Sisi ni wanachama wa Jumuiya ya Madola lakini tunatengwa katika fursa

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Mwezi wa 12, MK254 aliweka uzi hapa unaohusu Uingereza kuchukua Wakenya kwaajili ya ajira. Rafiki yangu alibahatika kwenda kwenye kongamano hilo lililofanyika Nairobi. Kwakua rafiki yangu anaishi Dar na ufuatilikiaji ulimshinda kwa vigezo.

Wanaajiri kada zote mradi tu ujue kuongea na kuandika Kiingereza, mpaka wafanya usafi wa hospital. Kwa kifupi mradi uwe umemaliza darasa la 12 na uwe na cheti cha IELTS. IELTS ni mtihani wa Kiingereza unaofanywa British

Rafiki yangu aliniomba ni fiat iLife. Nilipiga simu na kutaarifiwa kuwa, waliokidhi vigezo wamesha pata visa na wanasafiri baada ya Pasaka tayari kwa kuanza ajira nchini Uingereza. Zaidi ya hapo, kwakua wana shida sana ya wafanyakazi sekta ya afya, wenye degree hawahitaji cheti cha IELTS.

Sasa nafasi kama hizi mbona hazitangazwi kwa Watanzania? Wizara ya mambo ya Nje itusaidie, kukiwa na Watanzania wanaofanya kazi nje kunasaidia kuinua uchumi kwa pesa wanauotuma nyumbani.
 
Juzi tuu Uingereza wameupdate list ya nchi ambazo hawaruhusiwi ku-recruit sababu eti na wao pia wana shortage ya staffs hasa hasa kada ya afya.


Lakini ukija kwa ground kuna watu wengi wamegraduate hawana ajira wanateseka mtaani tuu.
Unforgetable
 
Juzi tuu Uingereza wameupdate list ya nchi ambazo hawaruhusiwi ku-recruit sababu eti na wao pia wana shortage ya staffs hasa hasa kada ya afya.


Lakini ukija kwa ground kuna watu wengi wamegraduate hawana ajira wanateseka mtaani tuu.
Unforgetable
Mwisho wa maelezo wamesema kama serikali ya nchi husika na Uingereza zikielewana wanaweza kuajiri.
 
Back
Top Bottom