YanguHaki
Senior Member
- Oct 11, 2010
- 129
- 9
Jamani mbona SISIEM inatupeleka pabaya! Kweli tuna sheria za kipuuzi za namna
hii zinazoweza kuruhusu mbunge wa viti maalum mkoa wa Tanga aitwye Mary Chitanda kushiriki uchaguzi wa umeya Arusha mjini unaofanywa na madiwani wa kule? Sijui kwa kuwa ni katibu wa SISIEM wa Wilaya Arusha? Tuite ni ulevi wa madaraka au kujisahau au ni nini hiki? Naona kila dalili ya kutaka kuvuruga amani ya nchi kwa uchu wa kutaka kupata kila nafasi ya uongozi nchini. Maslahi ya SISIEM yapo mbele ya WANANCHI wa taifa lake. Siku mambo yakiharibika hapa nchini hii lawama mtaikwepa vipi? Wako wapi wazee wa chama au nao ndo wamepofuka? Hawaoni? Ila tahadhari tuendako huko wengi mtaishia The Hague msipoangalia.
hii zinazoweza kuruhusu mbunge wa viti maalum mkoa wa Tanga aitwye Mary Chitanda kushiriki uchaguzi wa umeya Arusha mjini unaofanywa na madiwani wa kule? Sijui kwa kuwa ni katibu wa SISIEM wa Wilaya Arusha? Tuite ni ulevi wa madaraka au kujisahau au ni nini hiki? Naona kila dalili ya kutaka kuvuruga amani ya nchi kwa uchu wa kutaka kupata kila nafasi ya uongozi nchini. Maslahi ya SISIEM yapo mbele ya WANANCHI wa taifa lake. Siku mambo yakiharibika hapa nchini hii lawama mtaikwepa vipi? Wako wapi wazee wa chama au nao ndo wamepofuka? Hawaoni? Ila tahadhari tuendako huko wengi mtaishia The Hague msipoangalia.