Sitofanya upuuzi wa kwenda kupima DNA kwa mtoto aliyezaliwa na mke wangu wa ndoa

Haina haja ya kupima , mwanamke umemkuta si bikra sasa DNA ya nn , apo ni kutafuta Kabuli au majengo ya selikali
 
Mkuu mashaka ni upuuzi tu.

Unatakiwa uwe na uhakika kama kweli mkeo kachepuka na kama umehakikisha kachepuka kosa ni la mke sio mtoto.

Mtoto hana kosa mwenye kosa ni mke, ataondoka mke atabaki mtoto, haiwezekani mke nikose na mtoto nikose
Mtoto nae anakua anamtafuta baba yake halali biological,ndo utajua nini maana ya Dunia tambala bovu
 
Huu uzi utoto ni mwingi kuliko uhalisia. Infact nahisi wengi mnaochangia hapa wala hamjaoa na hata huyo mtoto wa kusingiziwa hamna.
 
Huu uzi utoto ni mwingi kuliko uhalisia. Infact nahisi wengi mnaochangia hapa wala hamjaoa na hata huyo mtoto wa kusingiziwa hamna.
Kama mtu mzima unahangaika na kwenda kupima DNA ujue kama mke wako wa ndoa kachepuka au laa basi utu uzima huo ni ovyo


Kwa nini uishi na mwanamke ambae una mashaka nae,
 
Watu wa Mara wanasema kila mtoto aliyeletwa ndani ya nyumba Mali ya baba

Sisi wakurya hatuna makuu! Hata ukisafiri baada ya miaka miwili ukakuta kuna watoto wamezaliwa na mkeo hata kumi wote ni mali ya baba! Na utakuta hata majina ya ubini ni ya kwako! Mtoa mada upo sahihi! Undugu sio kufanana.
 
Nikizaa na mke wangu ukaleta pua yako kuwa mtoto ni wako ukitegemea ntamfukuza au kukuachia mtoto unajidanganya, mtoto sikupi na mke akileta ujinga namtimua,
Yaani mimba nitunze mimi mtoto uje uchukue wewe?
Ngoja mke Na mtoto wakue ndo utaelewa kwamba Hujui unachosema
 
Tuliza presha mkuu hluyo mtoto uliopo nae ni wako usisikilize maneno ya watu.
 
Hata mimi kama nampenda na nimemtunza atabaki kuwa mwanangu na usisogeze pua yako ila nitamwambia ukweli na story nzima akipata akili,mfano sheria za US anaye sign cheti cha kuzaliwa ndio baba na hata kama wewe ni biological father utakuwa huna chako na huna haki yeyote hata ukishtaki na hakuna mtu yeyote anayeweza kuchukua hiyo haki
 
Sheria inasemaje kuhusu hili wakuu??
Unaweza kataa kata kata kua mtoto sio wao na je hao wenye mtoto wakaja kudai mtoto, kisheria imekaaje hii.

Huenda watu wanaogopa hilo kua unaweza kulea mwisho wa siku ikaamuliwa kua mtoto si wako.

Sheriia ya vinasaba,pamoja na sheria ya mtoto zote zinatambua wazazi halisi tu (biological parents).
Kwa mujibu wa sheria hizo kisheria mtu anaweza kuja kudai unamlelea mtoto wake kupitia ustawi wa jamii au advocate mahakamani.
Mahakama itatoa order ya kupima DNA na ikionekana kweli mahakama inadeclare kwamba mwenye mtoto ni nani kwa mujibu wa vipimo vya DNA.

Uingereza mbona matukio ya wanaume kudai watoto yapo sana,kuna moja niliona kwenye tv jamaa kajitokeza kudai mtoto wake yupo university .
Ishu iliamuliwa mahakamani kwa kupitia DNA mtoto anaambiwa baba yako huyu huyo mpya.
mtoto hamtaki anasema hamjui
Yaani ilisikitisha sana,yule baba aliyemlea yule mtoto akaambiwa anaweza kudai fidia ya gharama za kumtunza huyo mtoto.
Yule baba aliyejitokeza baada ya DNA ilionekana ndio biological father kwa hiyo akapewa haki ya kuishi na mtoto wake.
Yule baba mlezi akaambiwa sio baba wa yule mtoto.
 
Haina haja ya kupima , mwanamke umemkuta si bikra sasa DNA ya nn , apo ni kutafuta Kabuli au majengo ya selikali

yap wewe mwenyewe unaweza usione haja ya kufanya hivyo,
Ila sheria inaruhusu mtu mwingine kuweza kuomba afanye dna test kama anauhakika yeye ndio kazaa na huyo mke wako.
Hivyo ni baadhi ya vifungu vya sheria ya mtoto

"34 .-(1) The following persons may apply to a court for an order to confirm the parentage of a child -
(a) the child;
(b) the parent of a child;
(c) the guardian of a child;
(d) a social welfare officer; or Evidence of parentage
(e) with a special leave of the court, any other interested person.
(2) The application to the court may be made·
(a) before the child is born;
(b) after the death of the father or mother of a child;
(c) before a child is eighteen years of age or with special leave of the court, after the child has attained eighteen years.

35. The following shall be considered by a court as evidence of parentage -
(a) any marriage performed in accordance with the Law of Marriage Act;
(b) the name of the parent entered in the Register of Births kept by the Registrar-General;
(c) performance of customary ceremony by the father of the child;
(d) public acknowledgment of parentage; or
(e) DNA results.

36.-(1) The court may order the alleged parent to submit to a medical test and shall, on the basis of the evidence before it, make such order as it considers appropriate.
(2) Without prejudice to subsections
(1), where the evidence of a mother or independent evidence cannot be corroborated by other evidence available to the satisfaction of the court, the court may, upon request or suo moto, order DNA test to be conducted for the purpose of proving the biological father of the child.
(3) The court shall determine and make an order as to the party who shall bear the costs associated with the DNA test.
(4) Where the court has made an order on a biological father, such biological father shall assume the responsibility to the child in the same manner as may be in respect of a child born in wedlock and the child shall, subject to religious belief of the biological father, have such other rights devolving from the parent including a right to be an heir."
 
Kuna mdada wa kiarabu nadate nae uwa analazimisha sana nimzalishe mtoto lakini yeye ameolewa,uwa namuuliza mimi nitafaidika nini na huyo mtoto atakayezaliwa maana atakuwa sio wangu
 
Kuna jamaa maeneo ya pale magomeni DSM mke wake alizaa mtoto muarabu na yeye ni mswahili,jamaa akasema huyu ni mwanangu na haendi popote,bahati nzuri wakati ule hakuna ambae alikuja kudai kama ni mwanae yule mtoto,jamaa akaendelea kulea mpaka wakahamia kigoma mtoto anazidi kukua na uarabu unazidi jamaa akasema huyu ni mwanangu.

Baadae mtoto kakua familia ya waarabu ikaenda mpaka kigoma kuomba msamaha na kusema yule mtoto ni wao na kweli mtoto kafanana na wale jamaa,mzee kagoma hasa na hakutoa mtoto.

Kwa hiyo mkuu ni maamuzi tu haya mambo
Wakati huo mke wake wake na mchizi bado anaendelea kuishi naye au alitimuliwa baada ya kumzaa huyo mtoto?
 
Wakati huo mke wake wake na mchizi bado anaendelea kuishi naye au alitimuliwa baada ya kumzaa huyo mtoto?
Jamaa aliishi naye yule mwanamke
Wakati huo mke wake wake na mchizi bado anaendelea kuishi naye au alitimuliwa baada ya kumzaa huyo mtoto?
Mkuu yule jamaa nimeulizia bado yupo na mkewe na mwanawe yule yule,hajamuacha mkewe.

Naskia yule jamaa hajataka upuuzi wa kumuuliza mkewe kama alichepuka na mwarabu,jamaa amekomaa mtoto ni wake hadi hivi leo.

Nenda magomeni(dar) pale hiko kisa kipo sana tu
 
Ni upuuzi wa hali ya juu sana kwenda kupima D.N.A kwa kigezo cha kutaka kuhakikisha eti kama mtoto ni wako a sio wako.

Watu wanatafuta watoto kwenye ndoa zao wewe unapata unajifanya kwenda kufanya DNA kutaka uhakika.

Tulipopata mtoto wife akaniuliza kimasihara kwamba mtoto hajachukua sura zetu? Nikamuambia maadamu ulihakikisha unamzaa basi huyo ni wetu na mimi ndio baba yake.

Ingelikuwa watoto lazima wafanane na wazazi wao basi dunia nzima wpte tungekuwa na sura ya ADAM na hawa mana ndio binadamu wa mwanzo(kwa mujibu wa imani kadhaa).

Alafu uzuri ni kuwa hata kwa Mungu haupati dhambi ukijimilikisha mtoto kama huyo,yani kila upande unanipa sapoti.

Mimi mtu akipanda ndizi kwenye shamba langu sina haja ya kutafuta nani kapanda,zikiota nitakula na siulizi kitu chochote.

Kama mtu kaja kuweka laki moja yake kwenye mfuko wa suruali yangu alafu akaondoka mimi natumia hizo pesa na wala siulizi chochote.

Na kwa mtoto hivyo hivyo mtu kajipendekeza kupachika mimba kwa mkeo wewe mhodhi mtoto anakuwa wako daima.

Mtoto ni mali ya wazazi kama mungu amejaalia mtoto amezaliwa kwenye ndoa yenu usimuache komaa nae mpaka akue hata kama sio wako kibaiolojia ila ukimlea kimapenzi atakuita baba na atakuwa na mapenzi ya kweli kama baba yake mzazi tu.

Kinachowaweka karibu baba na mtoto sio uhusiano wa kibaoolojia bali ni ukaribu katika malezi yao,hivyo hata kama sio mwanao biologically lakini kimalezi atakuwa mwanao na mtaishi kwa upendo na yeye atajua hivyo.

NB : endapo unaishi na mtu hujamuoa alafu mnapiga washkaji kibao na demu akapata mimba hapo naweza kuona umuhimu wa DNA kwa sababu mali haina mtu maalumu hivyo DNA itatoa majibu nani mwenye mtoto.
Mimi nitalea.Staki mambo ya DNA
 
Back
Top Bottom