Sio siri, sema ulikuwa hujui. Mbona hiyo hongo ni ya tangu muda mrefu? Unadhani zile ndioooooooooooo ni za bure? Wanalipiza.Habari wana JF
Siku zote nimekuwa nikijiuliza jambo moja hapa Tz kwanini Ma Profesa, Wahandisi na wataalamu wabobezi kwenye fani mbalimbali wanaamua kuzipa kisogo fani zao na kukimbilia kwenye siasa hasa ubunge?!
Sasa leo Kisalala mbunge wa jimbo la Sumve amenipatia jibu. Wanafuata maslahi manono sana, kama kwa mwezi mbunge anapokea mshahara milioni 11 yaani huu ni nje ya posho zake unafikiri nani hatamani kupata fedha zote hizi?
Profesa wa chuo kikuu hapa bongo hata 7m hafikishi kwa mwezi sasa kwanini asiache kufundisha akakimbilia siasa?
Hayaaa bhana kuleni tu hizo milioni 11 za kila mwezi sisi wananchi tunaendelea kula msoto.
Wasalaam Xi JinPing