Siri ya kuachwa chiligati yatajwa....

Technician

JF-Expert Member
Mar 30, 2010
841
222
Siri ya kuachwa Chiligati yatajwa.


*Makamba upepo si mzuri ndani ya CCM.
*Kamati kuu kukutana D'Salaam kesho.
*Msekwa naye atoboa, ajenda ni moja.



Na John Daniel.

HATIMAYE siri ya kuachwa kwa aliyekuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika Baraza jipya la
Mawaziri, Bw. John Chiligati, imefichuka.

Siri hiyo imetajwa kuwa ni kuandaliwa kwa Bw. Chiligati kurithi mikoba wa Katibu Mkuu wa sasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bw. Yusuf Makamba, anayetakiwa kupangiwa kazi maalum au kupumzika kabisa siasa.

Vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya CCM vimeeleza kuwa Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete kupitia vikao husika vya chama hicho ana mpango kumpa nafasi hiyo, Bw. Chiligati kutokana na sababu mbalimbali kubwa ikiwa ni uwezo wa kuhimili kuweka sawa makundi yote na ushirikiano mzuri ndani ya chama.

Sababu nyingine iliyotajwa ni uzoefu wake ndani ya chama hicho pamoja na kushughulikia nyufa zilizotokana na Uchaguzi Mkuu ambapo ushindi wa CCM ulipungua ikilinganishwa na mwaka 2005.

"Mmekuwa mkiandika sana kuondolewa kwa Mhe. Makamba katika nafasi yake lakini safari hii habari hizo ni za kweli, chama kinahitaji mabadiliko ya Katibu Mkuu kama mtendaji mkuu.

Anayeandaliwa kuchukua nafasi yake muda wowote kuanzia sasa ni Mhe. Chiligati, anaonekana kuwa ni mzuri na mtu mwenye msimamo wa kati, anayemudu makundi yote, mwenye uhusiano mzuri na waandishi wa habari, anaweza kukisaidia chama kundoa nyufa za Uchaguzi Mkuu,"kilisema chanzo chetu.

Ilielezwa kwamba tayari Rais Kikwete amejiandaa kuwasilisha hoja hiyo katika kikao maalum cha Kamati Kuu (CC) kinachotarajiwa kufanyika kesho mjini Dar es Salaam kama ajenda ya mengineyo kutoka kwa Mwenyekiti.

Vyanzo vyetu vilieleza kuwa Rais Kikwete ameamua kubaki na ajenda hiyo mkononi mwake na kuhusisha wazee wachache ndani ya chama hicho bila kutaja sababu za kufanya hivyo.

Hata hivyo duru za kisiasa zimeeleza kuwa huenda uamuzi huo unatokana na kutaka kukwepa makundi na mgongano wa kimaslahi kuhusu suala hilo.

Majira ilipomtafuta Makamu Mwenyekiti wa CCM, Bw. Pius Msekwa ili kupata ufafanuzi wa suala hilo hakuwa tayari kuzungumzia taarifa hizo kwa kile alichoeleza kuwa hawezi kuzungumza kitu ambacho hakijaamuliwa na vikao rasmi vya chama hicho.

Alisema CCM si mali ya mtu mmoja hivyo maamuzi ya kumwondoa Katibu Mkuu na masuala yote yanayohusu chama hicho huamuliwa na kikao na si mtu mmoja huku akimtaka mwandishi wa habari hizi kumweleza kwanza alikopata taarifa hizo za kuenguliwa kwa Bw. Makamba.

Hata hivyo alipoulizwa kama ana taarifa za kikao cha CC cha kesho na ajenda zake, alikiri kwamba ana taarifa na kikao hicho huku akieleza kuwa kinatarajiwa kuwa na ajenda moja tu ya kupitisha majina ya wagombea umeya katika manispaa na majiji.

"Usipende kuandika habari za kufikirika, hayo ni maneno ya mitaani, hayana ukweli wowote wala hao waliokwambia hawawezi kuthibitisha, siwezi kuzungumzia jambo ambalo halijatoka kwenye kikao, maadili ya CCM ni kwamba taarifa inayotolewa ni ile iliyoamuliwa na kikao.

"Ni kweli kutakuwa na kikao cha Kamati Kuu tarehe moja Desemba hapa Dar es Saalam, tayari tumepewa ajenda ya Kamati Kuu, ni moja tu ya kupitisha majina ya wagombea umeya, kama ipo nyingine mimi sijui na si kweli, ni maneno ya uwongo tu,"alisisitiza Bw. Msekwa.

Alisema Katibu Mkuu mwenyewe, Bw. Makamba ndiye aliyewapa ajenda hiyo moja ya CC na kusisitiza kuwa baada ya Uchaguzi Mkuu hakuna kikao kilichoketi kujadili suala lolote kuhusu mabadiliko ya uongozi wa chama hicho.

Licha ya tetesi za kuenguliwa Bw. Makamba duru za kisiasa zilieleza kuwa Idara ya Usalama na Maadili pamoja na Kitengo cha Propaganda cha chama hicho, pia vinatarajiwa kukumbwa na mabadiliko makubwa kutokana na matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliopita.

Mbali ya Bw. Chiligati kutajwa kurithi mikoba ya Bw. Makamba pia Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Vijana Dkt. Emmanuel Nchimbi, anatajwatajwa katika nafasi hiyo.

Juhudi za kumpata Bw. Makamba ili kuzungumzia tetesi hizo zilishindikana kutokana kile kilichoelezwa kuwa amefiwa na yuko mkoani Tanga. Hata simu zake zote za mkononi hazikuweza kupatikana hadi tunakwenda mitamboni.

Kuondolewa kwa Bw. Makamba katika nafasi hiyo imekuwa gumzo la muda mrefu sasa, kwa mara ya mwisho ilidaiwa kuwa Katibu huyo alimsihi Rais Kikwete kumwacha ili akamilishe awamu ya kwanza ya ya miaka mitano kwa sababu mbalimbali.

SOURCE:MAJIRA
 
huyu si ndo alisema wabunge wa chadema watafukuzwa kwa kutoka bungeni wakati jk anahutubia
 
Alisema ataanda hoja ya kuwafukuza Chadema bungeni. Huyu hata haelewi maana ya vyama vingi . Ni fundermentalist wa CCm tuuu. Hawezi kuona kuna nini pembeni.
 
Hiyo tetesi kwamba Makamba uenda akalazimishwa kuachia ngazi imekuwepo kwa mda mrefu na kwa siku za hivi karibuni imepata nguvu mpya. Kuhusu ni nani anatarajiwa kuchukua nafasi yake, wadadisi wa mambo wanampa Kinana nafasi kubwa kuibuka mshindi. Hata hivyo mambo ya ccm hayatabiriki, kwakuwa chama hicho bado kinazidi kuhandamwa na mzimu wa uchaguzi wa 2005. Si unajua Kinana alikuwa anamuunga mkono Salim na Chiligati Sumaye, hali hiyo inaweza ikasababisha huyo waziri wa habari na michezo aibuke kama "compromising candidate".
 
Dr.slaa alimwambia kuwa huyo ni mbumbumbu wa sheria..hahaha, nilicheka sana siku ile. amekaa bungeni miaka yote hiyo halafu anatoa statement ya uelewa wa hali ya chini kama ile...ati ccm wataandaa hoja ili wana chadema wafukuzwe bungeni, na alijidai kweli kwa uhakika akisema kuwa wao ccm wanao wabunge wengi lolote watakalotaka kulipigia kura watashinda hata kama litapingwa na wapinzani walio wachache....

Kwa kuwasaidia wana ccm pamoja na kwamba ccm siipendi, wawe wanawapa watu wenye uelewa mkubwa na elimu kubwa position ya kutoa taarifa mbele ya jamii. mtu kama chiligati au makamba akiongea hoja zisizo na akili chama kizima kinaaibika...mimi picha niliyonayo kichwani ni kwamba, wana ccm wote wako kama chiligati...au makamba.
 
Walewale tu. Ila ni habari njema kwa CHADEMA kwasababu ukimweka Chiligati na Slaa kama watendaji wakuu wa vyama vyao,utaona dhahiri pumba ipi na mchele upi. Kwaiyo CHADEMA wanapaswa kuendelea kuutumia udhaifu wa uongozi wa CCM katika kuimarisha zaidi kisera na kiitikadi,kwani Chiligati si bingwa wa kutoa hoja za kueleweka.
 
Hakuna jipya hapo! kwangu mm sioni tafauti ya Makamba na Chiligati.
Yaani hapo ni sawa na timu ya mpira,ambapo kocha anamtoa mchezaji AFAZALI na
anamwingiza mchezaji POTELEA YA MBALI, liwalo na liwe
 
huyu nae ni sawa na makamba tofauti ni ndogo sana

tofauti hiyo ndogo ni ipi? huyu jamaa ni Mkamba xmakambax makamba. very useless. watajuta. Kama makamba kaitia ugonjwa ccm huyu ataipiga sindano ya sumu kabisa.
 
Nina uhakika Chiligati akiwa Katibu Mkuu wa ccm chama kimekufa jumla,na Dr Slaa atajipatia njia nyepesiiiii ya kuivuruga ccm.kwasababu Chiligati hana utashi wa kujieleza na kuonekana muungwana anaonekana ni mtu wa kutumia nguvu za hoja badala ya hoja za nguvu.
 
Ukweli ni kwamba CCM inataka mabadiliko makubwa. anatakiwa katibu mkuu mtendaji na sio mwanasiasa wa uongo kama Makamba. Katibu Mkuu anatakiwa awe na uwezo wa kuendesha chama na nidhamu ya hali ya juu sio kuwa na makundi ndani ya chama ambayo mengine yanashabikiwa na katibu mkuuu. all in all it is time for makamba and his cronies to go and let the party be run by professional and technocrat. mtu hata shule hajaenda anawezaje kupanga mikakati ya utendaji wa chama.
 
ameenda shule ya waganga wa jadi. ameongoza ccm kwa mitishamba ndio maana anakubalika na jk
 
Hakuna jipya hapo! kwangu mm sioni tafauti ya Makamba na Chiligati.
Yaani hapo ni sawa na timu ya mpira,ambapo kocha anamtoa mchezaji AFAZALI na
anamwingiza mchezaji POTELEA YA MBALI
, liwalo na liwe


hahahaaaa..... mkuu umeeleweka sana.
 
Please please CCM, mpeni Bw Chiligati hiyo nafasi ya Ukatibu Mkuu hata LEO.

Itakuwa raha kwa taifa kwani ataharibu vibaya. Anaongea kabla ya kufikiri.

CCM inapaswa iwe kama MBEGU, inabidi IOZE ili taifa LICHIPUKE upya likiwa na MATAWI ya chama cha mabadiliko, CDM.
 
jamani ccm ni kapu la samaki ambaye mmoja alishaozaga ndo maana wote wameshaoza, na hao wanaoonekana afadhali ni kwa sababu hawajawahi kuongea mbele ya hadhara, nafikiri tumejifunza kwa kauli ya huyu mama kombani kwa kusema 'hamna haja ya katiba mpya' wako wengi pumbaish humu.
-hivyo basi ndani ya ccm kwa sasa wanachagua samaki ambaye labda ameoza mkia peke yake,au kiuno au kichwa n.k. Huyu makamba na chiligati hata hadhi ya samaki hawana ni mapande yaliyooza tuu, na kwa sisi wanaharakati tunawaitaji zaidi ili kurahisisha kuuangusha uditecta wa ccm nchini
 
JF Senior Expert Member

Join Date
Fri Oct 2009
Posts
299
Thanks
55
Thanked 65 Times in 47 PostsRep Power
22
Re: John Chiligati kupewa ukatibu Mkuu wa CCM?
Originally Posted by Kasheshe
Hilo tulishalizungumza .
http://https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/91059-john-chiligati-kupewa-ukatibu-mkuu-wa-ccm.html#post1302696
Jamani,

Nina mashaka huyu kutokuwepo kwenye baraza la mawaziri ... huenda akaula ukatibu mkuu wa CCM... kwa sababu kura zilizoelekea kutotosha za CCM ni dalili za Makamba kushindwa kazi.

Mimi nasubiri kuona yatakayojiri.
Hii ni kweli kabisa Mh John Zephania Chiligati Mbunge wa Manyoni Mashariki Mkoani Singida ndiye katibu Mkuu wa CCM ajaye baada ya Yusuph Makamba.
Habari hizo ni za kweli kabisa na hii inawezekana ikawa hata kabla ya Uchaguzi mkuu wa CCM mwaka 2012.
Asante.
 
Huyu si ndiyo alisema kuwa Bashe si raia bila kuiconsult Wizara????????????
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom