Elections 2010 Sitomsahau nyerere kwa hili

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Kama kuna watu wanaosoma nyakati basi huyu babu alikuwa amejaliwa kimaanayake...
wakati wa kuchagua rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania alipopambanishwa
kikwete,mkapa huyu babu alioengea mengi sana juu ya rais wetu likiwemo tusichague sura
uzuri wa mtu auwezi kumuingiza mtu ikulu..yenye akili chanya ikajua nini cha kufanya kwenye
round inayofwata ndipo mh mkapa akapatikana..ni wengi walisononeka na wachache kukubali hali
halisi na kwa kuwa mkapa alichaguliwa awakuwa na means yoyote......ktk hilo alimshona live
kijana kwamba muda wake aujafika kabisa ni mapema sana kupewa ikulu avumilie miaka ijayo
masikini kama alijua atokuwepo ...nini maaana yake

Najaribu kujiuliza huu upuuzi unaofanywa na rais kikwete just kumbuka ni baada ya miaka kumi akapewa
urais anafanya vituko Je mtu huyu tungempa mapema si angetuvua nguo kabisa.....
Eeee mola mjaza neema ndogo ndogo na kubwa nene na nyembamba fupi na refu twakuomba mjalie mzee wetu huyu huruma zako kipindi tunaelekea kumuadhimisha miaka yake kadhaa kabla baada ya mauti

Raha ya milele umpe ee bwana na mwanga wa milele umuangazie apumzike kwa amani wote tuseme

AMEN
 
Watanzania hatujui kusoma "kwenye mistari". Yule mzee kwa kusema kikwete 'hajakomaa' alisema YOTE kimsingi. Wengi hawakumwelewa.
 
Na huyo Mkapa, chaguo la Nyerere, ndiyo mnaona alikuwa kiongozi wa maana? :confused2:
 
At least!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

At least kitu gani? Kuanzia rada, ndege ya rais, mgodi wa makaa ya mawe, BOT etc yote hayo bado utasema at least?

Hapo ndipo mtu anashangaa iweje huyo Mkapa atetewe na hawa wapenzi wa Chadema ambao kabla ya Kikwete kuingia madarakani wote walikuwa CCM? Hatudanganyiki lakini kudanganya kama kawaidai.

Kuna uzembe wa kufikiria halafu kuna ulemavu wa kufikiria. :becky:
 
At least kitu gani? Kuanzia rada, ndege ya rais, mgodi wa makaa ya mawe, BOT etc yote hayo bado utasema at least?

Hapo ndipo mtu anashangaa iweje huyo Mkapa atetewe na hawa wapenzi wa Chadema ambao kabla ya Kikwete kuingia madarakani wote walikuwa CCM? Hatudanganyiki lakini kudanganya kama kawaidai.

Kuna uzembe wa kufikiria halafu kuna ulemavu wa kufikiria. :becky:

Ujue ndugu haya madudu hata wakati wa mwalimu yalikuwapo.......MV BUKOBA;MAIKARUS;FERRY MBOVU nk
 
At least kitu gani? Kuanzia rada, ndege ya rais, mgodi wa makaa ya mawe, BOT etc yote hayo bado utasema at least?

Hapo ndipo mtu anashangaa iweje huyo Mkapa atetewe na hawa wapenzi wa Chadema ambao kabla ya Kikwete kuingia madarakani wote walikuwa CCM? Hatudanganyiki lakini kudanganya kama kawaidai.

Kuna uzembe wa kufikiria halafu kuna ulemavu wa kufikiria. :becky:

Ama, kumbe wewe ndugu huitakii mema nchi yetu? Kwa hiyo unataka nchi iendelee kutawaliwa na marais wabovu just for the sake of it! Ama kweli Tanzania itajengwa na wenye moyo na kuliwa na wenye meno! Huenda wewe ndugu ni mmoja wa Watanzania uliye kwenye mtandao wa wenye meno!!
 
Ujue ndugu haya madudu hata wakati wa mwalimu yalikuwapo.......MV BUKOBA;MAIKARUS;FERRY MBOVU nk

Usiwadangaye watu! Wakati wa Mwalimu ma-ikarus yalikuwa yanakuja mapya kutoka Hungary if I remember correctly yalikokuwa yanatoka na aliyekuwa anayaagiza alikuwa NDUGU Christopher Mahimbo alikuwa Mkurugenzi ama CEO wa UDA. MV Bukoba ililetwa mpyaaaaa, Ferry pia zilinunuliwa mpyaaa maana wakati wa Mkoloni wananchi walikuwa wakivuka kwa mitumbwi kwenda Kigamboni na hata sehemu zingine maziwani kulichokuwa kikitumika ni mitumbwi tu na si vivuko wala meli kubwa.
 
Leo hii siku ya nyerere day imefanywa mwa kina makamba na wenzake kwa kutoa risiti zisizo na mfano ktk kuidhimisha kumbukumbu hii mungu aturehemu na laaana hizi
laiti mama nyerere angekuwa akipelekewa risiti za fesha zilizotumika siku ya kumkumbuka mumewe nahisi angemfwata huko aliko kwa mshtuko....
 
kwa sisi tuliobaki tutaendelea kuyaenzi mema ya mwalimu na kuyaishi kwa vitendo hasa kutokuwa na taamaa ya mali na kutopendelea rafiki na familia zetu katika uongozi wa taifa.
 
Ama, kumbe wewe ndugu huitakii mema nchi yetu? Kwa hiyo unataka nchi iendelee kutawaliwa na marais wabovu just for the sake of it! Ama kweli Tanzania itajengwa na wenye moyo na kuliwa na wenye meno! Huenda wewe ndugu ni mmoja wa Watanzania uliye kwenye mtandao wa wenye meno!!

Sasa kama marais walikuwa wabovu basi isemwe hivyo. Siyo kumsifia mtu aliyeingiza nchi hii kwenye dimbwi la umaskini lakini anaendelea kusifiwa na tunaletewa haya mabandiko. :eyebrows:
 
Nyerere ndiyo chimbuko la viongozi wabovu. Yeye ndiye aliyetupa Mwinyi, Mkapa na sasa Kikwete na wote hao kwa jitihada zao pamoja ndiyo wametufikisha hapa tulipo kwa sababu viongozi tajwa hawapo tayari kubadilisha mfumo wa kupata viongozi bora kutoka Kamati Kuu ya CCM ambao wao hukaa na kutachagulia Raisi. Sisi wengine kazi yetu ni kubariki maamuzi ya hao wakubwa kwa kura zetu. Nasi kwa kutojua la kufanya tunasema kwa kauli moja hiyo ni demokrasiaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa. Wakati siyooooooooooooooooooooooooo

Vyama vya siasa vyapaswa kuwarudishia wanachama wao jukumu la kumpendekeza kiongozi wampendae katika ngazi zote siyo tu za udiwani na ubunge bali na Uraisi pia.

Kuanzia hapo tanuru za kupata viongozi bora litaanza kuwaka bila utani........na viongozi bora watahakikisha wanazungukwa na wanao shabihiana kiubora na wala siyo teuzi za makapi kama kejeli za Kikwete zinavyotuthibitishia................
 
icon1.gif
Sitomsahau nyerere kwa hili!!!


Kama kuna watu wanaosoma nyakati basi huyu babu alikuwa amejaliwa kimaanayake...
wakati wa kuchagua rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania alipopambanishwa
kikwete,mkapa huyu babu alioengea mengi sana juu ya rais wetu likiwemo tusichague sura
uzuri wa mtu auwezi kumuingiza mtu ikulu..yenye akili chanya ikajua nini cha kufanya kwenye
round inayofwata ndipo mh mkapa akapatikana..ni wengi walisononeka na wachache kukubali hali
halisi na kwa kuwa mkapa alichaguliwa awakuwa na means yoyote......ktk hilo alimshona live
kijana kwamba muda wake aujafika kabisa ni mapema sana kupewa ikulu avumilie miaka ijayo
masikini kama alijua atokuwepo ...nini maaana yake

Najaribu kujiuliza huu upuuzi unaofanywa na rais kikwete just kumbuka ni baada ya miaka kumi akapewa
urais anafanya vituko Je mtu huyu tungempa mapema si angetuvua nguo kabisa.....
Eeee mola mjaza neema ndogo ndogo na kubwa nene na nyembamba fupi na refu twakuomba mjalie mzee wetu huyu huruma zako kipindi tunaelekea kumuadhimisha miaka yake kadhaa kabla baada ya mauti

Raha ya milele umpe ee bwana na mwanga wa milele umuangazie apumzike kwa amani wote tuseme

AMEN



Nyerere alikuwa mtu wa aina yake. Yeye alikuwa thinker and philosopher. Unaweza ukamlinganisha na thinkers kama akina Plato; Karl Max, na wengineo. Bahati mbaya kwake ni kuwa alizaliwa katika nchi maskini kama Tanzania. Kama angekuwa Mmarekani, saa hizi angekuwa anaenziwa na dunia nzima.
 
Nyerere alikuwa mtu wa aina yake. Yeye alikuwa thinker and philosopher. Unaweza ukamlinganisha na thinkers kama akina Plato; Karl Max, na wengineo. Bahati mbaya kwake ni kuwa alizaliwa katika nchi maskini kama Tanzania. Kama angekuwa Mmarekani, saa hizi angekuwa anaenziwa na dunia nzima.
[/INDENT][/QUOTE]

Nakubaliana nawe 100%
 
Huu umasikini na maisha mabovu mnaomlaumu JK yote yamesababishwa na CCM iliyowalea watanzania kuwa waoga, wasiojiamini, wenye hofu ya mabadiliko, waliolishwa itikadi ya kuamini wananchosema viongozi ni sawa (slogan ya zidumu fikra za mwenyekiti)...n.k yote haya kasababisha Nyerere...kama asingefuta vyama vingi baada ya uhuru (mfano South Africa) basi leo watanganyika mungekwisha isahau CCM...am I lying...?
 
Pamoja na nia nzuri sana ya kuleta maendeleo aliyokuwa nayo Nyerere pia tusisahau alikua dictator mmoja hatari sana. Huu uhuru wa mawazo kuongelea tunayopata sasa na vyama vingi aliupinga kwa nguvu zote- na waliojaribu kuinua sauti kulezea mbadala walitupwa vizuizini bila kesi kwa miaka mingi-watu wengi walioona mbele mpaka leo hawajulikani walipo-kwa kifupi, alikua mpinzani wa demokrasia. Sijui mnakumbuka yale mambo ya kupigia mtu mmoja kura? Kwahiyo kwa hilo la yeye kuenziwa mimi ninawasiwasi nalo. Hastahili hata. Na siajabu wazee wengi wa zamani ambao bado wapo hai na pengine wanauwezo wa kuukemea uongozi wetu wa sasa kwa mabaya wanayoyafanya, hawana kwa kuwa nao wanajua mikono yao inadamu nyingi sana.
 
Back
Top Bottom