nusuhela
JF-Expert Member
- Jan 26, 2014
- 5,736
- 6,972
Ingekua hivyo basi ingekua balaa kweli kweliKwanza nianze kwa kuelezea ndoto maana yake,
Ndoto ni mkusanyiko wa matukio ambayo binadamu huyaweka kichwani kwake ambayo humjia bila zuio (involuntary) kwenye ubongo wakati akiwa amelala,matukio haya huwa hayaeleweki na saa nyingine huwa kinadharia zaidi mfano kuota unapaa wakati kiualisia haiwezejani.kiujumla sayansi imeshindwa kuja na jibu kamili kuhusu ndoto ,na matokeo yake wameishia kutoa tafsiri hiyo .
Ukija kwenye dini ndoto huwa ndio njia maalumu ambayo ulimwengu wa Roho hutumia kuwasiliana na binadamu,hapa sasa ndio nataka tuanze.
Kibibilia Mungu hutumia matukio tuliyoyaifadhi au kumbukumbu za vitu tulivyoifadhi moyoni ,ili kutengeneza codes za mawasiliano kati yake yeye na sisi .
Sasa kuna mambo kadhaa ambayo huwa ukiota lazima ujue kufungua hizo codes ,ni maarifa rahisi ila inahitaji uwe mcha Mungu na mwerevu.
Mfano
1:Ukiota unapaa angani :ndoto ya namna hii ukitaka kuifahamu lazima ujue kwa nini Mungu katumia anga,anga maana yake ni ulimwengu wa Nuru ,ardhi ni ulimwengu wa Giza ,hivyo ukiota unapaa ni taadhari kutoka kwa Mungu kwamba uache kutembea kwenye ulimwengu wa Giza ,hamia ulimwengu wa Nuru.nikuhakikishie ukifanya hivyo hutakaa uote tena kupaa sure.
2: Kuota unafanya mapenzi ;codes za ndoto hii ni mbili kulingana na mazingira yako,mfano ukiota unafanya mapenzi na ukiamka unajihisi mchovu na mara nyingine kama mwanaume unahisi umemaliza ,basis ujue kuna pepo wachafu wanakuchezea.
Ila ukiota unafanya mapenzi na ukiamka hakuna ishara yoyote nikimaanisha uchovu au uchafu basi ndoto hii huwa ni njema code ya mapenzi ni pesa maana ni kipi kinapendwa zaidi ya mapenzi kama si pesa hivyo ukiota unafanya mapenzi ni ishara ya kupata pesa,kama unayefanya naye humjui basi utapata pesa kwenye vyanzo usivyotarajia. Kama umeota unafanya mapenzi na MTU unayemjua basi ujue utapata pesa zaidi kwenye vyanzo vyako vya kiuchumi unavyovijua.
3;Kuota uko darasani ,na kufanya mitihani.Hii ndoto code yake ni hivi jiulize ni nini hukupa wasiwasi kama kama kipindi uko shule hasa wakati wa mitihani kama kukosa pesa wakati wa matatizo,hivyo ndoto hii ukiota ni onyo kutoka ulimwengu wa roho kwamba kuna matatizo makubwa yatakujia na yanahitaji pesa hivyo unahitaji kuweka akiba ya pesa ,upunguze matumizi la sivyo hilo tatizo litakuaibisha.
4;Kuota kusalitiwa kimapenzi ; code yake ni hivi ni nini huumiza moyo na kuuvunja moyo kama usaliti wa kimapenzi? jibu ni msiba.hivyo kama umeota mwenzi wako anakusaliti na kiuhalisia si kweli basi ni ujumbe wa kifo kwa huyo uliyemuota either yeye ,familia yake watakumbwa na tukio la msiba hivyo Muombee huenda bado ulimwengu wa Roho haujaidhinisha hilo janga.
Ntaendelea kesho...............pia ukumbuke somo la ndoto lilikuwapo tangu zamani Yusuph alisoma kupitia vitabu alivyoiba mama yake RHaheli wakati anatoka kwa baba yake aliyekua mganga na mtabiri alijulikana kama Laban ,
Danieli alisomea huko uajemi enzi za utumwa
Na binadamu huota zaid ya ndoto 20 kwa siku ,ndoto yenye ujumbe huwa unaikumbuka vema na huwa inaushtua moyo.nyingine huwez kuzikumbuka maana huwa kazi yake ni kuufanya ubongo ufanye kazi vizuri ,hivyo siyo ndoto zote ni ujumbe unatakiwa uwe mwerevu wa kusoma mazingira na hali yako.