hapa” akaniambia akiwa amesimama mahali fulani kando ya lile gari.
Nilipofika karibu yake akaniambia.
“Chimba mahali hapa”
Alinionesha pale aliposimama kisha akaondoka na kusimama kando yake.
Nikaanza kupachimba mahali hapo kwa kutumia lile shepe. Bahati nzuri mchanga ulikuwa laini, sikutumia nguvu nyingi. Niliendelea kuchimba mpaka shimo likafikia urefu wa wastani wa futi mbili.
“Nichimbe hadi wapi?”
“Bado. Endelea kuchimba” Maimun akaniambia.
Nikaendelea kuchimba. Mwili wangu ukaanza kutoka jasho. Nikaacha kuchimba na kuvua shati.
“Lete nikushikie” Maimun akaniambia.
Nikampa lile shati na kuendelea kuchimba.
SASA ENDELEA
Niliendelea kuchimba lile shimo mpaka likanifikia usawa wa kifua. Nilikuwa nikimwaga mchanga juu ya shimo hilo. Ghafla nikaona ninapiga kitu kama mwamba au jiwe lililokuwa chini ya ardhi.
“Sijui nimepiga nini hapa?” nikamuuliza Maimun kwa mshituko.
“Huo ni mwamba, upige tena” Maimun akaniambia.
Nikaupiga tena kwa shepe.
“Piga tena”
Nikaupiga kwa mara ya tatu. Ule mwamba ukapasuka.
“Umepasuka” nikamwambia Maimun.
“Hebu washa kitochi cha simu yako umulike hapo palipopasuka” Maimun akaniambia.
Nikajipapasa mfukoni na kutoa simu yangu. Niliwasha kitochi nikamulika pale chini.
Mama yangu! Niliona vipande vya madini yanayomeremeta vikiwa vimetawanyika!
“Nini hii?” nikamuuliza Maimun kwa mshituko.
“Kwani umeona nini?”
“Sijui ni madini haya. Huu mwaba ulikuwa na madini!”
“Ndiyo ni madini”
“Sijui ni madini ya aina gani?”
“Ni Tanzanite, ni yale aliyokuwa akiuza babu yako”
“Niyachukue”
“Ndiyo yachukue”
Nikainama haraka na kuyachukua yale madini.
Vilikuwa vipande saba vya madini.
“Huu ni utajiri hasa! Nikajiambia kimoyomoyo kisha nikamshukuru Mungu.
“Mungu anipe nini tena!”
Yakiwa mikononi mwangu madini hayo yalikuwa yakiakisi rangi mbali mbali za dunia. Zile rangi zilikuwa kama zinazunguka. Ilikuwa ni furaha hata kuyatazama.
“Ni vipande vingapi?” Maimun akaniuliza.
“Viko saba”
“Haya sasa toka kwenye hili shimo”
“Ngoja niendelee kuupiga huu mwamba”
“Hapana, usirudie tena. Toka kwenye shimo” Maimun akanionya.
Nikayatia yale madini mifukoni mwangu kisha nikalitoa lile shepe na kuliweka juu ya shimo hilo.
“Lete mkono wako nikutoe” Maimun akaniambia.
Nikampa mkono wangu Maimun, akaushika na kunivuta. Mara moja
nikjioan niko juu ya lile shimo.
“Anza kulifukia haraka haraka”
Nikalichukua shepe hilo na kufukia lile shimo.
“Tutakuja lini tena kuchimba?” nikamuuliza Maimun kwa tamaa huku nikiendelea kufukia shimo hilo.
“Baada ya miezi sita”
“Ah kwanini! Mbona mbali sana?”
“Ndiyo masharti yake. Haya madini yanakaliwa na majini. Huwezi kuja kienyeji tu na kuyachimba na hata ukija hutoyaona. Masharti yake ndiyo haya ninayokupa. Kila baada ya miezi sita tunakuja kuchimba tena”
“Sawa”
Niliendelea kulifukia lile shimo mpaka nikaliweka sawa.
“Watu wengine hawatakuja kufukua?” nikamuuliza Maimun.
“Ni nani atakayethubutu?”
“Wanaweza kutokea watu wakaja kufukua”
“Hawatapata kitu chochote. Chukua shati lako tuondoke”
Nililichukua lile shati alilokuwa amelishika Maimun nikalivaa.
“Twenzetu” akaniambia.
Nililiweka shepe nyuma ya gari.
“Utaendesha wewe?” Maimun akaniambia.
“Sawa” nikamjibu haraka haraka na kwenda kufungua mlango wa gari wa upande wa dereva.
Maimun alifungua mlango wa upande wa pili wa dereva na kujipakia.
“Washa gari tuondoke. Muda umekwenda sana”
Nikaliwsha gari na kuliondoa. Nilipokuja na Maimun mahali hapo nilikuwa nimefadhaika lakini wakati tunaondoka moyo wangu ulikuwa na furaha iliyopita kiasi.
“Hivi babu yangu ulikuwa unakuja naye hapa hapa kuchimba haya madini?”
“Ninajua mimi kama tulikuwa tunakuja hapa au mahali pengine”
“Hutaki kuniiambia”
“Si lazima kila kitu ukijue kwa sasa Kasim”
“Sawa mke wangu”
Nikabaki kimya mpaka tulipotokea pale mahali ambapo majambazi walitaka kulipora gari langu. Yule mtu aliyenata huku mkono wake mmoja ukipiga ngumi kwenye hewa alikuwa bado amenata vile vile na yule aliyeaguka alikuwa bado yuko chini. Lile gari lao pia lilikuwa pale pale.
“Kumbe hawa watu bado wapo?”nikamuuliza Maimun.
“Si uwaache tu. Majambazi wanakuhusu nini?”
“Nilikuwa nasema tu”
“Sema maneno yenye maana. Achana
na watu hao”
“Inaonekana walikuudhi sana”
ILIPOISHIA
Nikaenda nyuma ya gari na kulitoa lile shepe.
“Njoo hapa” akaniambia akiwa amesimama mahali fulani kando ya lile gari.
Nilipofika karibu yake akaniambia.
“Chimba mahali hapa”
Alinionesha pale aliposimama kisha akaondoka na kusimama kando yake.
Nikaanza kupachimba mahali hapo kwa kutumia lile shepe. Bahati nzuri mchanga ulikuwa laini, sikutumia nguvu nyingi. Niliendelea kuchimba mpaka shimo likafikia urefu wa wastani wa futi mbili.
“Nichimbe hadi wapi?”
“Bado. Endelea kuchimba” Maimun akaniambia.
Nikaendelea kuchimba. Mwili wangu ukaanza kutoka jasho. Nikaacha kuchimba na kuvua shati.
“Lete nikushikie” Maimun akaniambia.
Nikampa lile shati na kuendelea kuchimba.
SASA ENDELEA
Niliendelea kuchimba lile shimo mpaka likanifikia usawa wa kifua. Nilikuwa nikimwaga mchanga juu ya shimo hilo. Ghafla nikaona ninapiga kitu kama mwamba au jiwe lililokuwa chini ya ardhi.
“Sijui nimepiga nini hapa?” nikamuuliza Maimun kwa mshituko.
“Huo ni mwamba, upige tena” Maimun akaniambia.
Nikaupiga tena kwa shepe.
“Piga tena”
Nikaupiga kwa mara ya tatu. Ule mwamba ukapasuka.
“Umepasuka” nikamwambia Maimun.
“Hebu washa kitochi cha simu yako umulike hapo palipopasuka” Maimun akaniambia.
Nikajipapasa mfukoni na kutoa simu yangu. Niliwasha kitochi nikamulika pale chini.
Mama yangu! Niliona vipande vya madini yanayomeremeta vikiwa vimetawanyika!
“Nini hii?” nikamuuliza Maimun kwa mshituko.
“Kwani umeona nini?”
“Sijui ni madini haya. Huu mwaba ulikuwa na madini!”
“Ndiyo ni madini”
“Sijui ni madini ya aina gani?”
“Ni Tanzanite, ni yale aliyokuwa akiuza babu yako”
“Niyachukue”
“Ndiyo yachukue”
Nikainama haraka na kuyachukua yale madini.
Vilikuwa vipande saba vya madini.
“Huu ni utajiri hasa! Nikajiambia kimoyomoyo kisha nikamshukuru Mungu.
“Mungu anipe nini tena!”
Yakiwa mikononi mwangu madini hayo yalikuwa yakiakisi rangi mbali mbali za dunia. Zile rangi zilikuwa kama zinazunguka. Ilikuwa ni furaha hata kuyatazama.
“Ni vipande vingapi?” Maimun akaniuliza.
“Viko saba”
“Haya sasa toka kwenye hili shimo”
“Ngoja niendelee kuupiga huu mwamba”
“Hapana, usirudie tena. Toka kwenye shimo” Maimun akanionya.
Nikayatia yale madini mifukoni mwangu kisha nikalitoa lile shepe na kuliweka juu ya shimo hilo.
“Lete mkono wako nikutoe” Maimun akaniambia.
Nikampa mkono wangu Maimun, akaushika na kunivuta. Mara moja
nikjioan niko juu ya lile shimo.
“Anza kulifukia haraka haraka”
Nikalichukua shepe hilo na kufukia lile shimo.
“Tutakuja lini tena kuchimba?” nikamuuliza Maimun kwa tamaa huku nikiendelea kufukia shimo hilo.
“Baada ya miezi sita”
“Ah kwanini! Mbona mbali sana?”
“Ndiyo masharti yake. Haya madini yanakaliwa na majini. Huwezi kuja kienyeji tu na kuyachimba na hata ukija hutoyaona. Masharti yake ndiyo haya ninayokupa. Kila baada ya miezi sita tunakuja kuchimba tena”
“Sawa”
Niliendelea kulifukia lile shimo mpaka nikaliweka sawa.
“Watu wengine hawatakuja kufukua?” nikamuuliza Maimun.
“Ni nani atakayethubutu?”
“Wanaweza kutokea watu wakaja kufukua”
“Hawatapata kitu chochote. Chukua shati lako tuondoke”
Nililichukua lile shati alilokuwa amelishika Maimun nikalivaa.
“Twenzetu” akaniambia.
Nililiweka shepe nyuma ya gari.
“Utaendesha wewe?” Maimun akaniambia.
“Sawa” nikamjibu haraka haraka na kwenda kufungua mlango wa gari wa upande wa dereva.
Maimun alifungua mlango wa upande wa pili wa dereva na kujipakia.
“Washa gari tuondoke. Muda umekwenda sana”
Nikaliwsha gari na kuliondoa. Nilipokuja na Maimun mahali hapo nilikuwa nimefadhaika lakini wakati tunaondoka moyo wangu ulikuwa na furaha iliyopita kiasi.
“Hivi babu yangu ulikuwa unakuja naye hapa hapa kuchimba haya madini?”
“Ninajua mimi kama tulikuwa tunakuja hapa au mahali pengine”
“Hutaki kuniiambia”
“Si lazima kila kitu ukijue kwa sasa Kasim”
“Sawa mke wangu”
Nikabaki kimya mpaka tulipotokea pale mahali ambapo majambazi walitaka kulipora gari langu. Yule mtu aliyenata huku mkono wake mmoja ukipiga ngumi kwenye hewa alikuwa bado amenata vile vile na yule aliyeaguka alikuwa bado yuko chini. Lile gari lao pia lilikuwa pale pale.
“Kumbe hawa watu bado wapo?”nikamuuliza Maimun.
“Si uwaache tu. Majambazi wanakuhusu nini?”
“Nilikuwa nasema tu”
“Sema maneno yenye maana. Achana
na watu hao”
“Inaonekana walikuudhi sana”