Siri nje kujisalimisha kwa anayedaiwa kumteka Dr. Ulimboka

yaaani wamefikria njia zoote wameamua kuja na hii,duuh tat^zo mfumo wa majeshi upo hovyo wanaajiri form 4 failure ndio maana m2 anashindwa hata kudanganya,ishu nyingine ni walivyopanga kumteka hawakupanga mpango wa matokeo ya utekaji ule so walipanga nusu ss wanaumbuka,nimeamini jeshin wanatakiwa waajiriwe wasomi!duuuuh
 
Kwa mawazo yangu ya Hangover, ni hivi.

Utekaji wa Dr. Umewapa wengi hasira, na wengi tumeulaani sana. Na mtekaji

Anajua kabisa kuwa jamii ina hasira nae sana.

Anajua kuwa polisi nao wanahasira nae sana mana kawafanya wao wabebe kesi (Kama kweli si wao)

Anajua Ikulu ina hasira nae sana kwa kuwabebesha kesi ( kama kweli hawahusiki)

Anajua serikali ina hasira nae sana kwa kuichonganisha na wananchi (kama kweli haihusiki)

Na anajua CCM pia ina hasira nae sana (kama hawahusiki).

Sasa huyo mtu najiuliza ana courage kiasi gani ya kujitokeza wazi wazi tena kienyeji bila kuomba Protection huku akijua kuwa tayari ana hao maadui tajwa hapo juu??

Sio ujasiri wa kawaida, najua mtasema kuwa amejisikia guilty sana. Ndio kama ni kweli ndio mhusika ingewezekana "guilty concious" kumtesa ila sio kumtuma alichofanya, zaidi huyu angejiua na kuacha waraka.


NIONAVYO MIMI.
Hii ni njia tu ya whoever anaehusika kufunika tracks zake, lakini ni so cheap and ya kitoto.

Huyu Mkenya sio.
(Hapa hapa JF ilishatabiriwa hii trick yao)
 
Hadithi yote hii ni ya kusadikika sana katika uhalisia.Imeandaliwa story itakayoleta maana ili mtu huyo aliyepandikizwa apotoshe ushahidi wa kweli. Jiulize;
1. Jambazi gani linaweza kwenda kanisani kujitambulisha kirahisi tu kuwa ndiye lililomtaka Dr. Ulimboka? Hii inahitaji mabadiliko ya kweli ya moyo na tabia ambayo yanaambatana na toba ya kweli na kujutia tabia...SIYO TUKIO MOJA TU!!
Angejikuta anamtafuta yule aliyemtendea na ku-make peace nae kabla hata ya kanisani.Na kama angeenda kanisani angependa iwe siri sana kwanza ili aweze kueleza yaliyotokea si kujipeleka kirahisirahisi na kuweka viashiria waziwazi.THIS IS FAKE!
2. Mbona hawakuonesha picha yake jana kama huyo mtu wamemwamini kama wanavyofanyaga katiika wahalifu wengine?
3.Kwa nini huyo raia wa kesha kitambulisho chake ni cha miaka 2 tu wakati ana umri mkubwa sana wa kuwa na kitsmbulisho cha muda mrefu nyuma?

MY TAKE: Kuna usanii katika hili na jeshi la Polisi wanatuingiza watanzania wote kuamini hili ndio maana wametoa taarifa harakaharaka.It doesnt look true!

Kinachoniudhi ni jinsi akili za watanzania zinavyofanywa kuwa viza kila na siku na vyombo vya usalama. Polisi waliwezaje kumfikisha huyo mtu mahakamani with story kama hiyo, inanikumbusha yuke Dumisani Dube, aliyemgonga marehemu Sokoine. Huu mchezo wa kuua watu haujaanza juzi, umeanza siku nyingi na wanapandikizwa watu wa kutoka nje, huyu mkenya kapandikizwa kama alivyopandikizwa Dumisani Dube aliyetokea ANC ya South Africa

Tangu lini jambazi, mwenye kikundi cha ujambazi, anayejihusisha na silaha, ajisalimishe kwa tukio kama la Ulimboka ambaye wala hajafa.Kama ni jambazi sugu, amefanya mangapi makubwa kabla, why atubu kwa hili tukio moja tu. Kama ni kujisalimisha, aliacha makanisa mangapi hadi aende hilo? mbona hakwenda polisi? Polisi sio vyema kuwafanya watanzania viazi kiasi hicho, it is shameful kwa nchi kama Tanzania kuwa na jeshi la polisi lenye kuwafanya watanzania wapumbavu
 
Sijawai sikia toka tarehe 7/5/1984 nazaliwa kuwa jambazi mtekaji eti ameenda pahala kumuulizia mtu haf akajitambulisha eti mi ndo nlimteka dr ulimboka hawa wabhungaji nao wasituzingue bhana
 
Yule mkenya anayedaiwa kumteka Dr. Ulimboka na kisha kujisalimisha kwa mchungaji Gwajima hakwenda kutubu. Katika mahojiano kati ya mtangazaji Rita Chiwalo na mmojawapo wa wachungaji wa kanisa la Ufufuo na Uzima (anaitwa Gwandu Mwangasa) , mtu huyo alifika jana kanisani hapo na kukutana na baadhi ya wachungaji akitaka apelekwe kuonana na mchungaji Gwajima. Wachungaji hao walikataa katakata kumruhusu mtu huyo mpaka pale atakapowaeleza sababu hasa ya kutaka kuonana na Mchungaji wao mkuu. Ndio mkenya yule alipodai kuwa anajambo la kumweleza mchungaji Gwajima kwa vile ndiye aliyemteka Dr. Ulimboka.

Baada ya kusikia hivyo wachungaji wale walistuka na kuamua kumkagua simu yake na kukuta ujumbe unaosema "nimefika lakini bado najaribu kuwazoea." Ni ujumbe huu ndio uliopelekea wachungaji wale kumtilia mashaka mtu yule na kumwona si wa kawaida hivyoo kuamua kumripoti polisi. Pia mtu huyu hakwenda kanisani pale kutubu zaidi ya kujitambulisha tu kuwa ndiye mtekaji. Ndipo wachungaji wale wakaona suala lile si la kikanisa tena bali la polisi.

Katika hatua nyingine mchungaji huyo ametoa onyo dhidi ya watu wanaofanya usanii makanisani kwa lengo la kufanikisha mipango ya makundi fulani. Ameonya dhidi ya dhihaka zinazofanywa katika nyumba za ibada kwa malengo binafsi na kuwa wanaofanya hivyo wanachuma laana. Amesisitiza kuwa ule ujumbe wa simu unaashiria mtu yule alikuwa na ajenda ya siri.

Ssource: WAPO radio FM.

My take... You be a judge!

siasa ni mchezo unaonuka..kwa harufu tu urfinished! But as for me,hmm mm sijisumbui kuiweka akilini coz hata kwenye nywele zimegoma! Nastygame..
 
Haiyaaaaa. Tutasikia mengi.
Nimeshangazwa Na jambazi sijui gaidi Sugu, limeenda kutubu tena kwa Mchungaji, wakati hawa wachungaji hawaamini katika kutubu kwa mtu. Ni wakatoliki tu ndio huenda kutubu kwa padri. Sasa la huyu kiboko.
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Huyo jamaa mkenya wala sio muhusika wa tukio nahisi. Tokea lini muhusika akaenda kujisalimisha kiulaini namna hiyo?. Huu ni mchezo ambao Usalama wa Taifa wamepanga kuucheza kwa nia ya kuficha kilichotokea na wahusika halisi wa tukio.


Ulichoandika ndio ukweli halisi......hakunaga mtu wa hivyo eti akajisalimishe wakati anajua fika kuwa amefanya jambo baya la kumdhuru mtu......yaani hili ni bonge la movie afu nzuri zaidi stelingi kesha kufa sasa halinogi tena.....labda Kova aje kivingine!
 
.........kweli nimeamini ni heri kuwa mfuasi wa shetani na wanae kuliko kuwa mfuasi wa CCM na serikali yake lol!!

wameshindwa hata ku-plan vizuri jinsi ya kujinasua kwenye mchezo mchafu walioufanya wenyewe, matokeo yake wanajikanyaga kanyaga kwa kutunga tukio la kitoto.
 
Kwanini kova hakuwasiliana na gwajima? Sasa anaumbuka

ina maana kule kwa gwajima waumini criminal wanaotubu hupelekwa polisi sio?
Kanisa lina kazi ya kujisafisha HUYU SELEMANI AMEAMUA KUMTUKANISHA YOHANA MBATIZAJI
 
Tokea Jana najidunga tursker lakini bado hazipandi sijui niende kigogo kwa mama muuza nikanywe ile Yao inayozima macho

Mkulu nakusihi kigogo don't try that at home!! njoo nikuonyeshe manywaji ya kuondoa uchafu wa kina kova akilini, wanaumbuka mwaka huu, hii serikali!! yaani that is the best they can do!???, aliyesema Jk anaangushwa na watendaji wake naanza kumuamini,maana yeye(jk) alishaanguka tayari siku nyingi sasa hawa nao kila wakijaribu kumnyanyua wanambwaga tena, duh! No wonder anapenda kwenda nje, hata ningekuwa mimi I cant stand to see the flaws of my government! SHAME ON ME!
 
Yule mkenya anayedaiwa kumteka Dr. Ulimboka na kisha kujisalimisha kwa mchungaji Gwajima hakwenda kutubu. Katika mahojiano kati ya mtangazaji Rita Chiwalo na mmojawapo wa wachungaji wa kanisa la Ufufuo na Uzima (anaitwa Gwandu Mwangasa) , mtu huyo alifika jana kanisani hapo na kukutana na baadhi ya wachungaji akitaka apelekwe kuonana na mchungaji Gwajima. Wachungaji hao walikataa katakata kumruhusu mtu huyo mpaka pale atakapowaeleza sababu hasa ya kutaka kuonana na Mchungaji wao mkuu. Ndio mkenya yule alipodai kuwa anajambo la kumweleza mchungaji Gwajima kwa vile ndiye aliyemteka Dr. Ulimboka.

Baada ya kusikia hivyo wachungaji wale walistuka na kuamua kumkagua simu yake na kukuta ujumbe unaosema "nimefika lakini bado najaribu kuwazoea." Ni ujumbe huu ndio uliopelekea wachungaji wale kumtilia mashaka mtu yule na kumwona si wa kawaida hivyoo kuamua kumripoti polisi. Pia mtu huyu hakwenda kanisani pale kutubu zaidi ya kujitambulisha tu kuwa ndiye mtekaji. Ndipo wachungaji wale wakaona suala lile si la kikanisa tena bali la polisi.

Katika hatua nyingine mchungaji huyo ametoa onyo dhidi ya watu wanaofanya usanii makanisani kwa lengo la kufanikisha mipango ya makundi fulani. Ameonya dhidi ya dhihaka zinazofanywa katika nyumba za ibada kwa malengo binafsi na kuwa wanaofanya hivyo wanachuma laana. Amesisitiza kuwa ule ujumbe wa simu unaashiria mtu yule alikuwa na ajenda ya siri.

Ssource: WAPO radio FM.

My take... You be a judge!

Natamani sana kwenda kusali kwa gwajima kesho...najua lazima awapige madongo ya kweli
 
Wana Jf hivi huyu Prezdaa amewahi kutoa tamko lolote khs shutuma zinazotolewa dhidi ya serikali yake kuhusiana na matukio yanayoambatana na kutekwa kwa Dr. Ulimboka? Hivi si ndio viashiria vya wazi wazi vinavyo onyesha kwamba kumbe inawezekana hata wakati Dr. Ulimboka yuko katika mateso usiku ule Rais JK alikuwa anajua kilichokuwa kinaendelea? After 2015 huyu prezdaa anatakiwa aonje joto ya Segerea..
 
Sijawai sikia toka tarehe 7/5/1984 nazaliwa kuwa jambazi mtekaji eti ameenda pahala kumuulizia mtu haf akajitambulisha eti mi ndo nlimteka dr ulimboka hawa wabhungaji nao wasituzingue bhana

Laiti ungelimsikia mchungaji huyu. Amelaani vikali kitendo hicho. Inavyoonekana picha ilichezwa bila kumshirikisha Gwajima.
 
Huo ni mchezo2 haiwezekani muhusika kujitokeza kirahisi hvyo kwn alishindwa kwenda kutubia kwao,apo ni njama2 za serikali anahukumiwa miaka kumi na k2 hv anafungwa mi2 badae anapotea zake na dau nono...
 
Tetesi ni kuwa, ripoti iliandaliwa kabla ya utekaji, ambapo siku 3 baada ya kutoonekana kwa Uli, mwili wake ukiwaumeanza kuoza ungekutwa huko Magwepande ambapo uchunguzi wa kiitelijensia ungeanza mara moja na kuja na iyo ripoti. Bahati nzuri Mungu alikua upande wetu, dr hakufa, kuonyesha Mungu bado anatupigania, akawasahaulisha akina Kova na kenge lake, wakashindwa ku-edit ripoti.
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom