MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,562
Nimeifuma hii katika pita pita zangu kwenye masaluni. Ikanikumbusha story nyingi zifananazo kila ninapokwenda saluni inaelekea kina dada wengi kwetu hii ni hulka au sijui tunaona kawaida.
Wengi wetu tu wepesi kusimulia hadharani kama si kwa mashostito basi hata humo saluni au maofisini tunasimulia mambo yetu ya chumbani au waume wetu. Utasikia ah shost mie wangu mlevi sana bwana hadi anakera akirudi ye ni kukoroma tu hata hakumbuki ka kalala na mwanamke, au mh nimechoka leo, maana shughuli niliyopewa na shemeji yenu hata si ndogo!n.k
Kuna article moja sikumbuki ya gazeti gani ilishawahi kulizungumzia hili na kutoa angalizo kwa kina dada wenzangu wenye tabia kama hii. Nakumbuka lilisema kuwa tunapofanya hivyo tunawanadi waume zetu tunaowasifia na kuwatia mshawasha mashostito kutupa ndoano zao kwa mabwana zetu. Mara mashostisto hao wataanza kupanga mikakati ya kukupindua.
Ni mara ngapi wanawake wenzetu wanasalitiwa na wenzi wao kwa mashoga zao waliokuwa wakipiga soga na kubadilishana chanuo kwenye kusukana?
Hebu fikiria mara mbili, unawasimulia udhaifu wa mume wako, mara: Mimi mume wangu akiona paja tu basi, wazaramu wanampanda, bila kumpa staftahi hapo ujue network hazitosoma. Kesho, shoga yako akikuta bar atamkaribisha shemejiye na kumfunulia paja hiyo ni kumdatisha, si umeshamuambia kuwa wazimu wake upo kwenye mapaja?
Habari hii imenifanya nijiulize kama wanaume nao huwa wanazo tabia kama hizi, hivi huwa wanatusema kwa marafiki zao? Au wao mazungumzo yao ni tofauti?
Wengi wetu tu wepesi kusimulia hadharani kama si kwa mashostito basi hata humo saluni au maofisini tunasimulia mambo yetu ya chumbani au waume wetu. Utasikia ah shost mie wangu mlevi sana bwana hadi anakera akirudi ye ni kukoroma tu hata hakumbuki ka kalala na mwanamke, au mh nimechoka leo, maana shughuli niliyopewa na shemeji yenu hata si ndogo!n.k
Kuna article moja sikumbuki ya gazeti gani ilishawahi kulizungumzia hili na kutoa angalizo kwa kina dada wenzangu wenye tabia kama hii. Nakumbuka lilisema kuwa tunapofanya hivyo tunawanadi waume zetu tunaowasifia na kuwatia mshawasha mashostito kutupa ndoano zao kwa mabwana zetu. Mara mashostisto hao wataanza kupanga mikakati ya kukupindua.
Ni mara ngapi wanawake wenzetu wanasalitiwa na wenzi wao kwa mashoga zao waliokuwa wakipiga soga na kubadilishana chanuo kwenye kusukana?
Hebu fikiria mara mbili, unawasimulia udhaifu wa mume wako, mara: Mimi mume wangu akiona paja tu basi, wazaramu wanampanda, bila kumpa staftahi hapo ujue network hazitosoma. Kesho, shoga yako akikuta bar atamkaribisha shemejiye na kumfunulia paja hiyo ni kumdatisha, si umeshamuambia kuwa wazimu wake upo kwenye mapaja?
Habari hii imenifanya nijiulize kama wanaume nao huwa wanazo tabia kama hizi, hivi huwa wanatusema kwa marafiki zao? Au wao mazungumzo yao ni tofauti?