Sitasahau nilivyokumbana na jini mwanaume

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,445
SEHEMU YA 01:

Nilichozoea kusikia ni kwamba kuna majini wanawake wanaojigeuza binadamu na kuwatongoza wanaume.

Wengi wa majini hao hutaka kuishi na binadamu kama mke na mume, jambo ambalo baadhi ya watu linawavutia kutokana na tamaa ya kupata utajiri.

Lakini nimekuja kugundua kuwa hawapo majini wanawake pekee, bali pia wapo majini wanaume ambao huwatongoza wanawake wa kibinadamu na kutaka waishi nao kama mume na mke.

Hilo ndilo lililonitokea mimi na kuniingiza katika mkasa ulioyatatanisha maisha yangu. Nilifikia mahali sasa nikawa natamani kufa.

Jina langu naitwa Enjo. Ni mtoto wa tatu katika familia ya mzee Sabastian Chacha. Wa kwanza ni mwanaume, jina lake ni Raymond au Ray kama marafiki zake walivyozoea kumuita

Yeye anafanya kazi Uingereza. Ameshaoa na ana watoto wawili. Wa pili alikuwa mwanamke kama mimi, anaitwa Miriam. Anaishi Dar ninapoishi mimi, naye pia ameshaolewa na ana mtoto mmoja.

Kwa wanaomkumbuka mzee Sabastian Chacha aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni kisha akawa Mbunge wa Jimbo la Kibaha iliko nyumba yetu.

Mzee Chacha alifariki dunia miaka michache iliyopita kwa ajali ya gari. Miaka miwili baadaye, mama yetu naye alifariki dunia ghafla katika Hospitali ya Muhimbili kutokana na shinikizo la damu.

Baada ya masomo yangu ya chuo kikuu, nilipata kazi Wizara ya Afya. Haikutimia hata miaka miwili, nilifukuzwa kazi kutokana na sababu ambayo haikuelezwa wazi.

Lakini nilijua kuwa nilitofautiana na bosi wangu aliyekuwa akinitaka kimapenzi nikamkataa. Yeye ndiye aliyenisingizia madai ya kuwa mzembe hadi nikafukuzwa kazi.

Kulikuwa na mwanaume Mzanzibar ambaye nilikuwa na matarajio naye sana kwamba angekuja kunioa. Yeye alikuwa akisoma huko Uingereza. Kwa vile alikuwa na ndugu zake huko ambao walikuwa wakijiweza, alikuwa akinitumia pesa mara kwa mara.

Wakati ule nafanya kazi, nilipanga nyumba huko Sinza. Hiyo nyumba tulichangia watu wawili. Upande mmoja alipanga mtu mmoja aliyekuwa na familia yake na upande mwingine nilipanga mimi lakini tulikuwa tunatumia mlango mmoja.

Siku moja nilikuwa nimealikwa katika hafla iliyokuwa ikifanyika katika hoteli moja kule Masaki.Watu tulikuwa tumekaa kwenye viti tukipata vinywaji.

Katika meza ya pembeni kwangu aliketi mzungu mmoja aliyekuwa akinitazama sana.

Mzungu huyo alikuwa amevaa suti iliyokuwa imempendeza sana na alikuwa amejifunga kikuba cha rangi nyekundu shingoni. Jinsi alivyokuwa amezichonga vyema ndevu zake alionekana kama muungwana na mtu aliyejistahi sana.

Alikuwa akinywa kinywaji chake taratibu huku jicho lake likiwa upande wangu.
Sikuweza kujua ni kwa nini alikuwa akinitazama sana.

Kwanza, nilidhania pengine alikuwa amenifananisha na mtu aliyekuwa anamfahamu au aliniona mahali fulani na alikuwa akijaribu kunikumbuka.

Lakini nilipomuangalia ili niweze kumuelewa vyema alikuwa akikwepesha macho yake na kutazama upande mwingine. Na ninapogeuza uso wangu anaanza tena kunitazama bila kujua kuwa nilikuwa nikimtazama kwa pembeni mwa macho yangu.

Kusema kweli alinikosesha raha. “Kama amenipenda angeniambia tu kuliko kunitazama vile,” nikajiambia kimoyomoyo nikiwa nimekasirika.

Kwa vile muda ulikuwa umepita sana, niliona bora niondoke nirudi nyumbani.
Lakini kama aliyekuwa amesoma mawazo yangu, aliinuka haraka akanifuata nilipokuwa nimeketi na kuniambia.

“Samahani dada, kuna kitu nataka kukuomba,” akaniambia kwa Kiswahili fasaha.
Nikahisi alikuwa Mzungu mwenyeji kwani alikuwa akiifahamu vyema lugha yetu.
“Bila samahani, niombe tu,” nikamjibu.
“Lakini natanguliza samahani, sijui kama utaridhika.”
“Niambie tu, ni kitu gani?”
“Naomba namba yako.”
Nilielewa kuwa alikusudia namba yangu ya simu kwa sababu hiyo ni tabia ya wanaume wengi, lakini nikamuuliza.
“Namba yangu ya….?”
“Nilikuwa na maana namba yako ya simu.”
“Kama ni hilo tu, hakuna tatizo,” nikamwambia.
Nikampa namba yangu. Nilimpa ili anipigie na kunieleza kile alichokuwa nacho moyoni mwake.Nilipomtajia namba yangu aliiandika kwenye simu yake kisha akanipigia hapohapo.
Simu yangu ilipoita aliniambia.
“Namba yangu ndiyo hiyo, ahsante sana.”
Hakurudi tena kwenye meza yake, akatoka. Kwa vile mtu aliyefanya niamue kuondoka alishatangulia kutoka nikaona niendelee kukaa kidogo.

Lakini sikutimiza hata nusu saa, nikainuka na kutoka. Nilirudi nyumbani kwa teksi. Nikafikia kuoga na kujilaza kitandani.
Wakati usingizi unataka kunichukua, simu yangu ikaita.

Nilipoichukua na kutazama kwenye skrini niliona namba ya yule mzungu. Nikaipokea simu yake.
“Hello!” nikasema kwenye simu.
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 02:
Nilipomtajia namba yangu aliiandika kwenye simu yake kisha akanipigia hapo hapo.
Simu yangu ilipoita aliniambia:
“Namba yangu ndiyo hiyo, asante sana.”
Hakurudi tena kwenye meza yake akatoka. Kwa vile mtu aliyefanya niamue kuondoka alishatangulia kutoka nikaona niendelee kukaa kidogo.
Lakini sikutimiza hata nusu saa nikainuka na kutoka. Nilirudi nyumbani kwa teksi. Nikafikia kuoga na kujilaza kitandani.
Wakati usingizi unataka kunichukua, simu yangu ikaita. Nilipoichukua na kutazama kwenye skrini ya simu niliona namba ya yule mzungu. Nikaipokea simu yake.
“Hello!” nikasema kwenye simu.
SASA ENDELEA…

Hello! Mambo vipi?” Sauti ya yule mzungu ikasikika kwenye simu. Nilifurahi alivyoniuliza: “Mambo vipi?” Niliona alikuwa mzungu aliyebobea katika lugha ya Kiswahili.
“Poa,” na mimi nikamjibu kwa kutumia lugha ileile ya mitaani.
“Uko poa kabisa?” akaniuliza.
“Mimi niko poa, sijui wewe?”
“Mimi pia niko poa. Umesharudi nyumbani?”
Mara moja nikagundua kuwa mzungu huyo alikuwa anataka kurefusha mazungumzo.
“Nimesharudi. Hapa niko kitandani,” nikamjibu.
“Samahani sana. Mimi naitwa Mr Smith, sijui mwenzangu unaitwa nani?”
“Naitwa Enjo.”
“Okey. Jina lako zuri sana. Unaishi wapi?”
“Naishi Sinza.”
“Unafanya kazi?”
“Hapana. Kwa sasa niko nyumbani tu.”
“Okey. Mimi ni Muingereza. Ninapenda kuja Afrika Mashariki mara kwa mara kutembea. Huwa ninafikia hotelini tu.”
“Ndio…ndio.”
“Nimefurahi kukufahamu Enjo na ninapenda uwe rafiki yangu.”
“Kuna aina nyingi za urafiki, wewe umependelea urafiki wa aina gani?”
“Urafiki wowote tu lakini tutazungumza zaidi tutakapokutana. Enjo una mchumba?”
“Sina mchumba.”
“Vizuri. Unadhani tunaweza kukutana wapi kwa ajili ya mazungumzo zaidi.”
“Sema wewe.”
“Mimi si mwenyeji sana hapa Dar.”
“Umefikia katika hoteli gani?”
“Hoteli ya Lux hapa Masaki. Niko chumba namba 35. Unaweza kufika.”
Mzungu kanitajia hadi namba ya chumba chake akidhani ningeweza kwenda kwake.
“Kwa nini tusikutane mahali pengine?” nikamwambia.
“Tunaweza. Sasa sema wewe ni mahali gani.”
“Ngoja, kesho nitakupigia kukufahamisha.”
“Kesho saa ngapi.”
Nikafikiri kidogo kisha nikamjibu:
“Kesho mchana.”
“Ningefurahi zaidi kama utanitajia saa ili nisubiri simu yako.”
“Tufanye saa tano.”
“Sawa. Nipige mimi au utanipigia wewe?”
“Nitakupigia mimi.”
“Sawa. Nitasubiri simu yako saa tano.”
“Nashukuru. Usiku mwema.”
“Usiku mwema na kwako.”
Nikatangulia mimi kukata simu kisha nikaiweka kwenye kimeza cha mchagoni. Baadaye niliona niizime kabisa kwani sikupenda nikatishwe usingizi wangu kwa milio ya simu.
Usingizi haukuchelewa kunipitia, nikalala.
Wakati niko usingizini nikaota niko kwenye ufukwe wa bahari mimi na yule mzungu tukikimbizana huku tukirushiana michanga. Sote wawili tulikuwa tumevaa mavazi hafifu ya kuogelea.
Mimi nilivaa chupi na sidiria yake na mzungu alivaa chupi peke yake. Lakini rangi ya chupi yake na yangu zilikuwa zikifanana.
Baada ya kufukuzana na kuangushana kwa dakika kadhaa tuliingia kwenye maji na kuanza kuogelea kwa pamoja. Tuliogelea hadi tukafika maji mengi.
Mimi nilikuwa nyuma, yule mzungu alikuwa mbele yangu. Ghafla tukajikuta tuko katikati ya bahari. Ule ufukwe wa bahari hatukuuona tena.
Yule mzungu alikuwa akiendelea kuogelea tu na mimi nikimfuatia nyuma. Ghafla nikaona tumetokea kwenye kisiwa kizuri kilichokuwa na minazi mingi.
Tulipofika kwenye ufukwe wa kisiwa hicho tuliona jumba kubwa likiwa mbele yetu. Lilikuwa jumba zuri lililokuwa likimeremeta!
Yule mzungu akaniambia pale ndio nyumbani kwake. Akanikaribisha, tukaingia ndani.
Humo ndani tulitokea kwenye chumba kipana kilichokuwa na kitanda na kabati.
Kitu ambacho kilinishangaza ni kuwa godoro la kitanda hicho pamoja na mto wake zilikuwa ni noti tupu!
Yule mzungu akajilaza kwenye lile godoro la noti. Mimi nikawa nazishangaa zile noti jinsi zilivyokuwa nyingi.
Nikashikwa na tamaa ya kutaka kuchukua zile noti. Hapo hapo nikaona kama kivuli cha mtu kwenye dirisha. Nilipotazama vizuri nikamuona marehemu mama yangu amesimama nje ya dirisha akinifanyia ishara nitoke mle chumbani.
Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 03:

Yule mzungu alikuwa akiendelea kuogelea tu na mimi nikimfuatia nyuma. Ghafla nikaona tumetokea kwenye kisiwa kizuri kilichokuwa na minazi mingi.
Tulipofika kwenye ufukwe wa kisiwa hicho tuliona jumba kubwa likiwa mbele yetu. Lilikuwa jumba zuri lililokuwa likimeremeta!
Yule mzungu akaniambia pale ndiyo nyumbani kwake. Akanikaribisha, tukaingia ndani.
Humo ndani tulitokea kwenye chumba kipana kilichokuwa na kitanda na kabati. Kitu ambacho kilinishangaza ni kuwa godoro la kitanda hicho pamoja na mto wake zilikuwa ni noti tupu!
Yule mzungu akajilaza kwenye lile godoro la noti. Mimi nikawa nazishangaa zile noti jinsi zilivyokuwa nyingi.
Nikashikwa na tamaa ya kutaka kuchukua zile noti. Hapohapo nikaona kama kivuli cha mtu kwenye dirisha. Nilipotazama vizuri nikamuona marehemu mama yangu amesimama nje ya dirisha akinifanyia ishara nitoke mle chumbani.
SASA ENDELEA…
Lakini alinifanyia ishara hiyo kwa siri na kwa tahadhari ili yule mzungu asimuone.
Sasa mimi sikuelewa kwamba mama alinifanyia ishara ile kwa ajili ya kumkimbia yule mzungu au alitaka nitoke nionane naye kwa vile hatukuwa tumeonana kwa miaka mingi.
Kwa akili yangu nikachukulia kwamba mama alitaka nitoke nikasalimiane naye. Kwa vile dukuduku la kumuona mama yangu lilikuwa limeshanishika nikageuka haraka ili nitoke mle chumbani.
Yule mzungu akamuona mama akichungulia kwenye dirisha, akauliza.
“Nani yule?”
Wakati anauliza hivyo alikuwa akishuka kwenye kitanda ili aende pale dirishani.
Na mimi nikapata nafasi ya kuchukua burungutu la noti kutoka kwenye godoro na kutoka nalo mbio. Huku nyuma nikasikia mzungu akiniita.
“Wewe Enjo hebu rudi hapa!”
Ile sauti ya yule mzungu ndiyo iliyoniamsha usingizini. Nikafumbua macho. Kwa vile niliamka wakati natoka mbio, nilijikuta nikihema huku moyo ukinienda mbio.
Mkono wangu wa kulia ulikuwa kama ulioshika lile burungutu nililokuwa nakimbia nalo. Nikahisi niliamka nikiwa na noti hizo mkononi. Kwa haraka nikayapeleka macho yangu kuutazama mkono wangu.
Sikuona chochote. Mkono huo ulikuwa mtupu!
Nikajiinua na kuketi kitandani huku nikijiuliza kwa nini niliota ndoto ile?
Nikawasha taa ya mchagoni mwa kitanda nikatulia hapo kitandani na kuwaza.
“Kuna uwezekano mkubwa yule mzungu akawa ni tajiri, ndiyo maana nimemuota amelalia godoro la noti,” nikajiambia.
Niliendelea kujiambia kuwa kama nitashikamana naye anaweza kunitajirisha. Wazungu hawana tabia ya ugumu wa pesa.
Asubuhi kulipokucha niliamkia kufua nguo zangu nilizozitumia kwa wiki ile. Nilipomaliza niliinjika chai. Kwa kawaida napendelea kunywa chai ya rangi. Halafu nakunywa maziwa peke yake.
Nilikuwa sipendelei kunywa chai ya maziwa. Baada ya chai kuwa tayari niliimimina kwenye chupa nikaenda kuoga. Baada ya kuoga na kuvaa, nilikwenda mezani, nikapaka siagi slesi za mkate na kujinywea chai yangu.
Wakati nakunywa chai, simu yangu ikaita. Nilikuwa nimemsahau yule mzungu. Alipoona saa tano ilikuwa imefika alisubiri zipite dakika mbili ndipo akanipigia.
Nilipotazama simu, nikaona ni yeye aliyekuwa akinipigia. Ule msemo wa kuwa na ahadi ya kizungu ndipo nilipouthibitisha.
Kabla ya kuipokea simu hiyo nilijiuliza nitamwambia nini mzungu huyo kwa kutotimiza ahadi yangu ya kumpigia simu ikifika saa tano? Sikupata jibu. Nikaacha ile simu iite hadi ikakata yenyewe. Ndipo na mimi nikapiga.
Mzungu akaipokea mara moja.
“Hello Enjo!” akaniita.
“Hello Mr Smith, mambo vipi?”
“Kama kawa, kama dawa!” mzungu akanijibu.
Nikaangua kicheko. Kilichonichekesha hasa si vile alivyotumia maneno hayo ya mitaani bali alikuwa akitamka maneno hayo kwa lafudhi ya Kiingereza.
“Unacheka nini?” akaniuliza.
“Nimefurahi kwa jinsi ulivyonijibu.”
“Nimekosea?”
“Hapana, umepatia sana.”
“Nimeona kimya mpaka nimepiga mimi.”
“Ndiyo. Nilikuwa bafuni wakati unanipigia,” nikatoa uongo.
“Nilifikiri umesahau.”
“Hapana, sikusahau. Nilikuwa nikupigie nikitoka bafuni.”
Mzungu akanyamaza kimya kidogo. Pakapita ukimya wa sekunde kadhaa kabla ya sauti yake kusikika tena.
“Umeshafikiria tukutane wapi?” akaniuliza.
Nikamtajia hoteli moja ya palepale Sinza lakini ilikuwa mbali kidogo na nyumba ninayoishi.
“Unaweza kufika?” nikamuuliza.
“Ninaweza,” akaniambia.
Akanyamaza kidogo kisha akaniuliza.
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 04:

“Ndiyo. Nilikuwa bafuni wakati unanipigia,” nikatoa uongo.
“Nilifikiri umesahau.”
“Hapana, sikusahau. Nilikuwa nikupigie nikitoka bafuni.”
Mzungu akanyamaza kimya kidogo. Pakapita ukimya wa sekunde kadhaa kabla ya sauti yake kusikika tena.
“Umeshafikiria tukutane wapi,” akaniuliza.
Nikamtajia hoteli moja ya palepale Sinza lakini ilikuwa mbali kidogo na nyumba ninayoishi.
“Unaweza kufika?” nikamuuliza.
“Ninaweza,” akaniambia.
Akanyamaza kidogo kisha akaniuliza.
SASA ENDELEA…
“Tukutane saa ngapi?”
“Kama saa kumi jioni hivi.”
Ningeweza kukutana naye wakati wowote lakini niliona nimtajie tu muda huo ili aone sikuwa mtu rahisirahisi.
“Saa kumi nikukute mimi au utanikuta wewe?” akaniuliza baada ya kimya kifupi.
“Vyovyote itakavyokuwa. Kama utawahi wewe kufika utanisubiri. Kama nitawahi mimi nitakusubiri.”
“Ahadi za kizungu nitaziweza wapi?” Nilikuwa nikijisemea kimoyomoyo baada ya kuniuliza: “Nikukute mimi au utanikuta wewe?”
“Oke, hiyo ni ahadi nyingine itimize tafadhali.”
“Usijali Mr Smith.”
Nilipotaja jina lake akafurahi.
“Nitajali kama hutatimiza ahadi yako,” akaniambia huku akionesha furaha aliyokuwa nayo.
“Ondoa wasiwasi, nitafika.”
“Oke, asante sana.”
“Asante.”
Nikakata simu.
Nikaendelea kunywa chai yangu huku nikimfikiria mzungu huyo. Kwa jinsi nilivyokuwa nikizifahamu tabia za wanaume nilishatambua kuwa yule mzungu alikuwa akinitaka kimapenzi lakini alishindwa kuniambia wazi. Badala yake aliamua kuzungusha maneno kwa kuniambia anataka tuwe marafiki bila kufafanua urafiki huo ni wa aina gani.
Nilikuwa nimeshaweka msimamo kuwa endapo ataweka pesa mbele, nitakuwa tayari kuwa naye mradi tu tutumie kinga kwani sikuwa tayari kuzaa mtoto wa kizungu.
Nikakumbuka kwamba aliwahi kuniuliza kama nilikuwa na mchumba. Nikajiambia kama atataka kuwa na uchumba na mimi itabidi kwanza nimchunguze tabia zake kabla ya kumkubalia.
Baada ya kumaliza kunywa chai niliondoa vyombo nikaenda kuviosha kisha nikarudi sebuleni kwangu na kupumzika kidogo huku nikichezea simu yangu.
Saa sita mchana nikawa kwenye saluni moja kutengeneza nywele zangu. Nilitaka nikikutana na yule mzungu anione niko moto!
Ilikuwa saa tisa nilipotoka saluni nikakodi bodaboda iliyonirudisha nyumbani. Nilibadili nguo nyingine kisha nikatoka. Wakati bodaboda inanishusha pale hotelini ilikuwa saa kumi kasoro dakika mbili hivi. Nilitaka niwahi ili yule mzungu aone niko makini.
Wakati naingia kwenye lango la hoteli, kwa pembeni mwa macho yangu nilimuona mzungu huyo amesimama kando ya mti uliokuwa pembeni mwa ile hoteli.
Sikugeuza uso wangu kumtazama. Nilijifanya kama sikumuona. Nilihisi kwamba alifika mapema akisubiri saa kumi ya ahadi yetu aingie ndani.
Hata baada ya mimi kuingia hotelini na kuketi, yule mzungu hakunifuata japokuwa alishaniona wakati ninashushwa na wakati ninaingia.
Alisubiri mpaka ilipofika saa kumi kamili ndipo nilipomuona akiingia. Tabia yake ile ikanishangaza. Nikajiuliza ndiyo tabia za wazungu au?
Wakati nawaza hivyo yule mzungu alikuwa akitupatupa macho kwenye ukumbi ule wa hoteli, akaniona.
Akatembea taratibu kuelekea katika meza niliyokuwa nimeketi.
“Oh karibu,” nikamwambia mara tu alipofika karibu na meza yangu.
“Asante.”
Alivuta kiti akaketi.
“Habari ya kutoka muda ule?” akaniuliza.
“Nzuri. Ndiyo unafika?” nikajidai kumuuliza.
“Ndiyo ninafika,” akanijibu. Nikajua anasema uongo kwani nilishajua kuwa alifika mapema.
“Asante kwa kutimiza ahadi yako,” akaniambia.
Mhudumu naye alikuwa ameshafika.
“Naweza kuwahudumia,” akatuambia.
Nikamtazama yule mzungu.
“Utakunywa nini?” akaniuliza.
“Nitakunywa soda tu.”
“Hapana. Utakunywa bia. Sema unataka bia gani?”
Nikacheka kidogo kabla ya kumuuliza:
“Wewe unataka ninywe bia?”
“Ndiyo.”
“Haya niagizie.”
Mzungu akaagiza mzinga wa pombe kali mimi akaniagizia pombe ya kawaida.
Mhudumu alipoondoka, mzungu huyo aliniambia alikuwa amefurahi kuwa na mimi siku ile. Alinitajia sehemu mbalimbali ambazo alisema aliwahi kuniona kabla ya siku ile na akanipenda.
Sehemu alizonitajia ilikuwa ni kweli niliwahi kufika. Hapo nikajua kuwa kukutana kwetu hakukuwa kwa bahati tu bali alikuwa akinifuatilia.
Mazungumzo yetu hayo yalikatizwa wakati yule mhudumu alipotuletea vinywaji tulivyoagiza.
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 05:

Nikacheka kidogo kabla ya kumuuliza:
“Wewe unataka ninywe bia?”
“Ndiyo.”
Mzungu akaagiza mzinga wa pombe kali mimi akaniagizia pombe ya kawaida.
Mhudumu alipoondoka, mzungu huyo aliniambia alikuwa amefurahi kuwa na mimi siku ile. Alinitajia sehemu mbalimbali ambazo alisema aliwahi kuniona kabla ya siku ile na akanipenda.
Sehemu alizonitajia ilikuwa ni kweli niliwahi kufika. Hapo nikajua kuwa kukutana kwetu hakukuwa kwa bahati tu bali alikuwa akinifuatilia.
Mazungumzo yetu hayo yalikatizwa wakati yule mhudumu alipotuletea vileo tulivyoagiza.
SASA ENDELEA…
Wakati tunaendelea kunywa, Smith alinitamkia kuwa alikuwa amenipenda sana. Bila shaka ile pombe aliyokuwa anakunywa ndiyo iliyompa ujasiri wa kunitamkia maneno hayo waziwazi.
Kwa upande wangu nilikuwa nikichekacheka tu. Nikagundua kuwa mzungu huyo anapolewa anakuwa na maneno mengi sana na hana aibu ya kuzungumza.
Akataka na mimi nimtamkie kuwa nimempenda. Nikamwambia kuwa nimempenda.
Nilipomwambia hivyo akaanza kung’ang’ania aende na mimi nyumbani kwake akimaanisha kule hotelini alikokuwa akiishi.
“Tutakwenda siku nyingine siyo leo,” nikamwambia.
“Kwa nini isiwe leo?” akaniuliza huku akinitolea tabasamu.
“Leo sikupanga kuja kwako, nilipanga nije hapa tuzungumze.”
“Sasa utakuja lini?”
“Kwani wewe huna mke?” nikamuuliza.
Smith akatikisa kichwa.
“Mke wangu utakuwa wewe.”
“Huko kwenu London huna mke?”
“Sina.”
“Una maana hujaoa bado?”
“Bado.”
“Kwa nini?”
“Mimi nataka mke wa Kiafrika kama wewe.”
“Na hapa Dar huna msichana mwingine?”
Simith akatikisa kichwa.
“Bado sijampenda yeyote zaidi yako.”
Wakati tunazungumza nilikuwa ninakunywa ile bia taratibu huku nikimtazama mzungu huyo na kupima maneno yake.
Ingawa nilimtamkia kuwa nampenda lakini sikuwa nimeshafanya uamuzi wa kuwa naye kwa harakaharaka vile.
“Utakuja lini nyumbani kwangu?” akaniuliza tena baada ya kupita ukimya mfupi.
“Nitakwambia.”
Jibu langu hilo likaufanya uso wake ufadhaike.
“Sikiliza. Naona bado hujaniamini lakini mimi ni mtu wa ukweli. Nitahakikisha kuwa maisha yako yanakuwa ya furaha utakapokuwa na mimi. Nitakununulia nyumba, nitakununulia gari na kama utanizalia mtoto nitakupeleka kwetu ukaishi huko na utakuwa kama malkia wangu.”
Maneno yake yalianza kunitia tamaa. Nikaanza kufikiria kuachana na mpenzi wangu Eddie, Mzanzibari aliyekuwa akisoma huko Uingereza ambaye tulipanga kuja kuoana atakapomaliza masomo yake.
Wakati namuwazia mzungu huyo niliona akitia mkono kwenye mfuko wa suruali yake akatoa burungutu la noti. Akaniambia:
“Chukua.”
Nikanyoosha mkono wangu na kulichukua lile burungutu.
“Ni milioni kumi,” akaniambia na kuongeza:
“Utakwenda kuzihesabu nyumbani. Tia kwenye mkoba wako.”
Sikupenda kudhihirisha usoni kwangu ni kwa jinsi gani nilifurahi. Nikafungua mkoba wangu na kuzitia pesa hizo.
“Okey. Nenda kafikirie, ni siku gani utakuja kwangu kisha utaniambia.”
“Sawa. Nitakwambia kwenye simu,” nikamwambia haraka.
Nilikunywa bia moja tu, sikutaka kuongeza nyingine. Nilihisi mazungomzo yangu na yule mzungu yalikuwa yamefikia tamati. Baada ya kupata zile pesa sikutaka kukaa tena pale. Nikamwambia:
“Mimi nakwenda zangu.”
“Hutaki kuongeza bia?” Smith akaniuliza huku akitoa tabasamu laini. Tabasamu lake lilikuwa kama la kunicheka mimi nilivyotaharuki baada ya kunipa zile pesa.
“Basi imetosha. Mimi silewi sana. Huwa nakunywa bia moja tu.”
Smith hakusema kitu, akabaki kunitazama huku akiendelea kutabasamu.
Nikainuka kwenye kiti na kuchukua mkoba wangu ambao niliutundika begani.
Smith naye akainuka.
“Sikiliza nikuambie kitu,” akaniambia. Alinyamaza kidogo kisha akaendelea.
“Ukija kwangu nitakupa zawadi nzuri sana na hutaisahau maishani mwako.”
“Nimekusikia. Usijali Mr Smith, tutakuwa pamoja. Kwa sasa acha niende kwanza. Lakini tutaongea mengi kwenye simu.”
“Sawa. Hakuna tatizo lakini nakuomba uzingatie niliyokwambia.”
“Nimeshayazingatia. Usijali.”
Nikaondoka. Smith akarudi kwenye kiti na kuendelea kunywa pombe yake.
Nilikodi teksi iliyonirudisha nyumbani. Wakati wote nikiwa kwenye teksi hadi nafika nyumbani, yule mzungu alikuwa ametawala akili yangu.
Zile milioni kumi alizonipa pamoja na maelezo yake mengine yakiwemo yale aliyonieleza kuwa nikienda huko hotelini anakokaa atanipa zawadi ambayo sitaisahau maishani mwangu, yalikuwa yamenihamasisha.
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 06:

Nikaondoka. Smith akarudi kwenye kiti na kuendelea kunywa pombe yake.
Nilikodi teksi iliyonirudisha nyumbani. Wakati wote nikiwa kwenye teksi hadi nafika nyumbani, yule mzungu alikuwa ametawala akili yangu.
Zile milioni kumi alizonipa pamoja na maelezo yake mengine yakiwemo yale aliyonieleza kuwa nikienda huko hotelini anakokaa atanipa zawadi ambayo sitaisahau maishani mwangu, yalikuwa yamenihamasisha. SASA ENDELEA…
Nilipofika nyumbani niliketi sebuleni na kufungua mkoba wangu nikatoa zile pesa. Niliziweka kwenye kochi kisha nikaanza kuzihesabu.
Zilikuwa shilingi milioni kumi kamili. Nikapanga kesho yake niende nikaziweke benki. Nikazirudisha pesa hizo kwenye mkoba kisha nikaendelea kumuwaza yule mzungu.
Niseme ukweli kuwa sikuwa nimewahi kushika shilingi milioni kumi mkononi mwangu. Ile ilikuwa ni mara yangu ya kwanza.
Kwa pesa hizo na kwa ahadi nyingine alizoniahidi yule mzungu nikawa nimepata tamaa ya kuwa naye kwa kuamini kwamba angeweza kuyabadili maisha yangu.
Binafsi nilikuwa nikitamani kupata gari langu mwenyewe lakini sikujua ningeanzia wapi hadi niweze kulipata. Pia nilitaka kumiliki nyumba yangu niachane na nyumba za kupanga lakini sikuwa na uwezo.
Yule mzungu ameniahidi kuwa naweza kuvipata vyote kama nitakubali kuwa naye. Sikuona kama kulikuwa na kikwazo cha kuwa naye. Mwanaume ambaye tuliahidiana kuja kuoana hakuwa amenichumbia na inawezekana akapata msichana mwingine na akabadili mawazo yake. Mwanaume si wa kumtegemea sana.
Nikakumbuka ile methali ya Kiswahili isemayo “Hamadi kibindoni, silaha ni iliyo mkononi.” Nikajiambia kwa wakati ule Smith ndiye aliyekuwa mkononi na ndiye ambaye ningeweza kumtumia.
Baada ya kuwaza kwa dakika kadhaa nilinyanyuka na mkoba wangu uliokuwa na shilingi milioni kumi na kuingia nao chumbani. Nilizifungia zile pesa kwenye kabati. Wakati nataka kubadili nguo nilizokuwa nimevaa, simu yangu ikaita.
Nilipoitazama nikaona namba ya Smith, nikaipokea,
“Hellow Mr Smith…!”
“Ndiyo ninatoka hapa hoteli,” Smith akaniambia kwenye simu.
“Mimi niko nyumbani nimepumzika kidogo.”
“Nilidhani unanifikiri mimi.”
“Wewe nimeshakufikiria.”
“Kwa hiyo umeshapanga utakuja lini nyumbani kwangu?”
“Nitakuja kesho.”
“Nitafurahi sana kukuona. Utakuja saa ngapi?”
“Saa moja usiku.”
“Ukitaka kuja unifahamishe.”
“Nitakupigia simu.”
“Sawa.”
****
Asubuhi ya siku iliyofuata nilipotoka nyumbani nilikwenda benki nikaweka shilingi milioni saba katika akaunti yangu. Shilingi milioni tatu nilibaki nazo mkobani mwangu.
Nilipotoka benki nilizunguka katika maduka mbalimbali nikajifanyia manunuzi ya shilingi milioni mbili. Baada ya kununua kila kitu nilichohitaji nilikodi teksi iliyonirudisha nyumbani Sinza.
Niliingia chumbani mwangu nikazijaribu nguo nilizonunua pamoja na viatu. Nikaona zilikuwa sawa. Nilichukua wigi ambalo nililinunua kwa shilingi laki tatu nikaenda saluni kupachikwa wigi hilo.
Nilipotoka saluni nilikwenda kumtembelea dada nyumbani kwake. Baada ya kusalimiana naye aliniambia.
“Umependeza leo?”
“Kwa sababu ya hili wigi?” nikamuuliza.
“Nalijua bei yake, bila laki tatu hulitoi dukani.”
“Ni kama hivyo, nimepata mchumba wa kizungu ndiye anayenipendezesha.”
“Usiniambie!”
Nikamdokeza dada kuhusu uhusiano wangu na yule mzungu.
“Awe na nia kweli ya kukuoa, asikudanganye akakuchezea kisha akaja kukuacha,” dada akaniambia.
“Atanichezea mimi, atajichezea mwenyewe! Mi shida yangu nimle tu kwa sababu nimeona pesa yake iko njenje.”
“Kama ni kumla umle taratibu. Kama una pupa kama hivyo utajikuta unaliwa wewe!”
“Kwanza yule mtu mwenyewe naona kama ana nia njema na mimi, sijui lakini. Bado naendelea kumchunguza.”
Niliendelea kuzungumza na dada hadi jua lilipokuchwa nikaondoka kurudi nyumbani kujiandaa kwenda kwa mzungu wangu.
Baada ya kuvaa nguo nilizopenda nitoke nazo nikampigia simu kumjulisha kuwa ninakwenda kwake. Akaniambia kwamba ananisubiri.
Nakumbuka ilikuwa saa kumi na mbili na nusu nilipotoka nyumbani. Nilikodi teksi iliyonipeleka katika hoteli ya Lux ambayo mzungu huyo alikuwa amepanga chumba.
Nilipofika nilimpigia tena simu, akaniambia alikuwa chumba namba 35. Nikaenda. Kilikuwa ghorofa ya kwanza. Nilipomaliza kupanda ngazi nilianza kukitafuta chumba namba 35. Nikakiona. Nikaenda kubisha mlango.
Kitu kilichonishangaza ni kuwa licha ya kubisha mlango kwa sekunde kadhaa sikupata jibu. Nikaujaribu mlango ambao ulifunguka, nikaingia ndani. Smith mwenyewe hakuwemo chumbani ila niliona suti yake kwenye kitanda. Sikujua alikuwa ametoka au amekwenda wapi.
Nikajaribu kufungua mlango wa bafuni. Nilichokiona kwenye macho yangu kilipasua moyo na kunifanya niache mdomo wazi kwa mshituko.
Je, nini alichokiona bafuni?
 
SEHEMU YA 07:
Nikaenda. Kilikuwa ghorofa ya kwanza. Nilipomaliza kupanda ngazi, nilianza kukitafuta chumba namba 35. Nikakiona. Nikaenda kubisha mlango.
Kitu kilichonishangaza ni kuwa licha ya kubisha mlango kwa sekunde kadhaa sikupata jibu. Nikaujaribu mlango ambao ulifunguka, nikaingia ndani. Smith mwenyewe hakuwemo chumbani ila niliona suti yake kwenye kitanda. Sikujua alikuwa ametoka au amekwenda wapi.
Nikajaribu kufungua mlango wa bafuni. Nilichokiona kwenye macho yangu kilinipasua moyo na kunifanya niache mdomo wazi kwa mshtuko.
SASA ENDELEA…
Nilimuona Smith amesimama akioga. Alikuwa mtupu kama alivyozaliwa. Kwa vile alielekea upande uliokuwa na mlango wa bafu nilimuona waziwazi.
Kitu cha kwanza kilichonistaabisha ni ule weupe uliokuwa kwenye ngozi yake, haukuwa weupe wa kawaida na haukuwa weupe niliozoea kumuona nao ninapokutana naye. Ulikuwa weupe uliopitiliza! Isitoshe ngozi yake iliota manyoya marefu kama ngozi ya mnyama. Manyoya hayo yalimuota mwili mzima kwenye miguu, kwenye mikono, kwenye shingo na kwenye kifua na tumbo ndiyo kulikuwa na msitu kabisa!
Yalikuwa manyoya meupe kama yaliyopakwa rangi. Kwa vile manyoya hayo yalikuwa yameingia maji yalikuwa yamelala kwenye ngozi na kuonekana kama ya nyani mzee aliyenyeshewa na mvua.
Kioja hakikuwa hicho tu, macho yake ndiyo yaliyotisha zaidi. Yalikuwa kama ya paka mwitu yakiwa na mboni zilizounda mstari mwembamba wa kijivu halafu yalitoa nuru kali kama yalikuwa yanawaka.
Bado. Kucha zake za miguu na mikono zilikuwa ndefu kama kucha za kubandika. Yaani hazikuwa tofauti na mnyama!
Niliogopa. Nikajiambia, kumbe huyu mzungu yuko hivi! Huyu ni jini si binadamu!
Nikaufunga ule mlango haraka na kutetea maisha yangu. Nilikimbilia kwenye mlango wa chumbani nikaufungua na kutoka mbio!
Nilishuka ngazi mbilimbili hadi nikafika chini. Nikatoka nje ya ile hoteli huku nikishukuru Mungu kuwa nimenusurika.
“Yule jini angenifyonza damu leo!” nikajiambia.
Macho yangu yalikuwa yakiangaza huku na kule kutafuta teksi.
Kwa vile nilikuwa natetemeka kwa hofu, hadi makalio yangu yalikuwa yanacheza. Magoti nayo yalikuwa yakininyong’onyea, yaani nisingeweza tena kutembea kwa miguu. Ningeanguka tu.
Nikaiona teksi. Lakini wakati naifuata nilisikia nikiitwa nyuma yangu.
“Enjo!”
Nilipogeuka nyuma nikamuona yule mzungu amenifuata nje ya hoteli, sasa akionekana wa kawaida tu.
“Enjo hebu simama, unakwenda wapi sasa?” Smith akaniuliza.
Nilijuta kugeuka nyuma. Kwa kweli sasa nilikuwa namuogopa yule mzungu. Nikageuza uso wangu haraka kuelekea mbele. Nilikuwa nimeshaifikia ile teksi. Dereva alishanifungulia mlango wa nyuma.
“Ingia twende!” akaniambia.
Nikajipakia huku nikitetemeka. Mwili ulikuwa umeishiwa nguvu kabisa.
Wakati nafunga mlango nilimuona Smith naye akifuata teksi.
“Nikupeleke wapi?” Dereva wa teksi niliyojipakia akaniuliza.
“Nipeleke Sinza.”
Teksi ikaondoka.
Nilipomtazama tena yule mzungu kwenye kioo nilimuona akipanda teksi.
“Anakwenda wapi?” nikajiuliza kwa hofu.
Baada ya muda kidogo niligundua kuwa alikuwa ananifuata mimi. Teksi aliyopanda ilikuwa nyuma ya ile teksi niliyopakiwa.
“Mama yangu…leo nimekwisha!” nikajiambia na kutoa simu yangu.
Nikampigia dada huku jicho langu likiwa kwenye teksi aliyopanda Smith.
Dada akapokea simu.
“Dada kumbe yule mzungu niliyekuelezea mchana ni jini, nimemfuata hapa hotelini nikamuona bafuni anaoga lakini ana umbile la kijini. Nimemkimbia kwa teksi lakini ananifuata nyuma kwa teksi nyingine. Mwambie shemeji anifuate haraka…” Nilimwambia dada kwa sauti ya mtu aliyepatwa na hofu kiasi cha kukaribia kulia.
Tayari dada akawa amepatwa na wasiwasi. Akaniuliza tulikuwa wapi. Nikamwambia.
“Mzungushezungushe tunawafuata,” dada akaniambia na kukata simu.
Nikafungua pochi yangu na kutoa noti tatu za shilingi elfu kumikumi, nikampa yule dereva.
“Shika hii pesa, nataka uichenge hii teksi iliyo nyuma yetu kabla hatujaenda Sinza,” nikamwambia dereva huyo kisha nikamuuliza.
“Utaweza?”
Dereva aliitazama teksi hiyo kwenye kioo akaniambia.
“Kazi ndogo tu.”
Alitia gea. Teksi ikafyatuka na kuanza mbio. Alikata kona kadhaa kuikwepa teksi hiyo lakini baada ya muda kidogo tukaiona tena nyuma yetu. Tumbo lilikuwa likiniunguruma kwa kujua siku ile ulikuwa ndiyo mwisho wangu. Haja kubwa ilikuwa karibu kunitoka. Nilikuwa nimelikaza tumbo nisiadhirike.
“Huyu jamaa hachengeki,” dereva wa teksi akaniambia.
Kabla sijamjibu kitu dada akanipigia simu na kuniuliza tuko katika barabara gani. Nikamtajia.
Baada ya muda kidogo nikaona gari la shemeji limetokeza mbele yetu.
Je, kilifuatia nini? Usikose mwendelezo wake katika Gazeti la Ijumaa siku ya Ijumaa.
Lilitaka kutupita nikatoa mkono kwenye dirisha na kulipungia huku nikipiga kelele.
“Shemeji! Shemeji!”
Gari hilo llikasimama pembeni mwa barabara.
“Dereva rudi nyuma ulifuate lile gari,” nikamwambia dereva wa teksi huku nikijisikia ahueni kuliona gari hilo.
Dereva wa teksi akapunguza mwendo na kukata kona. Akalifuata gari hilo la shemeji lililokuwa limesimama.
Ile teksi iliyokuwa nyuma yetu ilipita moja kwa moja na kwenda kusimama mbele.
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 08:

“Dereva rudi nyuma ulifuate lile gari,” nikamwambia dereva wa teksi huku nikijisikia ahueni kuliona gari hilo.
Dereva wa teksi akapunguza mwendo na kukata kona. Akalifuata gari hilo la shemeji lililokuwa limesimama.
Ile teksi iliyokuwa nyuma yetu ilipita moja kwa moja na kwenda kusimama mbele.
SASA ENDELEA…
Kabla ya teksi kusimama sawasawa nilishafungua mlango. Teksi ilisimama ubavuni mwa gari la shemeji. Nikashuka na kufungua mlango wa nyuma wa gari la shemeji nikajipakia harakaharaka.
Nikampungia mkono dereva wa teksi aende zake. Ile teksi ikaondoka.
Ndani ya gari la shemeji kulikuwa na shemeji pamoja na dada.
“Iko wapi hiyo teksi yenye huyo jini anayekufuata?” Shemeji akaniuliza.
“Si ile pale.”
Nikawaonesha teksi hiyo iliyokuwa imesimama barabarani umbali wa hatua kadhaa kutoka pale tuliposimama sisi. Wakati nawaonesha ile teksi, teksi hiyo ikaondoka na kuendelea na safari yake.
“Niifuate?” Shemeji akauliza.
“Uifuate ya nini?” Dada naye akamuuliza shemeji kisha akaongeza:
“Umeshaambiwa ni jini, tuna kazi naye gani sisi!”
Dada aliponiona ninavyotetemeka alishuka kule mbele alikokuwa amekaa na shemeji akafungua mlango wa nyuma na kuketi na mimi. Shemeji akaliondoa gari.
“Kwani ilikuwaje?” Dada akaniuliza huku akinitazama kwa macho ya kunihurumia.
Nikamueleza vile ilivyokuwa.
“Yesu wangu! Sasa kama ni jini anakutaka wewe kwa kazi gani?”
“Sijui sasa,” nikamwambia huku nikibetua mabega yangu.
“Siku hizi kumekuwa na matukio mengi ya majini kutongoza binadamu, inatakiwa tahadhari sana,” shemeji akadakia.
“Sasa utamjuaje kuwa huyu ni jini na huyu ni binadamu wakati wanajigeuza kama binadamu?” Dada akamuuliza.
“Ndiyo hivyo, mwanaume akikutongoza mchunguze kwanza hasa ukiona mtu anakupa pesa nyingi, huyo ndiye umtilie mashaka sana.”
“Kweli dunia imekwisha. Zamani matukio ya aina hii hayakuwepo!” Dada akasema.
“Sasa sijui atanifuata tena au ataona nimeshamjua atanipotezea,” nikajisemea.
“Sidhani kama atashughulika na wewe tena, kwa vile umeshamgundua hawezi kukufuata,” dada akaniambia.
“Yaani kama nisingemfuma kule bafuni na kumuona vile alivyo, naona angenifyonza damu leo!”
“Nilivyosikia hawakufyonzi damu bali anakufanya uwe mwanamke wake,” dada akasema.
Nikatazama nyuma ya kioo kuiangalia ile teksi. Sikuiona tena.
“Ashindwe!” nikalaani.
Shemeji akanicheka.
“Lakini umeyataka mwenyewe shemu yangu.”
“Nimeyataka yapi?”
“Hayo yaliyokukuta.”
“Kwani mimi nilijua kama ni jini?”
“Si umechukua pesa zake.”
“Si amenipa mwenyewe?”
“Sasa mbona unamkimbia?”
“We shemeji nawe usinizingue…kwani aliponipa zile pesa nilijua kama ni jini. Au nilimwambia anipe, si alinipa mwenyewe? Tena ashindwe alegee!”
Shemeji akabaki kucheka.
“Sasa nikupeleke nyumbani kwako au…?” akaniuliza.
“Hapana. Leo sirudi nyumbani. Anaweza kunifuata.”
Dakika chache baadaye shemeji akalisimamisha gari mbele ya nyumba waliyokuwa wanaishi.
Tukashuka. Kule kutetemeka sasa kulikuwa kumeisha lakini ile hofu bado nilikuwa nayo ingawa ilipungua kidogo.
Tulipoingia ndani niligundua kuwa wenyewe walikuwa wakijiandaa kula nilipowapigia simu. Wakaacha chakula na kunifuata. Hivyo tulipoingia ndani wakafikia mezani.
“Enjo njoo tule,” dada akaniambia.
Nilikuwa sitaki kula kwa sababu ya ile hofu niliyokuwanayo lakini nikajikaza na kwenda mezani.
Wakati tunakula tulikuwa tukiendelea kuzungumza ile habari ya yule jini huku shemeji akiingiza utani wake ambao sikuupenda.
Baada ya chakula nilikwenda kupumzika kidogo kisha nikaenda kuoga. Mwili wangu ulikuwa umetota kwa jasho.
Saa nne usiku nikaingia katika chumba ambacho ningelala usiku huo. Hata hivyo, nilihisi nisingeweza kupata usingizi kutokana na mawazo ya hofu niliyokuwanayo. Nilijaribu sana kusali, kuomba Mungu ili hofu iniondoke na niweze kupata usingizi.
Kweli nilipata usingizi lakini sikulala sana, nikaamka. Nilipoamka usingizi wote ukaniruka. Sikujua ilikuwa saa ngapi lakini nilihisi ulikuwa usiku mwingi. Nikawa nimelala nikiwa macho. Nilikaa hivyo kwa muda mrefu nikiwaza.
Ghafla mlio wa simu yangu niliyokuwa nimeiweka kwenye kimeza cha mchagoni mwa kitanda ikaanza kuita. Nikaitazama ile simu kabla ya kuiinua na kutazama namba iliyokuwa inapiga. Nikashituka nilipoona namba ya yule mzungu, nikajiambia “Siipokei.” Nikairudisha simu kwenye kimeza.
Simu iliita mpaka ikakakata yenyewe. Baada ya muda kidogo ikaita tena. Nikaishika tena ile simu ili kuona kama ilikuwa namba ileile au nyingine. Nikaona ni namba ileile.
Wakati ule naitazama ile simu, simu hiyo ikajipokea yenyewe. Kwa maneno mengine ni kwamba ilijiunganisha yenyewe ikawa hewani. Nikaisikia ile sauti ya mzungu ikiniuliza. “Kwa nini hupokei simu? Sasa nakuja chumbani kwako!”
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 09:

Nikashtuka nilipoona namba ya yule mzungu, nikajiambia: “Siipokei.” Nikairudisha simu kwenye kimeza.
Simu iliita mpaka ikakakata yenyewe. Baada ya muda kidogo ikaita tena. Nikaishika tena ili kuona kama ilikuwa namba ileile au nyingine. Nikaona ni namba ileile.
Wakati ule naitazama ile simu, simu hiyo ikajipokea yenyewe. Kwa maneno mengine ilijiunganisha yenyewe ikawa hewani. Nikaisikia ile sauti ya mzungu ikiniuliza: “Kwa nini hupokei simu? Sasa nakuja chumbani kwako!”SASA ENDELEA…
Nilipoisikia ile sauti ikiniambia vile, nilishtuka nikaitupa chini kisha nikashuka kitandani na kukimbilia kwenye mlango huku nikipiga kelele.
“Usije! Usije! Usije…!”
Niliufungua mlango nikatoka ukumbuni. Kilichonisitiri ni kuwa nilikuwa nimevaa shumizi ya dada, vinginevyo ningetoka nikiwa mtupu kwani sikukumbuka kuvaa nguo.
Nilipotoka ukumbini nilikimbilia kwenye mlango wa chumba cha dada, nikaanza kuugonga kwa nguvu huku macho yangu yakiwa kwenye mlango wa mbele kwani kama huyo jini angekuja, angetumia mlango huo na ningemuona.
Nikaendelea kuugonga ule mlango huku nikimuita dada.
“Dada! Dada hebu fungua…!”
“Nani… Enjo?” nikaisikia sauti ya dada ikiuliza kutoka chumbani.
“Ndiyo ni mimi dada, nifungulie mlango!”
“Kumetokea nini?” Dada akaniuliza lakini sauti yake ilisikika kwa karibu. Nikajua alikuwa ameshashuka kitandani na yuko karibu na mlango.
Mara mlango ukafunguliwa, dada akatoka.
“Haya kumetokea nini?” Dada akaniuliza akiwa amenitolea macho. Nilikuwa nimemshtua.
Wakati ananiuliza nilikuwa nahema kama niliyekuwa ninafukuzwa. Nikajua ni kwa sababu moyo wangu ulikuwa ukienda kwa kasi kwa sababu ya hofu iliyonipata.
“Yule mzungu si amenipigia simu, sikuipokea. Akapiga tena simu ikajiunganisha yenyewe nikasikia sauti yake ikiniambia: “Kwa nini hupokei simu, ninakuja chumbani kwako!” Ndiyo nikaitupa ile simu nikatoka mle chumbani.” Dada alikunja uso na kuniuliza.
“Unasemaje?”
Nikajua kile kipengele cha simu kujipokea yenyewe ndicho hakukielewa.
Nikamfafanulia.
“Hebu twende huko chumbani kwako,” akaniambia.
Alitangulia yeye kuingia mle chumbani na mimi nikamfuata nyuma.
“Simu hiyo hapo chini,” nikamwambia.
Akainama na kuichukua. Japokuwa niliitupa kioo chake hakikuvunjika na taa yake ilikuwa inawaka ikionesha yule mzungu aliendelea kuwa hewani muda wote niliokimbia.
Bila shaka simu ilikatwa baada ya dada kuichukua pale chini.
“Namba yake ni ipi?” Dada akaniuliza.
Nikamuonesha namba ya yule mzungu. Wakati namuonesha shemeji naye akaingia.
“Kumetokea nini au yule jini amekuja humu chumbani?” akauliza huku akinitazama. Kwa tabia yake kila jambo alitaka kulitilia mzaha.
Mwenzake nilikuwa nimetaharuki na sikumjibu.
Dada ndiye aliyemueleza nilivyopigiwa ile simu na yule mzungu kisha ikajipokea yenyewe.
Shemeji alikuwa anajifanya hajali kitu lakini aliposikia ile habari alishtuka.
“Naona kama anataka kukutisha tu lakini sidhani kama anaweza kuja humu ndani,” akaniambia.
“Kwa nini? Jini ni jini, anaweza kuja. Yeye ameshakusudia kumtesa mdogo wangu,” dada akasema.
“Sasa atalala vipi?”
“Mimi silali tena humu chumbani peke yangu,” nikawaambia.
“Basi lala naye,” shemeji akamwambia dada.
“Kwanza twendeni tukakae sebuleni,” nikawaambia kwa vile wakati ule usingizi ulikuwa umeniruka.
Tukaenda kukaa sebuleni. Muda ule ilikuwa ni saa tisa usiku. Tukazungumza hadi saa kumi. Shemeji akaanza kusinzia. Baadaye nikamuona dada naye yuko kimya. Nikajipa moyo kwamba kutakucha muda si mrefu.
Baadaye na mimi nikapitiwa na usingizi hapohapo, nikalala.
Dada ndiye aliyeniamsha kukiwa kumeshakucha.
“Nenda kalale chumbani,” akaniambia.
Nilipotupa macho, shemeji alikuwa ameshaondoka. Nikainuka na kuingia chumbani. Wakati naingia tu chumbani, simu yangu ikaita. Kwa kweli nilishtuka kwa kudhani kuwa ni yule jini.
Nilipotazama skrini ya simu nikaona jina la Eddy, mpenzi wangu aliyekuwa masomoni Uingereza.
Je, kilifuatia nini?
 
SEHEMU YA 10:

Tukaenda kukaa sebuleni. Muda ule ilikuwa ni saa tisa usiku. Tukazungumza hadi saa kumi. Shemeji akaanza kusinzia. Baadaye nikamuona dada naye yuko kimya. Nikajipa moyo kwamba kutakucha muda si mrefu.
Baadaye na mimi nikapitiwa na usingizi hapohapo, nikalala.
Dada ndiye aliyeniamsha kukiwa kumeshakucha.
“Nenda kalale chumbani,” akaniambia.
Nilipotupa macho, shemeji alikuwa ameshaondoka. Nikainuka na kuingia chumbani. Wakati naingia tu chumbani, simu yangu ikaita. Kwa kweli nilishituka kwa kudhani kuwa ni yule jini. Nilipotazama sikrini ya simu nikaona jina la Eddy, mpenzi wangu aliyekuwa masomoni Uingereza.
SASA ENDELEA…
Pia sikuamini kuwa alikuwa ni Eddy kweli. Nikahisi labda yule jini amegeuza namba ili nipokee simu yake. Nikaipokea huku nikiwa na mashaka.
“Hello!” nikasema kwa kutega.
“Hello Baby…”
Naam ilikuwa sauti ya Eddy.
“Mbona unanipigia kwa namba ya Tanzania?” nikamuuliza.
“Nimewasili sasa hivi kutoka London, niko Uwanja wa Ndege wa Dar lakini ninakwenda Zanzibar kwa ndege nyingine.”
“Mbona umekuja ghafla?”
“Tulianza likizo jana ndiyo nikaona nije huku. Unaweza kuja Unguja?”
“Ninaweza.”
“Basi njoo, nitakuwa Hoteli ya Ziwani. Ukinipigia baadaye nitakwambia niko chumba namba ngapi.”
“Sawa. Ninajiandaa nitakapoondoka nitakujulisha.”
“Oke.”
Eddy akakakata simu. Simu ya Eddy ikawa imebadili fikira zangu. Ile hofu niliyokuwa nayo ikaondoka, badala yake nikawa na furaha ya kukutana na mpenzi wangu ambaye nilipoteana naye kwa mwaka mzima alipoondoka kwenda masomoni Uingereza.
Mpaka inafika saa nne nilikuwa nimeshajiandaa kwa safari ya kwenda Zanzibar. Nilimfahamisha dada yangu kuwa nakwenda Zanzibar kwa Eddy.
“Kwani Eddy amerudi?” Dada akaniuliza.
“Amenipigia simu asubuhi akiwa uwanja cha ndege hapa Dar akitokea London, ameniambia nimfuate Zanzibar.”
“Ina maana alipofika tu akaondoka kwenda Zanzibar.”
“Ndiyo, aliondoka kwenda Zanzibar.”
“Basi hizo zawadi za Ulaya usitukose.”
Baada ya hapo nikaenda zangu bandarini. Nilikata tiketi ya boti inayoondoka saa saba. Baada ya kukata tiketi nikampigia Eddy.
“Eddy Vipi?” nikamuuliza alipopokea simu yangu.
“Ndiyo unakuja?” Eddy akaniuliza.
“Niko bandarini. Boti itaondoka saa saba.”
“Ukifika njoo Hoteli ya Ziwani, niko chumba namba 85. Kipo ghorofa ya pili.”
“Sawa.”
Nilikata simu. Mimi na abiria wenzangu tukajipakia kwenye boti.
Safari ilianza saa saba. Tulipofika Unguja nilikodi Bajaj iliyonipeleka Hoteli ya Ziwani. Ilikuwa hoteli kubwa iliyokuwa karibu na ufukwe wa Bahari ya Hindi.
Nilipofika Hoteli ya Ziwani nilishuka kwenye Bajaj nikaingia ndani ya hoteli hiyo. Nilifika mapokezi nikaeleza kwamba kulikuwa na mgeni wangu aliyekuwa chumba namba 85.
“Chumba namba 85 kipo ghorofa ya pili.”
“Sawa.”
Nikapanda ngazi hadi ghorofa ya pili. Nikakitafuta chumba namba 85, nikakiona. Nilikwenda kwenye mlango wa chumba hicho nikabisha lakini sikupata jibu.
Kwa vile mwenyewe alishaniambia kuwa atakuwa katika chumba hicho, nilifungua mlango nikaingia. Nikamuona Eddy akipekua kwenye kabati. Alikuwa amenipa mgongo.
Nikaurusha mkoba wangu kwenye kitanda nikamfuata ili nimkumbatie. Kabla sijamfikia aligeuka akanitazama. Eh! Kumbe hakuwa Eddy. Alikuwa ni yule jini mzungu!
Moyo wangu ulishituka. Nikamuona akitabasamu na kuniambia:
“Karibu.”
Nilikuwa nimeshapeleka mikono yangu nimkumbatie, nikairudisha haraka kisha nikageuka na kurudi kwenye mlango. Niliufungua na kutoka mbio.
“Ah! Balaaa gani hili!” nilijisemea huku nikishuka ngazi harakaharaka.
Nilirudi pale mapokezi nikamuuliza yule msichana:
“Aliyekodi chumba namba 85 alikuwa ni nani?”
Msichana alitazama kwenye kitabu cha wageni kisha akaniambia:
“Ni Eddy.”
“Ni Mzungu au Mzanzibari?”
“Ni Mzanzibari.”
“Mbona nakuta Mzungu?”
“Inawezekana ni mwenzake lakini chumba kimetolewa kwa Eddy.”
Mkoba wangu nilikuwa nimeuacha kule chumbani. Nikatoka nje ya ile hoteli. Nilipotupatupa macho, nikaiona gari ya Eddy ikiwa imeegeshwa katika eneo la kuegesha magari. Nikaifuta. Nilimkuta Eddy amelalia usukani wa gari.
Nikafungua mlango wa dereva na kumuita.
“Eddy!”
Wakati mlango unafunguka nikamuona Eddy anachomoka kwenye mlango na kuanguka chini kama mzigo. Nikawahi kumdaka.
Alikuwa ametoa macho na damu ilikuwa ikimtoka puani na midomoni.
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 11:

Mkoba wangu nilikuwa nimeuacha kule chumbani. Nikatoka nje ya ile hoteli. Nilipotupa macho, nikaliona gari la Eddy likiwa limeegeshwa katika eneo la kuegesha magari. Nikalifuata. Nilimkuta Eddy amelalia usukani wa gari.
Nikafungua mlango wa dereva na kumuita.
“Eddy!”
Wakati mlango unafunguka nikamuona Eddy anachomoka kwenye mlango na kuanguka chini kama mzigo. Nikawahi kumdaka.
Alikuwa ametoa macho na damu ilikuwa ikimtoka puani na midomoni.
SASA ENDELEA…
“Eddy! Eddy! Una nini?” nikamuuliza nikiwa nimemshikilia.
Lakini Eddy alikuwa amelegea mwili mzima. Shingo yake ilikuwa imelegea kama iliyovunjwa.
Ilikuwa hali iliyonishtua sana na kunipotezea nguvu zangu zote. Mwili wa Eddy ulinielemea, nikauachia ukaanguka chini kama mzigo. Vile alivyoanguka ndivyo alivyolala hivyohivyo. Baada ya kuutazama uso wake mara moja niligundua kuwa Eddy hakuwa hai. Alikuwa ameshakufa!
Nilitaka nichutame ili nimchunguze vizuri lakini nikamuona mlinzi wa hoteli aliyekuwa ameketi mbali kidogo karibu na lango la kuingilia hotelini akinyanyuka.
“Kuna nini hapo?” akapaza sauti kuniuliza.
Alikuwa amekiona kile kitendo kilichotokea pale cha Eddy kuanguka chini kutoka kwenye gari lake huku na mimi nikionekana nimechanganyikiwa.
Nikajiuliza nitamueleza nini kuhusu hali ya Eddy wakati sijui kilichomtokea na wakati huohuo mimi ndiye niliyeonekana naye hapo? Nikaamua kuondoka haraka.
Mlinzi naye akanifuata. Alikuwa anakuja kwa upande wangu wa kushoto, mimi niliondoka kwa upande wa kulia.
Simu yangu ilikuwa mkononi lakini mkoba wangu niliuacha kule chumbani juu ya kitanda. Kwa vyovyote vile nisingeweza kuingia tena katika hoteli hiyo. Si kwa sababu nilitaka kumkimbia yule mlinzi bali pia kule chumbani kulikuwa na yule jini.
Huku nikizibwa na magari yaliyokuwa yameegeshwa, niliendelea kwenda huku nikitazama nyuma mara mojamoja. Sikuweza kumuona tena yule mlinzi kwa sababu alizibwa na magari na yeye hakuwa akiniona. Nikatokomea!
Kusema kweli nilikuwa natembea huku nimechanganyikiwa. Nilikuwa sijui naenda wapi. Nilikuwa nimeshalitoka eneo lile la hoteli na kuingia katika mtaa mwingine.
“Hili ni balaa!” nilijiambia kimoyomoyo.
Nilishindwa kugundua nini kilikuwa kimetokea. Yule mzungu alifikaje katika chumba cha Eddy wakati Eddy mwenyewe akiwa kwenye gari? Au kitu gani kimemtokea Eddy?
Kwa vyovyote vile, nilijiambia, chochote kile kilichomtokea Eddy kimetokana na yule jini.
“Kama Eddy atakuwa ameuawa, ameuawa na yule jini? Nikajiambia.
Na amemuua baada ya kuona alikuwa mpenzi wangu na nilikuja Unguja kumfuata yeye. Siku ile ya kwanza nilipokutana naye nilimwambia kwamba sikuwa na mpenzi wala mchumba.
Sasa ameamua kunikomoa!
Kutokana na damu iliyokuwa inamtoka Eddy puani na midomoni huenda alikabwa shingo au shingo yake ilinyongwa na kuvunjwa kabisa. Au, niliendelea kujiambia. Eddy atakuwa amefyonzwa damu na yule jini.
Akili yangu iliniambia kwamba yule mlinzi anaweza kuufahamisha uongozi wa hoteli kuhusu kifo cha Eddy. Na uongozi huo ukapiga simu polisi.
Polisi watakapofika mlinzi atasema alimuona msichana aliyeuangusha mwili huo na kukimbia. Hapo ni wazi kuwa mtuhumiwa nitakuwa mimi na polisi wataanza kunitafuta.
Kama itakuwa hivyo, niliendelea kujiambia, jambo la maana ni kuondoka pale Unguja haraka. lakini nikakumbuka kwamba pochi yangu iliyokuwa na pesa niliiacha kule chumbani. Pale nilipokuwa sikuwa hata na senti tano!
“Nitapata wapi pesa ya nauli ya kunirudisha Dar?” nikajiuliza bila kupata jibu.
Pale Unguja sikuwa na mwenyeji yeyote zaidi ya Eddy mwenyewe. Nilianza kufika Unguja baada ya kuwa na uhusiano na Eddy na tulikuwa tukikutana hotelini, hakuwahi kunipeleka nyumbani kwao hata siku moja.
“Sasa nitakwenda kumuomba nani pesa?” nikaendelea kujiuliza.
Nilipofika pale Unguja nilikuwa nikisikia baridi lakini muda ule niliokuwa nimetahayari nilihisi joto limepamba moto kiasi kwamba mwili wangu ulianza kutota jasho. Sikuwa hata na kitambaa cha kujifuta jasho usoni. Kitambaa changu kilikuwa ndani ya mkoba wangu.
Licha ya kutembea kwa mwendo wa haraka nilikielekea bandarini nilijua kuwa wakati wowote ningeweza kukamatwa na polisi. Kwa vile sikuwa na uzoefu wa kutenda vitendo vya uhalifu, kila nilipokutana na polisi nilijishtukia. Polisi yeyote mwenye saikolojia angeweza kugundua kuwa nilikuwa na hisi ya hatia.
Sasa mawazo yangu yote yakawa kwenye kufungwa. Nilijiambia penzi langu na Eddy sasa linanipeleka jela!
Wakati ule mawazo yangu yanatangatanga nikapata wazo la kumpigia simu dada yangu nimueleze yaliyonikuta.
Itaendelea
 
SEHEMU YA 12:


Sasa mawazo yangu yote yakawa kwenye kufungwa. Nilijiambia penzi langu na Eddy sasa linanipeleka jela!
Wakati ule mawazo yangu yanatangatanga nikapata wazo la kumpigia simu dada yangu nimueleze yaliyonikuta.
SASA ENDELEA…
Nikasimama chini ya mti uliokuwa kando ya barabara nikampigia simu dada yangu. Nilishukuru kwamba simu yangu ilikuwa na salio.
Dada yangu alipopokea simu aliniuliza:
“Umeshafika Unguja?”
“Nimefika lakini kumetokea matatizo.”
“Matatizo gani tena?”
Nikamueleza. Dada alishituka sana.
“Sasa dada nimekwama, naomba unitumie nauli nirudi Dar.”
“Nikutumie kiasi gani sasa?”
“Nitumie japokuwa elfu hamsini.”
“Ngoja nikutumie.”
Simu ikakatwa.
Wakati nainua uso, nikaona polisi wawili wanakuja huku wamenikodolea macho. Nikahisi kama walikuwa wananifuata mimi. Moyo wangu ukashituka ukawa unapiga kwa kasi. Nikahisi miguu yangu ikitetemeka.
Nikajiuliza nifanye nini, nisimame hapohapo polisi hao wanikamate, au nitoke mbio?
Nilikuwa tayari nimeshakusanya nguvu za kukimbia nilipobadili mawazo ghafla. Niliona nisikimbie, Nilijiambia nikikimbia nitajionesha wazi kuwa ni mwenye hatia. Na pia mimi ni mwanamke nisingeweza kushindana na wanaume wawili kwa mbio. Kwa vyovyote vile ningekamatwa kabla ya kufika popote.
Nikainamisha tena uso wangu na kuuelekeza kwenye ile simu, nikawa nabonyezabonyeza vitufe huku nikiwatazama polisi hao pembeni mwa macho.
Nikaona wanapita. Kumbe hawakuwa na shughuli na mimi. Waliponipa mgongo tu nikafyatuka na kukatiza njia nyingine. Wakati natembea kwa mwendo wa haraka nikasikia simu yangu ikitoa mlio wa kupokea meseji.
Nikaitazama huku nikiendelea kwenda. Nikaona meseji ya pesa kutoka kwa dada yangu. Alinitumia zile shilingi elfu hamsini nilizomuomba.
Sasa nikawa natafuta sehemu iliyokuwa na wakala ili nitoe zile pesa. Baada ya kupita kwenye maduka mawili matatu nikaliona duka lililokuwa na wakala wa mtandao niliokuwa nautumia. Nikaenda kutoa zile shilingi elfu hamsini.
Baada ya kupata pesa hizo nikakodi teksi iliyonipeleka bandarini. Nilipofika nilikwenda kuulizia kama kulikuwa na usafiri wa boti wa kwenda Dar.
Nikaambiwa kulikuwa na boti inaondoka saa kumi na mbili jioni, nikakata tiketi na kusubiri. Wakati nasubiri dada yangu akanipigia simu.
“Umeshatoa hiyo pesa?” akaniuliza baada ya kupokea simu yake.
“Nimeshatoa, niko bandarini.”
“Umepata boti ya kurudi?”
“Nimepata lakini inaondoka saa kumi na mbili.”
“Hakuna inayoondoka muda huu?”
“Hakuna.”
“Sasa umeshakata tiketi?”
“Nimekata, nasubiri huo muda.”
“Basi jihadhari, usianze kutangatanga huku na huku.”
“Nitangetange wapi dadaa’ngu, mwenyewe nimenywea kama maji ya mtungi.”
“Nitakupigia baadaye.”
Dada akakata simu. Nikaendelea kusubiri pamoja na abiria wenzangu hadi muda wa kujipakia kwenye boti ulipofika. Tukajipakia. Saa kumi na mbili juu ya alama safari ikaanza.
Kabla ya kufika Dar, dada alinipigia simu mara tatu tukiwa baharini. Alikuwa akitaka kujua kama nilikuwa salama. Mara zote nilimjibu kuwa nilikuwa salama na safari ilikuwa inaendelea.
Tulifika Dar es Salaam usiku. Kabla ya kushuka kwenye boti nikampigia simu dada kumjulisha kuwa tumeshafika.
“Mwambie shemeji anifuate bandarini na gari,” nikamwambia.
“Anakuja. Msubiri.”
Nikakata simu.
Nilishuka kwenye boti nikatoka nje kabisa ya bandari kumsubiri shemeji.
Wakati naangazaangaza macho kila upande nikiwa na tamaa ya kuliona gari la shemeji likitokea, simu yangu ikaita. Nikajua ni dada. Nilipotazama namba nikaona si ya dada bali ni ya yule jini mzungu. Moyo wangu ulishituka!
Vile nilivyokuwa nimeduwaa nikiitazama, ile simu ilijipokea yenyewe ikajiongezea sauti. Nikaisikia sauti ya Smith ikiniambia:
“Kama unajaribu kunikimbia mimi utapata matatizo mengi.”
Sikujibu kitu nikanyamaza kimya huku nikijiona wazi kuwa nilikuwa natetemeka.
“Hivi sasa polisi wanakutafuta kwa mauaji ya Eddy na Eddy nilimuua mimi kwa sababu uliniambia huna mpenzi,” sauti ya Smith ikaendelea kuniambia.
Nikaendelea kunyamaza.
“Usalama wako ni kuwa na mimi. Ukiwa na mimi matatizo yote yatakwisha na kesi yako ya Zanzibar pia itakwisha. Sasa niambie kama uko tayari kuwa na mimi.”
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 13:

Vile nilivyokuwa nimeduwaa nikiitazama, ile simu ilijipokea yenyewe ikajiongezea sauti. Nikaisikia sauti ya Smith ikiniambia.
“Kama unajaribu kunikimbia mimi utapata matatizo mengi.”
Sikujibu kitu, nikanyamaza kimya huku nikijiona wazi kuwa nilikuwa natetemeka.
“Hivi sasa polisi wanakutafuta kwa mauaji ya Eddy na Eddy nilimuua mimi kwa sababu uliniambia huna mpenzi,” sauti ya Smith ikaendelea kuniambia.
Nikaendelea kunyamaza.
“Usalama wako ni kuwa na mimi. Ukiwa na mimi matatizo yote yatakwisha na kesi yako ya Zanzibar pia itakwisha. Sasa niambie kama uko tayari kuwa na mimi.”
SASA ENDELEA…
Maneno ya yule jini yalikuwa yanauma kwenye moyo wangu. Mbali na kuuma, pia yalikuwa yamenipa mchanganyiko wa shauku na hofu.
Yalinipa shauku ya kutaka kuyasikiliza kwa sababu yalinifahamisha kile nilichokuwa nataka kukijua kuhusu Eddy. Sasa nilikwishajua na kupata uhakika kwamba Eddy ameuawa na Smith na ameuawa kwa sababu alikuwa mpenzi wangu.
Pia nilishajua kwamba polisi wa Zanzibar walikuwa wakinitafuta kwa tuhuma ya mauaji ya Eddy.
Lakini shauku yangu ilikuwa imechanganyikana na hofu ya kukamatwa na polisi na pengine nishitakiwe mimi kwa mauaji ya Eddy. Na pia nilikuwa na hofu ya kuandamwa na yule jini kiasi kwamba sasa alikuwa ameyaingilia maisha yangu na kutishia kuyaweka hatarini.
Wakati nikiwaza hayo, sauti ya Smith ilikuwa ikiendelea kusikika kwenye simu.
“Enjo usijidanganye kuwa utaweza kunikimbia mimi au kunidanganya kwa sababu ninakufahamu vizuri na nimeshashika kivuli chako. Ulikubali mwenyewe kuwa utanipenda, sitakuachia ufanye vinginevyo hata kidogo,” sauti ya Smith iliniambia.
“Naomba unisamehe…!” nikashtukia nikisema hivyo huku nikianza kulia kwa hofu.
“Nikusamehe nini?” Smith akaniuliza kwenye simu.
“Mimi nimekuona wewe uko tofauti ndiyo maana nimekukimbia.”
Niliposema hivyo nikaisikia sauti ya kicheko ya Smith. Lakini niligundua kilikuwa kicheko cha uongo.
“Oh! Kwa nini una hofu? Nilitaka kukuonesha kuwa umepata mpenzi wa kijini ambaye atakupa utajiri…” akaniambia baada ya kicheko.
“Kumbe wewe ni jini?” nikamuuliza baada ya kukiri yeye mwenyewe kuwa ni jini.
“Ndiyo, mimi ni jini kama ulivyoniona lakini usiogope utanizoea tu.”
“Sasa mimi sitaki tena urafiki na wewe.”
“Haitawezekana kwa sababu nimeshakupenda, lazima ukubaliane na mimi, vinginevyo utapata matatizo.”
“Mama yangu! Mimi najuta sasa…mimi siwezi kuwa na mpenzi kama wewe. Naomba unisamehe.”
“Majini wengi wana wapenzi binadamu na wanawapa utajiri. Wewe hutaki utajiri?”
“Sitaki.”
“Sikiliza Enjo, mimi naweza kuharibu maisha yako mara moja….” Sasa sauti yake ilikuwa imebadilika.
“Mama yangu wee…!”
Maneno ya jini huyo yalizidi kunitia hofu na sikutaka kuyasikiliza tena. Nikabonyeza kitufe cha kukata mawasiliano. Lakini mawasiliano hayakukatika. Nilikiminya tena na tena kitufe hicho bila mafanikio.
Nikaona sasa nifungue simu nitoe betri. Huku Smith akiendelea kunitishia, niliifungua simu harakaharaka, nikafanikiwa kuchomoa betri na hapohapo simu ikazima. Kitendo hicho kilinifanya niheme kama niliyekuwa nimefanya kazi kubwa.
Nikaendelea kuangaza macho yangu kila upande kulitazamia gari la shemeji. Gari sikuliona. Nikatamani nimpigie simu dada lakini nisingeweza tena kwa sababu betri nilishaitoa.
Nikabaki nimechanganyikiwa.
Ghafla nikaliona gari hilo. Nikakurupuka kulifuata huku nikilipungia mkono. Sikujali kuwa nilikuwa nimetokeza barabarani ambako ningeweza kugongwa na gari lingine.
Shemeji akaniona, akafunga breki. Nikakimbilia kwenye mlango wa upande wa pili wa dereva nikaufungua na kujipakia harakaharaka.
“Nilikuwa nakupigia simu nikuulize uko kwa wapi, naona simu haipatikani,” shemeji akaniambia.
Kabla sijamjibu, shemeji akauona uso wangu. Akaniuliza.
“Ulikuwa unalia?”
Nilijifuta uso kwa mikono. Ile kwikwi ya kilio ilinifanya nisiweze kumjibu chochote. Shemeji akaliondoa gari.
“Mbona sikuelewi Enjo. Naona simu umeifungua, betri iko mbali halafu uko kivingine kama ambaye hutoki safari. Mkoba wako uko wapi?”
“Ni makubwa shem, wewe acha tufike nyumbani. Siwezi kukueleza ndani ya gari.”
Shemeji akanielewa. Hakuniuliza kitu tena.
Tulipofika nyumbani ndipo nilipoeleza yaliyonikuta. Nilianzia yale ya Zanzibar, nikamalizia na ile simu aliyonipigia Smith.
Dada na mume wake wakashangaa.
“Ndiyo maana nikakukuta unalia?” Shemeji akaniuliza.
“Nisilie, unayaona hayo ni madogo!” nikamuuliza.
“Kwa kweli ni makubwa.”
“Lakini Enjo mdogo wangu, matatizo uliyataka mwenyewe, kwa nini mtu anakutongoza unamkubali wakati hamjuani?” Dada akaanza kunilaumu.
Je, kiliendelea nini? Usikose mwendelezo wa mchirizi huu
 
SEHEMU YA 14:

Tulipofika nyumbani ndipo nilipoeleza yaliyonikuta. Nilianzia yale ya Zanzibar, nikamalizia na ile simu aliyonipigia Smith.
Dada na mume wake wakashangaa.
“Ndiyo maana nikakukuta unalia?” Shemeji akaniuliza.
“Nisilie, unayaona hayo ni madogo?” nikamuuliza.
“Kwa kweli ni makubwa.”
“Lakini Enjo mdogo wangu, matatizo uliyataka mwenyewe, kwa nini mtu anakutongoza unamkubali wakati hamjuani?” Dada akaanza kunilaumu. SASA ENDELEA…

Sasa dada mimi nilijuaje kama ni jini? Utanilaumu bure. Mimi nilijua ni binadamu kama binadamu wengine, kumbe najiingiza kwenye matatizo nisiyoyajua. Tena ameniambia ameshika kivuli changu, sitaweza kumuepuka na nisipomkubali atanitia kwenye matatizo.”
Nilipowaeleza hivyo nikaanza tena kulia.
“Kwa matukio hayo ya Zanzibar, huyo jini tayari ameshakutia kwenye matatizo. Sasa kama unatafutwa na polisi, utasema kuna usalama hapo?” Dada akauliza.
Mimi niliendelea kulia nikiamini kuwa maisha yangu yalikuwa yamekwisha.
Kusema kweli nilijuta kukutana na jini yule.
“Lakini tusemeni huku na huku, hao polisi wa Zanzibar wanamtafuta, wanamjuaje au walimuona wapi?” Shemeji akahoji.
“Si huyo jini amemwambia kuwa anatafutwa na polisi,” dada akamjibu.
“Pamoja na kuambiwa na huyo jini na sisi tutafakari katika akili zetu. Polisi wanamkamata mtu wanayemfahamu, huyu hawamfahamu. Mimi sioni kama ni kitu cha urahisi kuja hapa Dar na kumkamata. Afadhali angekuwa yuko Zanzibar.”
“Na mimi sitaenda tena huko,” nikajisemea.
“Uende umfuate nani wakati unayemfuata ameshauawa?” dada akaniuliza.
“Ndiyo sitaenda.”
“Kutokana na haya mambo yalivyo, hapa shauri liliopo ni kutafuta mganga atakayemshughulikia Enjo,” Dada akatoa wazo.
“Hilo ndilo wazo nililonalo mimi,” nikamwambia na kuongeza:
“Hiyo kesi kama ipo tuiue na huyo jini afanyiwe kafara asinifuate tena.”
“Sasa mganga tutampata wapi?” Shemeji akauliza.
“Wanatoaga matangazo yao kwenye haya magazeti. Tena kwenye gazeti la leo niliona tangazo la mganga mmoja anatoaga majini na kuua kesi. Hebu ngoja nikalilete lile gazeti.”
Dada akainuka na kuingia chumbani. Alipotoka alikuwa ameshika nakala ya gazeti fulani akaja nalo sebuleni na kuketi. Alifungua ukurasa mmoja mmoja huku akivitupia macho kwa makini vichwa vya habari. Ghafla akaliona hilo tangazo alilotuambia.
“Enhe tangazo lenyewe hili hapa.”
Mimi na shemeji tukalisogelea gazeti na kulitupia macho tangazo hilo.
Lilikuwa tangazo la mganga wa kienyeji aliyekuwa akitoa majini, kuua kesi na kutoa dawa za mvuto wa kimapenzi.
Aliweka picha yake. Alikuwa mtu mzima aliyevaa kanzu na kofia ya darizi na kuonekana kama ustadhi wa madrasa.
Alijitambulisha kama mganga wa majini kutoka Tanga na alikuwa akipatikana maeneo ya Tegeta jijini Dar.
Kwa vile alikuwa ameweka namba yake ya simu, dada alishauri tumpigie tumueleze lakini shemeji akasema isingekuwa vyema kumpigia simu usiku ule.
“Tusubiri asubuhi.”
“Basi tutampigia asubuhi,” dada akamkubalia.
Usiku ule kwa sababu ya hofu ilibidi nilale na dada katika chumba nilichokuwa nikilala. Shemeji alilala peke yake. Nilijua kuwa alikasirika lakini hapakuwa na jinsi.
Kulipokucha baada ya kupata kifungua kinywa nilirudisha betrii kwenye simu yangu nikampigia yule mganga.
Alikuwa mswahili hasa kwani baada ya kupokea simu yangu aliniambia:
“Assalaam alaykum.”
Na mimi nikamuitikia kama mswahili.
“Waalayka salaam. Shikamoo.”
“Marahaba. Nani mwenzangu?”
“Mimi naitwa Enjo niko Sinza. Nina shida yangu.”
“Shida gani mama?”
“Kuna jini ananifuatafuata….”
Kabla sijamaliza kusema akadakia:
“Hiyo ndiyo kazi yangu mama. Mimi nafukuza majini wabaya, nazindika nyumba, natoa dawa za mvuto wa kimapenzi na nashughulikia matatizo mbalimbali.”
“Nimekuelewa. Sasa ngoja nikueleze vizuri.”
“Haya nieleze.”
“Huyo jini ananifuata waziwazi akiwa na umbo la kibinadamu na kunitaka kimapenzi….”
Mganga akang’aka:
“Kumbe ni majini wa aina hiyo! Hao wanasumbua sana mama.”
“Hutaweza kumfukuza?”
“Kwa nini nishindwe wakati ni kazi yangu. Mimi nafukuza jini hata akiwa mkubwa kama nyumba!”
“Sasa ameshanifanyia visa vingi sana na kutishia maisha yangu…”
“Usijali…usijali, mwisho wake ndiyo umefika. Wewe uje hii asubuhi nikushughulikie kabla watu hawajajaa.”
“Mengine nitakuja kukueleza huko huko.”
“Sawa. Sasa unakuja?”
“Ninakuja. Nichukue shilingi ngapi.”
“Hiyo kazi ni kubwa lakini kwanza uje na laki tano.”
Pesa alizonitajia zilikuwa nyingi lakini kutokana na tatizo lililokuwa limenikabili nilimkubalia.
“Sawa, ninakuja sasa hivi.”
“Nakusubiri.”
Nikakata simu.
Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 15:

“Kwa nini nishindwe wakati ni kazi yangu? Mimi nafukuza jini hata akiwa mkubwa kama nyumba!”
“Sasa ameshanifanyia visa vingi sana na kutishia maisha yangu…”
“Usijali…usijali, mwisho wake ndiyo umefika. Wewe uje hii asubuhi nikushughulikie kabla watu hawajajaa.”
“Mengine nitakuja kukueleza hukohuko.”
“Sawa. Sasa unakuja?”
“Ninakuja. Nichukue shilingi ngapi?”
“Hiyo kazi ni kubwa lakini kwanza uje na shilingi laki tano.”
Pesa alizonitajia zilikuwa nyingi lakini kutokana na tatizo lililokuwa limenikabili nilimkubalia.
“Sawa, ninakuja sasa hivi.”
“Nakusubiri.”
Nikakata simu.
SASA ENDELEA…
Nilimfuata dada chumbani kwake, shemeji alikuwa ameshatoka kwenda kazini kwake.
Nikamueleza nilivyozungumza na yule mganga.
“Sasa hizo pesa unazo?” Dada akaniuliza.
“Pesa zipi?”
“Hizo alizotaka huyo mganga.”
“Nina nusu tu.”
“Sasa itakuwaje?”
“Niongezee laki mbili, mimi nitatoa laki tatu.”
“Kama pesa unazo si utoe tu, unafanya mchango wa nini?”
“Sina dada, nina shilingi laki tatu tu.”
“Kwani juzi huyo shetani wako si alikupa shilingi milioni kumi, ziko wapi?”
“Sitaki kutumia pesa zile.”
“Zina nini?”
“Zile tuziache kwanza.”
“Lakini si umeshaanza kuzitumia, sasa unaziacha kwa nini?”
“Dada naye ana maswali, wee nipe tu hizo laki mbili. Nitakuja kukurudishia.”
“Mimi sina laki mbili, labda nikupe laki moja halafu uirudishe.”
“Haya, nipe, nitairudisha.”
Dada akafungua kabati, akanitolea shilingi laki moja na kunipa.
“Hizo laki nne utaongezea mwenyewe.”
Sikumjibu, nilimuazima mkoba wake, nikazitia zile pesa.
“Basi mimi naenda.”
“Utakwenda na usafiri gani?”
“Nitachukua bodaboda.”
Nilipotoka nyumbani kwa dada, nilikodi bodaboda ambayo ilinipeleka nyumbani kwangu. Niliingia ndani. Nilikuwa nimeweka akiba yangu ya shilingi milioni moja. Nikachukua shilingi laki saba na kuacha laki tatu.
Nikabadili nguo nilizokuwa nimevaa kisha nikatoka. Nilipakiwa tena kwenye bodaboda, tukaanza safari ya kuelekea Tegeta kwa mganga.
Tulipofika Tegeta, nyumba na mtaa aliokuwa akiishi mganga huyo sikuvifahamu. Nikamwambia mwenye bodaboda asimame ili niwasiliane na mganga huyo.
Bodaboda iliposimama nikampigia simu mganga huyo na kumuuliza alikuwa anaishi mtaa gani? Akanielekeza mtaa na nyumba yake ilipokuwa. Hapakuwa mbali sana na pale tuliposimama.
Kwa vile sikutaka kijana huyo mwenye bodaboda ajue kuwa nilikuwa nakwenda kwa mganga, niliamua niende kwa miguu. Nikamlipa pesa alizotaka. Sasa nikawa navuka barabara. Ghafla nikaona teksi ikisimama mbele yangu.
Na mimi nikasimama na kuitazama. Katika siti ya nyuma niliona mtu mweupe akifungua mlango na kushuka.
“Mama yangu wee…!” Unadhani alikuwa nani?
Alikuwa ni yule Mzungu. Nilijikuta niko naye uso kwa uso.
“Hujambo Enjo?” akaniuliza kwa sauti tulivu huku akinitolea tabasamu la kihaini.
“Sijambo,” nikamjibu. Sauti yangu ilikuwa imefifia kwa hofu.
“Unakwenda wapi?”
Swali lake hilo lilinipa changamoto. Nikajiuliza nimwambie kuwa ninakwenda kwa mganga kwa ajili yake? Nisingethubutu. Nilitumia sekunde kadhaa kufikiria la kumjibu huku vitone vya jasho vikipamba kwenye paji la uso wangu.
“Hujui unakokwenda?” akaniuliza aliponiona nipo kimya.
Nikajidai kutabasamu ili asigundue kuwa nilikuwa nimegwaya lakini hata sikufanikiwa kulionesha hilo tabasamu. Tayari moyo wangu ulishafadhaika kukutana na shetani yule.
“Hapana. Ninakwenda nyumbani,” nikamdanganya.
“Ulikuwa unatoka wapi?”
“Ninatoka kule kumtembelea rafiki yangu.”
Nilimuonesha ule upande niliotokea.
Nafikiri aligundua kuwa nilikuwa namdanganya, akaufungua ule mlango wa nyuma wa gari na kuniambia.
“Ingia nikupeleke.”
Nikasita na kugeuza uso wangu upande mwingine.
“Ah! Nilikuwa nakwenda kukodi bodaboda…”
“Si umesema unakwenda nyumbani?” akaniuliza.
“Ndiyo nakwenda nyumbani.”
“Basi ingia tukupeleke, teksi ipo hapa.”
Pamoja na hofu niliyokuwa nayo, nilijikuta nikiingia kwenye ile teksi. Wakati najipakia ndipo liliponijia wazo kwamba ningekimbia badala ya kuingia kwenye teksi hiyo au ningepiga kelele kuita watu. Pengine ningefanya hivyo ningepata msaada.
Wazo hilo lilichelewa na lisingenisaidia kwa sababu nilikuwa nimeshajipakia kwenye ile teksi.
Yule M zungu naye akajipakia, tukawa tumekaa bega kwa bega.
Ujanja wangu wote kwisha!
Nikauinamisha uso wangu, nikaanza kusali kimoyomoyo huku nikijihisi nataka kulia.
Teksi ikaondoka. Hata sikujua ilikuwa inaelekea wapi. Mwili ulinifumka jasho ghafla. Nikajikuta ninatota kama ninayemwagiwa maji.
“Leo naenda kuuawa jamani!” nikawa najiambia kimoyomoyo.
“Kwa nini nimekubali kuingia kwenye hii teksi? Huyu jini ananipeleka wapi sasa?” nikawa najiuliza bila kupata jibu.
Teksi iliendelea kuyoyoma kuelekea mahali nisipopajua.
Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 16:

Teksi ikaondoka. Hata sikujua ilikuwa inaelekea wapi. Mwili ulinifumka jasho ghafla. Nikajikuta ninatota kama ninayemwagiwa maji.
“Leo naenda kuuawa jamani!” nikawa najiambia kimoyomoyo.
“Kwa nini nimekubali kuingia kwenye hii teksi? Huyu jini ananipeleka wapi sasa?” nikawa najiuliza bila kupata jibu.
Teksi iliendelea kuyoyoma kuelekea mahali nisikokujua.
SASA ENDELEA…
Maneno ya jini huyu aliyoniambia kwamba anaweza kuyaharibu maisha yangu yakawa yananijia akilini mwangu.
Maneno hayo aliniambia jana yake wakati aliponipigia simu usiku nikiwa bandarini nikitokea Zanzibar.
“Mimi naweza kuyaharibu maisha yako mara moja!” jini huyo aliniambia kwa kitisho.
Lakini kwa jinsi maneno hayo yalivyokuwa yakijirudia kichwani mwangu wakati nikiwa ndani ya ile teksi, nilihisi kama vile alikuwa akiniambia wakati ule nikiwa naye ingawa sauti yake haikuwa ikisikika.
Kwa kweli mwili ulinisisimka, nikaogopa sana. Nikainua uso wangu na kumtazama yule Mzungu mara moja tu. Alikuwa akitazama mbele huku akionekana kuwa kwenye mawazo.
Bila shaka alikuwa akiniwazia mimi atakavyokwenda kunishughulikia huko tunakokwenda.
Wakati mawazo yangu yakitangatanga, ghafla simu yangu ikaita. Nikatazama kwenye skirini. Nikaona namba ya dada yangu. Nikaipokea simu haraka.
“Umeonana na huyo mganga?” dada akaniuliza.
Mama yangu wee! Dada ananiuliza kuhusu mganga wakati jini mwenyewe niko naye hapa!
“Sijaonana naye, nimekutana na yule Mzungu amenipakia kwenye teksi.”
“Mzungu gani tena huyo?” Dada akashtuka.
Nikamtazama yule jini usoni, nikaona na yeye alikuwa akinitazama.
Nikavunga. “Si yulee…”
“Yule jini?” dada akaniuliza.
“Ndiyo.”
“Mmekutana wapi?”
“Hukuhuku.”
Nilijua kuwa yule jini alikuwa anasikiliza yale maongezi nikaongea haraka.
“Anasema ananileta nyumbani.”
“Makubwa! Atakuleta nyumbani kweli huyo?”
“Nimpe simu uongee naye?”
“Mh! Haya mpe.”
“Mr Smith ongea na dada,” nikamwambia na kumpa ile simu.
Mzungu huyo akatikisa kichwa.
“Hapana. Siwezi kuongea na mtu,” akaniambia huku macho yake yakitazama mbele.
“Amekataa,” nikamwambia dada.
“Mwambie akuteremshe urudi nyumbani.”
“Mr Smith unaambiwa uniteremshe,” nikamwambia Smith.
Mzungu huyo aliyeonekana kukasirika hakunijibu chochote.
“Mteremshe mdogo wangu arudi nyumbani,” nikamsikia dada akifoka kwenye simu.
Ile sauti aliisikia yule Mzungu lakini alinyamaza kimya.
“Hataki dada, sijui ananipeleka wapi?” nikasema kwenye simu lakini nilijisemea peke yangu kwani simu hiyo ilikata mawasiliano ghafla.
Wakati naitazama ile simu kwa mshangao, yule Mzungu naye alikuwa akinitazama mimi kama aliyekuwa akinisuta kwa macho yake kutokana na kukatika kwa yale mawasiliano. Ilionesha wazi kuwa mawasiliano hayo aliyakata yeye.
Nikadhani dada angepiga tena lakini hakupiga labda alijaribu lakini aliona sipatikani.
Ghafla teksi ikasimama mbele ya hoteli moja.
“Tushuke hapa kwanza tuzungumze, teksi itatusubiri,” Mzungu akaniambia huku akifungua mlango.
Na mimi nikafungua mlango. Tukashuka. “Huyu amenileta hapa hoteli kwa ajili gani?” nikajiuliza.
Mbele ya hoteli kulikuwa na uwanja ambao uliwekwa viti. Mzungu huyo akaniambia:
“Tukae hapa.”
Ilikuwa vyema aliniambia tukae pale. Kama angeniambia anataka kuchukua chumba nisingekubaliana naye.
Tukakaa pale kwenye viti. Mhudumu alipotufuata, Mzungu huyo akaniuliza:
“Unataka nini?”
Nikatikisa kichwa.
“Sitaki kitu.”
“Kunywa japo soda,” akaniambia kisha akaniagizia soda, yeye mwenyewe akaagiza pombe kali.
“Nataka nikwambie kwamba hutaweza kuishi na mwanaume mwingine zaidi yangu,” akaniambia mara tu mhudumu huyo alipoondoka.
“Kama mimi nimeshakupenda wewe huwezi kunikwepa. Mimi nina uwezo wa kukufuata wewe mahali popote ulipo hata kama utakuwa Ulaya. Na usidhani kama kuna mganga hapa Afrika ataweza kuniondoa mimi. Usijidanganye kabisa,” Mzungu huyo aliendelea kuniambia.
Mzungu huyo aliendelea kuniambia maneno mengi ya kunitisha na kutaka nikubali kuwa naye. Mimi nilikuwa nimenyamaza kimya nikimsikiliza.
Kumbe pale simu ilipokata mawasiliano dada alijaribu kunipigia tena lakini hakunipata, akampigia yule mganga na kumueleza kuwa nilitekwa na yule jini wakati nakwenda kwake.
Mganga akataharuki. Baada ya kuzungumza na mashetani yake akamwambia dada ameshapajua mahali nilipo hivyo atakodi teksi kunifuta. Mganga akachukua vifaa vyake akaenda kukodi teksi.
Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 17:

Kumbe pale simu ilipokata mawasiliano, dada alijaribu kunipigia tena lakini hakunipata, akampigia yule mganga na kumweleza kuwa nilitekwa na yule jini wakati nakwenda kwa mganga huyo.
Mganga akataharuki. Baada ya kuzungumza na mashetani yake akamwambia dada ameshapajua mahali nilipo hivyo atakodi teksi kunifuata. Mganga akachukua vifaa vyake akaenda kukodi teksi.
SASA ENDELEA…
Kilichotokea ni kwamba ghafla tu yule jini aliniruhusu nirudi nyumbani baada ya kunipa onyo lake la mwisho.
Aliniambia: “Hii ni nafasi yako ya mwisho ya kuyasalimisha maisha yako. Kama nafasi hii hutaitumia vizuri, jua kwamba utakuja kujuta.”
Mimi nilijifanya namuitikia huku nimeinamisha kichwa. Akanikodia teksi nyingine na akailipia kabisa. Wakati mimi naondoka na teksi, teksi ya mganga nayo ikasimama nyuma yetu. Hapo nilimsifu yule mganga kwamba alipagundua kweli mahali nilipokuwa.
Lakini alipofika hapo hakunikuta ikabidi anipigie simu. Kwa vile nilikuwa nimeshaachana na yule jini, simu yangu ikaita. Nikaipokea.
“Uko wapi?” Mganga huyo akaniuliza kwa sauti ya wasiwasi.
“Nilikuwa kwenye hoteli moja lakini nimeshaondoka, niko kwenye teksi narudi nyumbani.”
“Si ulikuwa unakuja kwangu?”
“Nilikuwa nakuja kwako lakini ghafla nilikutana na yule jini akanipakia kwenye teksi na kunileta hapo hotelini, akaniambia maneno yake kisha ghafla akaniambia nirudi nyumbani.”
“Ameniogopa mimi, alijua kuwa ninamfuata yeye. Mimi nimefika hapa hotelini mlipokuwa. Lengo langu lilikuwa ni kumkomoa yeye.”
“Mimi nimeshaondoka lakini huyo jini naona bado yupo hapohapo anakunywa pombe.”
“Bila shaka na yeye pia ameshaondoka. Sasa nakuja hukohuko nyumbani kwenu. Nataka nihakikishe kuwa hakufuati tena.”
“Sawa. Wewe njoo nyumbani utanikuta.”
Mganga alipokata tu simu dada naye akanipigia.
“Uko wapi Enjo?” akaniuliza kwa wasiwasi.
“Niko kwenye teksi ninakuja nyumbani.”
“Mbona ulikuwa hupatikani, imekuwaje?”
“Yule Mzungu alinipeleka hotelini akaninunulia soda. Ameniambia yeye haogopi waganga na kama nitaendelea kumsumbua nitakuja kujuta.”
“Mimi nilipoona hupatikani nilimpigia yule mganga nikamweleza kuwa huyo jini amekutokea na amekuchukua kwenye teksi. Akaniambia ameshapajua alikokupeleka…”
“Huyo mganga amefika hadi hapo hotelini lakini nilikuwa nimeshaondoka, amenipigia simu.”
“Anaonekana ni mganga hodari sana. Sasa sijui itakuwaje?”
“Ameniambia anakuja nyumbani.”
“Itakuwa vizuri, aje akushughulikie hukuhuku.”
Baada ya kuzungumza na dada, kidogo moyo wangu ulipata faraja. Nikawaza kwamba iwapo mganga huyo atafanikiwa kumtokomeza huyu jini, atakuwa amenisaidia sana.
Kufumba na kufumbua teksi ikaingia Sinza. Nilimuelekeza dereva mtaa aliokuwa anaishi dada, akanipeleka hadi nyumbani kwake.
Wakati huo sikujua kwamba teksi iliyompakia yule mganga nayo ilikuwa imeshaingia kwenye mtaa huo. Wakati nashuka kwenye ile teksi mganga huyo akanipigia simu.
“Umeshafika nyumbani?” akaniuliza.
“Ndiyo nimeshafika, wewe uko wapi?”
“Tumeingia kwenye huu mtaa alionitajia dada yako, sasa ninaitafuta nyumba yenu sijui ni ipi?”
Kwa mbali nikaona teksi inakuja.
“Nimeona teksi inakuja iliko nyumba yetu, hebu endeleeni kuja. Mimi nimesimama nje nawasubiri.”
“Nimeshakuona. Umevaa dela la rangi ya njano,” mganga akaniambia.
“Ndiyo ni mimi.”
“Sawa. Nakuja.”
Mganga akakata simu.
Wakati ile teksi inakuja kulikuwa na lori la mchanga ambalo lilitokea upande wa pili wa barabara. Nyuma ya lori hilo kulikuwa na pikipiki iliyokuwa inaendeshwa kwa mwendo wa kasi.
Pikipiki ikalipita lori la mchanga na kukutana uso kwa uso na ile teksi. Teksi ikaikwepa pikipiki na kuelekeana uso kwa uso na lori. Dereva wa teksi alijaribu kulikwepa lori la mchanga lakini alishamchanganya dereva wa lori ambaye alimfuata hukohuko. Lori na teksi zikagongana uso kwa uso. Teksi ilipinduliwa na kulala chali huku tairi zake zikiendelea kuzunguka.
Kishindo kilichosikika hapo pamoja na vumbi lililorushwa vilifanya nitoke mbio na kwenda kugonga kwenye geti la nyumba ya dada.
“Dada! Dada. Hebu fungua!”
“Kumetokea nini Enjo?” dada akaniuliza kwa fadhaa. Kile kishindo na yeye kilimshtua humo ndani.
Nikamsikia anakuja mbio na kufungua geti.
“Nini?” akaniuliza huku akitupa macho barabarani.
Ile ajali ilikuwa imetokea karibu kabisa na nyumba ya dada.
“Ile teksi aliyopanda mganga imegongwa na lori,” nikamwambia.
“Hivi atakuwa amesalimika kweli?”
“Sijui.”
Wakati namjibu dada hivyo, tukaona michirizi ya damu ikivuja chini ya teksi, nikamsikia dada yangu akisema: “Yesu wangu!”
Tayari watu walikuwa wakikimbilia mahali hapo wakiwemo vibaka na wasamaria wema waliokuwa na nia njema ya kutoa msaada.
Je, mganga alisalimika katika ajali hiyo mbaya? Usikose kufuatilia mwendelezo wa mchirizi huu
 
Mganga akipona. Atakuaaa shujaaaa

Tuma nyingine....


Ile story nyngn mwenye riwaya yake alikupigaa onyoo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom