Siri kubwa kuliko zote kuhusu dunia yetu tambarare

JE Dunia ina umbo gani?


  • Total voters
    520
Mfano wako ndio mifano tuliyoaminishwa, coz hakuna aliyewahi kuthibitisha hilo la ukieleekea upande mmoja mnyoofu utatokea palepale, na wanapenda kutumia east na west vp kuhusu noth na south, je ukieleekea upande wa kusini ktk muelekea mnyoofu utatokea palepale?

Unaweza kututhibitishia juu ni wapi!? Ni kwanini wanaoendaga anga za mbali wanaeleekea angani na si east au west noth au south?

Mkuu usiseme tumeaminishwa.Ukianza kuwa na majibu ya hivyo na mimi ntasema umeaminishwa hivyo unavyosema.I am giving you facts.

Nnaanza kupata wasiwasi zaidi dhidi ya utafiti wako baada ya kuniambia kuwa hamna proof ya kuizunguka dunia from east to west.Je, unajua kuna flights from US zinahead west (mostly via polar norths for economical reasons)to reach Asia na wakati huo huo zipo flights zinahead east to reach Asia?This proves my point.
 
Mkuu usiseme tumeaminishwa.Ukianza kuwa na majibu ya hivyo na mimi ntasema umeaminishwa hivyo unavyosema.I am giving you facts.

Nnaanza kupata wasiwasi zaidi dhidi ya utafiti wako baada ya kuniambia kuwa hamna proof ya kuizunguka dunia from east to west.Je, unajua kuna flights from US zinahead west (mostly via polar norths for economical reasons)to reach Asia na wakati huo huo zipo flights zinahead east to reach Asia?This proves my point.
11263150_10153276907990575_2304405093164514023_n.jpg
U5dr4b3wV2zZzfCW2Gvfh9R15UwCH5c_1680x8400.png
 
Archaic conceptions without mathematical proof....ipo theoretical zaidi bro, mathematics is the language which doesn't lie so ukija na mathematical equations to proof your theory ntakuunga mkono....by the way it is conspiracy theory..
 
Mfano wako ndio mifano tuliyoaminishwa, coz hakuna aliyewahi kuthibitisha hilo la ukieleekea upande mmoja mnyoofu utatokea palepale, na wanapenda kutumia east na west vp kuhusu noth na south, je ukieleekea upande wa kusini ktk muelekea mnyoofu utatokea palepale?

Unaweza kututhibitishia juu ni wapi!? Ni kwanini wanaoendaga anga za mbali wanaeleekea angani na si east au west noth au south?
Mkuu hasa wakienda pande hizo si wanajiongea umbali kutokana na point waliyopo ni rhi wao kuelekea up ndio maana wanasayansi wa japan nao wakitaka kwenda angana wanaeleka upward hawaji kwenye point waliyoondokea wamarekani.
 
Tatizo umejiandaa kubishana wakati uzi haumlazimishi mtu kuuamini bali unakupa fursa yakutafakari ukweli ni upi na ukiona ni uongo basi amin ukweli uuaminio. Tunaoamini ni flat wengi tumeisoma dunia mviringo kama wewe yaani tuna habari nayo na mpaka ushahidi wa mviringo wake, upatikanaji wa majira kuzama na kuchomoza kwa jua, kupatwa kwa jua na mwezi mpaka mizunguko ya dunia yenyewe kulizunguka jua kujizungusha nk... Hivyo vyote tumejifunza shuleni it keans kabla ya shule tulikua hatujui dunia ikoje au sisi tupo wapi na sidhani kama ulikua unaweza kuamini kua dunia ni mviringo na sisi tumo juu yakenna kuna wakati tunakua kichwa chini miguu juu... Ila kupitia mafunzo darasani tukaoneshwa na picha, video za dunia yetu basi kuanzia hapontukaamini tupo ktk dunia duara mviringo.

Sasa basi, hivyo vyoooote vinavyosapoti uduara mviringo wa. Dunia, vimepingwa kwa hoja baada ya hoja na hadi evidence ya namana dunia ilivyo flat yaani duara tambarare, na jua na mwezi vikizunguka juu yake.

Hivi ni mjinga gani wa kisayansi awezae kupinga hoja bila hoja, yaani akwambie dunia sio mviringo ni flat bila kukupa hoja kua ni flat.? Hivyo basi usilazimishe kuelewa wewe mwenyewe kabla ya anayekujuza hajamaliza kukuelewesha yaani kama kweli unataka kupinga hoja ya dunia kuwa ni flat, inakubidi upoteze muda kweli kuisoma hiyo dunia flat kama ulivyoisoma duara kisha linganisha hoja ya huku na huku juu ya suala moja. Hapa na maanisha, ukitaka kujua kwenye flat earth usiku na mchana tunaupataje, anza kuusoma huu uzi wote mpaka ya wachangiaji maana wapo waliouliza na wakajibiwa vizuri tuu. Au kama vp tembelea youtube au google "day and night flat earth" na ukiona je itakufanya uamini?

Vitu vingi tunafundishwa kwa theory ndio maana mwalimu wa kwanza huwa anaaminiwa sana, maana hakuna hata mmoja wa kuthibitisha uduara wa dunia kwa kuuona yeye mwenye zaidi ya picha na video za NASA!

Kuhusu kuwa angani na kuuona uduara wa dunia wala sio uthibitishonwa uduara huo! Maana ukitaka kuuona hata ukiwa ardhini unaweza kuuona tena vizuri tuu ila sio kwa macho yako bali kwa msaadabwa lenzi mbinuko kama inayopatikana ktk vioo vya ndege na camera nyingi... Tafuta lens ya fish eye, hata ukiwa ardhini dunia itaonekana duara vp usipoitumia mbona uduara unapotea? Kwahiyo mkweli macho yetu au lenzi?

Uzi huu ni elimu kama masomo mengine ila haipo ktk mitaala yetu tuu, laiti kama utawafundisha wasio na habari ya dunia ni duara kama mpira, basi unaweza kukesha nao kuwaambia dunia sio duara flat, so ile elimu ya mwanzo ndio iwanyimao tafakuri watu wengi na hasa waaminio walitokana na Nyani!

mkuu je kivuli cha duara kwenye kupata kwa mwezi kinasababishwa na nini? pili kwanini sayari zote angani ziwe za duara dunia pekee iwe tambarare tatua je kwa dunia tambarare kupata kwa mwezi kunatokeaje
 
Ingekuwa tambarare tusingepata usiku na mchana, kuhusu uduara wa dunia vipi picha live zinazopigwa ISS na zile za voyager 1 na 2 na bado satellite kibao zinaonyesha uduara wa dunia
Ndio,duara flat!
 
Mkuu hasa wakienda pande hizo si wanajiongea umbali kutokana na point waliyopo ni rhi wao kuelekea up ndio maana wanasayansi wa japan nao wakitaka kwenda angana wanaeleka upward hawaji kwenye point waliyoondokea wamarekani.
Muelekeo wa upward unaujuaje kuwa huku ni juu ilhali muda huo kunaweza kukawa chini ya wengine. Kwa dunia mviringo kila mtu atakua na juu yake ila kwa dunia tambararevwote tutakua na juu moja.
Pitia picha za mfumo wa jua na sayari zake then utujuze waendso anga za mbali wanaelekea wapi? Kulifuata jua? Au kulikimbia jua?
 
mkuu je kivuli cha duara kwenye kupata kwa mwezi kinasababishwa na nini? pili kwanini sayari zote angani ziwe za duara dunia pekee iwe tambarare tatua je kwa dunia tambarare kupata kwa mwezi kunatokeaje
Maswali yako la kwanza na la tatu yatajibiwa na utakapoelewa kuwa hata dunia tambarare ni ya duara pia. Ila uduara huo unatofautiana kama mpira na sahani vyote vya duara ila kimoja mviringo kingine tambarare yaani ndio hyo flat iongelewayo.
 
Mkuu,nianze kusema tu kuwa nasikitika sana baada ya kusoma uzi huu kwa namna watu walivyochangia na wanavyochangia......

Mtoa mada amekuja na kuandika mambo mengi sana namna anavyosema juu ya umbo la dunia na ushahidi ameweka.Ameelezea kuwa yeye anaamini kuwa umbo la dunia ni flat,lakini akasema ni flat ya namna ipi anayoizungumzia.Shida ya kwanza ya watu inaanzia hapa...

Kuna watu wanapoona neno flat basi wanakimbilia kwenye fikra zao namna wanavyofikiria flat,wanafikiria flat kama ya meza tu,hapa ndipo panaponisikitisha kuliko mahala pengine popote pale.Mtoa mada ameelezea kuwa dunia ni flat duara yaani kama cd na michoro ameweka,watu wanakuja kujenga hoja kutoka na fikra za flat ya meza au umbo ambalo soyo duara kabisa.

Kwa kukuthibitishia hili angalia watu wanaojenga hoja kwa kuonesha kuwa mtu anaweza kutoka Dar hadi Sydney kisha akaenda Marekani kisha akarudi Accra na baadaye kurudi Dar.Ukiangalia hoja hii imelalia kwenye fikra za dunia isiyokuwa duara ya namna mleta mada aliyoizungumzia kwenye mada yake maana ukiangalia kwenye hoja za mtoa mada utaona kuwa mtoa mada naye anasema kuwa dunia ni duara lakini siyo mviringo kama tufe bali ni mviringo kama CD.Kwa mviringo huu unaweza kabisa kufanya safari hizo nilizotaja hapo juu bila kuhitajika kurudi nyuma.

Hoja ya watu kuzunguka dunia na kujikuta wamerudia pale pale,hoja hii nayo haishindikani kwenye hoja ya dunia duara ya kama sahani.Ukiangalia utaweza kuona kuwa inawezekana kabisa kuwa mtu akatoka Afrika ya kusini,akapitia Australia kisha akafika Amerika ya kusini kisha akarudi tena alipotoka maana atakuwa amezunguka duara inayosemwa na mtoa mada.Kwa maana hii bado hii haithibitishi kabisa kuwa dunia ni duara kwa maana ya tufe.....

Ameelezea mambo mengi sana pia,miongoni mwa mambo aliyozungumzia ni namna usiku na mchana unavyopatikana,watu hawasomi kabisa majibu na thread yote na unakuta mtu anakuja kurudia hoja ambazo zimeshajibiwa kwa uwazi kabisa na hili ni tatizo jingine,uviovu.Huwezi kujifunza mambo mazito kama haya huku ukiwa mvivu,huwezi na hutaweza kabisa kamwe......

Hoja nyingine ni route za ndege.Mtoa hoja amesema kuhusu hili,watu badala ya kujibu sababu ya ndege kutokuwa na rout hizi wameongeza swali kuwa vipi kuhusu ndege binafsi.Kwanza nafahamu kuwa kuna maswali ambayo ukiulizwa unaweza kuuliza aina fulani ya swali ambalo ukilijibu linaweza kukupa jibu la swali lako,lakini swali hili linaweza kujibu au kutokujibu swali kuu la mtoa mada kwasababu zifuatazo....

1;Hakuna uthibitisho ambao umetolewa hadi sasa wa uwepo wa ndege binafsi zinazokatiza north pole au south pole...

2;Kama kuna huo uwezekano wa ndege binasi kukatiza hapo,ni kwaninio ndege za kibiashara zisipite hapo ili kupunguza umbali mrefu? Kutoka South Afrika hadi Urusi kupitoa Siuth pole na kupitia katikati ya bara la Afrika hadi Geneva kisha Moscow wapi ni karibu?

Kimsingi hoja zote hizi ni mfu na zinaongeza maswali zaidi.Hakuna aliyejisumbua kujibu kuhusu ukweli wa binadamu kwenda mwezini.Hakuna ushahidi wa bibadamu kwenda mwezini....

Suala la meli kitoonekana kwa macho inapokuwa mbali ya macho yako hili mtoa mada amelijibu na ndiyo jibu bora kabisa linaloenezea suala hili.Watu walikuwa wanachukulia suala hili la meli kuzama kuwa ni moja ya ushahidi wa duara ya dunia,hii ikiwa na maana kuwa meli ile inakuwa imeshafika kwenye upande mwingine wa duara ya dunia.Mtoa mada amesema kuwa,kama inakuwa hivyo basi ukichukua kifaa maalum cha kuonea mbali usingeiona meli maana itakuwa iko kwenye upande mwingine wa duara ya dunia.

Mfano mzuri wa jambo hili ni kuchukua kijiti kifupi na ukakichoma kwenye chungwa kwenye upande mmoja kisha ukaligeuza chungwa lile upande mwingine kisha ukaanza kutazama,hutaweza kukiona kijiti kile kwakuwa kitakuwa kwenye upande ambao unazuiwa na muinuko wa chungwa lile hata kama utachukua kifaa cha kuonea mbali.Lakini ukichukua mti ukauchoma chini kwenye barabara iliyonyooka kisha ukaenda umbali wa kilomota 10 ukatazama mti ule hautauona bado lakini hii haimaanishi kuwa huuoni kwakuwa upo kwenye upande wa pili wa dunia bali ni kwasababu macho yako hayaoni tu,ukichukua kifaa utaweza kuuona mti huu.....

Kwa mfano huu ni dhahiri kuwa hoja za dunia duara bado zimegaragazwa kwenye mada hii,leteni nyingine......

Sisi tunajifunza na kuhoji pale ambapo tunaona kuna haja ya kufanya hivyo.......
Kaka nimereply kwa mara yakwanza kwako maana nadhani ww nimoja ya muelewa kama mimi, kifupi kila swali linaloulizwa humu lilishajibiwa kwenye mada ila uvivu wa kuchanganua ndio uliowajaa wauliza maswali
 
Flat earthers mnapotumia internet inayofanikishwa na satellite hizo hizo zinazowapa picha ya dunia iliyo duara mnanifurahisha sana.

Mngeikataa internet nayo kuwa si ya kweli ningewaona watu wa maana zaidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom