Elections 2010 Siri ya Mshahara wa Rais na Marupurupu ya Rais Wastaafu...

Kwa utajiri tulionao ,hiyo mishahara na posho ni vijisenti tudogo tu, sema kitu kimoja ambacho sisi hatukielewi ni mapato ya serikali hizi za CCM ,tunayoona pale bungeni ni mapato hewa mapato halisi hayaonyweshi ndio maana ukaona wanajipangia mishahara na marupurupu minono wakijua kuwa haitahatarisha kitu, maana kama feza ingekuwa haitoshi mahesabu yao yasingekubaliana na wangeambizana kuwa tukifanya hivi mahesabu ya bajeti yatakwenda upande ,ila uhakika walionao kwa fedha inayopata Tanzania basi ni wazi kabisa kuwa wanajua wanalolifanya na jinsi ya viongozi tulionao ambao wapo kwa faida ya maslahi binafsi hilo kwao si jambo kubwa ,Tanzania Fedha ipo tena nyingi sana lakini inaliwa kijanja na kuchukuliwa na wachache.Fikiria tu marupurupu hayo yote na mshahara anaolipwa raisi vipi ataweza kuwajibika katika mambo muhimu na kuyafuatilia wakati hana wasiwasi wa kuathirika ,kifedha ,kuna ule msemo unaosema mwisho wa mwezi ananyoosha mkono tu na kupokea mshahara wake ,sasa nyinyi mkilima msilime hayamuathiri kabisa ,mkilala kiza au na taa yeye hata habari hapati ,mkikatana viungo mkiuwana ili kuibiana yeye amekaa mguu juu,malizaneni hukohuko ,mradi mwisho wa mwezi jambo la muhimu fedha yake anahamishia nje.Maana BOT haziwekeki zinaweza kuchotwa na wajanja wa makampuni hewa.
 

Asalaam Aleykum,

Rais wetu mpendwa jana amekataa pendekezo la wafanyakazi kwa serikali kuongeza kima cha chini kifike kuwa 315,000/- ($225 only!). Swali langu kwa wana JF mliopo utumishi wa umma, mabenki na kwengineko ambao mnafahamu mishahara halisi serikalini, je viongozi wakuu wa nchi wafuatayo wanalipwa mshahara kiasi gani:

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

2. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

3. Rais wa Zanzibar

4. Waziri Mkuu

5. Katibu Mkuu Kiongozi

6. Mawaziri

7. Manaibu waziri

8. Makatibu Wakuu

9. Wakuu wa Mikoa

10. Wakuu wa Wilaya


Nadhani tukipata mishahara ya wakuu hawa tunaweza kufanya ulinganishi (comparison) nzuri na kima cha chini cha sasa cha 104,000/- ($75 only!) na mapendekezo ya TUCTA ya kima cha chini cha 315,000/- ($225 only!).


  • ANGALIZO: Kwenye mwaka huu wa fedha, serikali imeongeza fungu la posho za vigogo wanaosafiri kila kucha kufikia SHILINGI 216 BILIONI kutoka shilingi 171 billioni za mwaka wa fedha uliopita. Hili ni ongezeko la SHILINGI 45 BILIONI. Je, fedha hizi zisingetosha kuongeza kima cha chini kifikie 315,000/-.
Wana JF naombeni mchango wenu. Au mshahara wa Rais ni SIRI ya taifa (national secret)?
 
Mwinyi aliwahi kutaja mshahara wake just about when he was about kustaafu na ilikuwa 412,000/=
 

Asalaam Aleykum,

Rais wetu mpendwa jana amekataa pendekezo la wafanyakazi kwa serikali kuongeza kima cha chini kifike kuwa 315,000/- ($225 only!). Swali langu kwa wana JF mliopo utumishi wa umma, mabenki na kwengineko ambao mnafahamu mishahara halisi serikalini, je viongozi wakuu wa nchi wafuatayo wanalipwa mshahara kiasi gani:

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

2. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

3. Rais wa Zanzibar

4. Waziri Mkuu

5. Katibu Mkuu Kiongozi

6. Mawaziri

7. Manaibu waziri

8. Makatibu Wakuu

9. Wakuu wa Mikoa

10. Wakuu wa Wilaya


Nadhani tukipata mishahara ya wakuu hawa tunaweza kufanya ulinganishi (comparison) nzuri na kima cha chini cha sasa cha 104,000/- ($75 only!) na mapendekezo ya TUCTA ya kima cha chini cha 315,000/- ($225 only!).



  • ANGALIZO: Kwenye mwaka huu wa fedha, serikali imeongeza fungu la posho za vigogo wanaosafiri kila kucha kufikia SHILINGI 216 BILIONI kutoka shilingi 171 billioni za mwaka wa fedha uliopita. Hili ni ongezeko la SHILINGI 45 BILIONI. Je, fedha hizi zisingetosha kuongeza kima cha chini kifikie 315,000/-.

Wana JF naombeni mchango wenu. Au mshahara wa Rais ni SIRI ya taifa (national secret)?

hivi hatuwezi kupata scanned copy ya salary slip yake?
 
Mtu anajisifu kaongeza Mshahara toka 65,000 hadi 104,000. Hivi kweli unadiriki kujisifia mshahara wa namna hiyo!!!
Siamini.
 
Uliza Kitilya analipwa shilingi ngapi and then think of JK


Haina mjadala kuwa wakuu wa executive government agencies kama Bank of Tanzania, Tanzania Revenue Authority, Tanzania Investment Bank, TANROADS, NSSF, PPF na kwingineko huwa wanalipwa mshahara mkubwa kuliko viongozi wa serikali kuu so tuwatoe kwenye equation. Ni muhimu kujua hao viongozi wakuu waliotajwa ambao ndiyo wanashuhulikia matatizo ya wafanyakazi wanalipwa mishahara kiasi gani haswa.
 
Hii nchi inaendeshwe kisenge senge sana. Yaani mpaka leo hatujui mshahara wa raisi ni kiasi gani. Huu mshahara si unatokana na kodi za wananchi au?
 
Ndiyo maana watu wengine tunakuwa wagumu kuamini kama kweli hawa wanadhamira ya kweli.

Hii inaonesha rais na serikali yake wameridhika na kulewa madaraka tuliyo wapa,nadhani kwakuwa wanajua wataiba kura,then watashinda na kuingia madarkani tena (inawezekana)......Lakini I alwayz believe in changes, kunasiku mabadiliko yatatokea. Nadhani hi ni fulsa nzuri kwa wafanyakazi na wananchi wote kuelewa kuwa tunaongozwa na watu wenye dhamira tofauti na kile wanacho kihubiri majukwaani....Fareed ameuliza swali zuri sana...We always think our sides and not third parties...Sawa nchi hii ni yetu sote,lakini wa fanyakazi wanapewa wasicho sitahili.

USHAURI:Kwa hili hauhitaji kuwa na digrii kufanya maamuzi,watanzania jaribuni kuungana kwa pamoja Wafanyakazi,wakulima,machinga,ba_made,house girls,house boys na kila mtu aliye jiandikisha kupiga kura achague chama tofauti na cha kikwete tuone atapata wapi kura......Cha ajabu hakuna hata kundi moja linalo muunga mkono kwa maamuzi na vitisho vyake...maana yake ni kuwa kila mwananchi yupo upande wa Wafanyakazi......

"IPO SIKU WAFANYAKAZI MTASHINDA"
 
Huyu rais sasa anaonyesha rangi yake halisi; sio mtu wa watu kama wananchi wengi walivyodanganyika. Huyu ni mtu wa mafisadi na ndio maana hawezi kuwakemea. Badala yake anataka kugombana na wafanyakazi ambao ndio waliompa ajira. Nadhani amelewa madaraka huyu. Lakini kwa upande mwingine imetusaidia kwani kuropoka kwake kutamfanya awe rais wa muhula mmoja tu kwani ataambulia kura chache tu za wale waliokuwa wanamshangilia siku ile pale Diamond.
 
Niliwahi kusikia Rais analipwa shilingi milioni 9 za kitanzania ..Niliambiwa kuwa The G 3 yaani Rais,Makamu wake na PM wanapishana kwa shilingi milioni mbili..

N.B Sina hakika katika hili.Chanzo hakiaminiki.
 
Huyu rais sasa anaonyesha rangi yake halisi; sio mtu wa watu kama wananchi wengi walivyodanganyika. Huyu ni mtu wa mafisadi na ndio maana hawezi kuwakemea. Badala yake anataka kugombana na wafanyakazi ambao ndio waliompa ajira. Nadhani amelewa madaraka huyu. Lakini kwa upande mwingine imetusaidia kwani kuropoka kwake kutamfanya awe rais wa muhula mmoja tu kwani ataambulia kura chache tu za wale waliokuwa wanamshangilia siku ile pale Diamond.
Fanyeni kweli maanake naona watu wanaogopa kugombea kiti cha Urais..Utabiri uliopangwa na Mkwere kupitia Sheikh Yahya umewakimbiza wengi.
 
Hawa jamaa wanalipwa mishahara mikubwa, wanapewa nyumba full furnished (samani zinabadilishwa kila mwaka) bure, wanalipwa posho ya chakula milo yote (asubuhi, jioni na usiku) kila siku kwa familia yake yote. Anaousafiri limos, ulinzi kila mahali nk. Anaposho ya kazi kila siku, anasafari 2/3 ya mwezi za nje na ndani. Anapoenda nje ya nchi analipwa outfit allowance (pamba nyepesi) perdiem za nguvu. Kwa hiyo hata huo mshahara wake hauna matumizi.
 
Na tujue pia zaidi ya mshahara wake ana malupulupu mengi. Hivi waliokuwa wakimshangilia rais wakati wa hotuba wanakaa nchi gani? Inaweza kuwa mbali sana na Tanzania!

Niliwahi kusikia Rais analipwa shilingi milioni 9 za kitanzania ..Niliambiwa kuwa The G 3 yaani Rais,Makamu wake na PM wanapishana kwa shilingi milioni mbili..

N.B Sina hakika katika hili.Chanzo hakiaminiki.
 
Hawa jamaa wanalipwa mishahara mikubwa, wanapewa nyumba full furnished (samani zinabadilishwa kila mwaka) bure, wanalipwa posho ya chakula milo yote (asubuhi, jioni na usiku) kila siku kwa familia yake yote. Anaousafiri limos, ulinzi kila mahali nk. Anaposho ya kazi kila siku, anasafari 2/3 ya mwezi za nje na ndani. Anapoenda nje ya nchi analipwa outfit allowance (pamba nyepesi) perdiem za nguvu. Kwa hiyo hata huo mshahara wake hauna matumizi.

Huu ndo ukweli mkuu.

Jamaa wanaweza kuwa na mishahara ya kawaida sana lakini mishahara yao haina kazi maana kila kitu kinagharamiwa na serikali in the name of posho. Na marais na mawaziri wakuu wastaafu wanagharimiwa kila kitu pia hata wakitoka madarakani mpaka mwisho wa kuishi kwao chini ya jua.

Kwahiyo mawaziri wakuu na marais wanapokuwa wezi wa mali ya umma wawapo madarakani ni ubinafsi na uroho uliopindukia kwani ana uhakika wa kuishi maisha ya kifahari kwa kodi zetu mpaka mwisho wa maisha yake duniani.
 
Back
Top Bottom