Siri ya Nguvu ya CCM

Twawezaje kupona na ghiliba za CCM

  • Kutoa elimu kwa wingi zaidi

    Votes: 6 60.0%
  • Kupiga kampeni dhdi yake nchini kote

    Votes: 1 10.0%
  • Kuibua maovu yake mengi zaidi

    Votes: 1 10.0%
  • Kuimarisha mbinu za wapinzani

    Votes: 2 20.0%

  • Total voters
    10

Kamende

JF-Expert Member
Mar 1, 2008
416
45
Amani iwe nanyi wapendwa mnaotembelea jukwaa hili tukufu.

Nimechagua kuanzisha mjadala juu ya nguvu ya CCM kutokana na jinsi ambavyo kwa sasa wanayatumia mamlaka waliyo nayo kuchezea mustakabali wa nchi. Imekwisha kuwa bayana sasa kwamba uwepo na ukubwa wa mafisadi unatokana na ukubwa wa chumba walichowekewa na CCM. Iko bayana pia kuwa ukubwa wa rushwa hapa Tanzania unatokana na namna CCM inavyoenenda na kuendeshwa. Kwa hiyo ni muhimu kabisa kujadili nguvu yake inakotoka ili kuinusuru nchi yetu na makucha ya uovu huu unaowatesa sana wananchi wetu.

Katika Biblia yuko Mtu mmoja alijulikana kama Samson. Mtu huyu alikuwa na nguvu nyingi sana. aliheshimiwa kama mnadhiri wa Mungu. ( Mtu mwenye siri/nadhiri na Mungu) Samson alifanya maajabu mengi.
Akiwa askari wa jeshi la Israel Samson alitumia mfupa wa taya la bweha kuwaua askari 1000 wenye silaha. Samson alimrarua Simba vipande vipande kuanzia mdomoni, Samson alienda msituni akakamata bweha 300 akawafunga wawili wawili na kuweka kidakwa cha moto kwenye mikia yao wakapita katika mashamba ya wafilisti wakayachoma moto yote. Samson alikutwa kwa kahaba mmoja huko Gaza, askari wa kifilisti wakafunga lango la kuingia mjini ili wamsubiri hadi asubuhi wamuue. Usiku wa manane Samson akaamka akaling'oa lango la jiji na miimo yake na komeo lake akavibeba kutoka Gaza hadi mlima unaoelekea Habron. Hapo ni kama umbali wa Ubungo na Chalinze na lango alilolibeba lapata uzito wa tani 4 hivi.

Kwa ajili ya hoja yangu kwa CCM nije kwenye siri ya nguvu za Samson. Kijana huyu Shujaa wa ajabu alimpenda binti mmoja mzuri sana wa Kifilisti aitwaye Delila. Wafilisti walimtumia Delila kuchunguza siri ya nguvu za Samson. Ndipo Samson alipotoboa siri ya nguvu zake kuwa ni nywele zake. Mungu alimwekea Samson nguvu nyingi kwenye nywele zake. Kwa nadhiri kati ya Mungu na Samson, Samson hakutakiwa kunyoa nywele zake.
Zikinyolewa tu: Kwisha kazi yake Samson.

CCM!!
Nguvu yake iko wapi?

CCM!!!:- chama pekee ambacho kina Ofisi kubwa (complex) ya makao makuu. mikoa yote ya Tanzania, kina maofisi wilaya zote, kata zote na vijiji na mitaa mingi sana Tanzania na kila ofisi ina watendaji wanaolipwa mishahara. Ni chama chenye vitegauchumi vingi sana; vikiwepo viwanja vya michezo, viwanja vya kuegeshea magari, maofisi, nk.
CCM ni chama kinachoshindaga chaguzi zote za urais toka mfumo wa vyama vingi uanzishwe nchini. Kimekuwa kikipata idadi kubwa ya wabunge kila uchaguzi. Kimefanikiwa kupata mapenzi ya wafanyabiashara wengi, wasomi wengi, na wanachuo pia. CCM inakisiwa kuwa na wanachama wasiopungua 4,000,000.

Kama mchambuzi wa siasa ni hatari kuacha mambo kana kwamba yanatokea tu yenyewe. Lazima kila jambo linalotokea lichunguzwe limetokea wapi.
Hebu tuangalie kwa kiasi chanzo cha nguvu za CCM na pengine kwa kufanya hivyo tuweze kusaidia kupatikana kwa jibu kwa nini Vyama vya Upinzani havijaweza kuiadabisha CCM.

Nguvu ya CCM ya kwanza inatokana na Uozo ulioko kwenye katiba ya nchi yetu. Katika katiba ya nchi yetu kuna vipengele vingi vinavyokinzana. Kifungu kimoja kinatoa haki na kingine kinapora hiyo haki.

Nguvu ya pili ya CCM inatokana na dharau yake kwa maelekezo ya tume ya Jaji Nyalali wakati tukiingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa. katika mchakato wa kuingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa Tume ya Jaji Nyalali ilitoka na ushauri kuwa mali/vitega uchumi vyote ambavyo CCM ilipata kabla ya kuundwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa viondolewe kwenye miliki ya chama na kumilikishwa serikalini. Lakini CCM ilifanikiwa kuwalazimisha watanzania waingie kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa bila ushauri huu kutekelezwa na hivyo kubakia kuwa chama giant mbele ya vyama vingine vya siasa.

Nguvu ya Tatu ya CCM iko kwenye kukosa kwake aibu kutumia dola kujiimarisha. CCM imekuwa ikitumia Mamlaka ya Mapato na jeshi la Polisi kupambana na wafanyabiashara wanaoonyesha kushabikia upinzani na kuwawekea kuinga wale wanaoidhamini CCM.

Nguvu ya nne inatokana na watanzania kutojua haki zao za kiraia. Watanzania wengi hawajua haki zao. Hawajui wajibu wao, majukumu yao wala hawajui mamlaka walizo nazo. Hii inainclude hata wasomi wetu wengi. Watu hawa wasiojua haki na wajibu wao wanatawalika kirahisi sana na kijinga tu. Wakipewa haki yao fulani wanafikiri wapewa fadhila.

Nguvu ya Tano ya CCM inatokana na umasikini wa Tanzania na watanzania. CCM imemasikinisha wananchi. Hawa masikini hawawezi kufurukuta wakati wa uchaguzi kwani wanapewa bakhshishi kidogo tu wanatoa ridhaa ya kutawaliwa tena. Sera mbaya za CCM na utekelezaji wake mbaya umewapa nafasi waporaji wa rasilimali za nchi kuunyonya uchumi wa nchi na kuwaacha wanachi hoi kwa umasikini. Masikini hana nguvu ya kudai haki zake: Anaweza tu kuomba chakula cha siku!

Nguvu ya Sita ya CCM iko kwenye Ndoa baina yake na wafanyabiashara wasio waadilifu. Wafanyabiashara wasiopenda kufuata taratibu takatifu za biashara wanabebwa na CCM kwa masharti ya kufandhili shughuli za chama na kuwafadhili viongozi wa chama. Wengi wa wafanyabiashara hawa ni wale wenye asili ya kiasia.

Nguvu ya saba ya CCM iko kwenye tamaa ya kila mtu kutaka kupata fursa kwa njia ya mkato. Wasomi wengi wanataka kupewa madaraka kirahisi, hawataki kuyasotea, wazazi kadhaa wanataka watoto wao wasomeshwe kirahisi kwa kupata upendeleo bila ya wao (watoto) kutunisha musuli. wafanyakazi kadhaa wanataka promotion za upendeleo: watu hawa wote hawana njia nyingine zaidi ya kujiunga na CCM.

Nguvu ya nane ya CCM iko kwenye matumizi mabaya ya dhana ya AMANI tuliyo nayo nchini na namna tunavyotunza amani za majirani zetu. CCM imekuwa ikiwarubuni kwa mafanikio makubwa wananchi kuwa yenyewe ndiyo inayolea amani ya nchi. watanzania hawajaweza kuona kuwa amani tuliyo nayo ina mushkeli. wanafikiri kuwa tuna siasa nzuri sana. hawajui kuwa wenzetu wanaopigana walikuwaga na siasa nzuri kuliko sisi hapo kabla ya kufikia kupigana. Neno amani limewapumbaza watanzania wengi. Wanaogopa hata kudai haki ya kawaida tu wakihofia kuwa kwa kufanya hivyo watasababisha amani kuvunjika.

CCM imefanikiwa kufunikiza watanzania katika jungu la ujinga kwa muda mrefu sasa.

Nimeandika hapa ili kuwaamsha wenye akili na wanamikakati wote kufanya kila linalowezekana kupambana na ghiliba za CCM vinginevyo watatawala milele. Hofu yangu si tu kule CCM kutawala millele, ila ni kwa kuwa nina uhakika kuwa CCM haiwezi kuachana na mafisadi. CCM imewekeza nguvu zake katika uovu kwa hiyo haiwezi kupambana na uovu.

Hii ndiyo sababu naichukia CCM

KIGUMU CHAMA CHA MAFISADI!!!

Ulingo uko wazi .........
 
Nguvu ya CCM ya kwanza inatokana na [COLOR="DarkRed"[SIZE="4"]]Uozo ulioko kwenye katiba ya nchi yetu[/SIZE][/COLOR].

Nguvu ya pili ya CCM inatokana na dharau yake kwa maelekezo ya tume ya Jaji Nyalali

Nguvu ya Tatu ya CCM iko kwenye kukosa kwake aibu kutumia dola kujiimarisha.

nguvu ya nne inatokana na watanzania kutojua haki zao za kiraia.

Nguvu ya Tano ya CCM inatokana na umasikini wa Tanzania na watanzania.

Nguvu ya Sita ya CCM iko kwenye Ndoa baina yake na wafanyabiashara wasio waadilifu.

Nguvu ya saba ya CCM iko kwenye tamaa ya kila mtu kutaka kupata fursa kwa njia ya mkato.

Nguvu ya nane ya CCM iko kwenye matumizi mabaya ya dhana ya AMANI

Katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania ilitengenezwa wakati wa mazingira ya chama kimoja na kwa wakati huo ilikuwa inafaa kabisa na maanawatu wamekuwa wakiomba katiba mpya kila siku, lakini serikali ya CCM haitaweza hata siku moja kuruhusu katiba mpya kwani huo ndo utakuwa mwisho wa CCM na serikali yake, katiba imepitwa na wakati imejaa viraka sana kiasi cha kutokarabatiwa kwani ukikarabati hapa panafukmuka kwingine, mapambano ya kweli ya katiba mpya yanahitajika ili kuwepo mazingira yanayo kwenda na mfumo wa vyama vingi na hali ya uchumi ulimwenguni.

Walijua kabisa vile vitega uchumi vikirudishwa serikalini chama kitakufa ndo maana walivingangania, hivi vitu vilijengwa na wananchi wa tanzania bila kujali itikadi yao, kwahiyo mpaka sasa CCM ni wezi wa mali za watanzania wakajigawia mali za watanzania ili wapate base ya kuendelea kuwanyonya.Kama tunataka haki ya kweli lazima kwanza tudai mali za watanzania zilizoibiwa na CCM.

CCM wanatumia nguvu zote wakiwemo polisi wanaolipwa posho ya sh. 1000 wakienda kwenye operation maharumu kuwanyanyasa wapinzania mfano ni uchaguzi mdogo wa babati ambako polisi waliwapiga wagombea wa upinzania na wapambe wao huku komba akifanya fujo bila kuchukuliwa hatua. Hawa polisi wanahitaji kuelimishwa kidogo kwani wanapata shida kuwalinda mafisadi wakati wao hawana kitu, ndio maana wanaamua kufanya kazi na majambazi ili wapate chochote.

Watanzania sio masikini isipokuwa CCM wamewabatiza hivyo ili waendelee kuwanyonya, wamewateka kisaikolojia na kuakikisha kila mtu anatamani pesa hata kama anapewa sh. 5000 kuuza haki yake kwa miaka 5 haoni tabu kwani wamewaandaa kisaikolojia kuwa hivyo, watu watamani pesa kuliko maendelea.

Mwanzo wa mwisho wa CCM unaonekana sasa kwani kwa kufunga ndoa na wafanyabiashara matokeo yake ni kama tunavyoona sasa EPA, RD na mengine mengi ambayo yatawafumbua wananchi kuwa wanaibiwa sana halafu wanaongwa ili waendelee kuwaweka madarakani.

Hakuna amani kama hakuna haki na ndo maana amani wanayosema sasa inapotea kama theruji ya mlima kilimanjaro, watu wameanza kutambua kuwa amani bila haki haiwezekani.
 
Hakuna ufisadi hawa ni watu ambao wameapa kuiongoza nchi hivyo baadhi ya mitihani inawakumba na wanafeli ,mimi naona CCM ndio chama ambacho kwa sasa hakina mbadala ,utaona kuna vyama vingi vya upinzani lakini vinonekana havina muelekeo na kwa kweli kwa hali inavyoenda huenda vikageuka vyama vya mipasho ,na siku ya mikutano yao utaona watu wengu tu wanaenda kusikiliza habari nyeti ambazi hazijaandikwa na magazeti na pengine walirudi utaona waliokwenda huko wakirudi na furaha huku wakicheka njia nzima kwani ni kutokana na vichekesho vilivyokuwa vikiigizwa na wasemaji waliobahatika kuhutubia.
ukiangalia kuna mafisadi kwa upande wa watawala lakini vilevile ukitazama upande wa pili wa shilingi utaona hivi vyama vya upinzani hutegemea ruzuku kutoka serikalini hawana miradi ya aina yeyote ,siku serikali ikisema imefilisika na hivi vyama ndio mwisho wake sasa hii ruzuku wanayopewa ni kuharibu fedha za walala hoi bila ya kazi aidha naweza kusema ni vyama hewa ambavyo vinatumika kuibabaisha jamii.
CCM kama chama cha siasa na Chama tawala ni watawala wa nchi vile vile ni watawala wa vyama vingine huo ndio ukweli.
CCM Inaweza kuwatoa wanachama wake ikawapeleka vyama vingine na wakapata ukubwa na kisha ikawarejesha.
CCM inaweza kutumia vyombo vya dola ikafanya inavyotaka na kuzima juhudi zozote za vyama vya upinzani na hakuna wa kuwashitaki.
CCM ina uwezo wa kuamrisha nini kiandikwe kwenye gazeti na nini kisiandikwe.
CCM imeshutumiwa kwa mambo kadhaa wa kadhaa na yote yamekuwa na kufifia kama uyoga .Hakuna wa kuweza kuwanyooshea mkono.
CCM haiwakatazi viongozi wa upinzani kujitutumua kwenye majukwaa huwaacha wakasema wakatukana wanajua mwisho wao usiku watalala na kukoroma.
CCM imekuja na sera mpya ya kuwaacha wafuasi wanaodai kufanya maandamano wafanye watavyo saa na wakati wowote na pia kuwahahakikishia ulinzi mwanzo mpaka mwisho baada ya kung'amua vyama hivyo vikitumia ile sera ya zamani ya kuzuia maandamano kuwapaka matope kwa wateja wao na kuwatilia mchanga kitumbua japo wanakula hivyo hivyo.
CCM wanauwezo kwa kutumia vijana wake kupiga na kuharibu kikao chochote kile cha chama cha upinzani pasipo kuingiliwa kati na polisi au mtu yeyote.
Mbali ya matatizo yote CCM imeonyesha kuiendesha nchi bila ya kuyumba kutokana na makelele ya hapa na pale.
CCM ni chama ambacho hela inazungumza na kuweza kupita njia ya mkato unapokuwa na matatizo ambayo yatahitaji mlolongo hadi ufanikiwe.
Hivyo kupata Chama mbadala zaidi ya CCM ni kutafuta matatizo makubwa ndani ya nchi.
 
Siri ya nguvu ya chama cha ufisadi (deep green) ni ufisadi, tukiweza kuzuia ufisadi wao basi chama kimekwisha.
 
Yakhe yamekuwa hayo? Vipi chama chako cha CUF na haya maandishi yako?
Niliposema Si mpenzi wa Chama chochote ulifikiri natania,hapa hatembei mtu miguu chini ,ukweli utabakia kuwa ukweli tu ,na sioni sababu ya kujibarizi katika au kutetea chama fulani ,nitasema vile ambavyo naona ndivyo inayoelekea.
Hizo poiti nimemega si unaziona ,zinajieleza wenyewe ni ukweli usioyumba ,CCM ni chama ambacho wanaojaribu kukiharibu wanaweza kushughulikiwa kwa marefu na mapana.Na ndio maana ya chama tawala ,unajua watu wengine akili zao zinawafahamisha vibaya na wao kufika kuziamini ,hivi inaposemwa CCM ni Chama Tawala msemo ambao hata hawa wapinzani wanautumia sana kukiwakilisha Chama Cha Mapinduzi ,msifikirie ni Chama tawala kwa kuwa kipo kwa kuongoza Serikali kwa Miaka nenda miaka rudi bali ni watawala wa kila nyanja hawana wasipopaweza kwa upole au kwa vita ni majemadari waliobobea katika kutekeleza utawala wao.
Upinzani kwa upande wangu naona kama ni makachero wa CCM na hivyo kuifanya CCM ifaidike na makelele yao.
Makelele ya mlango hayamtishi mwenye Nyumba .hapo fahamu kuwa milango ni vyama vya upinzani Mwenye Nyumba ni CCM ,hivyo milango hii huwa inafanyiwa ukarabati na kutoa sauti nzuri tu ,si umeona bawaba ya Chadema "Zitto Kabwe" kavutwa ukosi kawekwa kwenye kamati .."Cheyo sijui kawekwa kwenye kamati ya kushughulikia kamradi fulani "..Hamad Rashid huyu aliwekwa kwenye kamati ya kushughulikia na kuchunguza hesabu za madini na kampuni za kiingereza kama sikosei.
Hiyo ndio CCM mambo yake yanakwenda kutokana na mazingira yalivyo kama hapa tulipo utaona kuna haya makelele ya mafisadi na ukiangalia kwa mbali yameanza kuwa under control ,only time will tell us mafanikio yake ya kumalizika wakati utakapowadia na kila mtu atakuwa na hamsini zake wakati milango ikianza kuchakaa na kutoa sauti zingine.
 
Tatizo sio CCM, tatizo na tabia ya walio wengi kutokujali yanayojili kwenye utawala au uongozi wa nchi mpaka wasikie kuna scandal imeandikwa kwenye gazeti.

Matokeo yake wanakuwa rahisi kudanganyika.
 
Nguvu ya CCM inatokana na ujinga na uoga wa wananchi wa Tanzania.
Ujinga na uoga wa kutojua haki zetu za Kikatiba kama wananchi.
Ujinga na uoga wa kuzidai na kuzidhibiti haki zetu hata pale tunapozijua.
Tu wagumu wa kuelewa na wepesi wa kusahau tunapoelewa.

"If you cannot blow up your trumpet, nobody else will blow it up for you."
PERIOD. Wake up Tanzania CCM ina wenyewe na hao wenyewe sio mimi na wewe!

Tuna macho, lakini hatuoni na tuna masikio, lakini hatusikii. Ole wetu!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom