Siri mpya EPA: Vigogo BoT waliamua 'kufa na mafisadi'

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
802
Siri mpya EPA:Vigogo BoT waliamua 'kufa na mafisadi'

*Benki 3 ziligoma kulipa,Balali akalazimisha
*Barclays ilijivua lawama, ikarejesha fedha
*Benki zilizohusika na ufisadi sasa zajitetea


Na Waandishi Wetu

MKAKATI mpana, uliotumika kuhakikisha kampuni tata ya Richmond isiyokuwa na uwezo wala rekodi yoyote katika sekta ya nishati popote duniani, inashinda zabuni ya mabilioni ya kufua umeme wa dharura nchini huku ikibebwa na vigogo Serikalini, Majira Jumapili leo linawathibitishia Watanzania kuwa ulitumika pia katika uchotaji wa sh. bilioni 133 kwenye akaunti ya EPA ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Siri hizo mpya kutoka vyanzo vya ndani vinavyofahamu yaliyoendelea wakati wa mchakato wa kuchotwa fedha hizo na nyaraka nzito ambazo gazeti hili limezinasa wiki hii, kwa pamoja zinazidi kuonesha jinsi utendaji wa aliyekuwa Gavana wa Benki hiyo, Dkt. Daud Balali ambaye Serikali wiki hii ilisema muda utakapofika, ikimtaka, itamkamata, ulivyokuwa na shaka

Kwa mujibu wa nyaraka hizo jumla ya benki 10 za hapa nchini ndizo zilizothibitika kutumiwa na waliochota fedha hizo ambapo kwanza walifungua akaunti za haraka haraka na za dharura na kisha ndipo katika hali iliyozishangaza nyingi kati ya benki hizo, BoT ikaingiza malipo ya mabilioni kupitia akaunti hizo.

Benki hizo na kiasi cha fedha zilizopitishwa kutoka BoT kikiwa kwenye mabano ni Bank of Baroda (T) Ltd (sh. 5,912,901,644), Barclays Bank of Tanzania Limited (sh. 1,548,897,757), CRDB Bank Limited (sh. 35,968,182,854), Diamond Trust Bank Limited (sh. 2,381,529,339) na Eurafrican Bank (T) Limited (6,300,402,225).

Benki nyingine ulikopitishwa mgao huo ni Exim Bank (T) Limited (sh. 2,225,035,393), Kenya Commercial Bank (Tanzania) Limited (sh. 18,188,468,486), NBC Limited (sh. 3,931,766,300), Standard Chartered Bank Tanzania Limited (sh. 48,350,913,759) na United Bank of Africa Limited (UBA) ambako zilipitishwa sh. 8,207,088,464.

Kutokana na kiwango hicho kikubwa kuingizwa kwenye akaunti za benki hizo, benki tatu kati ya 10 ambazo ni Barclays, Kenya Commercial Bank na Standard Chartered zilitushwa na hali hiyo hivyo zikafuata matakwa ya sheria kwa kutilia shaka fedha hizo kwa kutaka maelezo ya uthibitisho kutoka BoT.

Barua ya Novemba 2, 2005 ya benki ya Barclays ilijibiwa haraka na BoT iliyothibitisha na kuhakikisha pasi na shaka kuwa fedha hizo walikuwa wakizitambua na ni halali.

"Pamoja na uthibitisho huo kutoka BoT, Barclays iliamua kuzirejesha BoT fedha hizo na kisha ikaamua kufunga akaunti hiyo ya mteja wake huyo mpya," kimedokeza chanzo chetu. Haijafahamika mara moja baada ya Barclays kurejesha fedha hizo kiasi cha sh. bilioni 1.5 na kuifunga akaunti hiyo, zilikwenda kupitishiwa wapi?

Benki ya Kenya Commercial, kama ilivyokuwa kwa Barclays, ilistushwa na kiwango cha fedha ambacho mteja wake mpya alikuwa ameingiziwa kutoka BoT nayo ikaandika barua kuhoji uhalali wa fedha hizo kiasi cha sh. bilioni 18.

Kwa mujibu wa barua yao yenye kumbukumbu namba KCBTZ/MD/01/37 kwenda Kitengo cha Uchunguzi wa Fedha cha BoT, benki hiyo ilitaka kujua uhalali wa fedha hizo na walijibiwa kuwa ni halali, hazina matatizo.

Huku wakivunja matakwa ya kisheria kwa mujibu wa sheria ya Taasisi na Vyombo vya Fedha (The Banking and Financial Institution Act, 2006) watendaji wakuu wa BoT wakiongozwa na Dkt. Daud Balali aliyekuwa akijua kila kilichokuwa kikiendelea, kwa staili ile ile ya Richmond walionekana 'kuwa tayari kufa' wakihahakisha kampuni mahsusi zilizoteuliwa, zilikipata kila zilichokuwa zikikitaka kutoka akaunti ya EPA.

Vyanzo hivyo vinazidi kubainisha kuwa baada ya uchunguzi wa baadaye wa kina kubainisha kuwa malipo hayo yalikuwa yana utata, aliyekuwa Dkt. Balali katika vikao viwili vizito, alipobanwa, kwanza alizikingia kifua fedha hizo kuwa zililipwa kihalali lakini baadaye alipoona mambo yanakuwa mamgumu, alimsukumia mzigo aliyekuwa Waziri wa Fedha, Bibi Zakia Meghji kuwa ndiye aliyekuwa akijua kila kitu kuhusu fedha hizo.

Sheria ya Benki Kuu (The Bank of Tanzania Act, 2006) inaipa majukumu BoT kuwa msimamizi wa mabenki mengine na inayataka mabenki yatoe taarifa yanapobaini kuwepo fedha zenye utata.

Kubainika kuwa hata pale ilipoulizwa kuhusu utata wa malipo hayo, BoT iliyatetea, wanasema wataalamu wa masuala ya utawala, ni anguko kuu la kiutendaji kwa Serikali iliyoko madarakani ya CCM.

"Timu ya ukaguzi ilikosa ushahidi wa Kitengo cha Uchunguzi wa Fedha cha BoT kama kilifanya uchunguzi wowote kilipopewa taarifa za malipo yasiyo halali.Hata tulipokutana na kujadiliana na Dkt. Balali, hakuonesha kutaka kulishughulikia suala hili.

"Pia timu ya ukaguzi ilishangazwa na namna viongozi wa BoT walivyokuwa wakichukua muda mrefu kujibu au kushughulikia masuala yote yaliyoonekana kuwa yenye utata kwenye akaunti ya EPA," kilisema chanzo chetu.

Malipo hayo ambayo jumla yake ni takribani sh. bilioni 133 yalilipwa kwenye benki hizo kati ya mwaka 2005/2006 huku yakihusishwa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, baadhi ya taarifa zikieleza kuwa zilitumika kwenye kampuni za ubinge na urais.

Hata hivyo viongozi waandamizi karibu wote wa CCM wa sasa na waliostaafu, waliwahi kuliambia gazeti hili kuwa chama hicho kina vyanzo vya kujitosheleza kuendesha uchaguzi na kamwe hawakufaidika na fedha hizo kama inavyodaiwa.

Kutokana na staili hiyo ya BoT kukiuka majukumu yake ya msingi, hivi sasa, Majira Jumapili limebaini, benki zote zilizohusika katika sakata hili, zimepata utetezi wenye nguvu.

Maofisa waandamizi wa baadhi ya benki hizo walipoulizwa wiki hii kuhusu benki zao kuhusika katika upitishaji wa fedha za EPA waliitupia lawama nzito BoT yenyewe kuwa ndiyo tatizo si wao.

Hoja yao kuu ya kwanza katika kujivua lawama, wanasema kwamba isingekuwa jambo rahisi kwao kuzitilia shaka fedha hizo hasa kwa kuzingatia zilitoka BoT ambao ndio wasimamizi wakuu wa mabenki yote ya nchini.

Mmoja wa maofisa waandamizi wa CRDB aliyezungumza na gazeti hili kwa sharti ya kutotajwa jina lake kwa sababu si msemaji, alisema inawezekana benki zilizokataa kupokea fedha hizo zilipata tetesi kuhusiana na utata wake, zikajitoa matatizoni mapema.

"Sisi isingekuwa rahisi kuweza kuzishtukia kwa sababu zilitoka BoT ambao ndio wasimamizi wa shughuli zote za kibenki," alisema na kuongeza:

"Isingewezekana kuzikataa wakati zimetoka kwa mtu anayekusimamia na badala yake kuanza kumuuliza kama zina usalama."

Chanzo hicho kilieleza zaidi kuwa hata hivyo mtu akienda benki kuweka fedha hata kama zinatiliwa shaka, inabidi akubaliwe ziwekwe kwanza kwenye akaunti ndipo baadaye ufuatiliaji ufanyike BoT ili kujua kama si batili.

Alisema ikifanyika kinyume na hivyo mteja aliyepeleka fedha zake benki na kukataliwa anaweza kuishitaki benki husika, akidai ametuhumiwa kwa wizi.

Maofisa wa benki ya Exim nao walipoulizwa walisisitiza kuwa pia kwao ingekuwa ngumu kwa sababu ya uaminifu walionao kwa BoT.

"Wewe unachouliza hapa ni sawa na kumpa mtoto wako fedha lakini badala ya kuzipokea anaanza kukuuliza ulipozipata," kilidokeza chanzo chetu cha habari na kuongeza: "Baba ndiye anayepaswa kumuuliza mtoto amezipata wapi kama amezitilia shaka na si vinginevyo."

Ofisa Habari wa Benki ya NBC, Bi. Nector Pendaeli Foya naye alipoulizwa ili kutoa msimamo wa benki yake, alijibu: "Suala hilo siwezi kulizungumzia mimi, hebu nipe namba zako za simu nitakuunganisha na msemaji mkuu aweze kukujibu." Hadi tunakwenda mitamboni bado viongozi wa benki hiyo hawakuwa katika nafasi nzuri ya kulizungumzia suala hilo.

Source: Majira
tanzania-epa-report.pdf
 
Sheria zipo, tatizo ni watu. Watu wetu karibu wote ni mafisadi, kuanzia juu mpaka chini.

Laiti kila mtu angelikuwa anafuata sheria zilizopo, mafisadi wangepata shida sana kutekeleza ufisadi wao.

Bahati mbaya fisadi akitanguliza pesa basi anapokelewa kama shujaa mpaka makanisani na kwenye misikiti.

Ukisoma ya Chenge na Lowassa kupokelewa kama mashujaa, inaonyesha jinsi Watanzania karibu wote tulivyopoteza maadili. Watu siku hizi wanalalamika sio kwasababu wao ni clean, bali kwasababu ulaji huo hauwahusu, umewapita pembeni.

Ufisadi utashindwa pale tu ambapo kila mmoja wetu atauchukia kwa nguvu zote hata kama unatendwa na baba zetu au mama zetu.
 
sijui twawezaje kuzituhumu hizi bank, kwani wao hawarusiwi kujua mteja wao kazitoa wapi pesa, kazi yao ni kutunza tu, na hata kama walijua wangekuwa wazito kuzuia kwani hili liligusa serikali kuu, na viongozi wakuu wa kiserikali na kisiasa.
 
Sheria zipo, tatizo ni watu. Watu wetu karibu wote ni mafisadi, kuanzia juu mpaka chini.

Laiti kila mtu angelikuwa anafuata sheria zilizopo, mafisadi wangepata shida sana kutekeleza ufisadi wao.

Bahati mbaya fisadi akitanguliza pesa basi anapokelewa kama shujaa mpaka makanisani na kwenye misikiti.

Ukisoma ya Chenge na Lowassa kupokelewa kama mashujaa, inaonyesha jinsi Watanzania karibu wote tulivyopoteza maadili. Watu siku hizi wanalalamika sio kwasababu wao ni clean, bali kwasababu ulaji huo hauwahusu, umewapita pembeni.

Ufisadi utashindwa pale tu ambapo kila mmoja wetu atauchukia kwa nguvu zote hata kama unatendwa na baba zetu au mama zetu.




Nilisikitika sana kuona Lowasa alipokelewa mpaka na askofu mkuu Laiser!!! Fisadi anapokelewa na askofu mwenye waumini mamilioni wenye njaa kali, inaonekana viongozi wa dini huenda wananufaika na pesa za ufisadi kwa njia moja au nyingine ndo maana hata haya mambo hawakemei yanapotokea
 
sijui twawezaje kuzituhumu hizi bank, kwani wao hawarusiwi kujua mteja wao kazitoa wapi pesa, kazi yao ni kutunza tu, na hata kama walijua wangekuwa wazito kuzuia kwani hili liligusa serikali kuu, na viongozi wakuu wa kiserikali na kisiasa.

Isayamwita,

Bank wanaruhusiwa na wana wajibu wa kuwa na wasiwasi pale ambapo mapesa mengi yanaingia bila hata kujulikana yanatoka wapi na kwa lengo gani.

Mteja leo anafungua account, baada ya wiki anaingiza bilioni, kama bank lazima ushutuke. Vinginevyo hata akina Osama watapitisha pesa zao kwenye mabank yetu.

CRDB na hao wengine, laiti wangefuata sheria, huenda nao wangelazimika kufuatilia na kuuliza kama zilivyofanya hizo bank tatu.

Ingelikuwa kwa hawa wenzetu huku Ulaya, wanakuingizia hizo pesa na hapo hapo wanawajulisha polisi ili wafanye uchunguzi.
 
wasi wasi ulitokea, lakini balali akazima soo kiaina.
serikali tunawaambieni, tunamtaka balali aje ajibu shutuma hizi. kesi ya EPA bila ya balali ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa tu, hatuwezi kupata jawabu lolote la maana
 
Ufisadi na Benki Kuu... Ukistaajabu ya Musa ....

Inasikitisha kuona pale taasisi kama Benki kuu ambayo ndiyo mhimili wa uchumi inapoamua kupiga mbizi ktk kuutetea na kuurutubisha ufisadi.

Gavana wa benki kuu alipokuwa Uingereza ktk lile kongamano lililoandaliwa siku kadhaa zilizopita hakusema lolote kuhusiana na mikakati iliyopo kuhusu kuudhibiti ufisadi usitokee tena.
'Mkuu Kitila'ulimkoma nyani hadharani na kwa hili ulionyesha ujasiri wa hali ya juu.'Keep it up'

Inaeleweka kwamba Gavana alikuwa na maada aliyoandaliwa kuwasilisha lakini hiyo haifuti ukweli kwamba watu wamepoteza imani na benki kuu na vyombo vya fedha kwa ujumla wake maana benki kuu ndio benki mama.

Watu wanapopoteza imani na benki kuu maana yake ni kwamba pia wamepoteza imani na uchumi mzima unavyoendeshwa!! Hii ni HATARI.

''Nchi zenye uchumi mbovu, mara nyingi pia husababishwa na mfumo mbovu wa kibenki na vyombo vya fedha''(Author Unknown).

Alichotakiwa kukifanya gavana ni kutupa 'Assurance' maana ile public trust au confidence iliyokuwapo imekuwa 'eroded' dhidi ya benki kuu na uchumi wetu kwa ujumla.

Kama wameshindwa hata kulinda kile 'kihenga' chetu (Benki kuu) vipi tuwaamini kwamba wanao 'udhu' wa kulinda rasilimali zetu zingine ndani ya nchi.

EE Mungu tunakulilia utulinde dhidi ya mafisadi na vitimbi vyao, nasi tujipange kupambana nao. Hata kijiko kibebwe twendeni tukapambane. Kila mwenye silaha na aibebe....

Tafakari
 
Ufisadi na Benki Kuu... nasi tujipange kupambana nao. Hata kijiko kibebwe twendeni tukapambane. Kila mwenye silaha na aibebe....

Tafakari
Once again this is a clear declaration of WAR AGAINST GRAND CORRUPTION and Marauding.
To paraphrase Mwalimu;
Sababu tunayo,
Uwezo tunao,
Nia tu...?,=
Count me in the army, lets seriously strategize, let kumkoma nyani verbally do its work, let propaganda play its role, meanwhile the Infantry matches on, right in the bettle field!!!!
 
Nilisikitika sana kuona Lowasa alipokelewa mpaka na askofu mkuu Laiser!!! Fisadi anapokelewa na askofu mwenye waumini mamilioni wenye njaa kali, inaonekana viongozi wa dini huenda wananufaika na pesa za ufisadi kwa njia moja au nyingine ndo maana hata haya mambo hawakemei yanapotokea

Mwanakijiji alipowashukia hawa wanaoitwa maaskofu na viongozi wa dini watu walimuona shetani. Lakini ukweli ni kwamba hawa Viongozi wa dini ni kundi mojawapo linalowakumbatia hawa MAAFISADI kutokana na michango yao makanisani. Hawana wanachokemea kwenye ibada zaidi ya kusisitiza matoleo ili kuhahakikisha mlo wao unaongeza pamoja na pesa za kuiba. Wengi wao ni wezi tu wa pesa za waumini masikini.

Kwa mtindo huu wa nyeti kama hizi mpaka kitaeleweka tu.
 
Fedha za EPA na uchaguzi wa CCM wa mwaka 2005 ni sawa na mgonjwa na uji. Sasa utamfunga nani wakati kila mtu ukimuuliza anasema mimi nilipeleka kwenye uchaguzi?

I don't see how CCM is going to defend it.

Mabank ya Tanzania yanaongozwa na vilaza wasio jua nini maana ya neno sheria. Huwezi kuamini Bank kama CRDB inashindwa kupuliza filimbi katika swala la money laundering kama hili.
 
Mmh...kweli Danganyika Ouzo Mtupu!!hivi Unadhani Mafisadi Walivyokua Wanachonga Hiyo Mikataba Feki Hawakujua Kuna Siku Jogoo Atawika Kila Mtu Ataamkia Upande Wake?
Sishangai Kuona Jinsi Sirikali Inavyomkumbutia Balali Bila Kutupa Sababu Za Muhimu,sirikali Inaendeshwa Kimabavu,umafia Wazi Wazi.
Naamini Hata Wakimrudisha Balal Hakuna Kitakachofanyika Zaidi Ya Porojo Zao Za Kila Siku,uzuri Wamechaguana Wote Wapenda Soga
 
Anyangumi Sio Viongozi Wote Wa Dini Wanaoshirikiana Na Mafiisadi ...hao Ni Maaskofu Njaa Kama Wakina Laizer Kufikia Kuongea Ujinga....
Kama Kuna Hawa Baadhi Waliweka Misimamo Yao

kakobe:::mafisadi Wote Lazima Walipe Pesa Zetu Na Kufikishwa Mahakamani Kwa Kuwaibia Watanzania...

askofu Pengo::::kila Alieshiri Kwenye Ufisadi Mkono Wa Sheria Umdondokee....

askofu Laizer....
Hawa Watu Wanataka Kuendelleza Ukabila Na Mwisho Wake Ni Mbaya Sana....hapa Kazi Ipo

So Utaona Ni Wachungaji Na Maaskofu Wachache Wenye Njaa Ndio Wanaongea Ovyo Kama askofu Laizer Anategemea Hela Za El Kwanini Asimsafishe Jamani...

bwana Utuhurumie

kristo Utuhurumie
 
Sheria zipo, tatizo ni watu. Watu wetu karibu wote ni mafisadi, kuanzia juu mpaka chini.

Laiti kila mtu angelikuwa anafuata sheria zilizopo, mafisadi wangepata shida sana kutekeleza ufisadi wao.

Bahati mbaya fisadi akitanguliza pesa basi anapokelewa kama shujaa mpaka makanisani na kwenye misikiti.

Ukisoma ya Chenge na Lowassa kupokelewa kama mashujaa, inaonyesha jinsi Watanzania karibu wote tulivyopoteza maadili. Watu siku hizi wanalalamika sio kwasababu wao ni clean, bali kwasababu ulaji huo hauwahusu, umewapita pembeni.

Ufisadi utashindwa pale tu ambapo kila mmoja wetu atauchukia kwa nguvu zote hata kama unatendwa na baba zetu au mama zetu.

Kwa kweli Watanzania tunatakiwa kuwa wakereketwa sana wa nchi yetu. Kumpa kichwa mwizi ni kujichanganya sisi wenyewe, sidhani kama walikuwa wanataka kumuona alivyo maana ni mbunge wao. Solution sasa iwe ni kuwasusa hawa mafisadi kila wanapoitisha mikutano.
 
CCM hawawezi kumuacha Balali arudi ndani ya nchi hii kwani atawaumbua sana na ndo maana wanasisitiza hawajamuitaji, hivi huu uchunguzi utakamilika vipi kama Balali hakuojiwa?

Hii issue ya EPA inamuingiza pia mke wa mkapa, kubwa la mafisadi Mama Anna mkapa ndo maana wanajaribu kumpunguzia mkapa skendo kwa kuficha kinachoendelea kwenye uchunguzi.
 
Mimi Ninamsubiriaa Sana El Nimyuone Ataanzaje Na Term Mpya Inakujua?ataomba Tena Ubunge Au Atarudije Kilingeni??ndio Hapo Ninapomsubiria..nimuonee.........na Nione Wa Tz Wata React Vipi...maana Nasisi Kwelii Bongo Lala...........
 
[
Huku wakivunja matakwa ya kisheria kwa mujibu wa sheria ya Taasisi na Vyombo vya Fedha (The Banking and Financial Institution Act, 2006) watendaji wakuu wa BoT wakiongozwa na Dkt. Daud Balali aliyekuwa akijua kila kilichokuwa kikiendelea, kwa staili ile ile ya Richmond walionekana 'kuwa tayari kufa' wakihahakisha kampuni mahsusi zilizoteuliwa, zilikipata kila zilichokuwa zikikitaka kutoka akaunti ya EPA. Sheria ya Benki Kuu (The Bank of Tanzania Act, 2006) inaipa majukumu BoT kuwa msimamizi wa mabenki mengine na inayataka mabenki yatoe taarifa yanapobaini kuwepo fedha zenye utata. Kubainika kuwa hata pale ilipoulizwa kuhusu utata wa malipo hayo, BoT iliyatetea, wanasema wataalamu wa masuala ya utawala, ni anguko kuu la kiutendaji kwa Serikali iliyoko madarakani ya CCM.




Huu ndio ujinga wa mwafrika tuliosema wiki iliyopita!

Siyo Balali tu wa kuhukumiwa bali watendaji wote wa BOT na wizara yote ya fedha kwa makusudi walipitisha hili na wanastahili adhabu wote.
Hizi issue za pesa zenye utata si mpya Tanzania.

Nakumbuka mwaka 2003 BOT waligandisha zaidi ya billion 20 zilizotoka kisiwa cha Cyprus zilizotumwa kwa kikundi cha dini cha jiji DAR kiitwacho House of Prayer Reformation church,Tena vyombo vya polisi(ofisi ya DCI ) walilishughulikia hilo jambo kwa bidii kweli walimhoji mara nyingi sana yule Askofu Mhozya.

Kwa hili hamna wa kujitetea hakufahamu.Kuanzia Mr clean,JK,iwe BOT wala vyombo vya usalama.Huu wote ni ujinga wa mwafrika
 
Kuna haja ya kuanzisha usalama wa taifa wenye nia halisi ya kulinda masilahi ya taifa la sivyo kuna vita kubwa inakuja tanzania kati ya wanatanzania wenye uchungu na mafisadi hawa wasio na haya hata kidogo.
 
Anyangumi Sio Viongozi Wote Wa Dini Wanaoshirikiana Na Mafiisadi ...hao Ni Maaskofu Njaa Kama Wakina Laizer Kufikia Kuongea Ujinga....
Kama Kuna Hawa Baadhi Waliweka Misimamo Yao

kakobe:::mafisadi Wote Lazima Walipe Pesa Zetu Na Kufikishwa Mahakamani Kwa Kuwaibia Watanzania...

askofu Pengo::::kila Alieshiri Kwenye Ufisadi Mkono Wa Sheria Umdondokee....

askofu Laizer....
Hawa Watu Wanataka Kuendelleza Ukabila Na Mwisho Wake Ni Mbaya Sana....hapa Kazi Ipo

So Utaona Ni Wachungaji Na Maaskofu Wachache Wenye Njaa Ndio Wanaongea Ovyo Kama askofu Laizer Anategemea Hela Za El Kwanini Asimsafishe Jamani...

bwana Utuhurumie

kristo Utuhurumie


Kweli inasikitisha jinsi kiongozi wa dini wa wadhifa wa Askofu (Laizer) alivyokubali kuwa mshirika katika hekaheka za kisiasa. Alipaswa kusoma upepo kwanza ili kujua kondoo wake wengi wako upande gani, upande wa MAFISADI au upande wa UZALENDO wa kupambana na kuukemea ufisadi. Kwa elimu na upeo wake alipaswa kujua kuwa kondoo wake wako upande wa UZALENDO. Tatizo anasumbuliwa na NJAA ya pesa bila jasho (kamanyola)!!!! Mwenyezi Mungu uibariki Tanzania na ushushe miujiza yako MAFISADI wazidi kuumbuka mchana kweupe. Twasubiri bunge la BAJETI ambapo yai la EPA litanguliwa na mafisadi wataumbuka na kuaabika zaidi!! Amen!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom