mbu wa dengue
JF-Expert Member
- Jun 2, 2014
- 7,655
- 9,757
Kumbe nyumba uko nazo hapo sasa nimekuelewa,mwanzoni nilikunukuu vibaya nikafikiri unasema kujenga ni ujinga.Nar
Narudi kwenye comment ya juu kabisa.
"Tengeneza secondary/other source of incomes"
Mimi binafsi naishi mkoani Ila Nina nyumba ya kupangisha dar@kinondoni.
Kwa mwezi nakusanya si hapa.
Nataka kutengeneza nyengine G.Mboto (Bro kaniambia kasikia nyumba inauzwa pale G.Mboto mwisho)
Nimeajiriwa 2014 Ila nimepanga..!!
Kwasasa mkatengeneza MIFEREJI kwanza.
Hiyo MIFEREJI ndio ijenge nyumba za kuishi na inunue gari na sio mshahara wangu.
Lengo langu ikifike wakati niachane na mshahara ukae benki miaka
Yaani najaza standing order, mshahara ukitoka benki wapeleke saving account ukatengeneze return.
Achana na hizo liabilities, tengeneza kwanza asset za kukuingizia pesa, halafu hizo assets ndio zizalishe matumizi ya hizo liabilities
Nikupe mfano:- hiyo nyumba YAKO what if ingekuwa uswahilini mfano Mwananyamala na kule chumba 50k
Tuseme nyumba ina vyumba 6.
Inamaana wewe kila mwezi una laki 3.
Ungechukua hizo laki 3, ukajichanga na madili + mishahara, unatengeneza nyengine uswahilini kwengine.
Then baada ya miaka 5 - 10 hivi una nyumba 3 tuseme total vyumba 20.
Kwahiyo kila mwezi unaingiza Mil 1.
Halafu sasa ndio ujenge YAKO ya kuishi..!!!
#YNWA
Kama umejenga ukapangisha pia ni sawa,yaani ni kitu kile kile tu unapokea kodi ya nyumba kisha na wewe unailipa ulikopanga hakuna tatizo hapo hauwezi ukanyanyasika kwa sababu una uhakika wa kupokea kodi hata kama umeachishwa kazi.
Kimbembe ni pale haujajenga nyumba kabisa umepanga halafu kuna biashara unayoitegemea ikayumba au ikafilisika hapo ndio utajua kwa nini wimbo wa Taifa hauna video.
Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app