Siri usiyoijua kuhusu ndoto na tafsiri zake

Mkuu Mimi nakupinga ,swala la ndoto Ni Pana Sana,hivyo ndoto haziwezi kuwa na constants,eti ikiwa hivi basi itakuwa vile no ,nakupinga,mfano Mimi nikiota nakula ubwabwa na maharage basi hapa nijiandae kupata pesa mungu,

Kuota uko juuu unapaa hamuwezi kuwa na maana moja,lazima uangalie kwanini unapaa,na uko mazingira gani,hivyo kwa dhana hii utapata maana tofauti za ndoto ya kupata.
Mfano mtu anaota anapaa lakini chini yake anamuona mtu aliyekufa dhaman,ndoto hii inamaana Pana na haiwezi kuwa na constants Kama ulizozitaja.
 
Mkuu naomba unipe tafsiri ya ndoto hizi mbili,kwanza nilishawahi kuiota mara kama tatu nimefiwa na mzazi wangu ilhali bado yupo hai inatokea nalia sana mpla machizi ila nikiamka asubuhi sioni chozi lolote
Pili hii imeshanitokea si chini ya mara nne naota nipo shuleni na nimeshamaliza shule mda mrefu.
Msaada please
 
Mkuu shukrani kwa ufafanuzi, Mimi naota Mara kwa Mara kufanya Mapenzi na wanawake au naweza ota naona mwanamke yuko uchi kabisa kitandani, Mimi jinsia ya kiume. Mkuu naomba codes.
 
Kwanza nianze kwa kuelezea ndoto maana yake,

Ndoto ni mkusanyiko wa matukio ambayo binadamu huyaweka kichwani kwake ambayo humjia bila zuio (involuntary) kwenye ubongo wakati akiwa amelala,matukio haya huwa hayaeleweki na saa nyingine huwa kinadharia zaidi mfano kuota unapaa wakati kiualisia haiwezejani.kiujumla sayansi imeshindwa kuja na jibu kamili kuhusu ndoto ,na matokeo yake wameishia kutoa tafsiri hiyo .

Ukija kwenye dini ndoto huwa ndio njia maalumu ambayo ulimwengu wa Roho hutumia kuwasiliana na binadamu,hapa sasa ndio nataka tuanze.

Kibibilia Mungu hutumia matukio tuliyoyaifadhi au kumbukumbu za vitu tulivyoifadhi moyoni ,ili kutengeneza codes za mawasiliano kati yake yeye na sisi .

Sasa kuna mambo kadhaa ambayo huwa ukiota lazima ujue kufungua hizo codes ,ni maarifa rahisi ila inahitaji uwe mcha Mungu na mwerevu.

Mfano
1:Ukiota unapaa angani :ndoto ya namna hii ukitaka kuifahamu lazima ujue kwa nini Mungu katumia anga,anga maana yake ni ulimwengu wa Nuru ,ardhi ni ulimwengu wa Giza ,hivyo ukiota unapaa ni taadhari kutoka kwa Mungu kwamba uache kutembea kwenye ulimwengu wa Giza ,hamia ulimwengu wa Nuru.nikuhakikishie ukifanya hivyo hutakaa uote tena kupaa sure.

2: Kuota unafanya mapenzi ;codes za ndoto hii ni mbili kulingana na mazingira yako,mfano ukiota unafanya mapenzi na ukiamka unajihisi mchovu na mara nyingine kama mwanaume unahisi umemaliza ,basis ujue kuna pepo wachafu wanakuchezea.
Ila ukiota unafanya mapenzi na ukiamka hakuna ishara yoyote nikimaanisha uchovu au uchafu basi ndoto hii huwa ni njema code ya mapenzi ni pesa maana ni kipi kinapendwa zaidi ya mapenzi kama si pesa hivyo ukiota unafanya mapenzi ni ishara ya kupata pesa,kama unayefanya naye humjui basi utapata pesa kwenye vyanzo usivyotarajia. Kama umeota unafanya mapenzi na MTU unayemjua basi ujue utapata pesa zaidi kwenye vyanzo vyako vya kiuchumi unavyovijua.

3;Kuota uko darasani ,na kufanya mitihani.Hii ndoto code yake ni hivi jiulize ni nini hukupa wasiwasi kama kama kipindi uko shule hasa wakati wa mitihani kama kukosa pesa wakati wa matatizo,hivyo ndoto hii ukiota ni onyo kutoka ulimwengu wa roho kwamba kuna matatizo makubwa yatakujia na yanahitaji pesa hivyo unahitaji kuweka akiba ya pesa ,upunguze matumizi la sivyo hilo tatizo litakuaibisha.

4;Kuota kusalitiwa kimapenzi ; code yake ni hivi ni nini huumiza moyo na kuuvunja moyo kama usaliti wa kimapenzi? jibu ni msiba.hivyo kama umeota mwenzi wako anakusaliti na kiuhalisia si kweli basi ni ujumbe wa kifo kwa huyo uliyemuota either yeye ,familia yake watakumbwa na tukio la msiba hivyo Muombee huenda bado ulimwengu wa Roho haujaidhinisha hilo janga.

Ntaendelea kesho...............pia ukumbuke somo la ndoto lilikuwapo tangu zamani Yusuph alisoma kupitia vitabu alivyoiba mama yake RHaheli wakati anatoka kwa baba yake aliyekua mganga na mtabiri alijulikana kama Laban ,
Danieli alisomea huko uajemi enzi za utumwa

Na binadamu huota zaid ya ndoto 20 kwa siku ,ndoto yenye ujumbe huwa unaikumbuka vema na huwa inaushtua moyo.nyingine huwez kuzikumbuka maana huwa kazi yake ni kuufanya ubongo ufanye kazi vizuri ,hivyo siyo ndoto zote ni ujumbe unatakiwa uwe mwerevu wa kusoma mazingira na hali yako.
Naomba unifafanulie ndoto hizi ambazo huota Mara kwa Mara
1) Nliwahi kuota Mara kadhaa ngombe wa nyumbani kwetu maziwa yamejaa then akazaa nkastuka usingizini

2)Ngombe kwa zizi letu wako wanne akatokea mmoja akazaa boma likajaa then mama angu akaniuliza huyu ndama aliezaliwa hakuna pakumweka mm nkamjibu tupunguze ngombe mmoja tumuze then nkastuka usingizini.

3) Nliota ngombe mzuri wakike maziwa yamejaa ana ngozi ya kuteleza anazaa ila akikua kipofu hua sielewi maana zake kwa ulimwengu wa roho

4) Juzi juzi nliota kua kuna mama mmoja(sikumfaham) alizaa mtoto wa kiume na mtoto yule akakua gafla na kuanza ktumbea pale pale. Naomba tafsiri yake mkuu
 
Mimi nimeota mwanamke niliyeachana nae ndio mpenzi wangu kwa kipindI hiki lakini ana mwanaume mwingine ikafikia kipindi akaniacha akapata nae mtoto je hii ina maana gani
 
Mimi nimeota mwanamke niliyeachana nae ndio mpenzi wangu kwa kipindI hiki lakini ana mwanaume mwingine ikafikia kipindi akaniacha akapata nae mtoto je hii ina maana gani
Naomba unifafanulie ndoto hizi ambazo huota Mara kwa Mara
1) Nliwahi kuota Mara kadhaa ngombe wa nyumbani kwetu maziwa yamejaa then akazaa nkastuka usingizini

2)Ngombe kwa zizi letu wako wanne akatokea mmoja akazaa boma likajaa then mama angu akaniuliza huyu ndama aliezaliwa hakuna pakumweka mm nkamjibu tupunguze ngombe mmoja tumuze then nkastuka usingizini.

3) Nliota ngombe mzuri wakike maziwa yamejaa ana ngozi ya kuteleza anazaa ila akikua kipofu hua sielewi maana zake kwa ulimwengu wa roho

4) Juzi juzi nliota kua kuna mama mmoja(sikumfaham) alizaa mtoto wa kiume na mtoto yule akakua gafla na kuanza ktumbea pale pale. Naomba tafsiri yake mkuu
Ng'ombe huwa ni mwakilishi wa wanyama wote walao nyasi ,huwa kwenye bibilia hutamkwa kama ndama,kama umeota ng'ombe amenawiri basi unganisha jibu kwamba nyasi zitakua ni nyingi na kama nyasi ni nyingi basi ni kipindi cha neema,kwa hiyo utapitia kipindi cha neema lakini uwe na busara katika plan zako ,maana ni kwa mda tuu utapitia hicho kipindi ,kuzaliwa ndama kipofu codes zake no kuwa upofu =ulimwengu wa Giza ,hivyo ukipitia hicho kipindi cha neema omba sana maana itakupelekea kuangukia ulimwengu wa Giza .so mkuu piga goti na jichunge usije ukasombwa dhambini kipindi hicho
Kuhusu mama kuzaa mtoto akaanza kutembea,kwanza code ya mama na mtoto huwakilisha jamii au familiya hivyo kuna mambo ambayo utayashuhudia jamii au familia iliyokaribu nawe au inayokuzunguka ikikufanyia kinyume na unavyotarajia ,yaan hayaingii akilini ,pia yako kinyume na desturi ,sijui niwekeje ila ni kama kukuzushia ishu ambazo hazipo wala hukuwah kuwaza.
 
Inakuwaje story inaanza mwanzo mpaka inakamilika na wakati sii kweli?
 
Mimi nimeota mwanamke niliyeachana nae ndio mpenzi wangu kwa kipindI hiki lakini ana mwanaume mwingine ikafikia kipindi akaniacha akapata nae mtoto je hii ina maana gani
Hapo umeota usaliti,kiufupi kama huyo ex wako alikuaga na ugojwa flan unaoujua,au ndugu yake unayemjua ambaye alikua anaumwa ,basi itakua habari mbaya kwao.
 
Ng'ombe huwa ni mwakilishi wa wanyama wote walao nyasi ,huwa kwenye bibilia hutamkwa kama ndama,kama umeota ng'ombe amenawiri basi unganisha jibu kwamba nyasi zitakua ni nyingi na kama nyasi ni nyingi basi ni kipindi cha neema,kwa hiyo utapitia kipindi cha neema lakini uwe na busara katika plan zako ,maana ni kwa mda tuu utapitia hicho kipindi ,kuzaliwa ndama kipofu codes zake no kuwa upofu =ulimwengu wa Giza ,hivyo ukipitia hicho kipindi cha neema omba sana maana itakupelekea kuangukia ulimwengu wa Giza .so mkuu piga goti na jichunge usije ukasombwa dhambini kipindi hicho
Kuhusu mama kuzaa mtoto akaanza kutembea,kwanza code ya mama na mtoto huwakilisha jamii au familiya hivyo kuna mambo ambayo utayashuhudia jamii au familia iliyokaribu nawe au inayokuzunguka ikikufanyia kinyume na unavyotarajia ,yaan hayaingii akilini ,pia yako kinyume na desturi ,sijui niwekeje ila ni kama kukuzushia ishu ambazo hazipo wala hukuwah kuwaza.
Nashukuru sana mkuu,nikweli kuna baadhi ya matukio yameshanitokea katka ufafanuzi ulonipatia ila namshukuru Mungu nimeyashinda na sitachoka kumwomba Mungu japo napitia mitahani migumu sana, Ila ili dhahabu iwe bora zalima ipite kwenye moto. Barikiwa sana mkuu
 
niliota baba yangu mkubwa na babu yangu (wote ni marehemu) tulikua sehemu ambayo inaonekana ilikua ni nyumbani kwa ba mkubwa nikamwambia nataka kwenda shule (me ni mtu mzima saivi shule nlishamaliza mpaka chuo) akanambia nenda ndani sehemu fulaani utakuta hela chukua nenda shule kweli nikaenda nikachukua zile hela ila sikumbuki kama nlienda shule

ndoto nyingine nliota huyohuyo baba mkubwa ameacha familia yake na kwenda kusikojulikana na hakuna anaejua alipo/anafanya nini na roho ilikua inaniuma sana kumbe alienda kuanzisha maisha yake sehemu nyingine ila hakuoa mke mwingine na hakutaka mtu ajue yuko wapi na anafanya nn ila kumbe huko alikoenda alikua anaendelea na kazi yake ya ualimu na alikua anaishi mwenyewe tu hakutaka kujiusisha na mtu yaani kama alijitenga tu
 
Vipi na ndoto za kupanda milima Hadi juu, au kuota mlima mrefu na theluji yake?
 
Kwanza nianze kwa kuelezea ndoto maana yake,

Ndoto ni mkusanyiko wa matukio ambayo binadamu huyaweka kichwani kwake ambayo humjia bila zuio (involuntary) kwenye ubongo wakati akiwa amelala,matukio haya huwa hayaeleweki na saa nyingine huwa kinadharia zaidi mfano kuota unapaa wakati kiualisia haiwezejani.kiujumla sayansi imeshindwa kuja na jibu kamili kuhusu ndoto ,na matokeo yake wameishia kutoa tafsiri hiyo .

Ukija kwenye dini ndoto huwa ndio njia maalumu ambayo ulimwengu wa Roho hutumia kuwasiliana na binadamu,hapa sasa ndio nataka tuanze.

Kibibilia Mungu hutumia matukio tuliyoyaifadhi au kumbukumbu za vitu tulivyoifadhi moyoni ,ili kutengeneza codes za mawasiliano kati yake yeye na sisi .

Sasa kuna mambo kadhaa ambayo huwa ukiota lazima ujue kufungua hizo codes ,ni maarifa rahisi ila inahitaji uwe mcha Mungu na mwerevu.

Mfano
1:Ukiota unapaa angani :ndoto ya namna hii ukitaka kuifahamu lazima ujue kwa nini Mungu katumia anga,anga maana yake ni ulimwengu wa Nuru ,ardhi ni ulimwengu wa Giza ,hivyo ukiota unapaa ni taadhari kutoka kwa Mungu kwamba uache kutembea kwenye ulimwengu wa Giza ,hamia ulimwengu wa Nuru.nikuhakikishie ukifanya hivyo hutakaa uote tena kupaa sure.

2: Kuota unafanya mapenzi ;codes za ndoto hii ni mbili kulingana na mazingira yako,mfano ukiota unafanya mapenzi na ukiamka unajihisi mchovu na mara nyingine kama mwanaume unahisi umemaliza ,basis ujue kuna pepo wachafu wanakuchezea.
Ila ukiota unafanya mapenzi na ukiamka hakuna ishara yoyote nikimaanisha uchovu au uchafu basi ndoto hii huwa ni njema code ya mapenzi ni pesa maana ni kipi kinapendwa zaidi ya mapenzi kama si pesa hivyo ukiota unafanya mapenzi ni ishara ya kupata pesa,kama unayefanya naye humjui basi utapata pesa kwenye vyanzo usivyotarajia. Kama umeota unafanya mapenzi na MTU unayemjua basi ujue utapata pesa zaidi kwenye vyanzo vyako vya kiuchumi unavyovijua.

3;Kuota uko darasani ,na kufanya mitihani.Hii ndoto code yake ni hivi jiulize ni nini hukupa wasiwasi kama kama kipindi uko shule hasa wakati wa mitihani kama kukosa pesa wakati wa matatizo,hivyo ndoto hii ukiota ni onyo kutoka ulimwengu wa roho kwamba kuna matatizo makubwa yatakujia na yanahitaji pesa hivyo unahitaji kuweka akiba ya pesa ,upunguze matumizi la sivyo hilo tatizo litakuaibisha.

4;Kuota kusalitiwa kimapenzi ; code yake ni hivi ni nini huumiza moyo na kuuvunja moyo kama usaliti wa kimapenzi? jibu ni msiba.hivyo kama umeota mwenzi wako anakusaliti na kiuhalisia si kweli basi ni ujumbe wa kifo kwa huyo uliyemuota either yeye ,familia yake watakumbwa na tukio la msiba hivyo Muombee huenda bado ulimwengu wa Roho haujaidhinisha hilo janga.

Ntaendelea kesho...............pia ukumbuke somo la ndoto lilikuwapo tangu zamani Yusuph alisoma kupitia vitabu alivyoiba mama yake RHaheli wakati anatoka kwa baba yake aliyekua mganga na mtabiri alijulikana kama Laban ,
Danieli alisomea huko uajemi enzi za utumwa

Na binadamu huota zaid ya ndoto 20 kwa siku ,ndoto yenye ujumbe huwa unaikumbuka vema na huwa inaushtua moyo.nyingine huwez kuzikumbuka maana huwa kazi yake ni kuufanya ubongo ufanye kazi vizuri ,hivyo siyo ndoto zote ni ujumbe unatakiwa uwe mwerevu wa kusoma mazingira na hali yako.
Boss naitaj tafsiri hii pliz: usiku sa kuamkia leo nimeota nimesalitiwa. watu wangu ww mtaani kwetu nika amua kulipiza kisasi kwa wote walio nisaliti walikua 4 nikawasulubu then nika anza kuwadunga visu kila mmoja shingoni na kufariki... bada ya tukio hilo nika anza kutafutwa ili namimi niuliwe ila nikafanisha kutoroka jiji letu ambapo nilizaliwa nika elekea sehem mbali ambapo nika pokewa na askari wa2 waasi icho kijiji nimefika kulikuwepo vita ila mapigano yakawa yamesitishwa kwa kipindi ambacho nilikua huko na hivi karibuni kuliwahi kutoke mafuriko.....Mana ya ndoto hiyo nini nilipokua na tafutwa kwa kutukio ilibd mke wangu pia na yy akakusanye kila kitu chetu akashirikiana na mimi piaa!!! Nimeoa nina watoto2
 
H
Boss naitaj tafsiri hii pliz: usiku sa kuamkia leo nimeota nimesalitiwa. watu wangu ww mtaani kwetu nika amua kulipiza kisasi kwa wote walio nisaliti walikua 4 nikawasulubu then nika anza kuwadunga visu kila mmoja shingoni na kufariki... bada ya tukio hilo nika anza kutafutwa ili namimi niuliwe ila nikafanisha kutoroka jiji letu ambapo nilizaliwa nika elekea sehem mbali ambapo nika pokewa na askari wa2 waasi icho kijiji nimefika kulikuwepo vita ila mapigano yakawa yamesitishwa kwa kipindi ambacho nilikua huko na hivi karibuni kuliwahi kutoke mafuriko.....Mana ya ndoto hiyo nini nilipokua na tafutwa kwa kutukio ilibd mke wangu pia na yy akakusanye kila kitu chetu akashirikiana na mimi piaa!!! Nimeoa nina watoto2
Hiyo ndoto inamaanisha kuna tukio litampata mkeo ambalo litawaweka wote wawili kwenye wakat mgumu sana,hivyo piga magoti mkuu.
 
H

Hiyo ndoto inamaanisha kuna tukio litampata mkeo ambalo litawaweka wote wawili kwenye wakat mgumu sana,hivyo piga magoti mkuu.
Mungu akubariki kuna jambo tunapambana nalo mwaka sasa kabisa ila Kwa uwezo wa Mungu litakwishaa!! Na lina tu cost sote!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom