Sishauri Forker 50 na Forker 28 ziwe 'Branded' kama Ndege za Kibiashara za ATCL

Sio lazima uanze routes ndio ujue kama ndege ulizonazo zitatumika to full capacity; kuna wataalam wanafanya kazi yao na kujua demand ya seats za kila route. Mpaka sasa hizo safari na routes unazosema compétition ni very fierce mpaka hiyo DREAMLINER imeishia kubeba MBUZI kwenda Dubai. Hizo safari za India na China mpaka leo ni ndoto; kwani hata wakienda wana uhakika gani kuwa watakuwa na passengers na cargo ya kutosha wakati wa return leg!

Kuhusu kuziuza hizo ndege you will be better off kuziuza pale unapopata bei nzuri kuliko kuzifuga bila matumizi!! Locally mpaka sasa zile Bombardier na Airbus zinatosha kabisa na hata kuwa na excess capacity so the only rational decision ni kuuza hizo ndege za serikali kwa mbei nzuri.

Huwa nafurahi na napenda mno kukutana na ' Genius Members ' kama Wewe na baadhi hapa Jamvini JamiiForums. Mkuu uko vizuri ' Upstairs ' kiasi cha kunifanya nihisi labda na Wewe una ' Vinasaba ' vya Kiyahudi ( Israel ) ni ' nadra ' sana kukutana na Watu makini hapa Jamvini kama Wewe ila ni kawaida kukutana na ' Mipopoma ' ambayo yenyewe Kazi yao ni Kutetea tu hata kama ni ' Upuuzi ' ili mradi tu walinde ' Vitumbua ' vyao wakati badala ya kuzitumia vyema ' Akili ' zao katika ' Kupambanua ' na ' Kuchanganua ' mambo ili basi waweze Kumsaidia ' Master ' wao wanaemnyenyekea na kumlamba Miguu kila Uchao.

Cc: commonmwananchi , narumuk
 
Nashukuru Mungu kuwa kupitia tu ' Uzi ' wangu huu nimeweza sasa kuwajua wale ' Waliobarikiwa ' kwa ' Upumbavu ' hadi Milele. Nimeweka wazi sana Hoja yangu kuwa sishauri hizo Ndege za Rais ziwe ' branded ' hivyo na zibebe ' Abiria ' kwa Hoja ya Rais kama alivyosema na kama nia ni Kuiongezea Mapato ATCL na Kuimarisha Sekta ya Anga nchini basi hizo Ndege kama ziko Tatu mbili zibebe Abiria ila Ndege moja ibaki vile vile kuwa ni ' Maalum ' tu kwa Kumbeba Mheshimiwa Rais au Makamu wake au Waziri Mkuu wake lakini zote zisifanywe zikawa za Abiria. Na kama haitoshi katika Maelezo yangu nisema vyema tu kuwa kama ikiwezekana basi ni bora hizo Ndege ziuzwe na Hela inayopatikana hapo ielekezwe katika Sekta muhimu ya Kilimo ambayo Kwangu Mimi bado inahihati nguvu kubwa lakini bado ' Mifungulu Ngenge ' fulani isiyojua Kufikiri na inayojua tu Kujipendekeza kama siyo Kujikomba inatetea.

Ngoja niendelee ' Kuwadharau ' hapa.

Cc: Saguda47 , heavyload, narumuk , retweeted , jogoo_dume , idawa , sonaderm , Rogojin The Idiot , Elly official , kakolaki , Lokissa , MWALLA
hamna lolote bla bla tuu, leo umeingia cha kike kwa kusaka kwako sifa!.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilitegemea nikutane na uchambuzi makini labda juu ya gharama za uendeshaji wa hizo ndege au usalama wake kumbe ngonjera tu.
 
Huyu jamaa anajifanya ana akili sana na mjuzi wa mambo, na Mimi mwanzoni nilikuwa namchukulia hivyo lakini hili andiko, let me reserve my comments! Unajua kitendo alichofanya JPM ni cha kipongezwa cha kutoa hizi ndege zizalishe! Niliumia sana siku moja wakati mtoto wa (yule waziri wa ndani alofukuzwa kwa ulevi na Magufuli ) alipofariki ndege ya serikali ilikuwa imepaki mwanza airport ikiksubiri mama salma (enzi za JK) tangu asubuhi hadi jioni. Ni bora ibaki moja na nyingine zizalishe. After all kwa vile ni ndogo ATCL waweza kuwa wanasitumia kwa route ambazo zina abiria wachache. Aidha alinikosha aliposema ndege hizi zinaweza kukodishwa nikafikiria Dreamliner ni bora ikakodishwa kwa mtano Ethiopian airlines au mashirika mengine zizalishe

Siyo kwamba najifanya nina ' Akili ' bali ukweli na uhalisia ni kwamba nina ' Akili ' kiasi kwamba nina uhakika ungekuwa nazo angalau hata robo yake ' ungeringa ' kama siyo ' kutamba ' sana ila bahati mbaya Kwako wakati Mwenyezi Mungu ' anatubariki ' nazo Sisi wengine hakuona umuhimu wowote wa kukupa na Wewe na ndiyo maana hadi sasa unatudhihirishia ' Ufulu Ngenge ' wako hapa.
 
hizi ndege mbili Forker 50 na Forker 28 zinatumika na makamu wa Rais na nyingine Waziri Mkuu na ile iliyonunuliwa wakati wa Rais Mzee Mkapa chini ya waziri wa fedha Bazil Mramba(hata kama ni nyasi wananchi watakula lkn ndege ya rais ni lazima Bungeni) ndiyo inayotumiwa na Rais wetu John Maguful
Ni kwa nini watu wanalalamika ni kwa sababu kwanza ndege moja tulipewa kama zawadi na Malkia wa Ungereza kwa Rais wetu wa kwanza Mzee hayati Mwalimu Nyerere na ndani ya hiyo ndege ni VIP na imetenganishwa na vinyago vyenye uhalisia wa nchi yetu, kwa hiyo ni heshima na kumbukumbu kuendelea kuzitunza kwa matumizi sahihi ambayo ni kwa ajili ya viongozi wakuu wa nch na siyo kuzipeleka kwenye biashara
Tufanye biashara na hizi ndege sita ambazo tunazo kwa sasa na tuangalie maendeleo yake na ikiwezekana basi hizo hizo sita zijiendeshe zenyewe na ziweze kujiongeza ikiwezekana kila miaka 3 ziweze kununua nyingia moja
 
Mleta mada ilibidi aje na hoja kama hizi angeeleweka, kwa kuongeza hiyo Fokker 28 iuzwe tu kabla haijatufia jumla.
Mh. Rais kwa hili inabidi ashauriwe upya... Nina sbb za msingi mno mnoo..!!

1: Fokker 28, kwa kubebea abiria hailipi kabisaa kabisaa.. Sijui nisemeje mnielewe, yaani was not meant for paxs business.. Ni ndege inayokula mafuta sana, pia vifaa vyake vya matengenezo ni ngumu kuvipata sbb ni ndege mzee sana..!! Sbb hizo ndege F28 zilisha achwa kutengenezwa miaka mingi hivyo spears ni ngumu mno kupata, biashara haitaweza na ni fuel guzzler yaani..!! Yaani ni sawa na VX V8 upaki na dala dala upakie abiria utegemee profit..!! It doesn't work.. Hili tutapenyeza ushauri kwa mh Rais ili ajue ukweli halisi, mh Rais ni mtu mwelewa sana hana shida..!!

2: Fokker 50, hii biashara ya kubeba abiria inaweza na inalipa, ulaji wa mafuta ni mzuri, vifaa vya spears vinapatikana, hili halina tatizo..

Tatizo la kupeleka F50 ATCL ni hili hapa:
Fokker 50 ndio ndege pekee imebaki kama moyo na roho ya serikali kwa domestic flights zote za viongozi wa juu, ikiwemo Mh. Rais mwenyewe, Makamu, Rais wa Znz, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais wa Znz na National events zote za kitaifa za ndani.. G550 mostly ni kwa international flights..!! Sasa ingawa Mh. Rais haruki mara kwa mara, hawa viongozi wengine wote, wasaidizi wake hapo juu, huruka nyingi, karibu kila siku, nchi nzima, serikali hutegemea hiyo F-50 kwa asilimia 100% kusafirisha hao viongozi.. Sasa sielewi viongozi hao watasafiri vipi ikiwa F-50 itaenda ATCL..!! Nchi ni kubwa mno kusafiri kwa gari..!! Pia ndege ikiwa inatumia na abiria mara kwa mara itachoka haraka, sijui kama hilo wameliona, na ndege za viongozi zinatakiwa salama mno mnoo, sasa sielewi itakuaje, ugumu mkubwa itakuwa kwa wasaidizi wake Mh. Rais, sbb watapata shida sana kusafiri ikiwa F-50 itaenda ATCL.. Ujue ukishapanga ndege kwenye schedule ya abiria, na inaruka, tayari ushaingiza hasara na abiria watakuwa na usumbufu, sbb mfano imeruka asubuhi, mchana F-50 inatakiwa kuruka na kiongozi, na kuna route ya abiria na hakuna ndege ya kuwachukua hao abiria labda nyingine, tayari ni mvurugano kweli kweli..!!

Anyway, Mh. Rais ndio muamuzi wa mwisho, pamoja na nia njema sana aliyonayo, ila hili ni ngumu mno, ataja ona katika utekelezaji..!! Siku njema sana niwatakie..!!
 
hizi ndege mbili Forker 50 na Forker 28 zinatumika na makamu wa Rais na nyingine Waziri Mkuu na ile iliyonunuliwa wakati wa Rais Mzee Mkapa chini ya waziri wa fedha Bazil Mramba(hata kama ni nyasi wananchi watakula lkn ndege ya rais ni lazima Bungeni) ndiyo inayotumiwa na Rais wetu John Maguful
Ni kwa nini watu wanalalamika ni kwa sababu kwanza ndege moja tulipewa kama zawadi na Malkia wa Ungereza kwa Rais wetu wa kwanza Mzee hayati Mwalimu Nyerere na ndani ya hiyo ndege ni VIP na imetenganishwa na vinyago vyenye uhalisia wa nchi yetu, kwa hiyo ni heshima na kumbukumbu kuendelea kuzitunza kwa matumizi sahihi ambayo ni kwa ajili ya viongozi wakuu wa nch na siyo kuzipeleka kwenye biashara
Tufanye biashara na hizi ndege sita ambazo tunazo kwa sasa na tuangalie maendeleo yake na ikiwezekana basi hizo hizo sita zijiendeshe zenyewe na ziweze kujiongeza ikiwezekana kila miaka 3 ziweze kununua nyingia moja

Sidhani kama ' Wapuuzi ' waliojazana hapa watakuelewa kwa hili ila kwa Sisi ' Werevu ' wenzio na ambao kwa bahati mbaya sana hapa tuko wachache tumekuelewa vizuri kabisa kwa hiki ulichokiandika. Hongera Mkuu uko vyema.

Cc: commonmwananchi , narumuk
 
Mleta mada ilibidi aje na hoja kama hizi angeeleweka, kwa kuongeza hiyo Fokker 28 iuzwe tu kabla haijatufia jumla.

Kama sikuja na Hoja hiyo kuna tatizo gani Mtu mwingine akija nazo na Kuzijazilia kama huyo unayempongeza hapo? Mbona Wewe tokea uanze Kuchangia huu Uzi hakuna Hoja yoyote uliyoitoa hapa zaidi tu ya kila mara ukija unasema sijaweka Hoja katika Uzi wangu? Hivi baada ya Mimi labda ' Kuchokoza ' Mada hii Wewe ambaye umeona ' Mapungufu ' yako ulishindwa nini sasa kutuonyesha jinsi ulivyo ' Genius ' ili uje na ' Facts / Data ' zako za Kutosha kama walivyofanya Watu wengi hapa ambao wamekuzidi upeo / fikra? Idiot!
 
Yani kuna watu akili zao sipo chini sana tena sana sasa Rais anakuwa na ndege tatu za nini si bora zilete pesa zifanye kazi nyingine kuliko kupaki tu hadi Rais asafiri

Sent using Jamii Forums mobile app
Ebo!!!!! Ukiskia zoba ujue ni ww, usidandie kitu usichoelewa... Rais ni taasisi, vile vile ujue hatumii yy peke yake... Kuna makamu wake, Waziri mkuu.. So Tuliza bwambwa..
 
Ndege zikinunuliwa mnalalamika, zikipewa matumizi mnalalamika..hili la serikali kuwa na ndege tatu chadema walikuwa hawalijui..wangekuwa wamepiga kelele toka enzi za jk..wengi wanaijua ile ya kula nyasi ya mramba.
Jamaa kaonyesha uzalendo bado wao wanapiga keleke..

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu.
Sasa chadema imebadili jina na inaitwa chama cha machochezi .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni ' dharau ' kubwa kwa Marais waliopita kuanzia Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa na Mzee Kikwete kwa Mtu mmoja leo kuamua kwa ' Kukurupuka ' tu kuwa Ndege za Rais Forker 50 na Forker 28 ziwe ' Branded ' kama ' Commercial Planes ' za ATCL.

Hili halipo na halijawahi kutokea nchi yoyote ile duniani na naamini hata tungekuwa Mbinguni Kwake Mwenyezi Mungu hata Yeye pia asingefanya hiki ' Kituko ' ambacho GENTAMYCINE nakiita ni cha Kufungulia mwaka huu ambao bado ni mbichi kabisa wa 2019.

Hoja kwamba zipakwe rangi kisha zichuke Abiria kwakuwa huwa zinakuwa ' grounded ' tu na kwamba hata mwenye Kuhusika nazo huwa hazitumii kwakuwa hasafiri mara kwa mara kutolewa na ' PhD Holder ' kidogo ni kutaka Kuwadhalilisha ' Intellectuals ' wote nchini Tanzania.

Wasaidizi wa Rais hebu fanyeni Kazi zenu vyema Kwake kwa Kumshauri mnaogopa nini? Hivi Sekta ya Anga ya leo au ATCL ya leo inahitaji kweli hadi hata Ndege za Marais nazo ziwe ' branded ' na zijumuishwe kama Ndege za Biashara na Kubeba Abiria? Je kuna hilo hitaji kweli?

Ningeambiwa au ningesikia Hoja kwamba labda Ndege hizo ziuzwe na ibaki moja kisha hizo Hela zitumike Kuimarisha Sekta ya Kilimo au nyinginezo ambazo zinahitaji msaada na ungalizi mkubwa ningemwelewa Mheshimiwa Rais na ningekubaliana nae kwa 100% ila kwa hii Hoja yake ya leo nampinga na naona ni kama vile ' Tusi ' kwa Watangulizi wake.

Wengine tumeumbwa kuwa wakweli na wawazi hivi hivyo mtusamehe tu na tuvumiliane. Tuache Kukurupuka na kuwa na ' Mihemko ' isiyo na Tija wala Mantiki. Halafu akina Donald Trump ' wakitutukana ' Waafrika huwa tunalalamika na kuona labda anatuonea wakati kumbe huwa yuko sahihi tena kwa 100% zote kutokana na ' Madhaifu ' yetu ya asili.

Nimesikitika!

Nawasilisha.
Hivi unajua China hakuna ndege ya Rais Raid akitaka kusafiri wanachukua commercial jet wanabrand tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mh. Rais kwa hili inabidi ashauriwe upya... Nina sbb za msingi mno mnoo..!!

1: Fokker 28, kwa kubebea abiria hailipi kabisaa kabisaa.. Sijui nisemeje mnielewe, yaani was not meant for paxs business.. Ni ndege inayokula mafuta sana, pia vifaa vyake vya matengenezo ni ngumu kuvipata sbb ni ndege mzee sana..!! Sbb hizo ndege F28 zilisha achwa kutengenezwa miaka mingi hivyo spears ni ngumu mno kupata, biashara haitaweza na ni fuel guzzler yaani..!! Yaani ni sawa na VX V8 upaki na dala dala upakie abiria utegemee profit..!! It doesn't work.. Hili tutapenyeza ushauri kwa mh Rais ili ajue ukweli halisi, mh Rais ni mtu mwelewa sana hana shida..!!

2: Fokker 50, hii biashara ya kubeba abiria inaweza na inalipa, ulaji wa mafuta ni mzuri, vifaa vya spears vinapatikana, hili halina tatizo..

Tatizo la kupeleka F50 ATCL ni hili hapa:
Fokker 50 ndio ndege pekee imebaki kama moyo na roho ya serikali kwa domestic flights zote za viongozi wa juu, ikiwemo Mh. Rais mwenyewe, Makamu, Rais wa Znz, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais wa Znz na National events zote za kitaifa za ndani.. G550 mostly ni kwa international flights..!! Sasa ingawa Mh. Rais haruki mara kwa mara, hawa viongozi wengine wote, wasaidizi wake hapo juu, huruka nyingi, karibu kila siku, nchi nzima, serikali hutegemea hiyo F-50 kwa asilimia 100% kusafirisha hao viongozi.. Sasa sielewi viongozi hao watasafiri vipi ikiwa F-50 itaenda ATCL..!! Nchi ni kubwa mno kusafiri kwa gari..!! Pia ndege ikiwa inatumia na abiria mara kwa mara itachoka haraka, sijui kama hilo wameliona, na ndege za viongozi zinatakiwa salama mno mnoo, sasa sielewi itakuaje, ugumu mkubwa itakuwa kwa wasaidizi wake Mh. Rais, sbb watapata shida sana kusafiri ikiwa F-50 itaenda ATCL.. Ujue ukishapanga ndege kwenye schedule ya abiria, na inaruka, tayari ushaingiza hasara na abiria watakuwa na usumbufu, sbb mfano imeruka asubuhi, mchana F-50 inatakiwa kuruka na kiongozi, na kuna route ya abiria na hakuna ndege ya kuwachukua hao abiria labda nyingine, tayari ni mvurugano kweli kweli..!!

Anyway, Mh. Rais ndio muamuzi wa mwisho, pamoja na nia njema sana aliyonayo, ila hili ni ngumu mno, ataja ona katika utekelezaji..!! Siku njema sana niwatakie..!!
Mkuu!
Msilifanye hili kutafutia credits za kisiasa.
Tanzania tuna routes nyingi sana za kuitumia hii folker 50.
Viwanja kama seronera aistrip (serengeti national park).

Vinahitaji ndege kama hii. Tuna watalii kibao wa kuunganisha dsm kwenda serengeti na kurudi kupitia KIA na zanzibar.

Pia hili linakuwa ni suala la ubunifu wa kibiashara zaidi kuhusiana na mahitaji ya wakati husika.

Sio lazima ndege hizi zipangiwe permanently routine, bali zitatumika multiple sided kati ya huduma za kiserikali na business kwa ATCL kwa upande mwingine.

Viongozi wa serikali hawasafiri kila siku, hivyo sidhani kwamba viongozi wa idara husika watashindwa kupanga ratiba husika.
Na ndio maana wameajiriwa pale na sio humu JF.

Tuache wenye idara zao wawajibike, sisi acha tuwndelee kuvizia hotuba ijayo ya mh Rais kipenzi cha watanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesikitika
Pole sana mkuu
Fokker 28 ikibadilishwa viti inaweza kuchukua mpaka watu 28
Kuna route ya mafia,songea inalipa sana,inahitaji ndege ndogo kama hizo
Huna haja ya kuhuzunika Rais atabaki na ile ndege tulioambiwa hata nyasi tutakula,inamtosha,hizi zingine zilikua zinatumika vibaya tu,sasa ataehitaji atalipa,ka VP au Pm wana ziara za kikazi watatumia tu,kwa kua bado ni za serikali
 
Kama mpaka hivi leo upo hapa JamiiForums na hujui GENTAMYCINE yupo Chama gani cha Kisiasa hapa nchini Tanzania basi lazima tu utakua ni ' Mpumbavu Uliyethibitishwa Kimataifa ' kabisa. Hivi kuna ' Member ' ambaye mwaka 2015 alipambana na wana CHADEMA hapa Jamvini kumpigia Chapuo / Kampeni Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli kama Mimi na wale wana CCM wenzangu baadhi? Rejea ' posts ' na ' threads ' zangu zote za mwaka 2015 ili ujiridhishe juu yangu.

Tatizo lenu wana CCM wenzangu ' Wapumbavu ' baadhi mnadhani Kumpamba au Kumuunga Mkono sana na Kumpa matumaini Mwenyekiti wetu Taifa Ndugu Dkt. Magufuli ndiyo Kumsaidia wakati kumbe ni Kinyume chake. Nilimpigania na Kumpambania mwaka ule wa 2015 kwakuwa nilikuwa na Matumaini nae na hadi mpaka hivi leo / sasa bado namkubali tena mno tu na pengine kuliko hata nyie wana CCM ' Mapopoma ' mlivyo ila tofauti yangu na yenu ni ndogo sana tu ambapo Mimi huwa sijazoea Unafiki, Uwongo au Kujipendekeza bali huwa ' nanyoosha ' tu maelezo yangu ukiumia shauri yako na katika hili sitobadilika ng'o.

Kuna ' Threads ' nyingi sana hapa Jamvini nimezianzisha Kumsifu Rais Dkt. Magufuli mbona Wewe mwana CCM ' Popoma ' sijawahi hata Kukuona mara moja tu ukija Kunipongeza? Kwahiyo nyie GENTAMYCINE anakuwa ' Adui ' Kwenu na siyo mwana CCM mzuri pale tu akimkosoa tena kwa Kumjenga vyema Mwenyekiti Taifa pekee? Kama wana CCM wa sasa wengi wenu ndiyo wana aina hii ya Upeo wa ' Kifungulu Ngenge ' basi naona Chama kimekula hasara kubwa na kinahitaji Mabadiliko makubwa na ya haraka pia.

Cc: commonmwananchi
Mkuu, tuweke historia yako pembeni, ukweli wewe ukumuelewa raisi na pia ulisahau idadi ya ndege za raisi zilizopo na mwisho, pia ulisahau kuwa ndege zina umri na uimara wa ndege upungua kadri inavyokuwa imepaki bila kuruka. UKIKUBALIANA NA HAYA NITAONA BONGE LA MDAU ANAYEJIELEWA NA KUELEWA KUWA SISI BINADAMU WOTE TUNAWEZA KUKOSEA NA TUKAJISAHIHISHA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
54 Reactions
Reply
Back
Top Bottom