Mlalahoi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2006
- 2,182
- 883
Siri za wizi alizofichwa Mkaguzi Mkuu nje nje
Mwandishi Wetu
Aprili 20, 2011
- Mabilioni yaligawanywa kama njugu kufidia hasara hewa
- Ni kampuni 27 za vigogo, imo Al-Adawi iliyovuna mil 400/-
WAKATI Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) akiripoti kunyimwa orodha ya kampuni za ununuzi pamba zilizolipwa mabilioni wakati wa mtikisiko wa uchumi duniani, Raia Mwema, inayo orodha hiyo ya kampuni zaidi ya 26, ikiwamo kampuni inayoitwa Al-Adawi Limited.
Al Adawi ni jina linalofanana na jina la mtu aliyejitambulisha kuwa ni mmiliki wa kampuni ya Dowans, akiitwa Brigedia Jenerali (mstaafu) Sulaiman Al-Adawi. Kampuni hiyo ilipendekezwa kuchotewa Sh milioni 405.6.
Mbali na Al-Adawi, katika mchanganuo wa hesabu za kampuni husika, uliopendekezwa na baadhi ya benki nchini ambazo ni CRDB, Stanbic, Exim na Kenya Commercial, moja ya kampuni imebainika kulipwa hadi bilioni 1.4, wakati hasara iliyopata ni sh milioni 742, kampuni nyingine imefidiwa hasara ya Sh milioni 500, wakati ikibainika haikupata hasara yoyote.
Katika toleo namba 129 (Aprili 14 hadi Aprili 20) mwaka jana, gazeti hili liliripoti orodha ya kampuni hizo, ambazo kabla ya kulipwa mabilioni hayo, michanganuo ya hesabu zake ili kubaini hasara walizopata kutokana na mtikisiko wa uchumi, ililazimika kurejewa baada ya michanganuo ya awali kugubikwa na taarifa za uongo.
Lakini wakati Raia Mwema likiwa limepata orodha ya kampuni hizo kutokana njia zake za uchunguzi, CAG anaeleza kunyimwa orodha hiyo na kubainisha hayo katika ripoti yake kuhusu ukaguzi wa taarifa za fedha za Serikali Kuu kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2010.
Ingawa Bunge liliidhinisha Serikali kutumbukiza Sh trilioni 1.7 kwa ajili ya kudhibiti mtikisiko wa uchumi uliotajwa kuathiri zaidi kampuni za ununuzi wa pamba, CAG anaeleza kuwa kilichotolewa na Serikali ni Sh bilioni 48 na amenyimwa orodha ya kampuni zilizopewa mabilioni hayo.
"Serikali kupitia Hazina ililipa kiasi cha Sh 48,000,270,000 katika Benki ya Tanzania kama mchango wake katika kuchochea ukuaji wa uchumi kutokana na mtikisiko wa uchumi ulioikumba dunia.
"Hata hivyo, Hazina haikutoa orodha ya makampuni au watu binafsi walionufaika na fidia hiyo au malipo ya madeni yao kuahirishwa.
"Utaratibu wa kurekodi malipo na marejesho ya fedha hizi haukuwekwa bayana na hivyo kushindwa kujiridhisha endapo yalikuwa ni malipo halali ya fedha za umma," anaeleza CAG, Ludovick Utouh.
Hotuba ya Rais Kikwete
Kutokana na mtikisiko wa uchumi duniani, ulioanzia Marekani, Rais Jakaya Kikwete alitangaza mpango wa serikali kudhibiti mtikisiko huo nchini.
Mara baada ya hotuba yake, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, aliliomba Bunge kuidhinisha Sh trilioni 1.7 kwa ajili ya kudhibiti mtikisiko hasa kwa wanunuzi wa pamba, ili kutoathiri wakulima.
Kwa wakati huo, wanunuzi wa pamba walitajwa kuathirika kutokana na bei ya zao hilo kwenye soko la dunia kuporomoka na wao kupata hasara kiasi cha kukosa fedha za kununua tena pamba kwa wakulima.
Bunge lilipitisha maombi hayo ya Waziri Mkulo, ingawa pia baadhi ya wabunge walitaka fungu hilo maalumu lililioitwa ‘stimulus package' liundiwe sheria maalumu ya Bunge ili kudhibiti matumizi yake na kuepusha nchi kutumbukia katika kile kilichotajwa kama EPA namba mbili.
Hata hivyo, haikuridhiwa kuundwa kwa sheria mahsusi, na badala yake Serikali iliahidi bungeni kuwa CAG atakagua hesabu za mgawo huo.
Benki zilizohusika na mgawo
Serikali kupitia Hazina ilitoa fedha hizo kwa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), ambayo iliweka fedha hizo katika baadhi ya benki ambazo zilipewa jukumu la kuwafidia wanunuzi husika wa pamba, baada ya kufanyika michanganuo ya hesabu na hasara walizopata.
Benki zilizohusika ni CRDB, Tanzania Investment Bank (TIB), Exim Bank, Stanbic Bank na Kenya Commercial Bank.
Kampuni na michanganuo tata
Benki ya CRDB ilifanya michanganuo ya kampuni 26 na Benki ya TIB ikipitia mchanganuo wa kampuni ya Al-Adawi pekee na kupendekeza ilipwe Sh milioni 405.6.
Benki ya Kenya Commercial, nayo pia ilipitia michanganuo ya kampuni kadhaa na kutaka zilipwe. Kampuni hizo ni Birchand Oil Mills Ltd, ambayo Kenya Commercial ilitaka kampuni hiyo ilipwe Sh bilioni 1.66.
Hata hivyo, baada ya michanganuo hiyo kurejewa na watalaamu nje ya benki hiyo ilibainika kuwa kampuni hiyo ilistahili kulipwa Sh bilioni 4.642, kukiwa na ongezeko zaidi kulinganisha na mapendekezo ya awali.
Benki ya Exim ilipendekeza kampuni ya Bio Sustain kufidiwa Sh milioni 597.7 hata hivyo, baada ya kufanyika upya kwa uhakiki kampuni hiyo ikapendekezwa ilipwe Sh milioni 458.1 pungufu zaidi ikilinganishwa na awali.
Kwa upande wa benki ya Stanbic, ilipendekeza kampuni ya S & Ginning Co. Ltd kufidiwa Sh bilioni 5.69, na ulipofanyika uhakiki wa pili, ikabainika kuwa kampuni hiyo ilistahili kufidiwa Sh bilioni 2.86.
Benki ya CRDB ilipendekeza kampuni ya Badugu Ginning ya Musoma, ilipwe fidia ya Sh bilioni 1.4, wakati hasara iliyopata ni ya Sh milioni 742.2. Hata hivyo, ulipofanyika ukaguzi upya kampuni hiyo ilifidiwa Sh milioni 742.2 hasara halisi iliyopata.
Kampuni nyingine ni Chesano Cotton Ginning Ltd ya Bariadi, mkoani Shinyanga, katika mchanganuo wake kwa CRDB ilijieleza kuwa gharama za uendeshaji na ununuzi wake wa pamba ni Sh bilioni 2.6 na mapato yake ni Sh bilioni 1.99 (takriban bilioni 2).
Kwa mujibu wa mchanganuo wa kampuni hiyo, mauzo iliyopata kutokana na kuuza mbegu za pamba ni Sh milioni 586 na mapato yake ya jumla ni bilioni 2.6.
Utata unaoibuka hapo ni kwamba mchanganuo unabainisha ilipata faida ya Sh milioni 6.4 lakini CRDB ilipendekeza kampuni hiyo ifidiwe Sh milioni 580. Ukaguzi zaidi ulipofanyika kampuni hiyo ilipendekezwa ilipwe fidia yoyote kutokana na kutopata hasara.
Uchunguzi pia umebaini kuwa katika orodha ya kampuni hizo, kampuni ya Gaki Investment Ltd ya Shinyanga, mchanganuo wake wa hesabu unaonyesha kuwa ilinunua kilo milioni 19.8 za pamba, ikitumia Sh bilioni 12.9, mapato yake baada ya biashara ya nyuzi za pamba ni Sh bilioni 12.15, mapato yaliyotokana na kuuza mbegu za pamba ni Sh bilioni 1.727.
Kwa kuzingatia mchanganuo huo, mapato yake ya jumla kwa msimu husika ni Sh bilioni 13.9, ikiwa imepata faida ya Sh bilioni 1. Hata hivyo, licha ya kampuni hiyo kupata faida ya Sh bilioni moja wakati huo wa mtikisiko wa uchumi, benki ya CRDB ilionyesha imepata hasara ya Sh milioni 146 na ikipendekeza ifidiwe kiasi hicho cha fedha lakini ukaguzi ulipofanyika tena, kampuni ilitakiwa isilipwe.
Kampuni nyingine ni Igunga Cotton Ltd, ambayo kwenye nyaraka inatajwa kuwa na makao yake makuu Dar es Salaam, mchanganuo wa hesabu zake CRDB ulibainisha kuwa mapato yake ni Sh bilioni 1.7 na kwamba imepata hasara ya Sh milioni 205, lakini ikipendekezwa ifidiwe Sh milioni 839 na uhakiki uliporejewa ikatakiwa ilipwe fidia ya awali Sh milioni 205.
Orodha ya kampuni hizo iliyofichwa dhidi ya CAG inataja kampuni nyingine kuwa ni Ipililo AMCOs Ltd, ambayo mchanganuo uliokuwapo CRDB ulibainisha kuwa mapato yake ya jumla ni Sh milioni 65.35 ikiwa imepata hasara ya Sh milioni 16.7, hata hivyo, katika hali ya utata zaidi, CRDB ilipendekeza kampuni hiyo ilipwe fidia ya hasara Sh bilioni 51, marejeo ya uhakiki yalipofanyika ikaamriwa ilipwe Sh milioni 16.7 tu.
Kampuni ya Jambo Oil & Ginneries Ltd ya Shinyanga, ambayo nyaraka zinaonyesha kuwa katika msimu husika (wa mtikisiko) mapato yake ya jumla yalikuwa Sh bilioni 14.9, ikipata faida ya Sh milioni 927.1, katika hali ya kushangaza, ilipendekezwa ilipwe fidia ya Sh bilioni 1.06.
Kahama Oil Mill Ltd ya Kahama, Shinyanga, mapato yake ya jumla ni Sh bilioni 17 kwa wakati huo wa mtikisiko wa uchumi, mchaganuo ukibainisha ilipata hasara ya Sh bilioni 2.3, lakini cha kushangaza ililipwa fidia ya hasara ya Sh bilioni 4.4.
Kampuni ya Kisumwa Machinery Ltd, ambayo haikuwasilisha nyaraka za mchanganuo benki katika nyaraka za kampuni zilizolipwa inaonekana kufidiwa Sh milioni 377, kama kampuni ya Canvas Mills (1998) Ltd ya Morogoro ambayo nayo haikuwasilisha mchanganuo lakini imetajwa kwamba imelipwa fidia ya Sh bilioni 1.612.
CHANZO: Raia Mwema
Mwandishi Wetu
Aprili 20, 2011
- Mabilioni yaligawanywa kama njugu kufidia hasara hewa
- Ni kampuni 27 za vigogo, imo Al-Adawi iliyovuna mil 400/-
WAKATI Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) akiripoti kunyimwa orodha ya kampuni za ununuzi pamba zilizolipwa mabilioni wakati wa mtikisiko wa uchumi duniani, Raia Mwema, inayo orodha hiyo ya kampuni zaidi ya 26, ikiwamo kampuni inayoitwa Al-Adawi Limited.
Al Adawi ni jina linalofanana na jina la mtu aliyejitambulisha kuwa ni mmiliki wa kampuni ya Dowans, akiitwa Brigedia Jenerali (mstaafu) Sulaiman Al-Adawi. Kampuni hiyo ilipendekezwa kuchotewa Sh milioni 405.6.
Mbali na Al-Adawi, katika mchanganuo wa hesabu za kampuni husika, uliopendekezwa na baadhi ya benki nchini ambazo ni CRDB, Stanbic, Exim na Kenya Commercial, moja ya kampuni imebainika kulipwa hadi bilioni 1.4, wakati hasara iliyopata ni sh milioni 742, kampuni nyingine imefidiwa hasara ya Sh milioni 500, wakati ikibainika haikupata hasara yoyote.
Katika toleo namba 129 (Aprili 14 hadi Aprili 20) mwaka jana, gazeti hili liliripoti orodha ya kampuni hizo, ambazo kabla ya kulipwa mabilioni hayo, michanganuo ya hesabu zake ili kubaini hasara walizopata kutokana na mtikisiko wa uchumi, ililazimika kurejewa baada ya michanganuo ya awali kugubikwa na taarifa za uongo.
Lakini wakati Raia Mwema likiwa limepata orodha ya kampuni hizo kutokana njia zake za uchunguzi, CAG anaeleza kunyimwa orodha hiyo na kubainisha hayo katika ripoti yake kuhusu ukaguzi wa taarifa za fedha za Serikali Kuu kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2010.
Ingawa Bunge liliidhinisha Serikali kutumbukiza Sh trilioni 1.7 kwa ajili ya kudhibiti mtikisiko wa uchumi uliotajwa kuathiri zaidi kampuni za ununuzi wa pamba, CAG anaeleza kuwa kilichotolewa na Serikali ni Sh bilioni 48 na amenyimwa orodha ya kampuni zilizopewa mabilioni hayo.
"Serikali kupitia Hazina ililipa kiasi cha Sh 48,000,270,000 katika Benki ya Tanzania kama mchango wake katika kuchochea ukuaji wa uchumi kutokana na mtikisiko wa uchumi ulioikumba dunia.
"Hata hivyo, Hazina haikutoa orodha ya makampuni au watu binafsi walionufaika na fidia hiyo au malipo ya madeni yao kuahirishwa.
"Utaratibu wa kurekodi malipo na marejesho ya fedha hizi haukuwekwa bayana na hivyo kushindwa kujiridhisha endapo yalikuwa ni malipo halali ya fedha za umma," anaeleza CAG, Ludovick Utouh.
Hotuba ya Rais Kikwete
Kutokana na mtikisiko wa uchumi duniani, ulioanzia Marekani, Rais Jakaya Kikwete alitangaza mpango wa serikali kudhibiti mtikisiko huo nchini.
Mara baada ya hotuba yake, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, aliliomba Bunge kuidhinisha Sh trilioni 1.7 kwa ajili ya kudhibiti mtikisiko hasa kwa wanunuzi wa pamba, ili kutoathiri wakulima.
Kwa wakati huo, wanunuzi wa pamba walitajwa kuathirika kutokana na bei ya zao hilo kwenye soko la dunia kuporomoka na wao kupata hasara kiasi cha kukosa fedha za kununua tena pamba kwa wakulima.
Bunge lilipitisha maombi hayo ya Waziri Mkulo, ingawa pia baadhi ya wabunge walitaka fungu hilo maalumu lililioitwa ‘stimulus package' liundiwe sheria maalumu ya Bunge ili kudhibiti matumizi yake na kuepusha nchi kutumbukia katika kile kilichotajwa kama EPA namba mbili.
Hata hivyo, haikuridhiwa kuundwa kwa sheria mahsusi, na badala yake Serikali iliahidi bungeni kuwa CAG atakagua hesabu za mgawo huo.
Benki zilizohusika na mgawo
Serikali kupitia Hazina ilitoa fedha hizo kwa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), ambayo iliweka fedha hizo katika baadhi ya benki ambazo zilipewa jukumu la kuwafidia wanunuzi husika wa pamba, baada ya kufanyika michanganuo ya hesabu na hasara walizopata.
Benki zilizohusika ni CRDB, Tanzania Investment Bank (TIB), Exim Bank, Stanbic Bank na Kenya Commercial Bank.
Kampuni na michanganuo tata
Benki ya CRDB ilifanya michanganuo ya kampuni 26 na Benki ya TIB ikipitia mchanganuo wa kampuni ya Al-Adawi pekee na kupendekeza ilipwe Sh milioni 405.6.
Benki ya Kenya Commercial, nayo pia ilipitia michanganuo ya kampuni kadhaa na kutaka zilipwe. Kampuni hizo ni Birchand Oil Mills Ltd, ambayo Kenya Commercial ilitaka kampuni hiyo ilipwe Sh bilioni 1.66.
Hata hivyo, baada ya michanganuo hiyo kurejewa na watalaamu nje ya benki hiyo ilibainika kuwa kampuni hiyo ilistahili kulipwa Sh bilioni 4.642, kukiwa na ongezeko zaidi kulinganisha na mapendekezo ya awali.
Benki ya Exim ilipendekeza kampuni ya Bio Sustain kufidiwa Sh milioni 597.7 hata hivyo, baada ya kufanyika upya kwa uhakiki kampuni hiyo ikapendekezwa ilipwe Sh milioni 458.1 pungufu zaidi ikilinganishwa na awali.
Kwa upande wa benki ya Stanbic, ilipendekeza kampuni ya S & Ginning Co. Ltd kufidiwa Sh bilioni 5.69, na ulipofanyika uhakiki wa pili, ikabainika kuwa kampuni hiyo ilistahili kufidiwa Sh bilioni 2.86.
Benki ya CRDB ilipendekeza kampuni ya Badugu Ginning ya Musoma, ilipwe fidia ya Sh bilioni 1.4, wakati hasara iliyopata ni ya Sh milioni 742.2. Hata hivyo, ulipofanyika ukaguzi upya kampuni hiyo ilifidiwa Sh milioni 742.2 hasara halisi iliyopata.
Kampuni nyingine ni Chesano Cotton Ginning Ltd ya Bariadi, mkoani Shinyanga, katika mchanganuo wake kwa CRDB ilijieleza kuwa gharama za uendeshaji na ununuzi wake wa pamba ni Sh bilioni 2.6 na mapato yake ni Sh bilioni 1.99 (takriban bilioni 2).
Kwa mujibu wa mchanganuo wa kampuni hiyo, mauzo iliyopata kutokana na kuuza mbegu za pamba ni Sh milioni 586 na mapato yake ya jumla ni bilioni 2.6.
Utata unaoibuka hapo ni kwamba mchanganuo unabainisha ilipata faida ya Sh milioni 6.4 lakini CRDB ilipendekeza kampuni hiyo ifidiwe Sh milioni 580. Ukaguzi zaidi ulipofanyika kampuni hiyo ilipendekezwa ilipwe fidia yoyote kutokana na kutopata hasara.
Uchunguzi pia umebaini kuwa katika orodha ya kampuni hizo, kampuni ya Gaki Investment Ltd ya Shinyanga, mchanganuo wake wa hesabu unaonyesha kuwa ilinunua kilo milioni 19.8 za pamba, ikitumia Sh bilioni 12.9, mapato yake baada ya biashara ya nyuzi za pamba ni Sh bilioni 12.15, mapato yaliyotokana na kuuza mbegu za pamba ni Sh bilioni 1.727.
Kwa kuzingatia mchanganuo huo, mapato yake ya jumla kwa msimu husika ni Sh bilioni 13.9, ikiwa imepata faida ya Sh bilioni 1. Hata hivyo, licha ya kampuni hiyo kupata faida ya Sh bilioni moja wakati huo wa mtikisiko wa uchumi, benki ya CRDB ilionyesha imepata hasara ya Sh milioni 146 na ikipendekeza ifidiwe kiasi hicho cha fedha lakini ukaguzi ulipofanyika tena, kampuni ilitakiwa isilipwe.
Kampuni nyingine ni Igunga Cotton Ltd, ambayo kwenye nyaraka inatajwa kuwa na makao yake makuu Dar es Salaam, mchanganuo wa hesabu zake CRDB ulibainisha kuwa mapato yake ni Sh bilioni 1.7 na kwamba imepata hasara ya Sh milioni 205, lakini ikipendekezwa ifidiwe Sh milioni 839 na uhakiki uliporejewa ikatakiwa ilipwe fidia ya awali Sh milioni 205.
Orodha ya kampuni hizo iliyofichwa dhidi ya CAG inataja kampuni nyingine kuwa ni Ipililo AMCOs Ltd, ambayo mchanganuo uliokuwapo CRDB ulibainisha kuwa mapato yake ya jumla ni Sh milioni 65.35 ikiwa imepata hasara ya Sh milioni 16.7, hata hivyo, katika hali ya utata zaidi, CRDB ilipendekeza kampuni hiyo ilipwe fidia ya hasara Sh bilioni 51, marejeo ya uhakiki yalipofanyika ikaamriwa ilipwe Sh milioni 16.7 tu.
Kampuni ya Jambo Oil & Ginneries Ltd ya Shinyanga, ambayo nyaraka zinaonyesha kuwa katika msimu husika (wa mtikisiko) mapato yake ya jumla yalikuwa Sh bilioni 14.9, ikipata faida ya Sh milioni 927.1, katika hali ya kushangaza, ilipendekezwa ilipwe fidia ya Sh bilioni 1.06.
Kahama Oil Mill Ltd ya Kahama, Shinyanga, mapato yake ya jumla ni Sh bilioni 17 kwa wakati huo wa mtikisiko wa uchumi, mchaganuo ukibainisha ilipata hasara ya Sh bilioni 2.3, lakini cha kushangaza ililipwa fidia ya hasara ya Sh bilioni 4.4.
Kampuni ya Kisumwa Machinery Ltd, ambayo haikuwasilisha nyaraka za mchanganuo benki katika nyaraka za kampuni zilizolipwa inaonekana kufidiwa Sh milioni 377, kama kampuni ya Canvas Mills (1998) Ltd ya Morogoro ambayo nayo haikuwasilisha mchanganuo lakini imetajwa kwamba imelipwa fidia ya Sh bilioni 1.612.
CHANZO: Raia Mwema