Siri nyingine ya Ngeleja: Wamarekani tayari wanachimba Uranium Tunduru kisiri siri?

Nyambala tutakuwaje serious wakati wewe unaonyesha udhaifu mkubwa kwa kubeza uranium, dhahabu nk eti coal na iron ore ndio itatutoa, kama tumeshindwa dhahabu ambayo ingetutoa kama tungeisimamia vizuri tutawezaje coal na iron ore. Kwataarifa tu ni kwamba huko serikalini wengi kama sio wote wana mawazo ya kijinga kama yako na ndio maana rasilimali zetu hazitunufaishi kitu ila zinamnufaisha mwekezaji, huo ni 'ukilaza' ndugu yangu

Mkuu sielewi huo unaouita udhaifu na nilichokizungumza si kubeza bali kuweka wazi facts ila kwa sababu stori kuhusu uranium, mabomu, marekani zinasensitize na kuburudisha hadhira basi watu hawataki hata kufikiri japo hata kupay attention kwa wanaofahamu hayo mambo.

Nachokizungumza unatakiwa ukielewe dhahabu au uranium processing yake ni complicated na expensive. Mfano average ya dhahabu inyopatikana hapo Tanzania ni gramme kama 3.8 per tonne, sasa kuitoa hiyo tani km20, kuiprocess mpaka upate gold unaweza kukuta kwa bei ya sasa ya 1oz = $1600, zaidi ya nusu inaishia kwenye gharama za uzalishaji. Halafu sasa siyo kwamba kila udongo around the mine utakuwa na hiyo dhahabu ndiyo maana kuna undergrounds. Ukija kwenye Coal, say Cocking coal gharama ya uzalishaji ni around $35 - $74, kwa huko Afrtica inaweza hata kuwa nusu ya hizo estimate bei yake ni $238 per ton. Na coal ukishapata ile seam unazoa tu mitani kwa mitanni. Process ya coal sana sana ni kuisafisha, chemical inayotumika ni moja tu na wala sio gharama.

Anyways on top of that kwa sababu coal na iron ore ni bulk handing yake inahitaji alot of infrastucture, hivyo kuzalisha ajira kibao, reli kama hiyo Tazara inaweza kuwa operational kwa faida for the coming 100 years. Bandari ya kuhandle coal kama ya Mchuchuma kwa makadirio inaweza kuwa mara tano ya hiyo ya Dar es salaam. U can imagine ni watanzania wangapi wataajiriwa hapo, well maintained roads, railways bado kuna suporting contractors etc.

Mkuu angalia nchi zote zilizoendelea, Germany, USA, Japan, Australia na sasa China none has done it without coal and iron ore. That is a fact ila u can choose to remain defiant.
 



Nyambala ndg yangu,
Are you there for Country first au? Tatizo ni kuwa watueleze ni kuna shughuli gani hapo tunduru na kama ni kweli uchimbaji wa siri upo we need an answer from the Government period kwani kuna activity hiyo ina mikataba au ni shagharabagala, Unajua wananchi sasa wameisha choka kwani serikali yao ina mambo mengi ya siri mno na ndio maana wameisha poteza uaminifu kwa kila serikali ikifanyacho.

Waziri / Naibu wake watupe details za hapo Tunduru period then waka resign effectively before end of this Assembly

Nadhani watu tunashindwa kuelewana, kwa grades za hapo Mkuju, Nyota huwezi kufanya mining iwe siri. Mnatakiwa mfahamu kwamba madini hayapatikani kama nuggets. Yamechanganyikana na udongo. Mfano unaweza kukuta tani 200 zina pound moja ya hiyo uranium ambayo bei yake ni $53, sasa ili upate faida inabidi uwe na huge machinery kama dump trucks, diggers, excavators u name it.

Bado kunatakiwa kuwe na process plant, kuwe na plan ya kudispose waste. You are talking of hundreds of million of dollars. Kuna mashine tairi yake tu ni kama milioni 40 za kibongo. Sasa nani yuko tayari kufanya upuuzi huo wa kurisk hela zake eti aje achimbe uranium kisirisiri. Tena mara nyingi ni hela watu wameraise from a stock market. Sasa hela za watu eti unachimbia uranium kisirisiri Tunduru-Tanzania, serious????? Logically hiyo haipo na narudia kusema tena confidently hiyo habari ni ya uongo period.

Naomba nieleweke sitetei wizi wa raslimali yeyote ile ya mtanzania ila hatuwezi kulinda raslimali zetu kwa fabrication ya stories wakati zile tunazoziona zikichukuliwa wazi wazi na kiwizi wizi tunafumbia macho.

Kingine watanzania tunatakiwa tuelewe hayo madini hayapo Tanzania tu, kuna nchi tayari infrastructure za kumwaga, unafungua kampuni siku moja, terms za mikataba zipo tayari wewe ni kuhakikisha unafuata taratibu,kumobilize na kuanza mzigo. Sasa sisi pamoja na hivyo virushwa bado ukiritimba, wizi, poor infrastructure.
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Mkuu Nyambala nashindwa kukuelewa unamanisha nini.
Kwamba ni sahihi wageni kuja na kuchimba bila utaratibu?
Kwamba kwa vile enriched uranium ndio yenye thamani kwa hiyo tuwaache wachime ili wakaenrich wao kwa vile hata Australia inafanya hivyo??
Kama hakuna barabara maana yake hakuna uchimbaji???? Kakola, Buhemba na Nyamongo kuna barabara za juu???

Ukituliza akili utaelewa context ya mtoa mada.
FYI, jana mbunge wa Bahi-Dodoma kalalamika the same thing. wananchi wameporwa ardhi kisa madini ya uranium.
Kwa upande mwingine mama Kaihula ni moja ya wamama wasomi sidhani kama amekurupuka


We jidanganye tuu.. wasomi ndio wakurupukaji wakubwa kuliko kada zote nchi hii( rejea maandishi ya bluu hapo juu)
 
jana mbunge wa viti maalim (chadema) naomi amy kaihula kasema kuwa kuna kampuni ya kimarekani inachomba uranium kisirisiri (clandestinely) katika wilaya ya tunduru .

Alisema kaona kwa macho yake uchimbaji ukiwa unaendelea. Sasa cha kujiuliza mbona hili hatuna habari nalo? Mkataba wake ulisainiwa lini? Environmental impact assessment ilifanywa na nani? Mkataba una worth how much? Serikali inapata kiasi gani?

Lakini sitoshangaa kusikia kama huu ulikuwa ni mchongo wa bilionea jairo na dumber mwenzie ngeleja.

Why keep it secret? Kwa nini wananchi hawajulishwi kinachoeendelea ndani ya maeneo yao? Hivi law & order iki break katika mazingira haya serikali itajibu nini?

Habari ndio hiyo
wanatunduru wanasemaje?kama wanafurahia vile?why hatujawasiki kama wenzao wa geita ?
 
Napenda Kujau Ngeleja kabla ya kuwa mbunge na kuwa waziri alikuwa akifanya kazi kwa nani, Company ya nani, Rostam, JK, EL, au Serikalini?

Najaribu kuja Uzalendo wake umeegemea wapi?
Legal advisor - vodacom ltd, Ambayo mwanahisa mkuu ni RA ambaye pia ndiye alikuwa chief kampenia wa CCM 1995.

Haya unga intelligencia yako hapo.
 
Jana mbunge wa viti maalim (CHADEMA) Naomi Amy Kaihula kasema kuwa kuna kampuni ya Kimarekani inachomba Uranium kisirisiri (clandestinely) katika wilaya ya Tunduru .

Alisema kaona kwa macho yake uchimbaji ukiwa unaendelea. Sasa cha kujiuliza mbona hili hatuna habari nalo? Mkataba wake ulisainiwa lini? environmental impact assessment ilifanywa na nani? Mkataba una worth how much? serikali inapata kiasi gani?

Lakini sitoshangaa kusikia kama huu ulikuwa ni mchongo wa BILIONEA Jairo na dumber mwenzie Ngeleja.

Why keep it secret? kwa nini wananchi hawajulishwi kinachoeendelea ndani ya maeneo yao? Hivi law & order iki break katika mazingira haya serikali itajibu nini?

Habari ndio hiyo

Hayo ndo matunda ya ziara za rais na tabasamu jing lilokuwepo wakati wa bush, Sio lazima ngeleja asaini
 
CCM lazima waondoke kwanza ndo tujipange upya maana bila CCM nothing is possible
 
Tutapiga makelele weeee ukweli ni kwamba uchimbaji unaendelea huko Tunduru. Kuna jamaa zangu walipewa tenda ya kupeleka malory yao (12 lof 18tons each kwenda kutengeneza barabara huko. Kuna airstrip kwenye hilo eneo, udongo rich in Uranium inajazwa kwenye plastic tanks zinaingizwa kwenye chopper zinaenda Nairobi/Uganda for shipment. Pia Hao jamaa waanaajiri watu kutokea Mikoa ya mbali unafanya kazi 3months unapumzika 3 months (unalipwa) after miezi 9 unalipwa haki zako unachapa lapa. Eneo la mradi liko very remote. chunguzeni zaidi mtafahamu
 
Mkuu hiyo uranium haina thamani kiasi hicho mpaka kampuni ya nje ya nchi irisk kuja kuchimba kisirisiri na after all lazima uelewe kuna masuala ya grade per ton. Jmani watanzania tunahitaji tuelimike kuhusu haya mambo sasa kama hata mbunge anaweza kuongea hii (kama ni kweli) basi tuna tatizo kubwa!!!!!! Uchimbaji industrialized si sawa na "uchoji" (uchimbaji wa sululu).

Uranuim yenye thamani kubwa ni ile enriched ambayo hata kuna baadhi ya nchi zilizoendelea kama Australia, Canada still wanauza raw (not enriched). Sasa mtu eti kwenda Tunduru ambako hata umeme hakuna, barabara ya lami hakuna, maji hakuna, reli hakuna halafu ikafanyika hiyo mining ya uranium is just a HOAX.
Jibu kinachofanyika ni nini?!!!
 
Tutapiga makelele weeee ukweli ni kwamba uchimbaji unaendelea huko Tunduru. Kuna jamaa zangu walipewa tenda ya kupeleka malory yao (12 lof 18tons each kwenda kutengeneza barabara huko. Kuna airstrip kwenye hilo eneo, udongo rich in Uranium inajazwa kwenye plastic tanks zinaingizwa kwenye chopper zinaenda Nairobi/Uganda for shipment. Pia Hao jamaa waanaajiri watu kutokea Mikoa ya mbali unafanya kazi 3months unapumzika 3 months (unalipwa) after miezi 9 unalipwa haki zako unachapa lapa. Eneo la mradi liko very remote. chunguzeni zaidi mtafahamu
Nyambala soma hapa!
 
CCM lazima waondoke kwanza ndo tujipange upya maana bila CCM nothing is possible
Hawawezi kuondoka kabla ya kukomba kila kitu.
Wanafahamu kila uluwa ulipo wataacha mahandaki yaliyochimbwa madini! makampuni yote ya umma yamekufa.
CHUKUA CHAKO MAPEMA in action.
tufanyeje hivi SASA ni suala muhimu!!!
 
Ni kweli wanachimba kuna mdogo wangu anafanya kazi huko na pia kuna uwanja wa ndege mkubwa mandege makubwa makubwa yanatua na kuondoka. Mi nafikiri tuendelee kutafuta source za ndani za uhakika.
 
Jana mbunge wa viti maalim (CHADEMA) Naomi Amy Kaihula kasema kuwa kuna kampuni ya Kimarekani inachomba Uranium kisirisiri (clandestinely) katika wilaya ya Tunduru . Alisema kaona kwa macho yake uchimbaji ukiwa unaendelea. Sasa cha kujiuliza mbona hili hatuna habari nalo? Mkataba wake ulisainiwa lini? environmental impact assessment ilifanywa na nani? Mkataba una worth how much? serikali inapata kiasi gani?Lakini sitoshangaa kusikia kama huu ulikuwa ni mchongo wa BILIONEA Jairo na dumber mwenzie Ngeleja.Why keep it secret? kwa nini wananchi hawajulishwi kinachoeendelea ndani ya maeneo yao? Hivi law & order iki break katika mazingira haya serikali itajibu nini?Habari ndio hiyo
tatizo ni mipango ndo hatuna na kingine kikifanyika kitu kama hicho utasikia kuna mkubwa yaani we acha tu nalia mbaya na maisha yetu watz..
 
Ni kweli wanachimba kuna mdogo wangu anafanya kazi huko na pia kuna uwanja wa ndege mkubwa mandege makubwa makubwa yanatua na kuondoka. Mi nafikiri tuendelee kutafuta source za ndani za uhakika.
inafaa hilo swala ungemuuliza zaidi huyo mdogo wako lazima atakuwa anajua zaid..
 
Ni kweli wanachimba kuna mdogo wangu anafanya kazi huko na pia kuna uwanja wa ndege mkubwa mandege makubwa makubwa yanatua na kuondoka. Mi nafikiri tuendelee kutafuta source za ndani za uhakika.
 
Tutapiga makelele weeee ukweli ni kwamba uchimbaji unaendelea huko Tunduru. Kuna jamaa zangu walipewa tenda ya kupeleka malory yao (12 lof 18tons each kwenda kutengeneza barabara huko. Kuna airstrip kwenye hilo eneo, udongo rich in Uranium inajazwa kwenye plastic tanks zinaingizwa kwenye chopper zinaenda Nairobi/Uganda for shipment. Pia Hao jamaa waanaajiri watu kutokea Mikoa ya mbali unafanya kazi 3months unapumzika 3 months (unalipwa) after miezi 9 unalipwa haki zako unachapa lapa. Eneo la mradi liko very remote. chunguzeni zaidi mtafahamu

Nyambala soma hapa!

Kionachofanyika ni utafiti (exploration). I too have friends wanaofanya kazi za geology huko........ Sasa tatizo watanzania wengi tunapenda ubishi mtu akiona rigger na sample zinatolewa na kupelekwa maabara tayari watu wanajua ni kuchimba. Wakuu ni vema kama mtu hufahamu jambo ukalifanyia reaserach au ukasikiliza kwa wanaojua. Cha kusikitisha ni kwamba ni hulka yetu watanzania kutokudili na facts as long as they don't please you.

udongo rich in Uranium inajazwa kwenye plastic tanks zinaingizwa kwenye chopper zinaenda Nairobi/Uganda for shipment

Sasa angalia habari kama hii, huko uganda au Kenya toka lini kuna maabara za kuassess uranium? Anywayz mimi naona huu mjadala muendelee wenyewe na stori za vijiweni ila tu muelewe JF is bigger than that!!!!!!!!!
 
Ni kweli wanachimba kuna mdogo wangu anafanya kazi huko na pia kuna uwanja wa ndege mkubwa mandege makubwa makubwa yanatua na kuondoka. Mi nafikiri tuendelee kutafuta source za ndani za uhakika.

Hii ndiyo haswaa the bongo way of sensitizing issues, mandege makubwa lakini hayatajwi make, model, size. Mkuu muulize huyo mdogo wako (kama anafanya kazi ya kitaalam lakini) kinachofanyika huko ni nini???
 
Back
Top Bottom