Siri ya Mahakama ya Kadhi yafichuka

Nadhani hujanielewa kabisa na kwa hili la mahakama ya kadhi huta nielewa kama utasimamia misimamo ya dini yako dhidi ya dini nyingine.

Mwaka 2005 Waislam waliahidiwa kupewa mahakama ya kadhi kwa kutumia ilani iliyowekwa na awamu ya 3 iliyokua inaongozwa na Rais mkristo tena wa kanisa katoliki na waziri mkuu akiwa kanisa la kiluteri.Na makada wengi wakiwa ni maaskofu wa makanisa hayo ambao walimwita kikwete na CCM kuwa ni chaguo la mungu .Sijui huyo mungu hakuona mbali au ilikuaje!!!Leo hii maaskofu hao hao wanapinga ilani ya chama chao na mungu wao.!!Unafiki ndio stahiki yao kuitwa!!

Kuhusu kuogopwa kwa waislam nadhani sio hoja yangu.
Hoja yangu ni misingi ya kuimarisha amani.
Hatuwezi kutumia CCM kuwafanya waislam kuwa sehemu ya kupata kura tu halafu wanapodai kutekelezwa kwa ilani na ahadi iliyotolewa iwe ni kuwaogopa.
Hili suala limekua ni sababu tu ya CCM kujipatia kura na kuwagawa watanzania kwa kuwadanganya waislam kuwa chama chao kimeshaanza mchakato wa mahakama ya kadhi hiyo wakichagu chama kingine basi wajue huo mchakato utakwisha.
Leo hii kanisa ndio limekuwa adui wa mahakama ya kadhi.
Na watu badala ya kuibana serikali ili ilete maendelea kwa watu wake na kuongeza fursa za ajira zikiwemo kuanzisha mahakama ya kadhi wao wanaweka mapingamizi ya mahakama ya kadhi.
Kwa waislam wameona hiyo ndio fursa kwao yamaendeleo!!!Mnashangaa nini sasa!!
Wakristo nasema pelekeni mswada bungeni wa kupatiwa ruzuku za kuwalipa mapadri na wachungaji mishahara kwani wanatoa huduma za kijamii na kuhamasisha upendo na Amani!!
Hapa napo hujanielewa.

Kaka 1000 digits nimekuelewa sana, kama ni CCm ndo wamekuwa wakiwa ahidi na kuwa hadaa waisilamu kwa muda wote huo, basi mahakama ya kadhi iwekwe kwenye katiba ya CCM na si katika ya nchi ya Tanzania, hatuwezi tukakubali kila upumbavu wa CCM ukawagharimu Watanzania wote, CCM na viongozi wake wote waliopita na waliopo wanatakiwa kujibu hili kwa waisilamu. It has nothing to do with Tanzania as a nation.

"You can fool some people some times but you cant fool all the people all the time" Mwaka 2005( kutokana na maelezo yako). Waisilamu walidanganywa na wakakubali kuiweka serikali ya CCM madarakani, mwaka 2010, wakakubali tena wakarudia makosa, na sasa bado tunawaona wengi tu wakiunga mkono CCM iliyo wadanganya na wengi wako teyari kuipigia kura CCM tena mwaka huu.

Kwanini wewe uwaonee huruma watu wasio jionea huruma, watanzania lazima tukubali kuteseka kwaajili ya shingo zetu ngumu kwa kukubali wenyewe kuiweka CCM madarakani mwaka 2010, na kama kunaupumbavu wa maisha na wahistoria ambao watanzanzania wataufanya ni kuirudisha CCM madarakani tena mwaka huu 2015. Itakuwa ni kilio na kusaga meno.
 
Na mnaolipa kodi ni nyinyi tu? kwanza nyinyi ndiyo wezi wakubwa Serikalini, mmejazana huko miaka na miaka mnaididimiza tu nchi. Huyaoni?

mkuu FF,eti ni kweli kuwa mwanamke wa kiislamu akiwa hedhini hatakiwi kuhudumia (kama madaktari,manesi,mahakimu,walimu etc)?
 
Kwa kweli mi naona hapa busara itumike,maana nchi hii inakaliwa na watu wote,wenye dini na wasio na dini
kama mahakama hii itapitishwa,ikitokea wenye dini tofauti wakatofautiana ktk jambo fulani
ni sheria ipi au ya mahakama gani itatumika kuwasuluhishi endapo sheria za mahakama hizo mbili
zitakuwa zinakinzana?
Na huo ndo utakuwa mwanzo wa machafuko.ni vyema mambo ya dini yabaki kwa waumini wa dini husika
kwao ni rahisi kuwapatanisha maana watakuwa na imani moja na kiongozi wao ni mmoja.
 
Kuna ile adhabu ya viboko na kufukia mzinifu kwenye shimo na kumpiga mawe hadi kifo itaanzishwa na kadhi au?
 
Mimi siamini katika hiyo mahakama ya kadhi .....ni Utoto , upumbavu na kupoteza mda. Sio waislamu wote tunao itaka hiyo na wengi wanashabikia tu bila kuelewa vizuri ila badae mtajutia.
 
Ha ha ha! ccm ni wajanja sana. Yaani hii issue ya mahakama ya kadhi wanajua wakiikomalia itawapasua hata hao Ukawa. Ndio karata ya mwisho wanataka kuitupa.

Namuomba rais, kama alivyokataa kuitambua Tanganyika kwa kisingizio cha kutotaka kuvunja muungano wa watanzania, vivyo hivyo aachane na mpango wa kupitisha muswada huu!
 
mbona mkataba wa MOU unawapa fursa wakristo kupewa pesa kuchangia maendeleo yao kama AFYA ,ELIMU KUKOPESHANA kushamiri kwa makanisa hata kama sehemu hakuna wakiristo.pesa za MOU mnazopewa kodi mnalipa peke yenu?
vichwa vingine ni taabu sana. wakiambiwa kula pumba ya mpunga hawana uwezo wa kuchambua kuona hili ni sahihi au siyo. Hiyo MoU ndiyo nini? watu wanatoa hela zao mifukoni kujenga makanisa,wengine huku mitaani wanasema MoU na serkali. Kama kweli MoU ipo ni ya huduma za hospitali KCMC, Bugando nk.ambazo ni za wakristo. Serkali inaweza kuingia mkataba na wenye hospitali ili huduma za matibabu zipunguzwe ili hata wanaosema MoU waweze kupata matibabu.
 
Amekuambia serikali haina dini, ila watanzania wana imanizao ndio maana wana apa. Sasa usitake kujichetua akili.
 
Maelezo marefu ila UJINGA tuu ulioandika!
Serikali haina dini vp mbona wasile kiapo kimya kimya wakiteuliwa kwenye nyadhifa mpya? Hujui hata kuwa UPAGANI nao ni Dini?

kwa ukichaa wako na upeo mdogo huwezi kuona ila sisi tunaona msingi na umuhimu na kujifunza kikubwa sana kutokana na maalezo hayo.
 
Hivi kwa sasa kesi za ndoa& Talaka pamoja na Kesi za Mirathi zinasikilizwa na mahakama gani? Na kwa sheria zipi? Hivi wanao zisikiliza kesi hizo wanalipwa na nani?? Na zikiondolewa(kutenganishwa) kutoka ktk mahakama hizo au zikisikilizwa na mtalaamu mwengine ni makosa kulipwa na Serikali??? Hivi sheria zilizopo zina tambua ndoa za aina ngapi???

Haraka haraka wengi hatuoni ni kwanini ni makosa. Lakini naendelea kuamini kuwa hili litakuwa ni kosa kubwa manake zitaibuka dini nyingine nazo zitakuja na sheria zao na "makadhi" wao na watataka tuwalipe mishahara. Hapa sijui tutakataaje kuwalipia wengine.

Naendelea kuamini ushari aliotoa JK wakati alipokutana na waislam kuwa kama mnataka mahakama ya Kadhi anzisha wenyewe ulikuwa sahihi.

Wanaosukuma agenda hii nafikiri wataona matokeo yake wakati wa mijadala bungeni. Kwa uzoefu wetu mijadala ya dini uchangiwa na hisia za dini zao na huwa hawafuati hata nguvu za hoja, kwa wabunge wengi na matokeo yake ni mgawanyiko. Nawatakia kila la kheri katika majaribio ya mifarakano ambayo tunakimbilia kuliingiza taifa hili.

Maskini Tanzania yetu!
 
proisra

Umeandika meeengi kama huna ubongo vile. Sema mahakama ya kadhi ianzishwe ila ijigharamie yenyewe ingetosha. Ila ni kwanini ijigharamie yenyewe na inatoa huduma kwa wananchi? Ushani tibua na akili yako ndogo.
Wewe ndiye pungu4n! kuliko wote. Mbona kujenga misikiti mnajenga wenyewe? Kwanini gharama za mahakama muwatwishe na isiowahusu?
 
Akina mama wengi hawataki kuisikia hii kadhi kwasababu inawakandamiza sana,mtoto wa kiume anapewa urithi mara 2 ya mtoto wa kike,pia ushahidi wa mwanamke mmoja ni nusu ya ushahidi wa mwanaume.Mtoto wa nje ya ndoa ni haramu na hana stahiki zozote juu ya mirathi,hivi huyu poor child alijitakia mwenyewe kuzaliwa nje ya ndoa?Dou you really know what you are getting yourself into au mnashadadia tu!Misuli iwatoke mkipigania bomu hilo la kadhi ila mtajua utekelezaji ukianza.
Wengine wanakimbilia kusema ni ibada!duuuh ibada gani za kuoa na kupeana talaka kila uchao?Hili linapelekea vijana wengi wa kiislamu kuoa kwa haraka haraka bila tafakari ya kina kwasababu anajua likiharibika jambo ni talaka anabeba mwingine.Kuoa na kuacha ni ibada??????
Mungu ametuumba na hekima na busara ili tuweze kuyaendesha maisha yetu kwa kumpendeza yeye,kwa mantiki hiyo sisi kama binadamu tunaouwezo wa kujua jema na baya.Kama utekelezaji wa sharia ni ibada mbona hamjumuishi kukatana mikono(wezi) au kipigo cha mawe mpaka kufa(wanaochepuka) kwenye hizo mahakama??Kama ambavyo mlijua kuna mambo hayakuwa sahihi ni wakati wa kujua mahakama tulizonazo zinajibu kwa kiwango kikubwa changamoto zilizopo,kama kuna mapungufu tuyarekebishe na tuongeze mahakama hizi ili basi ziweze kuendana na kasi ya kesi hizi za kuoa na kuachana.
Nafikiri tujadili upungufu wa mahakama zetu then tuangalie kadhi imejibu vipi haya mapungufu na je kuna usawa???
Kuna watu wameshupalia sana kadhi,ukiwaomba wabainishe ni vipi kadhi itajibu kasoro hizo wanakimbilia kusema ooooh ni ibada.Ndugu zangu,tusome kwanza hizi sheria vizuri.

kwa upande mwingine napendekeza mjadala huu ukijadiliwa bungeni basi usiwe wa wazi,kuna hatari ya kuwagawa wananchi,tutajikuta kuna makundi makubwa mawili makubwa.Haya mambo yanaweza kwenda mpaka kwenye uchaguzi mkuu ujao.Uliye muweza tuepushe na nchi yetu kuingia kwenye mpasuko.Tujadili
 
Wacha uongo wewe. Unajuwa sana kuwa makafiri kama wewe ndiyo wanaoziharibu hizo nchi kwa roho mbaya tu ya kuona zimefanikiwa.

Na mtafanya kila njia lakini Uislam utaendelea kukuwa kwa kasi duniani. Na mahakama ya kadhi tutaipata tu Tanzania hii, hata mfanye nini.

malizia tu,mtaipata hata kwa jihadi
 
malizia tu,mtaipata hata kwa jihadi

Naam, tupo kwenye jihadi, na ambae hayupo kwenye kufanya juhudi kila siku ya maisha yake huyo ana walakin, iwe Muislam au si Muislam.

Wewe hufanyi juhudi katika maisha yako ya kila siku? na umebweteka tu?
 
Maelezo marefu ila UJINGA tuu ulioandika!
Serikali haina dini vp mbona wasile kiapo kimya kimya wakiteuliwa kwenye nyadhifa mpya? Hujui hata kuwa UPAGANI nao ni Dini?

utamjua tu punguani wa akili si tatizo lako but ni dini yqko ndio imekupumbaza
 
Tutadanganywa oh! mirathi, talaka, ndoa , wakfu nk. Lakini wataalamu husema kwenye tundu dogo ukishafanikiwa kuingiza kichwa tu !! basi mwili mzima umeingia
 
Back
Top Bottom