Sokomoko
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,915
- 127
Spika wa Tatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel John Tegeza Sitta amesema kuwa utumishi wake bungeni umetosha, hivyo ni wakati wake kustaafu. Amesema anastaafu bunge lakini siyo siasa, hivyo bunge la sasa atalitumia kunoa uwezo wa vijana kabla ya kuachana na siasa za bunge 2015.
Akizungumza bungeni Jumatano iliyopita, kabla ya Kamati Kuu ya CCM (CC) kuengua jina lake katika mbio za kuwania Uspika, Sitta alisema kuwa hatarajii kustaafu kwa sababu anaweza kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu kwenye chama chake.
Awali, siku hiyo Sitta alimpongeza Mbunge wa Viti Maalum CCM (Vyama vya Wafanyakazi), Zainab Kawawa kwa ushindi aliopata na kumuahidi kumjenga kiuwezo kabla ya kuachia bunge mwaka 2015.
Hongera sana, umerudi tuwajenge ili mwaka 2015 tutakapowaacha, muwe tayari na uzoefu, alisema Sitta akizungumza na Zainab.
Baada ya kunasa kauli hiyo, mwandishi wetu alimuuliza Mbunge huyo wa Urambo Mashariki kama hilo ni tamko rasmi au limetoka tu bila kudhamiria ambapo alijibu: Ni tamko rasmi, sitagombea tena na hili ni bunge langu la mwisho.
Sitta alisema kuwa anafikiri kuwa utumishi wake ndani ya bunge umetosha, kwahiyo anataka kukuza vijana.
Wakati akizungumza hayo Jumatano asubuhi kwenye viunga wa bunge, jioni ya siku hiyo, CC ilitangaza kumuengua Sitta katika mbio za kuwania uspika na kubakiza majina ya wanawake watatu ambapo mwisho Anna Makinda alishinda.
http://www.wavuti.com/habari.html#ixzz15QQPqptc
Awali, siku hiyo Sitta alimpongeza Mbunge wa Viti Maalum CCM (Vyama vya Wafanyakazi), Zainab Kawawa kwa ushindi aliopata na kumuahidi kumjenga kiuwezo kabla ya kuachia bunge mwaka 2015.
Hongera sana, umerudi tuwajenge ili mwaka 2015 tutakapowaacha, muwe tayari na uzoefu, alisema Sitta akizungumza na Zainab.
Baada ya kunasa kauli hiyo, mwandishi wetu alimuuliza Mbunge huyo wa Urambo Mashariki kama hilo ni tamko rasmi au limetoka tu bila kudhamiria ambapo alijibu: Ni tamko rasmi, sitagombea tena na hili ni bunge langu la mwisho.
Sitta alisema kuwa anafikiri kuwa utumishi wake ndani ya bunge umetosha, kwahiyo anataka kukuza vijana.
Wakati akizungumza hayo Jumatano asubuhi kwenye viunga wa bunge, jioni ya siku hiyo, CC ilitangaza kumuengua Sitta katika mbio za kuwania uspika na kubakiza majina ya wanawake watatu ambapo mwisho Anna Makinda alishinda.
http://www.wavuti.com/habari.html#ixzz15QQPqptc