Sitaacha kuisemea Bulyanhulu hata kama nitawaudhi

Ng'wanapagi

JF-Expert Member
Sep 18, 2013
9,125
8,627
Nimezaliwa na kukulia huko hata nikifa naamini taletwa kuzikwa huko. Huko ndiko ndugu, marafiki na watoto wangu wanaishi.

Naifahamu Bulyanhulu hata kabla ya kuja hao whites, nawakumbuka marafiki zangu waliofukiwa kwenye mashimo wakijificha ili wazungu waliolindwa na polisi wetu chini ya amri ya Mkapa wachukue sehemu hiyo walifukiwa ili kuwapisha wawekezaji hao kutoka mikononi mwa wachimbaji wadogo (wachimaji wadogo waliitwa wachimbaji haramu).

Nakukumbuka Hamisi Mgunga kama mmoja wa rafiki zangu waliofia kwenye hilo sakata. Tangu 1996 hadi leo 2020 hakuna barabara ya lami wala maji ya uhakika. Wana CCM kulisema hili mbele yao utaitwa si mzalendo na huungi mkono juhudi za mtu wa kwetu!

Kule Chato tangu mtu wetu akiwa ujenzi alipapendelea kwa barabara za lami, leo hii kuna taa za barabarani, kuna uwanja mkubwa wa ndege, kuna jengo la mahakama la kisasa kuliko hata lile la mkoa wa Geita, kuna maandalizi ya kujengwa hospital ya rufaa na sasa kuna mbuga ya wanyama (artificial game) wanyama wanahamishwa kupelekwa huko. Kutoka Nyakumbu Geita hadi Kakola (kitovu cha dhahabu) hakuna lami!

Kutoka Kakola hadi Kahama hakuna lami! Naamini hana habari na Bulyanhulu kwa sababu wanaotakiwa kumwambia wanamuogopa na ukimtajia Bulyanhulu moja kwa moja atawawazia mabeberu ACACIA ambao wameshaondoka tayari.

Inauma ila ipo siku
FB_IMG_1581275490834.jpeg
FB_IMG_1581275481049.jpeg
FB_IMG_1581275500457.jpeg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ebu ngoja nikae kwa hapa, labda nitaelewa badae baada ya comments kuongezeka.

Sawa, sote tunatambua sakata la yalio jiri Bulyanhulu kuanzia mwaka 1996. Sasa ndio ungesema nini unahisi hakikufanyika na nani alie sababisha?

Baada ya hapo ungependekeza nini unadhani kifanyike na unadhani ni jukumu la nani kutimiza hilo pendekezo lako?
 
Mtu anawabeba simba na twiga kuwapeleka Chato bado mnamwita mzalendo.

Tanzania kuna hifadhi nyingi na nzuri, kabla hatujaanzisha hifadhi mpya ni bora tungetatua changamoto zilizopo kwenye hifadhi za awali.
Huyo ndio anayepigiwa makofi na kusifiwa kila siku kwa lazima. Sasa naelewa vizuri kwanini alianza kwa kuminya uhuru wa vyombo vya habari na baadaye vyama vya upinzani...
 
Huyo ndio anayepigiwa makofi na kusifiwa kila siku kwa lazima. Sasa naelewa vizuri kwanini alianza kwa kuminya uhuru wa vyombo vya habari na baadaye vyama vya upinzani...
Huyo ni mwizi kama wezi wengine, kajificha nyuma ya neno uzalendo na madaraja anayojenga.

Ushawahi kujiuliza dhuruma anayowafanyia watumishi wa umma hizo pesa zao anapelekaga wapi? na kwa nini aliweka mpwa wake jikoni?

Tutajua hatujui.
 
Mkuu, minaona bado unauzunguka tu m-buyu, ebu fungua koo uongee kwa sauti kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
Ushirombomen nafahamu kwenye mambo ya msingi huwa unaingiza ukabila, hebu tafakari, vaa viatu vya watu wa Bulyanhulu na maisha wanayoyaishi ukweli bado natamani bora hata mwizi Lowassa angewajali watu wa Bulyanhulu kama alipambana kuleta maji Kahama kuyatoa Ziwa Victoria pamoja na mkwara wa Misri kuwa asitishe huo mradi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa nini hauhami kutoka huko Nhulu kama Wachaga wanavyokimbia kwao kama ni kubaya hivyo? TZ yetu ni kubwa, unaweza hamia Chato pia kama kuna yote hayo mazuri uliyoyataja, Chiluba familia yako hamia Chato, problem solved!
 
Ushirombomen nafahamu kwenye mambo ya msingi huwa unaingiza ukabila, hebu tafakari, vaa viatu vya watu wa Bulyanhulu na maisha wanayoyaishi ukweli bado natamani bora hata mwizi Lowassa angewajali watu wa Bulyanhulu kama alipambana kuleta maji Kahama kuyatoa Ziwa Victoria pamoja na mkwara wa Misri kuwa asitishe huo mradi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, naona tayari umeanza kulewa. Pamoja na kwamba ulianzisha mada nzuri na yenye kuhitaji uchambuzi yakinifu na hoja za maana, lakini naona tayari umeingiza siasa na chuki za ukabila na hata kuwataja akina Lowasa na miradi ya maji.
Yaani kwakifupi haueleweki mkuu.

Mimi nilidhani ungeanza kwa kuwataja akina marehemu Njile, Toloka, Jonathan, Ernest na Mororasa ni baadhi ya majina yanayotamkwa na wengi na kutajwa kuwa walifukiwa na magreda ya Kampuni ya Kahama Mining Corporation Ltd (KMCL) – wachimbaji dhahabu Bulyanhulu. Na pengine nilidhani hoja yako hapa ingekuwa kama makazi wa Kakola, mkoani Shinyanya, unge endelea kudai ufanyike uchunguzi huru juu ya tukio hilo ambalo linatajwa kuangamiza maisha ya watu karibu 52.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushirombomen nafahamu kwenye mambo ya msingi huwa unaingiza ukabila, hebu tafakari, vaa viatu vya watu wa Bulyanhulu na maisha wanayoyaishi ukweli bado natamani bora hata mwizi Lowassa angewajali watu wa Bulyanhulu kama alipambana kuleta maji Kahama kuyatoa Ziwa Victoria pamoja na mkwara wa Misri kuwa asitishe huo mradi

Sent using Jamii Forums mobile app
Kahàma ilikuwa inafaha iwe job ya South

Mikatba yote waliosaini ndio wamegawana na wazungu

Pia sijui kwanini wazungu wanajenga barabara za vumbi hata hapa buzwagi yale yale

Hawa viongozi pia wakipowe hela za kujenga barabara kutoka migodini huwa wanazila barabara wanajenga ovyo ovyo

Mradi wa kujenga chuo kakola kahama ulihamishwa kàbisa

Maishi ya watu wanaoishi karibu na migodi na wanaofanya kazi za machimboni maisha yao magumu hatari sana



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mayor Slum,

Mkuu naomba nikujibu hoja sako kama ifuatavyo:

1- Ukisema kahama ilitakiwa kwa mfanano iwe job ya South, hapo unamaanisha nini?

Yawezekana sana hapa ulikuwa una hoja ya msingi lakini haujaiweka vizuri bado.

2- Unapo sema Mikatba yote waliosaini ndio wamegawana na wazungu, hapa unamaanisha mikataba ipi na niakina nani walio gawana na wazungu?

3- Akina nani waliwahi kupewa fedha za ujenzi wa barabara na wakazikula..?? Na je unao ushaidi wa waliotoa fedha ama walio pokea fedha za barabara?

4- Je unatambua nani mwenye jukumu la kujenga barabara? Je, uliwahi kuona ama kusikia muwekezaji kwenye mgodi wa Bulyanhulu akipewa jukumu la ujenzi wa barabara kama sehem ya makubaliano kwenye sehemu ya uchimbaji?

5- Ebu tuweke sawa nasi tujuwe huu mradi wa kujenga chuo kakola kahama ulihamishwa wapi?

Lakini kama kumbukumbu zangu zipo sawa, nakumbuka watoto walioishi kwenye maeneo yanao izunguka mgodi walikuwa wakipelekwa chuo cha ufundi Moshi ili wakapate ujuzi na kisha walikuwa wanakuja kuajiriwa tena mgodini pale.

6- Ugumu wa maisha ya wafanya kazi wa migodini unao usemea wewe ni ugumu wa kujitakia. Na sababu ya mimi kusema hili ni kwamba ugumu huu ulitokana na wafanyakazi kupenda starehe pamoja na anasa zikizo pita kiasi aiseeee.

Na hata wakazi walio zunguka eneo la mgodi walijikuta wanaacha kulima na kufanya shughuli zingine za maendeleo kwa kutarajia kwamba mgodi utakuwa unawalipa mishahara for nothing. Hawa wakazi walipaswa kuilaumu serikali yao iliyo ingia mikataba mibovu na kutokusimamia maslahi ya wakazi/wanakijiji walio zunguka maeneo ya mgodi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushimen, Kipengele namba 5: Mgodi wa Bulyanhulu kwa nia njema kabisa ulitaka ujenge VETA ya kisasa jirani na eneo la mafunzo la mgodi liitwalo MABINGWA pale BUGARAMA ili vijana wanaohitimu masomo shule za msingi na sekondari wafundishwe namna ya kuendesha mitambo mbalimbali iliyopo migodini ili mgodi usitumie gharama kubwa kupata wafanyakazi na pia lengo la mgodi ilikuwa kuwafanya vijana wapate fani mbalimbali.

Serikali ikishirikiana na kaburu Mtanzania (kwa tafasiri ya Mwalimu Nyerere) bibi Frida Kessy wakapeleka huu mradi Moshi. Yaani mtoto au kijana anayetoka maeneo haya akasomee Moshi!! Hili lilifanyika huku mbuge Maige akiwa yupo busy na twiga kipindi hicho. Inauma ila ipo siku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ng'wanapagi, Mkuu, naona kabisa hapa unazungumzia simulizi.

Naomba nikukumbushe kwamba mgodi ulianza kusomesha watoto enzi za Mama Suguti watoto walio maliza kidato cha nne walipelekwa kujifunza ufundi huko Moshi, kipindikile hata Mabingwa haikuwa imebuniwa (R.i.P Mayunga).

Mgodi wa Bully uliharibiwa na sisi wenyewe, ilhali wawekezaji sikuzile walikuwa na nia njema na good plans kwa future ya wakazi wa pale.

Kumbuka hata lile soko lililo jengwa pale mwembe maua, ebu naomba uwe shuhuda nini kilitokea..??
Mgodi ulijenga shule ya sekondari pale kakola baada ya kupita kidogo Jensen, je unakumbuka wazazi waliwajaza nini watoto/wanafunzi wale na nini walicho kifanya..??

Mkuu, ebu usidanganye kwa kulaumu Wazungu/wawekezaji/KMCL/Palcer Dome/ABGML/Barrick/Acaccia.

Mnapaswa mjilaumu ninyi pamoja na viongozi wenu kuanzia ngazi ya kijiji na kupanda juu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushimen, Siko hapa kubishana au kujionyesha mjuaji kama unavyotaka. Soko unadaganya lilijengwa Mwembemaua wakati soko lilijengwa Bugarama kitongoji cha Bunango secondary walijenga Bugarama na ilifunguliwa na Raisi mstaafu Jakaya Kikwete tena kipindi anafungua mie niko kazini Zanzibar na jiwe la msingi na tarehe nitaomba mtu anitumie kwa picha uone

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siko hapa kubishana au kujionyesha mjuaji kama unavyotaka. Soko unadaganya lilijengwa Mwembemaua wakati soko lilijengwa Bugarama kitongoji cha Bunango secondary walijenga Bugarama na ilifunguliwa na Raisi mstaafu Jakaya Kikwete tena kipindi anafungua mie niko kazini Zanzibar na jiwe la msingi na tarehe nitaomba mtu anitumie kwa picha uone

Sent using Jamii Forums mobile app
Ohhh....
Kumbe hautaki kupingwa kwa hoja eehhhh....

Na nimeona kuanzia hoja yangu ya kwanza hakuna ulicho kijibu kikaelekewa, pengine ulitani utuburuze tu kama utakavyo na tusihie kusikitika.

Basi ngoja nikuunge mkono tu mkuu.
Bilashaka nimekufurahisha sasa
 
Back
Top Bottom