Siri ya BABA kunenepa akipigania maslai ya familia

Baba jayaron

JF-Expert Member
Jun 29, 2015
4,007
5,446
Habari wanajamvi,
Leo nataka mnipe jibu juu ya sintofahamu yangu katika hii familia.....

Ikiwa ni mama mwenye watoto na rasilimali nying za utajiri, lakini amekua akiwa na utaratibu wa kutaftia watoto hao baba wa kuilea familia yake baba ambaye atazitumia rasilimali hizo kwa faida ya familia na kuboresha maisha ya watoto wake.

Amejiwekea mfumo wa muda kwakila baba atakea mpata aweze kutengeneza mfumo mzuri kwa familia yake.
Mama huyu anashoga ake watu wa mjini wanamuita kugwi ambaye mara nyingi ndio humleteaga ma baba wa kuongoza familia yake.

Kwa muda mrefu watoto wa familia hiyo wana hali mbaya kiafya hata wengi kuanza kuichukia nyumba yao hata mama yao.
Mbaya zaidi hata wakaanza kumgomea baba yao.

Ndipo katika hali isiyo ya kawaida akapatikana baba mwingine aliyekuja kwa gia ya kua na uchungu na familia hiyo hata kufa kwakua yeye ni mtu wa dini saana na mungu anampenda.

Watoto wakamwamini maana waliamini.huyo.ni bora kuliko baba aliyetoka mwanzo wakampa mapenz na imani yao kwakua alionesha mapungufu na mabaya ya mababa wa nyuma japo walitoka ukoo mmoja.

Ghafla hali ilizidi kua mbaya kufikia watoto wale kuugua uchizi maana utafiti ulionesha watoto wale wanne mmoja alikua kichaa kutokana na ugumu wa maisha.

Mbaya zaidi baba anaomba aombewe maana anawasaidia watoto hao maskini kwakuwanunulia ndege za kwendea shule wakati shule wanazosoma hazina walimu.

Baba ukimtazama anazidi kunenepa kuliko alivokua kabla ya uBABA familia haileweke wanaelekea wapi,
Je huyu baba anania ya dhati au nae ana lake???
 
Back
Top Bottom